Rais Samia, kuna mtu mmoja tu hapa Tanzania anaweza kukusaidia kuuvuka huu mtihani wa DP World na TEC - muite, ongea nae, msikilize, ufanye atachosema

Rais Samia, kuna mtu mmoja tu hapa Tanzania anaweza kukusaidia kuuvuka huu mtihani wa DP World na TEC - muite, ongea nae, msikilize, ufanye atachosema

Hapo ulipoandika kuna MTU MMOJA TU
Yaani Tanzania nzima yenye watu zaidi ya milioni sitini kuna mtu mmoja tu

Ndugu yangu Synthesizer ule uamuzi wa kutokuleta nyuzi hapa endelea nao mana mawazo yako yanakaribia kugota
MTU MMOJA TU kati ya wote ninaowafahamu mie, na ambae najua utendaji wake katika masuala kama haya. Kama yupo mwingine unaona ni mwenye busara zaidi ya Prof Mwandosya mtaje basi, na useme wazi ni vitu gani amefanya kama nilivyojieleza juu ya Prof. Mwandosya. Sio lazima awe Prof. Mwandosya, kama ambavyo sio lazima Waziri Mkuu awe Majaliwa, lakini Majaliwa alipoteuliwa yeye ndio alifahamika kati ya Watanzania milioni 60 kuwa apewe uwaziri Mkuu.

Kwa nini ushindwe kuelewa lojiki ndogo namna hii?
 
Sasa wewe umemjuaje huyu mtu?

Jamaa umetumia kigezo gani cha kisayansi kujua, he is the one and only One can do that??

Tunahitaji muafaka ila walau njia tunazopendekeza walau ziwe scientifically hata kwa 75% tu inatosha

Sijabisha ila nataka kujua hiyo randomized sampling technique yako umefanyaje??
Kuna mambo huitaji sayansi kujua acha ubwege,
 
Raisi Samia alipaswa kuteua timu yake ya kumshauri masuala yake yeye mwenyewe binafsi yaani "Personally".

Hivi ndivyo wafanyavyo viongozi wengi wenye nia njema na nchi zao.

Kuna watu hadi wanasaikolojia ambao humshauri kiongozi pale penye matatizo yanohitaji akili kuchambua kwa makini masuala mazito kabla ya kuja na uamuzi.

Timu ya washauri binafsi ambao si lazima wawe kwenye payroll ya serikali.

Hivyo, badala ya kumteua profesa Mwandosya kwenda EWURA kula pensheni ni bora awe mshauri wako wa karibu umlipe kama "private consultant or adviser" kuliko kwenda EWURA kuzuia nafasi kwa vijana.

NB
Naomba nitofautishe wasaidizi na washauri wa raisi ni watu tofauti.
Ni kipi hamjui? Hivi mnadhani hajui watu wanaoweza kumshauri? Ukweli ni kwamba Samia anataka wale watu wenye kusema ndiyo mama. Hivi ukiwa rais mwenye akili nzuri unaweza kumpa ukuu wa mkoa mtu kama Chalamila? Au uwaziri mtu kama Mwingulu?
 
Raisi Samia, kwa sababu ya mambo fulani yaliyojitokeza hupa JF Forums, niliahidi kutotoa post tena. Lakini kwa ajili yako nimeamua kuvunja mwiko huo.

Nimefuatilia kwa makini sana yanayoendelea juu ya suala la DP World, jinsi lilivyoshughulikiwa Bungeni, na sasa kufikia hatua ya tamko la TEC. NI kweli kwamba suala hili linazidi kuweka taswira mbaya sana nchini, na huenda linakukosesha usingizi kwa kuwa hukutarajia litafika huku. Nahisi pia kuna mambo ambayo hatujui, labda upande wa UAE-Dubai, yanayolifanya liwe gumu hata zaidi. Na usipoangalia mambo yatazidi kuharibika.

Sasa maraisi wa kabla yako wamewahi kupitia vipindi vigumu kama vyako. Raisi Mkapa kuna wakati kulikuwa na suala na rada ya BAE. Serikali ya Uingereza ikamsumbua sana. Akaomba huyu mtu nitakaekutajia mwishoni amsaidie kulitatua. Na matokeo ni kwamba huyu mtu alilitatua kwa namna ambayo ilimfanya Raisi Mkapa amheshimu sana, kwa kuwa alilitatua kwa namna ya hekima, na ufahamu wa hali ya juu, hata Uingereza wakamsifia kwa hekima zake kwa jinsi alivyolitatua.

