Rais Samia kuanza safari ya kikazi nchini DR Congo

Rais Samia kuanza safari ya kikazi nchini DR Congo

Yule mwingine alikuwa hasafiri watu wakasema anasababisha nchi kuwa na mahusiano mabaya ya nje,sasa huyu mwingine anatoka naye wanasema anatafuna kodi za wananchi,sijajua bado watanzania tunataka raisi wa aina gani...

Labda malaika....

#KaziIendelee
 
Umesoma nilichoandika?Wapi nimepinga Rais kusafiri?Hoja yangu ni kwamba Rais anapotoa kipaumbele cha kusafiri kwenda Congo,Burundi sijui Zimbabwe,je hizo ndiyo nchi zenye tija kwa Taifa letu kuliko nchi nyingine duniani?
Nchi nyingine zipi zenye tija kwa uchumi wetu mkuu? Za magharibi zinazotupa mikopo ya masharti makubwa au?
 
Wakuu Kazi Iendeleee.

Taarifa zilizopo ni kwamba Rais Samia ana ziara ya kikazi nchini Congo.

Ataanza ziara hiyo wakati atakapotoka Zambia kwenye inauguration ya Hakainde Hichilema.

Akifika Congo atapokekewa na Mwenyeji Wake Rais Felix Tshisekedi.

Hakika Ziara zimeanza na Zimetaradadi
Msafara wake una watu wangapi? Kuna nini huko?
 
Kama mshauri wake ni vasco da gama unategemea nini?

Halafu nchi anazosafiri kwenda zina mchango mdogo kwenye uchumi wetu.

Asafiri kutafta wawekezaji wa maana huko Ulaya walete mitaji kutusaidia ku exploit hizi natural resources tulizonazo.

Sio muda utasikia ana ziara Somalia.

Yaani hapa tumeingia cha kike kweli.
Wajumbe wa msafara kina nani? Wale wazee wa Saigon waliokuwa wanatafuta wawekezaji enzi zile inabidi watupe mrejesho
 
Hoja yangu ni kwamba mtu hapaswi kutoa taarifa za kupotosha katika jukwaa hili.Kwa kuwa ulitoa taarifa za kupotosha na ambazo hazina evidence unapaswa kwanza kukiri kuwa umekosea na uwaombe msamaha wana jukwaa hili halafu baada ya hapo ndipo mimi nikusaidie kuweka evidences zinazoonyesha ni nchi gani zinapaswa kuwa kipaumbele chetu.

Mimi sijakutukana popote pale labda uniwekee ushahidi hapa kuwa nimekutukana.
Hakuna sehemu niliyopotosha.....unapotosha ili nionekane mpotoshaji?!!!

Mtiririko wa comments zangu uliangazia tija ya safari za mh.Rais na nchi zinazotuzunguka...nikatolea mfano wa Burundi,Zambia ,Kongo(land locked countries) na matumizi ya bandari yetu kwao.....nikauliza kwa hiyo bandari yetu haina tija.....ukaja na kusema sina STATISTICS za wao KUTUINUA KIUCHUMI.....nikaendelea kukutaka UNIWEKEE STATISTICS zako kinzani....matokeo yake hujaniwekea na unang'ang'ana tu kuwa NIMEPOTOSHA...khaa😲😲😲
 
Wengine wanataka labda aende UJERUMANI....

Mathalani Ujerumani ni marafiki zetu Sana.....lakini tukumbuke ya kwamba ni miaka tu ya karibuni ambako BAADHI YA WABUNGE WA CDU (marafiki wa Chadema) wakiwa ndani ya BUNGE lao(BUNDESTAG) walitupinga TUSIENDELEE NA UJENZI wa kituo cha uzalishaji wa megawati 2200 za umeme pale Mwalimu Nyerere....kisa tutaharibu TURATHI la dunia la SELOUS.....

