Rais Samia kuwa makini, Sukuma Gang na CHADEMA wanaweza kuungana

Rais Samia kuwa makini, Sukuma Gang na CHADEMA wanaweza kuungana

Johnny Sack

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2017
Posts
8,984
Reaction score
19,288
Urusi na Marekani japo walikuwa mahasimu waliungana na kumuangusha Hitler kwenye vita ya dunia. Ni jambo ambalo Hitler mwenyewe hakua analifikiria.

Hii inatupa somo kuwa, watu ambao ni mahasimu wakubwa ambao hata hukufikiria wataungana, wanaweza kuungana ikiwa malengo yao yanafanana.

SG na Chadema malengo yao wote ni kumuondoa Samia madarakani 2025. Watu hawa pia siasa zao zinafanana, utawasikia wote wakilaumu serikali kwa bei za vyakula kupanda na kutaka ifunge mipaka.

Utawasikia wote wakipinga tozo, kodi na mikopo. Utawasikia wote wakipinga machinga kuondolewa barabarani. Sukuma Gang hivi sasa nao wameanza kudai Katiba mpya baada ya kundi lao kuondolewa madarakani

Samia anatakiwa kucheza karata zake kijasusi, anatakiwa kuhakikisha watu hawa wanaendelea kuchukiana na kupingana. Ama wakiungana wanaweza kuitoa ama kuijeruhi vibaya CCM.
 
Unafikiri kumdhibiti chairman mapema sababu ya nini? Kuna vuguvugu lingewasha moto ndio maana ni bora katiba iwe topic tusigane huko then handling yake huko mbele ni simple kuliko wimbi la kupasua kampuni.

Tawala wanaendesha mambo kwa akili mingi mno! Kuruhusu siasa ni ili kupunguza vita from within maana huko nje wanajua kucheza nao [emoji1787]

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Unafikiri kumdhibiti chairman mapema sababu ya nini? Kuna vuguvugu lingewasha moto ndio maana ni bora katiba iwe topic tusigane huko then handling yake huko mbele ni simple kuliko wimbi la kupasua kampuni...
Hisia zako tu hizi🤣🤣
 
Back
Top Bottom