Rais Samia, nani kakushauri kununua Treni zenye muundo mbovu namna hii?

Wanakupa kile kinachoendana na uwezo wako wa kiuchumi. Tube train haiwezi kutumia reli ya 1.435 M hii ni kwa ajili ya Boxcab (Diesel/Electric Locomotives) tu na ndio itakayonunuliwa na TRC. Tube trains kwa Afrika bado tutasubiri sana.
aaa si ndio picha wakina mwanantala walikuwa wanatuonyesha sasa ndio kusema walikuwa wanatudanganya,muonekano wa sura ya kitu unazuia kitu kisitumike mahali fulani?
 
Wewe kweli sokwe unaona aibu kuitwa maskini wakati ndio hali yako, nyinyi ndio wale mkifika ulaya mnajifutia makaratas wakati wa haja kubwa eti mufanane na wazungu mana ukinawa kwa maji utaonekana mbongo, Tanzania ni nchi maskini sana mpaka leo wananchi wanaishi kwa tabu kupata mlo 1 wa chakula lakini unataka upande treni za ulaya.

Vaa herini basi wenzako kule ulaya wamepiga hatua wanatoboa masikio wanavaa herini na bangili., pumbv
 
Inaelekea hujui hata unacho changia kwa kukosa wisdom. Hivi wewe kabla hujawatukana wenzio, pumbavu, kwanini kwanza hujajiuliza hiyo treni tuliyo iagiza inatoka wapi? Mbona hujiulizi pia kwanini sasa tuna SGR ya matrilion ya fedha? Kulikuwa na unuhimu wowote wa kutumia matrilioni ya fedha yote hayo kugharimia hiyo infrastructure, wakati tunajua kuwa watu wanapata mlo mmoja kwa siku?

Ili utambue utajiri tulio nao naomba tafuta hiki kitabu hapa kwenye picha ili uone rasilimali za thamni ya utajiri wa kutupwa ambazo mungu wetu wa mbinguni kaijalia nchi yetu.

Usinilaumu mimi na wala usimlaumu Hayati Magufuli. Hayati ametuambia ukweli kuhusu utajiri tulio nao, ila kinacho shindikana na ndiyo shida kubwa iliyopo ni matumizi mazuri ya bongo za watawala wetu, jinsi ya kui-transform hii rasilimali yetu kuwa pesa ambazo zitatuwezesha sisi ku enjoy utajiri wa nchi yetu kwa manufaa yetu sote.

Kwa mfano, sasa hivi tuna Rais ambaye mawazo yake yote, ninavyo mwona mimi, yame-fix kwenye kusubiri wawekezaji kutoka nje waje wawekeze kwenye ardhi yetu na rasilimali zetu, badala ya kutumia akili yake na potential hii nchi inayo, kuwarudisha na kuwawezesha diaspora wetu waliopata skills na exposure kwenye mataifa tajiri kwa tecknolojia, wakaja kutumia maarifa yao kutransform rasilimali zetu zikatuletea neema tunayo stahili kuwa nayo.

Sitaki kujua una umri gani, lakini zingatia kitu kimoja ninacho kuambia, kama tutampata Rais au kiongozi mwenye kutambua utajiri wetu na kutumia maarifa na akili zake ambazo mungu amemjalia, ndugu yangu nakuhakikishia matatizo yote ambayo inasadikika tunayo, yatatoweka mara moja. Na wewe utalitafuta kaburi langu na lile la Hayati Magufuli ili utunong'oneze kwenye sikio kuwa tulikuwa tunakueleza mambo sahihi.

Naweza tu kumwombea Mama Samia Suluhu Hassani Rais wetu awe na hekima na busara hizo ili awavushe watanzania kwenda kweny neema.

 
Jf ni platiform kubwa kwenye mitandao ya kijamii ya Tanzania. Karibu viongozi wakuu wote wa serikali na taasisi zake wamo kwenye mtandao huu na huwa wanapitia mara kwa mara mijadala inayohusu sekta zao zinazotolewa au kulalamikiwa humu. Hususani tanesco huwa hawachelewi kuzitolea ufafanuzi. Kwa nini Bw. Kadogosa amekuwa kimya kutolea ufafanuzi wa suala hili kama ni la kweli au si la kweli? Waziri wa uchukuzi naye kimya kwa nini? Lazima kuna jambo walilolivurunda hapa. Kimya chao kitaeleweka hivyo ie ufisadi. Ni vyema wakajitokeza kututoa kwenye hisia hizi za ufisadi.