#KaziIendelee
 
Ziara ya nchi za maziwa makuu,Zina manufaa kwa nchi yetu,kibiashara (kuuza mazao yetu-Mahindi au kushawishi nchi hizo kupitishia bidhaa zao bandari ya Dar es Salaam. Serikali kuanzia awamu ya tano, imefanya uwekezaji mkubwa bandari ya Dar na reli ya SGR inayojengwa,ni busara kuanza kuingia mikataba ya kibiashara na nchi zinazo zunguka maziwa makuu watumie huduma zetu sasa na siku za usoni,vinginevyo uwekezaji wote unaweza usiwe na tija(white elephant).

Ninadhani kupitia jamiiforum, tunapoona Rais anatembelea nchi fulani, tunaweza kutoa maoni yetu ya kujenga (constructive idea) nchi yetu, kwa mfano nini Mheshimiwa akatuzungumzie wananchi wake huko ughaibuni (yenye kuleta tija kwa nchi), kwa maana wakati mwingine wasaidizi wake wanakuwa hawayajua matatizo ya huku chini (grassroot level) kwa mfano tumshauri Kama Kuna vikwazo vya biashara kati ya Tanzania na nchi anayokwenda,nk.
Kuwauzia bidhaa/mazao maskini wenzetu hatutapiga hatua yoyote. Tutafute masoko huko dunia ya kwanza.
 
Safari zao ni vinchi vya ovyo tu kama jiwe
Huwezi kusikia wameenda ulaya na marekani
Au wanaziogopa cnn na fox news
 
Hakuna sehemu niliyopotosha.....unapotosha ili nionekane mpotoshaji?!!!

Mtiririko wa comments zangu uliangazia tija ya safari za mh.Rais na nchi zinazotuzunguka...nikatolea mfano wa Burundi,Zambia ,Kongo(land locked countries) na matumizi ya bandari yetu kwao.....nikauliza kwa hiyo bandari yetu haina tija.....ukaja na kusema sina STATISTICS za wao KUTUINUA KIUCHUMI.....nikaendelea kukutaka UNIWEKEE STATISTICS zako kinzani....matokeo yake hujaniwekea na unang'ang'ana tu kuwa NIMEPOTOSHA...khaa😲😲😲
Umepotosha uma kwa sababu huwezi kuibuka tu na kusema kuwa Congo au Burundi ina tija kuliko nchi nyingine duniani kwa hiyo inafaa kupewa kipaumbele katika ziara za Rais wakati huna ushahidi unaosupport kauli yako hiyo.

Unapoongea masuala yanayohitaji shahidi za data bila kuwa na shahidi hizo ni upotoshaji.
 
Wakuu Kazi Iendeleee.

Taarifa zilizopo ni kwamba Rais Samia ana ziara ya kikazi nchini Congo.

Ataanza ziara hiyo wakati atakapotoka Zambia kwenye inauguration ya Hakainde Hichilema.

Akifika Congo atapokekewa na Mwenyeji Wake Rais Felix Tshisekedi.

Hakika Ziara zimeanza na Zimetaradadi
Safi sana, hii ndio staili yake ya kukuza na kudumisha uhusiano kati ya nchi yetu na nchi nyingine ikiwa ni pamoja hizi za majirani wetu. Binafsi sioni ubaya wala tatizo to this approach by our President. Si mnajua in life, kila mtu na in this sense, kila kiongozi, ana staili yake na approach yake ya kutawala na kuongoza nchi na watu wake na kufanya vile anayodhani ndiyo NJIA NA APPROACH SAHIHI ya kufikia malengo yake ya muda mfupi na muda mrefu kwa manufaa ya nchi na watu wake.
 
Hii ziara inaweza kuwa ya kimkakati na ya muhimu pengine kuliko ziara zote zilizofanyika toka mama aingie ikulu. Ni jambo la wazi kuwa katika nchi zote za maziwa makuu, DRC imejaaliwa kuwa na idadi kubwa ya watu takriban watu 120,000,000.

Itakumbukwa kuwa Tanzania tumejaaliwa kuwa na bandari, ambapo miongoni mwa nchi zinazotumia bandari yetu ni DRC.

Tanzania imekuwa ujenzi mkubwa wa reli ya mwendokasi ambayo inategemewa kuwa msaada mkubwa wa usafirishaji wa watu na mizigo kuelekea nchi za Rwanda, Burundi na DRC. Kimkakati, kama ujenzi huo utakamilika, Tanzania itakuwa imalamba dume kwa sababu tutaweza kujiinua kiuchumi kupitia sekta ya usafirishaji pamoja na kufaidika na masoko ya bidhaa zetu kupitia wato miliuoni miamoja waliopo mashariki mwa Kongo.

