Lancashire
JF-Expert Member
- Sep 20, 2014
- 14,057
- 10,367
Habari za jumatatu Mh. Rais
Nimesikia kuwa baadhi ya wasaidizi wako wa karibu wanawatumia baadhi ya watu kukuchafua ( kukutukana). Nilikua nataka nikushauri Rais usije ukakubali kuyumbishwa na watu hao kwasababu ukiyumba wewe kama kiongozi wetu na sisi wananchi tutapoteza mwelekeo.
Kama umezisikia taarifa hizo za hao wanaotuma watu kukutukana tafadhali thibitisha na kama ukijua ni kweli basi nakushauri uwape (option) aidha kukaa kando ya serikali unayoingoza au laa sivyo wakueleze hasa nini wanachokitaka ikikupendeza wape ONYO kazi iendelee.
Lakini pia ushauri wangu wa pili fitina kipindi hiki zitakua nyingi sana hasa kuelekea uchaguzi nakuomba Rais najua ni vigumu sana kushindwa kuwaamini wasaidizi wako lakini usiwaamini kwa 100% fanya nao kazi kwa tahadhari sana usimwamini yeyote yule hata awe ni Makamu wako wa Rais.
Vyama vya upinzani nao hawatabaki nyuma kupitia mambo haya nao watazidisha kila uzushi ilimradi tu kukupotezea vision. Hilo usilikubali. Kazi ya CCM kwa sasa ni kusafisha hali ya hewa ndani ya serikali. Naamini chama wapo vizuri kazi inaendelea.
Mimi siyo mshauri wako rasmi wa Rais lakini kwa niliyoyasikia recently nilipenda nikushauri Rais wangu. Nikutakie kazi njema katika ujenzi wa Taifa letu.
Wasalaam!
Nimesikia kuwa baadhi ya wasaidizi wako wa karibu wanawatumia baadhi ya watu kukuchafua ( kukutukana). Nilikua nataka nikushauri Rais usije ukakubali kuyumbishwa na watu hao kwasababu ukiyumba wewe kama kiongozi wetu na sisi wananchi tutapoteza mwelekeo.
Kama umezisikia taarifa hizo za hao wanaotuma watu kukutukana tafadhali thibitisha na kama ukijua ni kweli basi nakushauri uwape (option) aidha kukaa kando ya serikali unayoingoza au laa sivyo wakueleze hasa nini wanachokitaka ikikupendeza wape ONYO kazi iendelee.
Lakini pia ushauri wangu wa pili fitina kipindi hiki zitakua nyingi sana hasa kuelekea uchaguzi nakuomba Rais najua ni vigumu sana kushindwa kuwaamini wasaidizi wako lakini usiwaamini kwa 100% fanya nao kazi kwa tahadhari sana usimwamini yeyote yule hata awe ni Makamu wako wa Rais.
Vyama vya upinzani nao hawatabaki nyuma kupitia mambo haya nao watazidisha kila uzushi ilimradi tu kukupotezea vision. Hilo usilikubali. Kazi ya CCM kwa sasa ni kusafisha hali ya hewa ndani ya serikali. Naamini chama wapo vizuri kazi inaendelea.
Mimi siyo mshauri wako rasmi wa Rais lakini kwa niliyoyasikia recently nilipenda nikushauri Rais wangu. Nikutakie kazi njema katika ujenzi wa Taifa letu.
Wasalaam!