Rais Samia, kwa unyenyekevu mkubwa epuka huo mtego

Rais Samia, kwa unyenyekevu mkubwa epuka huo mtego

Mheshimiwa Rais, suala la Mkataba wa Bandari limefichua nyufa kubwa za Taifa letu hasa katika suala la Dini, Muungano, Ukabila, Ukanda, Jinsia na Itikadi za Siasa. Sasa naomba nikushauri kwa unyenyekevu mkubwa epuka mtego wa wasaidizi wako hasa huu wa kukamata watu na kuwaambia ni wahaini.

Huu ni mtego Mkubwa kwako ili 2025 ubaki mkiwa na watakutoa sadaka. Usicheze na Hawa Jamaa wana mbinu balaa. Hivi unadhani unaweza mfunga Dr. Slaa halafu watu wa dini za mlengo wake wakakaa kimya, watakuandama balaa na watataka kuthibitisha madai ambayo mimi sitaki kuamini ya udini na mambo kama hayo. Vilevile waliokamatwa kwa uhaini wote ni watanzania bara, hili nalo litaongeza ufa uliopo katika Muungano.

Ushauri Wangu, kuwa makini kubali sauti za kila upande, amua kwa busara, jikabidhi kwa Mungui akupe busara, hekima na uthabiti.
Umeongea vitu sensible sana
 
Unaongelea dini gani? Wakristu, Wakatoliki!! Wakristu tuko very objective, hatuwezi kuunga mkono mtu ambaye anataka kutuharibia amani ya taifa letu.

Tofauti na Waislamu wanaangalia kila maamuzi na kuhusisha na kwenye dini ya mtu. Wakristu tunapima ubora (merit) ya maamuzi na kuyaunga au kuyapinga.

Dr Slaa hana jipya zaidi ya FRUSTRATION. na siyo mtu wa kuaminika.

Toka kuwa Padri wa RC hadi kuwa Mume wa Rose Kamili na Mushumbushi ni kukosa focus. Kisha Mgombea wa CCM Karatu mwaka 1995 na kuhmia CHADEMA. Mbunge na kuwa Katibu mkuu wa CDM na mgombea uRais mwaka 2010. Halafu akasaliti chama kwa kununuliwa na Magufuli kama andazi au bakuli. Kafanya ubalozi lakini kioindi kiliookwisha mke kakataa kurudi Tanzania

Baada ya Ubalozi ku expire maana aliyempa hayupo alikufa, ndipo anakuja na munkari wa kutaka kupindua Serikali.

Dr Slaa ni mnafiki, msaliti, mtu asuyekuwa na msimamo na yuko tayari kuuzwa kama bidhaa
Siwezi msamehe silaha Kwa kile alichokufanyia 2020
 
Sasa hata hao DPW watafanyaje kazi na wananchi ambao hawawakubali? Kama mwekezaji, hawezi kuogopa juu ya vitendea kazi vyake kuharibiwa in case wananchi wakapata hasira ya kumtimua kinguvu? Ipo siku wananchi wataamua kuwa na maamuzi wao wenyewe.

Na kwa nini iwe lazima aje hivyo hivyo kwa mkataba huu huu? Hata kwa kutumia nguvu lazima aje!! Duh, huyu Mama amejishushia credibility yake sana.
 
Hapa wewe ndiyo mjinga ndg, maana hakuna mahali mtoa mada amepinga uwekezaji wa bandari, na hakuna mtanzania yeyote yule mwenye akili timamu anaepinga uwekezaji wa bandari, isipokuwa ni watu wanapinga aina ya mkataba baina ya DP world na Tanzania Government, ndiyo maana wadau mbali mbali wanasema huo mkataba ufanyiwe marekebisho maana una mapungufu mengi na hauna maslai kwa Tanzania, ni hayo tuu, sasa jipime kati yako wewe na mtoa mada ni nani mjinga, kumzidi mwenzie
Hakuna tatizo lolote kwenye mkataba usisikilize hizi kelele za wanaharakati. Mkataba unaolalamikiwa una kipengele cha serikali kutaifisha biashara tafuta mikataba waliyoingia na mataifa mengine kama utakuta kipengele kama hicho.