Kisha wakati fulani uhusiano kati ya Raisi Kikwete na Raisi Kagame uliharibika sana, hata Raisi Kagame akatishia kumpiga Raisi Kikwete. Kuona hivyo, Raisi Kikwete ikabidi amuombe huyu mtu asaidie kulimaliza hili suala, na kwa mara nyingine akalimaliza kwa namna ya busara sana iliyorejesha uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda kwenye hali ya kawaida. Kutoka hapo Raisi Kikwete aliamua huyu mtu akae karibu yake katika ofisi ya Raisi ili azidi kumsaidia mambo mengine mengi.

Na labda nikuambie pia wakati fulani kulikuwa na suala la kupeleka boti za abiria kwenye ziwa Victoria, na mtangulizi wako Raisi Magufuli akagoma katakata kuzipeleka boti hizi kupitia barabara zetu. Hii ilileta mtafaruku sana kati ya mfanyabiashara maarufu nchini na serikali. Huyo huyo mtu ninaekuambia akaamua kuingilia kati na kuwasiliana na serikali ya Kenya. Kwa diplomasia yake serikali ya Kenya ilikubali kutatua tatizo hili. Jinsi alivyotatua tatizo hili ilimletea heshima sana kwa baraza la mawaziri Kenya na Tanzania, japo ilimfadhaisha sana Magufuli, wakati huo akiwa waziri katika serikali ya Kikwete, na kufanya awe na chuki nae, chuki aliyoiendeleza hata alipochaguliwa kuwa raisi.

Na labda utakuwa unajua kwamba huyu mtu aliingizwa katika serikali kutokana na ushauri wa Raisi Clinton kwa Mkapa. Raisi Clinton alishangaa sana kwamba kwa nini serikali ilikuwa haimtumii mtu huyu ambae Raisi Bill Clinton na Makamu wake Al Gore walimsifia sana kwa jinsi alivyoshughulikia kwa umakini mkubwa na busara za hali ya juu negotiations za climate change akiwa msemaji wa Group of 77 and China. Mkapa akawasikiliza.

Japo si mwanasheria, kuna wakati, Tanzania na nchi nyingine za mto Nile wakiwa katika mkutano wa kusign makubaliano ya Mto Nile, alizuia utiaji sahihi wa makubaliano hayo baada ya kugundua vipengele katika mkataba huo ambavyo mawaziri wa nchi nyingine hawakuviona. Vilikuwa vipengele ambavyo vilitoa faida kubwa kwa nchi moja ya mto Nile na kuondoa haki ya matumizi ya maji kwa nchi nyingine, vikiwa vimeandikwa kimaficho. Hizi nchi nyingine zikamsifia sana kwa umakini wake hadi kugundua hilo.

Kuna mambo mengi sana amefanya ambayo watu walimsifia kwa busara na hekima zake, ndani na nje ya Tanzania, siwezi kuyaweka yote hapa.

Mtu huyu anaitwa Prof. Mark Mwandosya. Muite, kaa nae, mwache akushauri kwenye hili jambo, na tekeleza atakachokuambia. Umekuwa ukiwasikiliza watu ambao wanakuambia nguo yako isiyoonekana inakupendeza sana - wanakudanganya na wanakupotosha wakidhani wanakuambia kile unachotaka kusikia ili uendelee kuwa nao. Mwite Prof. Mwandosya mkae nyie wawili tu kutafuta way forward juu ya jambo hili - na nakuambia utanitafuta kunishukuru kwa huu ushauri wa bure ninaokupa hapa. Kila la kheri.
Karibu sana Professor. Ulikuwa umepotea sana!
 
Tatizo watu mnarukia propaganda chafu za watu waliokuwa wakimchafua Prof. Mwandosya na mnajitoa akili kabisa. Kumbuka ni watu walipoona propaganda zao hazifanikiwi waliamua kumnywesha sumu ikabidi akae hospitali India miezi karibu sita.

Kama unafikiri Prof. Mwandosya ni mtu ambae angeweza kuhongwa "scholarship" ya mtoto wake ili auze shirika la umma basi huna akili za kukufanya uweze kufikiri. Na kumbuka sponsorship waliyoisema ni pale mtoto wake alienda South Africa study tour, wiki mbili sijui. Kwamba Mwondosya angeshindwa kumgharamia ticket ya economy na kukaa South kwa wiki mbili, ikiwa watoto wake wengine alikuwa akiwasomesha nje ya nchi kwa hela yake? Does it make sense to you?