Inauma sana. Yaani treni zetu zinazonunuliwa zinapitwa hadi na zile za Kenya zinazotumia dizeli wakati sisi ni za umeme? SGR yetu ni ya kisasa kabisa inayoruhusu hadi treni za spidi ya 400 kph?

Tazama hapa treni za dizeli za Kenya halafu ulinganishe na hizo za Kadogosa:




Yaani hili halikubaliki. Tunahitaji bullet trains za kisasa. Nchi yetu ni tajiri sana barani Afrika. Tuanze sasa kujionesha hivyo kama tulivyofanya kwenye Dreamliners. We should think Big.Tuanze na bullet trains chache kama uwezo hautoshi kwa sasa, zenye uwezo wa kusafiri masaa matatu kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza, sangara wa Mwanza wafike Kariakoo wakiwa fresh kabisa pamoja na senene wa kutoka huko Katerero. Mama yetu wa Taifa aingilie suala hili.
 
Ndugu hii ya kwamba SGR yetu ina uwezo wa kuruhusu treni itembee kwa 400kph umeitoa wapi? Maana wajenzi wenyewe wanasema ni design speed ya 160kph na imekuwa ikijulikana hivyo siku zote na hata hayati magufuli amewahi kuongea sana kuhusu hilo.

Mimi sio mtaalamu wa reli ila naona kwa hizo speed za 400kph reli yao inakuwa na double track halafu vituo ni vichache sio kama hapo dar moro kila km kadhaa ka-kituo, Sasa kwa hali hii 400kph inaweza fikiwa au kuwa chaguo sahihi kweli.?

Ukweli ni kuwa reli yetu imeundwa kwa kuzingatia kasi ya 160 kph kwa treni za abiria na 120 kwa ya mizigo. Sio high speed 'bullet train' kivile ila ni semi-high speed.

Ila bwana kama ndio hizo ni mbaya kwa kweli, treni za kasi ya 160km/p zipo zina sura nzuri sana ya kuchongoka ingawa si sana kama zile za kasi ya 300+.
 
Asante mkuu kwa mchango wako. Ni kweli tunamwomba Mama Samia Suluhu Hassan kuingilia hili swala. Ni kweli pia haitakubalika sisi kuwa na treni ambayo imepitwa na wakati. Tunataka vitu vinavyo endana na SGR yetu nasi tujidai kama wengine wanavyo fanya na vyao. Hela tunazao. Nchi yetu imejaliwa kuwa na rasilimali kem kem.

Viongozi husika na hasa waziri wa Ujenzi na Madini washughulikie haraka iwezekanavyo transformation ya madini yetu kwenye kuondoa umasikini wa watanzania.

Na pia tunamwomba Mkurugenzi wa TRC ndugu Kadogosa atuonyeshe kitabu kijulikanacho kwa watalaam wa mambo ya Rail Vehicle kama "Technical Requirement Document" ambacho aidha TRC Tanzania itakuwa imewapa kampuni ya Hyundai au kimetumika katika makubaliano ya vitu vinavyo paswa kuwepo kwenye hizo trains, ikiwepo mwuudo na kadhalika kama PDF document.
 
Ndugu sijaona treni ya umeme Tanzania, wewe umeshaiona??
Aisee kwakweli kazi iendeleee!

