Rais Samia: Nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?

Rais Samia: Nani kasema Maendeleo yanaletwa na Kitabu? Mbona Vitabu vya Dini tunavikiuka?

Hapa tulipigwa na kitu kizito Sana, hizi habari za makamu kua Raisi baada ya Raisi kufariki inabidi zitupiliwe mbali kabisa ili kuepusha kua na kiongozi mkuu wa hovyo, japo hata wanao chaguliwa na wenyewe ndio wale wale
 
Tangu lini Mwanamke akawa Kiongozi?,Mwanamke anafaa akae nyumbani amfulie mumewe,kupika na kuosha vyombo
Kikwete kwa kuwa sponsor wa huyu bibi alikuwa anajitengenezea namna ya kutengeneza himaya ya kuwarithisha watoto wake!! Baada ya Mangulla kuondoka simuoni mtu mwingine kwenye safu ya uongozi wa ccm atakayeweza kumthibiti Mkwere na genge lake!!
Kama mnakumbuka kuwa ni Kikwete huyu huyu ndio aliiweka rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na wananchi kwapani ili kulinda maslahi ya kikundi chao! Na watatatumia kila mbinu ili uchaguzi wa serikali za mitaa na ule wa 2025 ufanyike bila marekebisho yoyote ya maana ya katiba ili institutions zitakazohakikisha anashinda zibaki intact!!
Unfortunately, Samia hajui kusoma alama za nyakati, kwani Tanzania ya leo sio ya jana na haya anayosema maendeleo hayaji wakati nchi ina machafuko!! Vijana hawana ajira kwa sababu ya katiba iliyopo na hawatakuwa tayari kuona kuwa ndoto zao hazitimii kwasababu ya kikundi cha watu kutaka kukaa madarakani bila kuwa na uwezo wa kuwakwamua kutoka kwenye lindi la umaskini!!
 
Kwa hiyo Rais Samia alitaka kusema nini?
Hakuna haja ya kuwa na vitabu vitakatifu au katiba?
Hata tukiwa na hivyo vitabu bado hatupaswi kuvifuata?

Kuna vitu mtu mwenye heshima au mamlaka hupaswi kuvisema mbele za watu, maana ukivisema watu watagundua ujinga ulionao.
 
Rais ni nani, ama unaona kuwa rais ni kuwa na uelewa sana wa mambo? Huyo ni bogus tu ndio maana ameongea alichoongea. Katiba ni kwa ajili ya kutengeneza mazingira mazuri na madhubuti ya kiutawala na kiungozi ndani ya nchi. Anayesema katiba haileti maendeleo, ni dhahiri uwezo wake ni mdogo, au analeta hila za kitoto kwenye utawala wa nchi.
Kwani Katiba ya Sasa haileti hayo mazingira mazuri ya kiutawala? Ingekuwa haileti Tanzania ingekuwa unarudi nyuma.

Katiba haileti maendeleo na Wala haijawahi leta maendeleo popote.

Kwa kuwa mnadhani Katiba itawasaisia kushika Dola Rais aipige chini mazima kwanza haipo kwenye ilani ya ccm,yeye anatekeleza ilani ipi Kwa kuzungumzia Katiba?
Screenshot_20230911-133447.jpg
 
Jinsia yake haihusiki. Dini yake haihusiki. Sehemu ya Kijiografia anayotokea nayo haihusiki.

Kinachohusika hapa ni uwezo wake mdogo alionao.

Uwezo mdogo wa kiuongozi. Uwezo mdogo wa kuchanganua mambo. Na uwezo mdogo wa kujenga hoja.

Mara kadhaa sasa nimeona ona humu baadhi ya watu wakisema kwamba Rais Samia kaonyesha na kuthibitisha kuwa wanawake hawafai katika nafasi kiuongozi.

Mimi hilo nalikataa. Mtu mmoja mwenye uwezo mdogo si mwakilishi wa wanawake wote nchini wala duniani, kwa ujumla.

Uwezo wake mdogo alionao ni wa kwake yeye tu, Rais Samia.

Kilichonisukuma kuileta hii mada hapa ni yale maoni yake aliyoyatoa hapo jana.


View: https://youtu.be/O8SVrOeYtck?si=zAtsS1VP_q_B5Hmo

Rais anahoji kuwa kwani katiba ndo inaleta maendeleo?

Hivi huyu Rais hajui kuwa katiba ya nchi ndo framework ya uongozi na utawala ulio bora?

Bila uongozi na utawala ulio bora, kuna maendeleo gani yaliyo ya maana yanayoweza kupatikana?