Mnyonge mnyongeni lakini haki haki yake apewe. Ziara ya Rais wetu huko DRC haipaswi kubezwa kwa sababu kiuchumi inalipa tofauti na nchi kama Rwanda, Burundi na Uganda ambazo zinapitisha mizigo yao katika bandari yetu ya Dar Es Salaam lakini, mizigo yao kidogo kuliko ile DRC kutokana na idadi ya watu katika nchi hizo ni ndogo.

Hongera Mh. Raisi wetu kwa kupanga ziara ya kimkakati ya DRC ambayo ni muhimu sana kwa musakabali wa uchumi wa nchi yetu.
Mkuu, umesomea uchumi?
Kama jibu ni Ndiyo basi unatumia vibaya taaluma yako kutetea Uzurulaji wa Miss Vasco da Gama.
Wewe unawaza ujenzi wa Reli na uwepo wa Bandari uta/unasaidia kukuza Uchumi wetu ila wachumi na Viongozi wetu wameona Tozo ndo zitasaidia kukuza Uchumi.
 
Nchi nyingine zipi zenye tija kwa uchumi wetu mkuu? Za magharibi zinazotupa mikopo ya masharti makubwa au?
Siyo kweli kwamba nchi za Magharibi huwa zinatupa mikopo ya gharama kubwa kwa kuwa tumeshuhudia mara nyingi nchi hizi zikitoa mikopo ya gharama nafuu hata mara nyingine kutusamehe mikopo hiyo.
 
Siyo kweli kwamba nchi za Magharibi huwa zinatupa mikopo ya gharama kubwa kwa kuwa tumeshuhudia mara nyingi nchi hizi zikitoa mikopo ya gharama nafuu hata mara nyingine kutusamehe mikopo hiyo.
Kweli tunahitaji kubishana on this kuwa nchi za magharibi huwa zinatupa au hazitupi mikopo migumu na yenye masharti magumu!? Kweli hakuna ajuaye haya na namna walivyotuwekea ngumu juu ya ujenzi wa Bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere huko Rufiji, eti kwa kigezo cha kuharibu mazingira ya Selous Gama Reserve!? Hakuna ajuaye hili na mengine mengi!? Tusijifanye hamnazo kwa mambo yaliyo wazi!
 
Naam!

Rais wa Jamhuri ya MUUNGANO WA TOZO.
Hayo ni maneno ya watu wasioitakia mema na maendeleo nchi hii; ni mfano mzuri wa mchawi anayetaka kukulelea mwanao kwa nia ya kumtumia kichawi! Ndivyo walivyo wasioitakia mema nchi, watatoa majina mengi ili kuwakatisha tamaa wazalendo wa nchi hii katika kujenga uchumi na kujiletea maendeleo yao. Hivi hiyo misaada kutoka Japani au Amerika au Uchina na kwingineko, unadhani wao wanazipata wapi kama siyo kwenye KODI NA TOZO ZA WATU WAO!? Hebu tujiongeze kwa faida ya nchi yetu.
 
Hayo ni maneno ya watu wasioitakia mema na maendeleo nchi hii; ni mfano mzuri wa mchawi anayetaka kukulelea mwanao kwa nia ya kumtumia kichawi! Ndivyo walivyo wasioitakia mema nchi, watatoa majina mengi ili kuwakatisha tamaa wazalendo wa nchi hii katika kujenga uchumi na kujiletea maendeleo yao. Hivi hiyo misaada kutoka Japani au Amerika au Uchina na kwingineko, unadhani wao wanazipata wapi kama siyo kwenye KODI NA TOZO ZA WATU WAO!? Hebu tujiongeze kwa faida ya nchi yetu.
Sio nchi hii mtu anaiba mabilioni ya pesa anakaa miaka yake mitano jela, anapigwa faini ya milioni 8 anaenda kutumia uswahilini.
 
Back
Top Bottom