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Kiwango cha reli ni hicho hicho kwa bullet trains aka express trains na standard electrical trains. Mambo mengine ni mpangilio tu wa kimenejiment. Aina zote mbili zinaweza kupita kwenye hiyo reli na hata zile za dizeli zinaweza kupita humo. Hata kama njia yetu siyo double lane ni mpangilio tu. Kwa mfano: bullet train inaondoka DSM saa 12 asubuhi na haitasimama stesheni yo yote isipokuwa Dodoma (makao makuu ya nchi) na Mwanza tu ambako itafika saa tatu na nusu asubuhi. kwa spidi ya 400 kph. Ile standard train (ya watu wengi) inaondoka Dar saa 12 na nusu asubuhi, itasimama kila stesheni na kufika Mwanza saa 8 mchana. Bullet train itatoka Mwanza saa 9 mchana (baada ya standard train kufika Mwanza na hivyo njia kuwa wazi) na itafika Dar es Salaam saa 12 na nusu jioni baada ya kusimama kidogo makao makuu Dodoma. Na bei kati ya hizi treni zitakuwa tofauti. Ile bullet train ya 400+ kph itakuwa nusu ya bei ya ya tiketi ya ndege wakati ile ya standard train itakuwa robo tatu ya tiketi ya bus. Hapo vipi mkuu? Hizo za mizigo zitatakiwa kusubiri kwenye any station kwa muda wo wote kupisha treni hizi za abiria.

Bullet trains hizi zitawezesha mtu kutoka buisness capital saa 12 asubuhi na kufika government capital saa moja na nusu asubuhi. Hivyo rais wa JMT anaweza kumuita afisa yeyote aliyeko Dar es Salaam kufika Dodoma na ofisa huyo akaweza kufanya hivyo kwa muda kama wa kutoka Mbagala hadi magogoni ya Dar. Mtu ataweza kuishi Dar na kufanya kazi Dodoma, sawa na anayeishi Mbagala na kufanya kazi Dar city centre. Haya ndiyo tunataka.
 
Hivi hiyo bullet train na na SGR yenywe ni ipi ghali kuifance kama tumejenga SGR ya umeme kwa nini tusiitendee haki ,mabon Dreamliner tumenunua Sasa hivyo vibullet ndo vitushinde Kama nchi ,
 
Umeongea kitaalam sana kamanda watu wanjua bullet train mpaka iwejengewe railway mpya wakati hiyo hiyo ipo tu itakidhi vigezo hivyo
 
Sidhani kama ni swala rahisi kihivyo ndugu, kwanini waunde reli ya kumudu 160km/p? Si wangesema tu kwamba reli hii ina uwezo wa kumudu treni ya kasi yoyote ile?.

Hebu tuache kuzungumzia speed ya 400kph kwanza maana ni nchi chache zinazo-operate treni kwa 400+kph hadi sasa, nyingi ni 200 hadi 300+. Ngoja tukomae kwanza na hii ambayo iko realistic. 160kph bado hatua kubwa kwetu ila tu zinunuliwe model nzuri bwana sio kama hizo zilizo sawa na majirani.

Hii hapa chini ni ya China na imetengenezwa kwenda speed hio.

 
Umeongea kitaalam sana kamanda watu wanjua bullet train mpaka iwejengewe railway mpya wakati hiyo hiyo ipo tu itakidhi vigezo hivyo
Hapana alichozungumza practically kinaleta delay sana ili kusubiriana, hivi unaijua 400kph? Hapo itabidi treni ya kusimama kila kituo isubiriwe baadae treni ya mizigo ya kasi ndogo zaidi isubiriwe.

Speed kubwa inahitaji dedicated line isio na muingiliano sana ili kwamba hio speed iweze kufikiwa, vinginevyo itafanya kazi chini ya kiwango chake.

Tusijipe ukuu kiasi hicho mkandarasi si mjinga ku-design hio speed ya 160kph na makubaliano ya ujenzi yalikuwa hivyo kwani nchi ngapi zina treni za kwenda 400kph duniani?
 
Hivi hiyo bullet train na na SGR yenywe ni ipi ghali kuifance kama tumejenga SGR ya umeme kwa nini tusiitendee haki ,mabon Dreamliner tumenunua Sasa hivyo vibullet ndo vitushinde Kama nchi ,
Hata watu binafsi na makampuni binafsi yakiruhusiwa ku operate kwenye hii SGR yetu yanaweza kuleta hizo bullet trains kama walivyoleta jet planes hao Fastjet kwenye anga letu enzi zile. Bei ya bullet trains siyo kubwa kama tunavyofikiria. Bei yake ni kama hii hapa walivyonunua India toka Japan:


India walinunua kutoka Japani bullet trains 18, kila moja ikiwa na mabehewa 20 kwa jumla ya gharama ya Rs 7,000 crore, crore 1 = 100 lakh. Hii ni sawa na TSh 5 trillion tu kwa bullet trains 18 sawa na TSh 280 billion kwa kila bullet train moja yenye mabehewa 20 ambayo ni ndogo kuliko bei ya Dreamliner moja. Hawa akina Kadogosa hawatuambii hizo treni za enzi ya Hitler wamezinunua kwa bei gani? Hatutashangaa kama wamezinunua kwa bei mbaya kuliko hiyo ya bullet trains.
 
