Rais Samia kwa hili la kuruhusu Mashirika ya Umma kuajiri nakupa pongezi sana

Rais Samia kwa hili la kuruhusu Mashirika ya Umma kuajiri nakupa pongezi sana

Dola ya Tanzania isiruhusu hili jambo. Huyu mama aache haraka haraka. Haraka haraka haina baraka. Atapotea. Apewe ile ripoti ilipropose kuanzishwa kwa utaratibu wa ajira unaotumika sasa.
“Kuna mashirika ambayo wenyewe wangehitaji ajira za harakaharaka lakini unaambiwa subiri Tume ya Utumishi ikae, subiri sijui utumishi ifanyeje mwaka mzima taasisi kwa mfano TRA inataka watu wakakusanye mapato mwaka mzima watu hawajapatikana, vivyo hivyo TANESCO, REA wanataka watu utumishi paka izunguke iseme ifanye mikutano ifanye semina, hapana hatuendi hivyo.

Kama wanataka wafanyakazi mishahara ya kulipa wanayo haitoki hazina wanataka wafanyakazi kwa ajili ya mradi au kazi fulani wapewe ruhusa wafanye. Wapewe ruhusa wafanye sabahu ajira hizi wala nyingine sio za kudumu mradi ukimalizika na ajira imekwenda. Kwa hiyo wapewe ruhusa waajiri ili miradi ikatekelezwe kwa haraka.”

Rais Samia Suluhu Hassan

Napenda kujikita hapa kwa TRA: Nafasi za kazi za TRA zilitangazwa mwezi wa nne 2022, watu wamekuja kuitwa kwenye usaili mwezi wa 12 2022. Wakati huohuo watu wameitwa kazini mwezi wa pili 2023. Muda mwingi umepotea hapo.

View attachment 2517434
sawa tumesikia
 
Moja ya vikwazo vikubwa vya maendeleo nchini ni wizara ya utumishi! Imejaa watu wenye urasimu uliokithiri kiasi hata mtu mwingine ukihamishiwa hapo unaambukizwa!

Ni vema wizara hii ifumuliwe kabisa kuanzia katibu mkuu hadi muhudumu vinginevyo hali hii itaendelea na wanaoathiriwa ni wananchi!
imekua na urasimu wa kishenzi.imeanza kuingilia hata taratibu za watumishi kwenye mashirika na kuwaita watumishi wa umma hadi maslahi yao.
tena ndumbaro wamle tu kichwa
 
Dola ya Tanzania isiruhusu hili jambo. Huyu mama aache haraka haraka. Haraka haraka haina baraka. Atapotea. Apewe ile ripoti ilipropose kuanzishwa kwa utaratibu wa ajira unaotumika sasa.
Syo kitu kigeni.
wakati wa mkapa alibadilisha sheriia kuruhusu mashirika kuajiri na kujilipa kwa jinsi wanavyozalisha.
sheitwan alipoingia kaanza ujinga bila hata,sheria kubadilishwa.
anachotaka mama ni ile sheria kufatwa
 
Kuna watu wanapayuka ila hawajui wanacho kiongea,ila Utumishi wanafanya kazi kubwa sana, nina wanangu wametoka life la chini kabisa tena wengine walikata tamaa leo wapo kwenye taasisi kubwa sababu ya Utumishi.Hii siku ya leo nina mwanangu mwengine katoboa TRA sababu ya Utumishi nae katokea life bovu kinyama.

Hii kuhusu Tasisi au shirika liajiri wenyewe wataja wakina KAMLETE.

Daaah bi mkubwa hapa kachemka.
 
Kuna watu wanapayuka ila hawajui wanacho kiongea,ila Utumishi wanafanya kazi kubwa sana, nina wanangu wametoka life la chini kabisa tena wengine walikata tamaa leo wapo kwenye taasisi kubwa sababu ya Utumishi.Hii siku ya leo nina mwanangu mwengine katoboa TRA sababu ya Utumishi nae katokea life bovu kinyama.

Hii kuhusu Tasisi au shirika liajiri wenyewe wataja wakina KAMLETE.

Daaah bi mkubwa hapa kachemka.
Kumbe.
 
Moja ya vikwazo vikubwa vya maendeleo nchini ni wizara ya utumishi! Imejaa watu wenye urasimu uliokithiri kiasi hata mtu mwingine ukihamishiwa hapo unaambukizwa!

Ni vema wizara hii ifumuliwe kabisa kuanzia katibu mkuu hadi muhudumu vinginevyo hali hii itaendelea na wanaoathiriwa ni wananchi!
Barua yangu imepotea hapo Utumishi zaidi ya mara nne...inaonekana imepokelewa ila hauonekani iko wapi?
 
Watoto wa walalahoi ndio msahau kupata kazi katika hizo taasisi. Utumishi sifahamu makando kando yao mengine ila kwenye suala la ajira wako fair sana. Ni kupitia mfumo wao wa ajira nimeona vijana waliotokea familia za kawaida (akina sie watoto wa mama ntilie) wakipata kazi mashirika/vitengo nyeti Serikalini.

Rais Mama Samia Usijaribu kuua mende kwa nyundo, fikiria tena kuhusu kauli/maamuzi yako, elewa tatizo lilipo kisha tatua ila sio kwa kuondoa mfumo rasmi uliopo. Kati ya Mashirika yaliyoongoza kwa vi Memo kabla ya mfumo wa ajira kuwepo ilikua ni TTCL na hapo TRA, ofisi nzima ilikua inaongozwa na familia.
 
Ila mmemlisha maneno amesema kwa zile za muda mfupi ambazo pesa hazitoki hazina wanazitoa mashirika yenyewe utumishi iwape go ahead mashirika yaendelee lakini zile permanent hajazizungumzia.

Ila utumishi nao waangalie kama ni kanuni ndizo zinachelewesha basi wazirekebishe.
 
Secretariat ya ajira nao wanachukua muda mrefu sana mpaka mtu apate ajira.

Huko kwenye taasisi nako ni majipu tu.

Kujuana kwingi.

Kifupi hakuna mahali kuna unafuu.

usemalo ni Kweli!
Taasisi wanapenda Hire&Fire wawe na Huo Uwezo!
Yaani Wakikuajiri Ukizingua Tuu au Ikitokea hitilafu Flani Kesho asubuhi hauna Chako[emoji12]
 
Maagizo yametoka kishkaji sana, hizo taasisi mfano TANESCO ilivyo na Miungu watu. Wao wanawazia kupunguza watu kisha kazi wabinafsishe Mh Raisi anataka waajiriwe watu kwa projects husika ajira za mikataba au za kudumu ikibidi, Watampuuzia bila shaka kwakuwa hapawezi pale , yetu macho.
 
Back
Top Bottom