Huo ni uwezo mdogo sana wa kufikiri ambao siutegemei utoke kwa kiongozi aliye wa juu kabisa nchini.

Au labda yeye anadhani maendeleo yanatoka wapi au yanakujaje?

Jingine la ajabu alilolizungumzia ni suala la elimu. Kwamba eti watu walio wengi hawajui hata katiba ni kitu gani. Hivyo ni lazima kwanza watu wapewe elimu kabla ya kuiandika hiyo katiba mpya.

Nilichoking’amua hapo ni ‘projection’ yake yeye kuhusu katiba.

Kulingana na kauli zake kuhusu katiba, nadhani yeye ndo hajui katiba ni kitu gani na hivyo anadhani hata wengine nao hawajui katiba ni nini!

Kenya waliandika katiba mpya mwaka 2010 [kama sijakosea].

Afrika Kusini waliandika katiba mpya baada ya kuachana na sheria za ubaguzi wa rangi kwenye miaka ya 90.

Marekani waliandika katiba yao miaka zaidi ya 200 iliyopita na ambayo wameifanyia marekebisho mara 27.

Sehemu nyingi tu duniani zimeandika katiba mpya na zingine kuzifanyia marekebisho katiba zilizopo.

Ni wapi ambako waliielimisha jamii kwanza kabla ya kuandika mpya?

Afrika Kusini walifanya elimu gani kwa wananchi kabla ya kuandika katiba yao mpya?

Waliwakalisha watu madarasani na kuanza kuwafundisha somo la katiba?

Katiba iliyopo sasa hivi wakati inaandikwa elimu ya katiba ilitolewa na nani? Lini? Wapi?

Naona sasa suala la kwamba wananchi hawana elimu ya katiba ndo litakuwa ‘narrative’ ya CCM kukwepa kujadili hoja za katiba mpya.

Kwa nilichokisikia jana, ni dhahiri shahiri kwamba anayehitaji elimu ya kujua katiba ni nini, ni Rais Samia.

Samia hafai kuwa Rais. Alichaguliwa kuwa mgombea mwenza kwa sababu zingine na si kwa sababu alikuwa ni mtu mwenye uwezo unaofaa.

Tuna Rais bomu ambaye hafai kuwepo madarakani hata kwa sekunde moja.

Nadiriki kusema kuwa Samia ndo Rais bomu kushinda marais wote tuliowahi kuwa nao Tanzania.

Hoja yake kubwa ni kwamba wananchi wasiendeshwe kwa kisingizio cha Katiba Mpya. Hiyo hiyo Katiba ya 1977 mbona imeleta mambo mengi mazuri!! Kimsingi hata hiyo Katiba ya 1977 ambayo inapondwa kama ukiiheshimu inaweza ikakupa maendeleo.

Wapinzani wanataka katiba mpya ili waweze kuitoa CCM madarakani, na CCM wanataka Katiba ya 1977 ili wasitoke madarakani.

Kimsingi matakwa ya wananchi walio wengi siyo katiba bali maendeleo. Wanaotaka Katiba Mpya wanataka kuingia madarakani.

Hata wao wenyewe wanaotaka Katiba Mpya, vyama vyao havina Katiba Mpya. Na vina Udikteta kuliko hata wa CCM. Kuna Mbowe ni M/Kiti wa CHADEMA toka 2003, je kweli hicho chama kina Katiba?

Clean your linen first before raising your hand to others.

Ukutuliza akili utamuelewa Samia.
 
Aliongea pumba tupu!

Uliziona nyuso za Mwamakula na Warioba kamera zilipowaonyesha?

Samia hana hata uwezo wa kujistukia kuwa anachoongea ni pumba.

Mimi sina akili nyingi. Ila nina akili za kutosha walau kujistukia kuwa ninachokiongea ni pumba na hivyo ni bora kunyamaza tu.

Samia hata uwezo huo hana.
Mwamakula na Warioba wakikunja nyuso ndiyo kiashiria cha katiba mbovu? Kweli hii nchi ina mahayawani wengi, yaani tuangalie uso wa Mwamakula badala ya kuangalia content.?

Nyinyi mlijiandalia hotuba yenu, lakini Samia ametoa hotuba yake
 
Kosoa kwa staha na adabu na siyo kutumia lugha kama kichaa na mwendawazimu.
Yeye hiyo staha na adabu anayo? Kusema Watanzania hawajui katiba huoni ni kukosa adabu?

Wangekuwa hawajui katiba maana yake hata yeye angepingwa asiwe Rais, lakini tunajuwa katiba inasema nini baada ya Rais Magufuli kufa.
 
