Rais Samia: Mbowe alijificha Nairobi aliporudi akaanza harakati za madai ya Katiba, nadhani ni Calculation akijua kwamba ana kesi

Rais Samia: Mbowe alijificha Nairobi aliporudi akaanza harakati za madai ya Katiba, nadhani ni Calculation akijua kwamba ana kesi

Nimemsikiliza huyu mama na kweli amesema hivi. Na mimi pia nimemshangaa sana...

Kwanza alitaka kukwepa kulijibu swali hilo kwa kuwa liko mahakamani...

Lakini ghafla akajikuta anaanza kutoa maelezo ya kile kilichokuwa ndani ya moyo wake na kujikuta anatoa pre judgement ya mahakama...

Kama IGP Simon Sirro, huyu mama naye akajikuta anasema:

"....Mbowe alikuwa anajua ana kesi. Lakini alikuwa amejificha Nairobi Kenya. Aliporudi na kutoka huko alikokuwa amejificha Nairobi Kenya na akafikia ku - instigate fujo za maandamano ya kisiasa hapa nchini ili akikamatwa waseme amematwa ili kuzuiwa kufanya kazi zao kisiasa. Kwa hiyo hayo madai yao siyo kweli...."

Sasa ni wazi kabisa, ugaidi wa Mbowe ni ishu ya kubumba 100%. Lakini kosa la huyu kamanda ni kuongoza madai ya katiba mpya ya wananchi ambayo kwa tafsiri ya watawala ni "...kui - instigate fujo za kisiasa..."

The true colour of this woman has been revealed....
 
Kauli ga ni hii! Kujificha Nairobi ndiyo kunamfanya gaidi? Au kudai katiba mpya ni ugaidi?
Msipotoshe, kasema alikuwa na kesi lakini upelelezi haukuwa umekamilika, ila kwakua yeye alijua kuwa ana kesi Mh. Ana hisi, hana uhakika ametumia Katiba kutafuta sympathy....Si vizuri kupotosha maneno ya mtu...
 
Na Kuna ajabu gani mfanya biashara Kama Mbowe kuwa Nairobi ,yaani haata mamangu mwenye Elimu ya Watu Wazima hawezzi kutoaa hoja za kiwangi Cha chininkama hiki!
Ameshikiwa akili na akina Sirro!
 
Mahojiano na salim kikeke.
Inaonekana rais yupo nyuma ya hii yote. Na yoote yanayofanyika anaangalia tuu....
Anyway Leo ndo nimemjua rais tulienae

..lakini Rais hawezi kuwapinga Polisi wake kupitia vyombo vya habari.

..tatizo utetezi wa hoja yake ndio umekuwa na walakini na mapungufu makubwa.

..nawalaumu Polisi kwa kumuweka Rais ktk wakati mgumu mpaka akalazimika kutoa kauli za kibabaishaji kuwatetea.

..haiwezekani Mbowe ajifiche Nairobi, halafu arudi Tanzania na kuonekana Dsm, Moshi, na Mwanza.
 
Tulikuwa tunaambiwa mama anaupiga mwingi.......vp ball possession huko uliko?

Daaah sielewi mwelekeo wa mama Tanzania
 
Sijui kwa nini rais anaongea uongo kwenye swala kubwa kama hili
 
Nimemsikiliza huyu mama na kweli amesema hivi. Na mimi pia nimemshangaa sana...

Kwanza alitaka kukwepa kulijibu swali hilo kwa kuwa liko mahakamani...

Lakini ghafla akajikuta anamwaga yaliyokuwa ndani ya moyo wake na kujikuta anatoa pre judgement ya mahakama...

Amesema ametoka huko alikikuwa amejificha Nairobi Kenya na kuanza instigate fujo za kisiasa hapa nchini...

Sasa ni wazi kabisa, ugaidi ni ishu ya kubumba. Lakini kosa la huyu kamanda ni kuongoza madai ya katiba mpya ya wananchi ambayo kwa tafsiri ya watawala ni "...kui - instigate fujo za kisiasa..."

The true colour of this woman has been revealed....
Hapa kwa kweli amebugi. Maana ameonesha moja kwa moja anajua a-z na anatoa maelekezo
 
Mahojiano na salim kikeke.
Inaonekana rais yupo nyuma ya hii yote. Na yoote yanayofanyika anaangalia tuu....
Anyway Leo ndo nimemjua rais tulienae
mama amefeli kabla hajaanza na atashindwa vibaya sana !
 
Hayo ndio ya ndani
 
Msipotoshe, kasema alikuwa na kesi lakini upelelezi haukuwa umekamilika, ila kwakua yeye alijua kuwa ana kesi Mh. Ana hisi, hana uhakika ametumia Katiba kutafuta sympathy....Si vizuri kupotosha maneno ya mtu...

..hata angesema hivyo bado haileti mantiki.

..Ni afadhali Rais angekaa kimya na kutozungumzia suala lililoko mahakamani.
 
Msipotoshe, kasema alikuwa na kesi lakini upelelezi haukuwa umekamilika,
Kwa sasa umekamilika?
Mbona kesi ina kona kona?
ila kwakua yeye alijua kuwa ana kesi Mh. Ana hisi, hana uhakika ametumia Katiba kutafuta sympathy..
Alijua kesi imekamilika ndio maana akaja?
Kama alienda kujificha alipita boda gani?
..Si vizuri kupotosha maneno ya mtu...
 
Huyu mama sasa ndio nimepata picha kamili!

Nilikuwa nawaza anahujumiwa kumbe anahujumu.

Okay!...
 
Anadangaywa labda

..Rais hawezi kupinga maamuzi ya Polisi kupitia mahojiano na vyombo vya habari.

..alichojaribu kufanya ni kuwatetea Polisi, ila kwa bahati mbaya utetezi alioutoa hauna mantiki.
 
Mama anafungua nchi na anaupiga mwingi sana🤣🤣🤣
Sasa kinakuchekesha nini?!!

Anyway, labda niseme hivi....

Magu wakati anaingia madarakani, nilikuwa nam-support kwa kiasi kikubwa hadi pale alipoanza kuonesha elements za kidikteta na kuelekea kuidumaza sekta binafsi!!

Mama alipoingia madarakani, sikumpa support kubwa kama ile niliyokuwa nampa Magu, lakini vile vile sikuwa nampinga kwa sababu sikuwa na sababu ya kumpinga!!

That having been said, nothing personal!

Mtu anapotoa muelekeo mzuri, nitamuunga mkono kwa sababu sishabikii chama chochote, na akifanya ndivyo sivyo, lazima nitampa vitasa!!! Ni nyie wafuasi wa vyama vya siasa ndio tatizo kubwa nchi hii!!
 
Back
Top Bottom