Wabongo wajinga tu.
 
Shida sio Uwekezaji! Shida tutapata NINI? Acha kuzunguka zunguka sijui Kagame alisema!
TRA wanapata trilioni 7 kwa mwaka muda huu watakapoanza kazi DP World hapo bandarini zinakwenda kupatikana trilioni 21 kwa mwaka, zaidi ya mara tatu.

Foleni ya bandarini ya meli inakwenda kuondoka. Sasa fanya utafiti kwa muda wako binafsi, ili ujue hasara wanazopata wamiliki wa meli na bandari kwa ujumla, kwa kila zinapochelewa kushushwa.
 
TRA wanapata trilioni 7 kwa mwaka muda huu watakapoanza kazi DP World hapo bandarini zinakwenda kupatikana trilioni 21 kwa mwaka, zaidi ya mara tatu.
Acha uongo hizo tril 21 zitapatikana after 10 yrs projections. Whi most probable they wont make it kwa uswahili huu tunaouona.
 
Acha inyeshe tujue panapovuja..........
 
Samia yupo kati kati naamini hata yeye haelewi wapi pakwenda, akitulia moto wa mkataba wa hovyo unaendelea kumuwakia, akisema awafunge midomo wanaouwasha moto, hapo napo anaenda kuuwasha moto mwingine kwa namna tofauti..

Huyu mama hii nchi imemshinda, hawezi kufanya lolote kwa sasa, ameamua kuacha mambo yajiendee, bahati mbaya hata hayo mambo yanavyojiendea, bado yanaendelea kumuharibikia, mwanamke ana bahati mbaya sana.
Bandari inakutesa.
Utakuwa umepungua ht uzito kwa jambo lisokuhusu si kwa sikio wala ndewe
 
TRA wanapata trilioni 7 kwa mwaka muda huu watakapoanza kazi DP World hapo bandarini zinakwenda kupatikana trilioni 21 kwa mwaka, zaidi ya mara tatu.

Foleni ya bandarini ya meli inakwenda kuondoka. Sasa fanya utafiti kwa muda wako binafsi, ili ujue hasara wanazopata wamiliki wa meli na bandari kwa ujumla, kwa kila zinapochelewa kushushwa.
Unaamini hii porojo? Zinapatikana kutoka wapi? TRA ataendelea kukusanya kodi kama kawaidi huduma za bandari tu ndio zitaendeshwa na DP World na mapato ya bandari tutagawana nao. Uliza Dijbout baada ya kuona mgao umekuwa mdogo kuliko walivyokuwa wanaedesha wao wakatibuana.
 
Acha uongo hizo tril 21 zitapatikana after 10 yrs projections. Whi most probable they wont make it kwa uswahili huu tunaouona.
Wengi wanaohoji kuhusu mkataba wana akili kama za kwako, hamjui mnaongea kitu gani.

Unapoondoa foleni ya meli kule nje maana yake moja kwa moja umeongeza ufanisi ambao unamaanisha kama kwa siku inahudumiwa meli moja na TPA basi zitahudumiwa meli mbili.

Hapo umeongeza pato kwa mamlaka zote zinazoshughulika na bandari kwa kutumia muda mchache.
 
Unaamini hii porojo? Zinapatikana kutoka wapi? TRA ataendelea kukusanya kodi kama kawaidi huduma za bandari tu ndio zitaendeshwa na DP World na mapato ya bandari tutagawana nao. Uliza Dijbout baada ya kuona mgao umekuwa mdogo kuliko walivyokuwa wanaedesha wao wakatibuana.
Djibouti sio Tanzania, ni vitu viwili tofauti.

Mapato yatapatikana baada ya kufungwa mitambo ya kisasa na muda wa kushusha na kupakia mizigo unakwenda kupunguzwa. Kumbuka kuwa urasimu pale TPA ndio unaochelewesha meli na kulazimisha uwepo wa ICDs nyingi, tumetengeneza mazingira ya foleni zisizo na ulazima ili taasisi za wapigaji ziweze kupata faida.
 
Back
Top Bottom