Jibu swali Katiba Mpya imeleta maendeleo Nchi gani hapa Africa.

Kunitukana Wala hakupunguzi ujinga wako
Hebu kamuuliza mpuuzi mwenzio kwamba anaongoza Nchi kwa taratibu zipi?, Au ndio mmebakiza kuhamsisha ushoqer na Kitenge wenu?.
 
Hebu kamuuliza mpuuzi mwenzio kwamba anaongoza Nchi kwa taratibu zipi?, Au ndio mmebakiza kuhamsisha ushoqer na Kitenge wenu?.
Kwa taratibu za Katiba iliyopo ambayo imeivusha Nchi Toka 1961 Hadi Sasa.

Ni hivi kama mliyegemea Kulazimisha Katiba Mpya ya Kisiasa imewakata,kilochobakia toeni mapovu weeee kama ya DP World harafu mtaacha wenyewe baada ya watu kuwapuuza
 
NN , sikuwa disappointed nilikuwa stressed and depressed

Kwamba tuna Rais anayeongoza nchi kwa fikra zake na si muongozo unaoitwa Katiba.
Pengine ndiyo maana alimtuma mwanae Uganda bila kuwa na nyadhifa serikalini

Tuna kiongozi anayedhani ameingia madarakani kwa mazingaombwe na siyo katiba.

Wale waliodai na kulalamikia katiba (Zanzibar) wapo kimyaaaa! angsema Mbowe mama yangu! leo wangekuwa Bumbwini, Kibandamaiti, Kojoawima, wakibwbwaja.
 
Uhusiano wa hawa wawili inabidi iwekwe wazi kwa manufaa ya taifa
Sasa watu wakiandika unwell mnasema wanawatukana!! Wenye kujua kingereza someni hayo aliyoandika Ridhwani Kikwete ambae ni naibu Waziri katika serikali ya Samia ; na next time atapewa wizara kamili! Hicho kingereza ni cha mtu mwenye shahada ya sheria kweli? Ni aibu kwa waliomteua kwenye huo wadhifa kwani inaonesha wazi kuwa aliteuliwa sio kwa sababu ya weledi wake bali kwa sababu ya jina la baba yake!! Shame.
 
Ni tafsiri tu ya kile alichokisema...

Mh.Rais anaiheshimu katiba ila haijiendeshi.....inatafsiriwa na BINADAMU na inasimamiwa nao....

Katiba ni jengo ambalo ndani yake kuna shughuli na Maisha ya watu.....

MAENDELEO hufanywa humo ndani ya nyumba na hao binadamu.....

Si katiba itakayoleta hayo MAENDELEO bali ni hao wakazi wa hiyo nyumba.....

Binafsi nimemuelewa mh.Rais SSH [emoji120]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
NDIYO

Yaliongelewa ya busara kabisa na tena kuwekwa kinaga ubaga kuhusiana na mawili: 'uwepo wa Katiba' na 'kuuishi mwongozo wa kiKatiba'.

Maneno yaliyozungumzwa yanao mwanzo mzuri wa kuuleta uamsho katika Jamii; kila mwanajamii anaowajibu wa kuifahamu Katiba--katiba iliyopo, lau misingi ya Katiba katika Jamhuri... Kuifahamu na Kuiishi.

Hufikirika, kwa kasumba, Katiba ni kitabu kigumu kukielewa labda(?) Jambo hili si ukweli, katiba inaweza kueleweka kwa ufasaha na ufanisi miongoni mwa wanajamii ikiwa kuna 'Uono na Ufikirifu Mifumo' ilivyo ni Elimu 2.0.

Elimu inayoweza kuleta chachu ya Watu na Katiba ni Elimu 2.0 na Elimu 3.0... Hii siyo tu inawajibisha 'Wanajamii'--inawajibisha pia na watu wenye dhamana ya Uongozi katika Jamii.

Rais Samia, kwenye hili kazungumza ukweli mtupu na kaweka 'siasa za hadaa' pembeni, tushukuru.

Ikiwa Rais Samia, katika hili anaweka nia thabiti ya kujisahihisha kitaasisi na mifumo, kuna mengi 'yaliyozorota kitaifa' ambayo yanayosahihishika hata leo na sasa--pasipo kujali 'mtihani' wowote alionao kisiasa.

 
Kwani Rais Dr.Samia je anakosea kila kitu?.Bandari amekosea ,Katiba anakosea. Ivi nyie mnataka nini ? BANDARI AU Katiba? Acheni kukusumbua Rais nyie ndio maana wananchi hata mkitangaza maandamano hatuendi. Ni ujinga kukosoa kila kitu
 
Back
Top Bottom