Japo sina hela kama ya Prof. Mwandosya na mie sio waziri, ili kukuondoa ujinga ningeweza kukukatia ticket ya ndege kwenda South Africa ukakae wiki mbili unakula na kulala tu, ili siku nyingine usiamini kila unachoambiwa, na kukuonyesha kwamba kwenda South Afrika na kukaa wiki mbili ni kitu kidogo sana hata mfanyakazi wa kawaida anaweza kukimudu. Epuka dhana ya kuona ili upande ndege kwenda mahali kama South Africa lazima uwe tajiri kama Dewji na waziri hawezi ku-afford kumlipia mtoto wake safari ya South Africa inabidi ahongwe kuuza shirika ili mtoto wake aende South Africa study tour.
hata wewe umeleta propaganda kama angekuwa na uwezo wa kusuluhisha mgogoro ni wazi angepewa uwaziri wa mambo ya nje, kuhusu boti yeye alikuwa analazimisha kama waziri wa uchukuzi anayedili na maswala ya usafiri wa bahari na maziwa wakati Magufuli alikuwa anakataa kupitishwa barabarani Kwa sababu kama waziri wa ujenzi barabara zipo chino yake.Mwisho aliyeshindwa no Magufuli.
Habari za mtoto wake kufadhiliwa zilielezwa kiundani na gazeti la Rai wakati huo kabla halijauzwa, kama alichafuliwa kwanini hakwenda mahakamani?
 
Mimi pia nipo na ni Mtanzania mwaminifu. Aniite nimshauri. Nipo tayari wakati wowote kuanzia sasa.
 
Toka nianze kupiga kura miaka ya 90s' sikuwahi kuona Wala kishuhudia Rais wa Nchi anawatumia wajinga Kama kitenge,mwijaku na Zembwela kwenye issues nyeti Kama suala la Bandari[emoji24][emoji24].
yaani mwijaku au Zembwela anabishana na mwanadiplomasia nguli Kama Dr Slaa?, Mwanasheria nguli na jaji na waziri mkuu mstaafu Warioba?, Mzee Shivuji?, Dr Nshalla, Mzee Butiku... Afu bado Kuna wapumbavu wanaamini tuna Rais anayeweza kutupeleka mahali?. Watanzania tumezidi kuwa wajinga asee!.
Etii
 
Raisi Samia, kwa sababu ya mambo fulani yaliyojitokeza hupa JF Forums, niliahidi kutotoa post tena. Lakini kwa ajili yako nimeamua kuvunja mwiko huo.

Nimefuatilia kwa makini sana yanayoendelea juu ya suala la DP World, jinsi lilivyoshughulikiwa Bungeni, na sasa kufikia hatua ya tamko la TEC. NI kweli kwamba suala hili linazidi kuweka taswira mbaya sana nchini, na huenda linakukosesha usingizi kwa kuwa hukutarajia litafika huku. Nahisi pia kuna mambo ambayo hatujui, labda upande wa UAE-Dubai, yanayolifanya liwe gumu hata zaidi. Na usipoangalia mambo yatazidi kuharibika.

Sasa maraisi wa kabla yako wamewahi kupitia vipindi vigumu kama vyako. Raisi Mkapa kuna wakati kulikuwa na suala na rada ya BAE. Serikali ya Uingereza ikamsumbua sana. Akaomba huyu mtu nitakaekutajia mwishoni amsaidie kulitatua. Na matokeo ni kwamba huyu mtu alilitatua kwa namna ambayo ilimfanya Raisi Mkapa amheshimu sana, kwa kuwa alilitatua kwa namna ya hekima, na ufahamu wa hali ya juu, hata Uingereza wakamsifia kwa hekima zake kwa jinsi alivyolitatua.

Kisha wakati fulani uhusiano kati ya Raisi Kikwete na Raisi Kagame uliharibika sana, hata Raisi Kagame akatishia kumpiga Raisi Kikwete. Kuona hivyo, Raisi Kikwete ikabidi amuombe huyu mtu asaidie kulimaliza hili suala, na kwa mara nyingine akalimaliza kwa namna ya busara sana iliyorejesha uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda kwenye hali ya kawaida. Kutoka hapo Raisi Kikwete aliamua huyu mtu akae karibu yake katika ofisi ya Raisi ili azidi kumsaidia mambo mengine mengi.

