Rais Samia kayataka mwenyewe, alikuwa ameanza vizuri tu

Rais Samia kayataka mwenyewe, alikuwa ameanza vizuri tu

Hizo siasa za mivutano mbona alizianza mapema tu, pale alipombambikia Mbowe kesi, aliyekuwa akiidai Katiba Mpya kaa nguvu, baada ya Samia kusikika akisema ukinipara nitakuparua.

Baada ya pale kelele za watu kudai Mbowe aachiwe huru zaidi ya miezi sita mfululizo ndizo zikamlainisha, akamtoa, na kumualika ikulu moja kwa moja akijua wazi alipogusa alikosea.

Baada ya hapo ndipo akaja na ile issue ya maridhiano, haya maridhiano aliyafanya akidhani wapinzani akiwemo Mbowe atawateka akili, hasa baada ya "kumtuliza" ikulu, kwamba hata akikosea mbele ya safari, hawatamgusa..

Bahati mbaya huu mkataba wa hovyo wa bandari umekuja kumvurugia kila kitu, sasa kazi kwake, naona uzalendo umeshaanza kumshinda, anawakabidhi hiyo kazi wakina Kingai ili wamsaidie kuwanyamazisha wanaozidai bandari zetu.

Sasa ngoja tuone, baada ya hii stage ya kwanza ya kuwaita na kuwahoji wala tusijue wanawaambia nini, watakuwepo waoga wataonyamaza, na wale wakaidi wataoendelea kuhoji, tuone next time watafanywa kitu gani na kina Kingai.
Yule Mama ana dharau sana na kiburi juu,mchunguzeni vizuri!
 
Katika vitu ambavyo rais Samia alikosea ni kuita maridhiano wakati hapakuwa na kitu mgogoro kati ya serikali na wapinzani bali kulikuwa na ujinga kama wa sasa wa kupinga kila kitu. Yeye alipaswa aelewe kuwa wapinzani wao kazi yao ni kupinga, kutukana hivyo ni vizuri kuwafuta na kuleta upinzani mwingine wenye staha. Sasa angalia anabyotukanwa rais wetu Samia tena mwenye mamlaka ya kusema ondoa huyu na akaondoka eti anafananishwa na matopeeee, yaani rais na urais wa Tanzania ni matopeee, nadhani sasa ataelewa vizuri kwanini Dkt Magufuli alikuwa vile
Comment ya mwaka hii kwangu ,hongera kwa kuona mbali. Labdac kwa kuongezea tu hayo meridhiano ni upambe tu wa kuonyesha jpm aliendesha nchi vibaya na kwa sasa samia ni mzuri kuliko mtangulizi wake ,
 
Bandari imeleta mtafaruku mkubwa sana
 
Nioneshe kauli zao kuhusu Bandari nami nikuoneshe matusi yao.
Angalia sababu za maombi yoo ya kikatiba kupinga mkataba waliyowasilisha mahakamani unionyeshe tusi.

 
Suala la Bandari ni sera ya chama CCM,chama kilicho madarakani hakiwezi kusikiliza kelele za wapinzani dhidi ya sera yake.
Ukiwa na Akili nzuri ni lazima utajua hivyo !!

Sasa wale wanaoona eti mama yupo kwenye wakati mgumu naona kama wamekosea mahesabu !!
 
Ukiwa na Akili nzuri ni lazima utajua hivyo !!

Sasa wale wanaoona eti mama yupo kwenye wakati mgumu naona kama wamekosea mahesabu !!
Nyie mnaoona yuko kwenye wakati mzuri endeleeni kumpotosha hadi atakaposhtuka mwenyewe, Magu alichelewa kuliona hilo kwa upambe wenu mkamponza.
 
Siasa za mivutano ‘Confrontational Politics’ aliziweza Mwendazake, sidhani kama Rais Samia ataziweza.

Samia alikuja na hoja ya ‘Maridhiano’, hoja ambayo ilipokelewa vizuri na pande zote ingawa kwa shingo upande, baadhi hawakufurahishwa.

Kwa kiasi kikubwa siasa za vyama vya Upinzani hasa CHADEMA zilianza kupoa si kwa sababu ya vitisho vya vyombo vya dola bali walitegemea siasa za Rais Samia zinaweza kuwa tofauti na siasa za Mwendazake.

Hali imekuwa more of the same, mambo yameanza kubadilika, mabadiliko haya naweza kusema yamechagizwa zaidi na ujio wa Mkataba wa Bandari.

Wananchi wanasema wazi kuwa hawakubaliani na uamuzi wa Rais, yeye na wapambe wake wanasema anatukanwa.

Rais (CCM) kwa kutumia vyombo vya dola wanataka kuonesha wao ndio walioshika mpini, wanaompinga wameanza kushughulikiwa kama ilivyokuwa kipindi cha Magufuli.

Je, Samia ataziweza siasa za Mwendazake? Anao uhuru na uwezo wa kufunika kombe mwanahalamu apite ili amalizie kipindi chake.
Unadhani huyu mama hajui analolifanya. Ukimsikiliza kwa makini rais mstaafu Jakaya utagundua mama huyu ni stadi sana wa kucheza rafu.
 
Nyie mnaoona yuko kwenye wakati mzuri endeleeni kumpotosha hadi atakaposhtuka mwenyewe, Magu alichelewa kuliona hilo kwa upambe wenu mkamponza.
Collective responsibility ndivyo ilivyo !
Haamui jambo peke yake !!
 