Kingine cha muhimu pia ambacho inatupasa tuweke akilini ni kwamba reli hii wanaita ya kimkakati ikiwa na lengo la kuleta tija zaidi na lengo ili litimie huduma ya usafirishaji mizigo ndilo lilikuwa la kwanza katika ku-design na abiria ni kipaumbele cha pili. Lengo la kuweka mkazo kwenye abiria tu si la afya katika uchumi wa nchi yetu hii maskini(utajiri uliopo wa asili bado haujaweza kubadirishwa kuwa fedha)

Tukifanya hivyo basi itakuwa kama TAZARA kwa sasa inasafirisha abiria tu na imechoka kweli hadi fedha za kujiendesha hazitoshi. Tujifunze kupitia hilo kwanza. Vinginevyo hakuna haja ya kuwekeza matrilioni ya fedha kwa treni yenye lengo kuu la huduma kwa abiria. Itakuwa vyema kama tungepeleka kwenye ile project ya mtwara au chuma cha liganga ili kuchochea viwanda mama halafu hizo luxury za 400kph kwa ajili ya abiria zingefuata.

Kwa kweli kama ningelikuwa kuwa na mamlaka kama kiongozi, ningelifanya hivyo, huwa inaniuma sana kuona tunanunua vitu ambavyo tunaweza zalisha. Mataluma ya reli, bidhaa nyepesi kuunda za chuma, mbolea wakati gesi(malighafi kuu ya mbolea) tunayo na mengine mengi mengi mengi...
 
Sijamaanisha hadi kufika 400km/ hr kama ulivyosema ni nchi uchache sana lakini hoja yangu sio kila bullet train inayotembea 300km/ hr zipo nying tu zinawaz zikamudu aka kwa dizaini yetu ya 160km hr
 
..ninachotaka kujua ni kama sgr itaendeshwa kibiashara na kwa faida.

..sitaki kusikia habari ya serikali kupata hasara kama inavyotokea kwa atcl.
 
India walinunua kutoka Japani bullet trains 18, kila moja ikiwa na mabehewa 20 kwa jumla ya gharama ya Rs 7,000 crore, crore 1 = 100 lakh. Hii ni sawa na TSh 5 trillion tu kwa bullet trains 18 sawa na TSh 280 billion kwa kila bullet train moja yenye mabehewa 20 ambayo ni ndogo kuliko bei ya Dreamliner moja. Hawa akina Kadogosa hawatuambii hizo treni za enzi ya Hitler wamezinunua kwa bei gani? Hatutashangaa kama wamezinunua kwa bei mbaya kuliko hiyo ya bullet trains. Wajitokeze humu watuambie laa sivyo tutawashitaki kwa wabunge wetu na kwa akina Mbatia na Mbowe.
 
..ninachotaka kujua ni kama sgr itaendeshwa kibiashara na kwa faida.

..sitaki kusikia habari ya serikali kupata hasara kama inavyotokea kwa atcl.
Wewe faida unayoijua ni hiyo ya hesabu nyepesi nyepesi za kihasibu. Tukijenga mitandao ya barabara za lami nchi nzima za matrillioni ya fedha, wewe unakuja na hesabu zako nyepesi nyepesi kujua zimepata faida au hasara ya shillingi ngapi. Tukijenga mashule na mahospitali, wewe unakuja kuona zimeingiza pesa ngapi na faida au hasara ni pesa ngapi. Kwenye bwawa la Nyerere, Tanzannite bridge, JPM bridge huko Mwanza etc utafanya hivyo hivyo. Umepotea na CAG wako. Serikali huwa haiwagawii pesa mfukoni wananchi wake bali huwawekea mfukoni maendeleo. Maendeleo hayapimwi kwa hesabu zenu hizo za kujumlisha 2 + 2!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…