Na labda nikuambie pia wakati fulani kulikuwa na suala la kupeleka boti za abiria kwenye ziwa Victoria, na mtangulizi wako Raisi Magufuli akagoma katakata kuzipeleka boti hizi kupitia barabara zetu. Hii ilileta mtafaruku sana kati ya mfanyabiashara maarufu nchini na serikali. Huyo huyo mtu ninaekuambia akaamua kuingilia kati na kuwasiliana na serikali ya Kenya. Kwa diplomasia yake serikali ya Kenya ilikubali kutatua tatizo hili. Jinsi alivyotatua tatizo hili ilimletea heshima sana kwa baraza la mawaziri Kenya na Tanzania, japo ilimfadhaisha sana Magufuli, wakati huo akiwa waziri katika serikali ya Kikwete, na kufanya awe na chuki nae, chuki aliyoiendeleza hata alipochaguliwa kuwa raisi.

Na labda utakuwa unajua kwamba huyu mtu aliingizwa katika serikali kutokana na ushauri wa Raisi Clinton kwa Mkapa. Raisi Clinton alishangaa sana kwamba kwa nini serikali ilikuwa haimtumii mtu huyu ambae Raisi Bill Clinton na Makamu wake Al Gore walimsifia sana kwa jinsi alivyoshughulikia kwa umakini mkubwa na busara za hali ya juu negotiations za climate change akiwa msemaji wa Group of 77 and China. Mkapa akawasikiliza.

Japo si mwanasheria, kuna wakati, Tanzania na nchi nyingine za mto Nile wakiwa katika mkutano wa kusign makubaliano ya Mto Nile, alizuia utiaji sahihi wa makubaliano hayo baada ya kugundua vipengele katika mkataba huo ambavyo mawaziri wa nchi nyingine hawakuviona. Vilikuwa vipengele ambavyo vilitoa faida kubwa kwa nchi moja ya mto Nile na kuondoa haki ya matumizi ya maji kwa nchi nyingine, vikiwa vimeandikwa kimaficho. Hizi nchi nyingine zikamsifia sana kwa umakini wake hadi kugundua hilo.

Kuna mambo mengi sana amefanya ambayo watu walimsifia kwa busara na hekima zake, ndani na nje ya Tanzania, siwezi kuyaweka yote hapa.

Mtu huyu anaitwa Prof. Mark Mwandosya. Muite, kaa nae, mwache akushauri kwenye hili jambo, na tekeleza atakachokuambia. Umekuwa ukiwasikiliza watu ambao wanakuambia nguo yako isiyoonekana inakupendeza sana - wanakudanganya na wanakupotosha wakidhani wanakuambia kile unachotaka kusikia ili uendelee kuwa nao. Mwite Prof. Mwandosya mkae nyie wawili tu kutafuta way forward juu ya jambo hili - na nakuambia utanitafuta kunishukuru kwa huu ushauri wa bure ninaokupa hapa. Kila la kheri.
Mwizi anamshauri mwizi mwenzake
 
Pamoja na huyu unayemsema hapa kuna chuma hiki kina roho wa Mungu na hakina udhehebu wala udini bali hunena maagizo ya yeye aliye juu akiite kitamuambia yampasayo kufanya nacho si kingine bali ni Mwl. Christopher Mwakasege. Azingatie sana hili maana aendapo kuna giza totoro kwake na ni hakika asipokuwa makini akiendelea kuendekeza machawa basi ataandika historia mbaya sana. Itakuwa heri endapo akilisikia neno hili la Mungu.
Yaani huyu akija na bible verses, hata mama hatakiwi kutuongoza!
 
Raisi Samia, kwa sababu ya mambo fulani yaliyojitokeza hupa JF Forums, niliahidi kutotoa post tena. Lakini kwa ajili yako nimeamua kuvunja mwiko huo.

Nimefuatilia kwa makini sana yanayoendelea juu ya suala la DP World, jinsi lilivyoshughulikiwa Bungeni, na sasa kufikia hatua ya tamko la TEC. NI kweli kwamba suala hili linazidi kuweka taswira mbaya sana nchini, na huenda linakukosesha usingizi kwa kuwa hukutarajia litafika huku. Nahisi pia kuna mambo ambayo hatujui, labda upande wa UAE-Dubai, yanayolifanya liwe gumu hata zaidi. Na usipoangalia mambo yatazidi kuharibika.