Collective responsibility ndivyo ilivyo !
Haamui jambo peke yake !!
Rais ni final say, Collective Responsibility iko kwa wasaidizi wake mawaziri, RCs nk. ndio maana hata sheria ikitungwa bungeni hupelekewa yeye ana uwezo wa kuipitisha au kuikataa. Hata mkataba anaweza kuukubali au kuukataa.
 
Katika vitu ambavyo rais Samia alikosea ni kuita maridhiano wakati hapakuwa na kitu mgogoro kati ya serikali na wapinzani bali kulikuwa na ujinga kama wa sasa wa kupinga kila kitu. Yeye alipaswa aelewe kuwa wapinzani wao kazi yao ni kupinga, kutukana hivyo ni vizuri kuwafuta na kuleta upinzani mwingine wenye staha. Sasa angalia anabyotukanwa rais wetu Samia tena mwenye mamlaka ya kusema ondoa huyu na akaondoka eti anafananishwa na matopeeee, yaani rais na urais wa Tanzania ni matopeee, nadhani sasa ataelewa vizuri kwanini Dkt Magufuli alikuwa vile
Wewe ni sifuri, watu wanapinga mkataba wa Kimangungo wewe unaunga mkono? Chief Mangungo alikuwa hajui kusoma miaka hiyo ya 1877 akabambikiwa mkataba kwa malipo ya shanga, Sasa Hawa wanajua kusoma na elimu kubwa wamesaini mkataba wa Kimangungo watu wasiseme?
 
Rais ni final say, Collective Responsibility iko kwa wasaidizi wake mawaziri, RCs nk. ndio maana hata sheria ikitungwa bungeni hupelekewa yeye ana uwezo wa kuipitisha au kuikataa. Hata mkataba anaweza kuukubali au kuukataa.
Na mara zote ataliafiki lile lililokubaliwa na wengi tu na si vinginevyo !!
 
Katika vitu ambavyo rais Samia alikosea ni kuita maridhiano wakati hapakuwa na kitu mgogoro kati ya serikali na wapinzani bali kulikuwa na ujinga kama wa sasa wa kupinga kila kitu. Yeye alipaswa aelewe kuwa wapinzani wao kazi yao ni kupinga, kutukana hivyo ni vizuri kuwafuta na kuleta upinzani mwingine wenye staha. Sasa angalia anabyotukanwa rais wetu Samia tena mwenye mamlaka ya kusema ondoa huyu na akaondoka eti anafananishwa na matopeeee, yaani rais na urais wa Tanzania ni matopeee, nadhani sasa ataelewa vizuri kwanini Dkt Magufuli alikuwa vile
Mama hawezi dhulumu nafsi ya mtu, ni Muislam safi.
 
Siasa za mivutano ‘Confrontational Politics’ aliziweza Mwendazake, sidhani kama Rais Samia ataziweza.

Samia alikuja na hoja ya ‘Maridhiano’, hoja ambayo ilipokelewa vizuri na pande zote ingawa kwa shingo upande, baadhi hawakufurahishwa.

Kwa kiasi kikubwa siasa za vyama vya Upinzani hasa CHADEMA zilianza kupoa si kwa sababu ya vitisho vya vyombo vya dola bali walitegemea siasa za Rais Samia zinaweza kuwa tofauti na siasa za Mwendazake.

Hali imekuwa more of the same, mambo yameanza kubadilika, mabadiliko haya naweza kusema yamechagizwa zaidi na ujio wa Mkataba wa Bandari.

Wananchi wanasema wazi kuwa hawakubaliani na uamuzi wa Rais, yeye na wapambe wake wanasema anatukanwa.

Rais (CCM) kwa kutumia vyombo vya dola wanataka kuonesha wao ndio walioshika mpini, wanaompinga wameanza kushughulikiwa kama ilivyokuwa kipindi cha Magufuli.

Je, Samia ataziweza siasa za Mwendazake? Anao uhuru na uwezo wa kufunika kombe mwanahalamu apite ili amalizie kipindi chake.
Kicha mada kinavutia kweli ila sasa ndugu ulicho weka kwenye content kimekua cha ajabu. Sio vibaya ukiandika upya na kuweka mizania sawa
 
Siasa za mivutano ‘Confrontational Politics’ aliziweza Mwendazake, sidhani kama Rais Samia ataziweza.

Samia alikuja na hoja ya ‘Maridhiano’, hoja ambayo ilipokelewa vizuri na pande zote ingawa kwa shingo upande, baadhi hawakufurahishwa.

Kwa kiasi kikubwa siasa za vyama vya Upinzani hasa CHADEMA zilianza kupoa si kwa sababu ya vitisho vya vyombo vya dola bali walitegemea siasa za Rais Samia zinaweza kuwa tofauti na siasa za Mwendazake.

Hali imekuwa more of the same, mambo yameanza kubadilika, mabadiliko haya naweza kusema yamechagizwa zaidi na ujio wa Mkataba wa Bandari.

Wananchi wanasema wazi kuwa hawakubaliani na uamuzi wa Rais, yeye na wapambe wake wanasema anatukanwa.

Rais (CCM) kwa kutumia vyombo vya dola wanataka kuonesha wao ndio walioshika mpini, wanaompinga wameanza kushughulikiwa kama ilivyokuwa kipindi cha Magufuli.

Je, Samia ataziweza siasa za Mwendazake? Anao uhuru na uwezo wa kufunika kombe mwanahalamu apite ili amalizie kipindi chake.
 

Attachments

  • 3E34DBDB-CC68-4AF3-B001-C0BE9C82F9D9.jpeg
    3E34DBDB-CC68-4AF3-B001-C0BE9C82F9D9.jpeg
    54 KB · Views: 2
Back
Top Bottom