Rais Samia kayataka mwenyewe, alikuwa ameanza vizuri tu

Rais Samia kayataka mwenyewe, alikuwa ameanza vizuri tu

Siasa za mivutano ‘Confrontational Politics’ aliziweza Mwendazake, sidhani kama Rais Samia ataziweza.

Alipoingia madarakani Samia alikuja na hoja ya ‘Maridhiano’, hoja ambayo ilipokelewa vizuri na pande zote ingawa kwa shingo upande, baadhi hawakufurahishwa.

Kwa kiasi kikubwa siasa za vyama vya Upinzani hasa CHADEMA zilianza kupoa si kwa sababu ya vitisho vya vyombo vya dola bali walitegemea siasa za Rais Samia zinaweza kuwa tofauti na siasa za Mwendazake.

Hali imekuwa more of the same, imeanza kubadilika, mabadiliko haya naweza kusema yamechagizwa zaidi na ujio wa Mkataba wa Bandari.

Wananchi wameanza kusema wazi kuwa hawakubaliani na uamuzi wa Rais, yeye na wapambe wake wanasema anatukanwa.

Rais (CCM) kwa kutumia vyombo vya dola wanataka kuonesha wao ndio walioshika mpini, wanaompinga wameanza kushughulikiwa kama ilivyokuwa kipindi cha Magufuli.

Je, Samia ataziweza siasa za Mwendazake? Anao uhuru na uwezo wa kufunika kombe mwanahalamu apite ili amalizie kipindi chake.
Magufuli alilaaniwa na baadhi yetu kwa siasa zake hizo hizo ambazo leo mleta mada unaziona zina afadhali kuliko za sasa.

Mkuu awamu ya tano watu walificha pesa mpaka JPM akaongelea suala hilo hadharani, leo hii biashara nyingi mpya zinafunguliwa na hakuna anayeficha pesa.

Hakuna wamiliki wa bureau de change wanaoteseka kwa kunyang'anywa biashara zao mpaka wanapata presha zinazowaua kama ilivyokuwa awamu ya tano.

Kila rais anayekuwa ikulu hubebeshwa mzigo wa lawama, na mpaka akiondoka ndio tunakumbuka mema yake.
 
Katika vitu ambavyo rais Samia alikosea ni kuita maridhiano wakati hapakuwa na kitu mgogoro kati ya serikali na wapinzani bali kulikuwa na ujinga kama wa sasa wa kupinga kila kitu. Yeye alipaswa aelewe kuwa wapinzani wao kazi yao ni kupinga, kutukana hivyo ni vizuri kuwafuta na kuleta upinzani mwingine wenye staha. Sasa angalia anabyotukanwa rais wetu Samia tena mwenye mamlaka ya kusema ondoa huyu na akaondoka eti anafananishwa na matopeeee, yaani rais na urais wa Tanzania ni matopeee, nadhani sasa ataelewa vizuri kwanini Dkt Magufuli alikuwa vile
Ni nguvu ya wafadhili huko nje inayomuongoza Rais Samia. Tunategemea misaada kwa sehemu pana ya bajeti yetu na akawa hana cha kufanya ili mambo ya ndani yaweze kwenda vizuri.

Kukaa meza moja na wapinzani ni katika kutekeleza matakwa ya wenye pesa, hivyo huwezi kumsikia Rais SSH akiongea licha ya kutukanwa na kina Lissu tena matusi ya kukera sana.

Anachokifanya SSH kilimshinda JPM aliyekubali kufa na tai shingoni. Hakukubali kutii kila amri ya mzungu aliamini katika uhuru na jeuri ya mwafrika.
 
Katika vitu ambavyo rais Samia alikosea ni kuita maridhiano wakati hapakuwa na kitu mgogoro kati ya serikali na wapinzani bali kulikuwa na ujinga kama wa sasa wa kupinga kila kitu. Yeye alipaswa aelewe kuwa wapinzani wao kazi yao ni kupinga, kutukana hivyo ni vizuri kuwafuta na kuleta upinzani mwingine wenye staha. Sasa angalia anabyotukanwa rais wetu Samia tena mwenye mamlaka ya kusema ondoa huyu na akaondoka eti anafananishwa na matopeeee, yaani rais na urais wa Tanzania ni matopeee, nadhani sasa ataelewa vizuri kwanini Dkt Magufuli alikuwa vile
Kufuta upinzani na kuleta upya??Fara
 
Huu mkataba umeleta mpasuko mkubwa. Umefufua kwa nguvu JPM spirit. Na bahati mbaya, wanaoipigia debe wengi hawajiwezi kwa hoja, akili, ushawishi wala mvuto wa kisiasa.
Wamebaki kutukana watu mitandaoni. Kiburi si maungwana. Kusema kweli watanzania wamesema na wamesikika. Kuwadharau ni kujidharau wenyewe
 
Magufuli alilaaniwa na baadhi yetu kwa siasa zake hizo hizo ambazo leo mleta mada unaziona zina afadhali kuliko za sasa.