Sasa maraisi wa kabla yako wamewahi kupitia vipindi vigumu kama vyako. Raisi Mkapa kuna wakati kulikuwa na suala na rada ya BAE. Serikali ya Uingereza ikamsumbua sana. Akaomba huyu mtu nitakaekutajia mwishoni amsaidie kulitatua. Na matokeo ni kwamba huyu mtu alilitatua kwa namna ambayo ilimfanya Raisi Mkapa amheshimu sana, kwa kuwa alilitatua kwa namna ya hekima, na ufahamu wa hali ya juu, hata Uingereza wakamsifia kwa hekima zake kwa jinsi alivyolitatua.

Kisha wakati fulani uhusiano kati ya Raisi Kikwete na Raisi Kagame uliharibika sana, hata Raisi Kagame akatishia kumpiga Raisi Kikwete. Kuona hivyo, Raisi Kikwete ikabidi amuombe huyu mtu asaidie kulimaliza hili suala, na kwa mara nyingine akalimaliza kwa namna ya busara sana iliyorejesha uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda kwenye hali ya kawaida. Kutoka hapo Raisi Kikwete aliamua huyu mtu akae karibu yake katika ofisi ya Raisi ili azidi kumsaidia mambo mengine mengi.

Na labda nikuambie pia wakati fulani kulikuwa na suala la kupeleka boti za abiria kwenye ziwa Victoria, na mtangulizi wako Raisi Magufuli akagoma katakata kuzipeleka boti hizi kupitia barabara zetu. Hii ilileta mtafaruku sana kati ya mfanyabiashara maarufu nchini na serikali. Huyo huyo mtu ninaekuambia akaamua kuingilia kati na kuwasiliana na serikali ya Kenya. Kwa diplomasia yake serikali ya Kenya ilikubali kutatua tatizo hili. Jinsi alivyotatua tatizo hili ilimletea heshima sana kwa baraza la mawaziri Kenya na Tanzania, japo ilimfadhaisha sana Magufuli, wakati huo akiwa waziri katika serikali ya Kikwete, na kufanya awe na chuki nae, chuki aliyoiendeleza hata alipochaguliwa kuwa raisi.

Na labda utakuwa unajua kwamba huyu mtu aliingizwa katika serikali kutokana na ushauri wa Raisi Clinton kwa Mkapa. Raisi Clinton alishangaa sana kwamba kwa nini serikali ilikuwa haimtumii mtu huyu ambae Raisi Bill Clinton na Makamu wake Al Gore walimsifia sana kwa jinsi alivyoshughulikia kwa umakini mkubwa na busara za hali ya juu negotiations za climate change akiwa msemaji wa Group of 77 and China. Mkapa akawasikiliza.

Japo si mwanasheria, kuna wakati, Tanzania na nchi nyingine za mto Nile wakiwa katika mkutano wa kusign makubaliano ya Mto Nile, alizuia utiaji sahihi wa makubaliano hayo baada ya kugundua vipengele katika mkataba huo ambavyo mawaziri wa nchi nyingine hawakuviona. Vilikuwa vipengele ambavyo vilitoa faida kubwa kwa nchi moja ya mto Nile na kuondoa haki ya matumizi ya maji kwa nchi nyingine, vikiwa vimeandikwa kimaficho. Hizi nchi nyingine zikamsifia sana kwa umakini wake hadi kugundua hilo.

Kuna mambo mengi sana amefanya ambayo watu walimsifia kwa busara na hekima zake, ndani na nje ya Tanzania, siwezi kuyaweka yote hapa.

Mtu huyu anaitwa Prof. Mark Mwandosya. Muite, kaa nae, mwache akushauri kwenye hili jambo, na tekeleza atakachokuambia. Umekuwa ukiwasikiliza watu ambao wanakuambia nguo yako isiyoonekana inakupendeza sana - wanakudanganya na wanakupotosha wakidhani wanakuambia kile unachotaka kusikia ili uendelee kuwa nao. Mwite Prof. Mwandosya mkae nyie wawili tu kutafuta way forward juu ya jambo hili - na nakuambia utanitafuta kunishukuru kwa huu ushauri wa bure ninaokupa hapa. Kila la kheri.
samia ameshakula hela za ufisadi wa huo mkataba, shida ndipo ilipo
 
Sasa wewe umemjuaje huyu mtu?

Jamaa umetumia kigezo gani cha kisayansi kujua, he is the one and only One can do that??

Tunahitaji muafaka ila walau njia tunazopendekeza walau ziwe scientifically hata kwa 75% tu inatosha

Sijabisha ila nataka kujua hiyo randomized sampling technique yako umefanyaje??
Jamani akuambie nn tena wakati kesha weka facts zote with examples?
 
Back
Top Bottom