Mkuu awamu ya tano watu walificha pesa mpaka JPM akaongelea suala hilo hadharani, leo hii biashara nyingi mpya zinafunguliwa na hakuna anayeficha pesa.

Hakuna wamiliki wa bureau de change wanaoteseka kwa kunyang'anywa biashara zao mpaka wanapata presha zinazowaua kama ilivyokuwa awamu ya tano.

Kila rais anayekuwa ikulu hubebeshwa mzigo wa lawama, na mpaka akiondoka ndio tunakumbuka mema yake.
Kila shetani na mbuyu wake Magufuli alikuwa na mazuri na mabaya yake lkn hakuwa na mawazo ya kuuza rasilimali za nchi kama huyu wa leo.
 
Yawezekana ni mchezo ndani ya CCM wanahakikisha avuruge kuelekea 2025 then watu wa Usalama waseme mama pumzika upepo umekugomea kabisa. Afu jamaa waibuke dk ya 90 ya mchezo kuchukua ndoo.
 
Siasa za mivutano ‘Confrontational Politics’ aliziweza Mwendazake, sidhani kama Rais Samia ataziweza.

Alipoingia madarakani Samia alikuja na hoja ya ‘Maridhiano’, hoja ambayo ilipokelewa vizuri na pande zote ingawa kwa shingo upande, baadhi hawakufurahishwa.

Kwa kiasi kikubwa siasa za vyama vya Upinzani hasa CHADEMA zilianza kupoa si kwa sababu ya vitisho vya vyombo vya dola bali walitegemea siasa za Rais Samia zinaweza kuwa tofauti na siasa za Mwendazake.

Hali imekuwa more of the same, imeanza kubadilika, mabadiliko haya naweza kusema yamechagizwa zaidi na ujio wa Mkataba wa Bandari.

Wananchi wameanza kusema wazi kuwa hawakubaliani na uamuzi wa Rais, yeye na wapambe wake wanasema anatukanwa.

Rais (CCM) kwa kutumia vyombo vya dola wanataka kuonesha wao ndio walioshika mpini, wanaompinga wameanza kushughulikiwa kama ilivyokuwa kipindi cha Magufuli.

Je, Samia ataziweza siasa za Mwendazake? Anao uhuru na uwezo wa kufunika kombe mwanahalamu apite ili amalizie kipindi chake.
tulia maza ni bingwa

Sent from my CPH2371 using JamiiForums mobile app
 
Kila shetani na mbuyu wake Magufuli alikuwa na mazuri na mabaya yake lkn hakuwa na mawazo ya kuuza rasilimali za nchi kama huyu wa leo.
Tatizo naloliona kwako lipo kwa watanzania wengi.

Kuamini katika maneno ya upotoshaji yasiyo na ukweli wowote. Hakuna anayeuza nchi hata robo ya Mita moja.

Ni uwekezaji ambao hata Magufuli angeufanya kama angekuwa hai. Kwani SGR ilijengwa kwa ajili ya shughuli hii hii tunayomtukania Samia leo hii!!

Watanzania aliyeturoga keshakufa kitambo.
 
Katika vitu ambavyo rais Samia alikosea ni kuita maridhiano wakati hapakuwa na kitu mgogoro kati ya serikali na wapinzani bali kulikuwa na ujinga kama wa sasa wa kupinga kila kitu. Yeye alipaswa aelewe kuwa wapinzani wao kazi yao ni kupinga, kutukana hivyo ni vizuri kuwafuta na kuleta upinzani mwingine wenye staha. Sasa angalia anabyotukanwa rais wetu Samia tena mwenye mamlaka ya kusema ondoa huyu na akaondoka eti anafananishwa na matopeeee, yaani rais na urais wa Tanzania ni matopeee, nadhani sasa ataelewa vizuri kwanini Dkt Magufuli alikuwa vile
Magufuli hakupaswa kuwa kiongozi haswa ngazi ya urais, ndio maana aklitawaliwa na jazba. Eti kwamba afute upinzani alete upinzani wenye staha, kwani upinzani unawekwa na CCM? Kama unaingia madarakani kwa njia zisizo za staha, ni staha gani unaitaka baada ya kupora uchaguzi?
 
Tatizo naloliona kwako lipo kwa watanzania wengi.

Kuamini katika maneno ya upotoshaji yasiyo na ukweli wowote. Hakuna anayeuza nchi hata robo ya Mita moja.

Ni uwekezaji ambao hata Magufuli angeufanya kama angekuwa hai. Kwani SGR ilijengwa kwa ajili ya shughuli hii hii tunayomtukania Samia leo hii!!

Watanzania aliyeturoga keshakufa kitambo.
Mkataba usio na kikomo ni sawa na kuiuza tu.
 
Back
Top Bottom