Rais Samia naomba usimsahau Elia Wilinasi hata kwenye ukuu wa wilaya

Ukuu wa Wilaya sio ajira bali ni utumishi tu wa kisiasa.
Vijana wanakaa uwezo wa kufikiria umefika mwisho wanabaki kusubiri nafasi za uteuzi.
Ndiyo maana wengi wamekuwa watu wa kusifia na machawa tu.
Njaaa zimetoka tumboni zimehamia vichwani, Taifa halina critical thinkers bali kuna makuadi wa wanasiasa na watawala.
Tunazalisha taifa la hovyo sana mbeleniπŸ₯²πŸ₯²
 
Boss lakini sio wote. Wengine wana wito tu wa kuongoza ili kutatua matatizo mbalimbali yanayolikumba taifa letu.
 
Boss lakini sio wote. Wengine wana wito tu wa kuongoza ili kutatua matatizo mbalimbali yanayolikumba taifa letu.
Sasahivi ana nafasi gani ya kiutumishi?
Kama ana wito na anayo nafasi tayari ya kiutumishi na ameitendea haki basi, anastahili kupanda ngazi inayofuata ili aonyeshe zaidi uwezo wake.
ALL in All tuombeane Mema na Kheri.πŸ™πŸ™πŸ€£
 
Sasahivi ana nafasi gani ya kiutumishi?
Kama ana wito na anayo nafasi tayari ya kiutumishi na ameitendea haki basi, anastahili kupanda ngazi inayofuata ili aonyeshe zaidi uwezo wake.
ALL in All tuombeane Mema na Kheri.πŸ™πŸ™πŸ€£
Amen boss
 
Under which qualifications that Elias served that post mentioned above between 2014-2015?
 
Boss lakini sio wote. Wengine wana wito tu wa kuongoza ili kutatua matatizo mbalimbali yanayolikumba taifa letu.
Sasa mtu alisomeshwa masters na serikali bado anarudi kuomba uDC tena, nadhani serikali inahitaji utaalam wake zaidi kwenye fani aliyosoma, kusema tu anapenda siasa haitoshi kumfanya awe DC wote wanaosoma wakisema hivyo nani atabaki kwenye fani walizosomea? Kama ameajiriwa TPDC bado ana nafasi ya kutumikia taifa lake kuliko kutaka siasa..hiyo sasa ni tamaa na ubinafsi unamsumbua, nafasi za uteuzi aachie wengine wateuliwe yeye atumie ujuzi wake aliosomeshwa na serikali..
 
KUVAA VIZURI NA KUJICHEKESHA HOVYO SIO ISHARA YA UELEWA.

Wanaccm ni lazima tujikumbushe kila mara
Tuna jukumu la kuiongoza nchi hii na kuisimamia Serikali ili iweze kuitekeleza ilani ya CCM 2020 ambayo ni mkataba Kati yetu CCM na Wananchi.
Ili tufanikiwe ni lazima tuwachague Viongozi wenye Uelewa Mpana na wenye Maono Makubwa.

Viongozi Aina hiyo tunao wengi nchini ila maisha wanayoyaishi wamezungukwa na watu walio wengi wajinga kabisa ambao nyakati za Uchaguzi huleta mizaha na ushabiki wa kipumbavu ambao Matokeo ya hayo hupelekea kupenya watu wasio na sifa za Uongozi na Matokeo yake Viongozi hao Maboya huonekana vituko mbele ya Viongozi wa Serikali ambao Viongozi hao wa Serikali Daima Wana viapo vya uhakika na hulazimika kuishi wakisimamiwa na baadhi ya Viongozi wenye Uelewa Mdogo ambao viapo vyao huwa ni Danganya toto .
Pia history ya baadhi ya Viongozi wa Chama husomeka walivyopatikana kwa Rushwa ila wao huwa Makauzu hujitoa *Ufahamu na kujifanya na wao wanakemea* Rushwa ilihali wao wametokana na Rushwa.
Ifikie Mahali Wanaccm tujielewe tuache kutumika na kushangilia Mambo ya hovyo hovyo.

Wasomi wa Serikalini baadhi wanatushangaa na wanasikitika hata Post tunazo Post kwenye Magroup hasa kwa kuzingatia Sisi ndiyo watawala.

Ni lazima Sasa tuanze kuwakabili watu wajinga wajinga pale wanapopotosha Raia
NI kwa kufanya hivi tutakuwa pia tunayatekeleza Mapenzi ya Mwenyezi Mungu anayetutaka kutumia Uelewa wetu kuwasaidia wasio jielewa.

Nakumbuka Tarehe 22/08/2021
Askofu Dkt Josephat Gwajima alisema,

" Mimi kumkabili mtu Mjinga Mjinga , nimeambiwa hivyo na Mungu.
Akitokea mtu Mjinga Mjinga mkabili hasa anayechezea Mungu na nguvu zake..

Wanaccm tukibahatika tukakuza Uelewa tukakataa kutumikishwa na kufikiri kwa mizani ya njaa zetu naamini kabisa hata Sisi hatutakuwa Omba Omba na kuishi kwa kutegemea huruma za Viongozi Baadhi walio kwenye Vyombo vya Dola ambao wakinuna TU Sisi huku na familia zetu tunachanganyikiwa na kutafuta umbea wa kuwapelekea ili wacheke walau kidogo ili nasi familia zichangamke.

πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”πŸ€”

Tubadilike turudi kwenye malengo mapana ambayo Wananchi wenzetu Makapuku wenzetu walituamini na tukakubaliana nao kupitia ilani.

Nakumbuka Tarehe 07 / July/2021
Comrade Kanali Mstaafu
Mheshimiwa Ngemela Lubinga .
Katibu NEC Siasa na Mahisiano ya Kimataifa
Alisema,

" Kazi kubwa tunayokuja kufanya ni kusimamia ilani kwamba tulipoingia Madarakani tuliwaomba Wananchi kura .
Tukisema tutatekeleza hili tutatekeleza hili, tutatekeleza hili, Sasa tunataka kuona je, hayo yanatekelezwa?"

Mwisho wa kunukuu

Tusome Kitabu cha Ilani ya CCM 2020 uk 01 ibara 04 na uk 161-168.

Ili Mambo yaende ni lazima Muhali tuuweke pembeni , tuchukuwe kila hatua inayostahiki ikiwa ni Pamoja na kuto wachagua Viongozi wenye Uelewa Mdogo
Ambao baadhi yao wanapenya kwa Rushwa Kisha kulindwa kwa nguvu zote na baadhi ya Viongozi Wasio Waadilifu kwa visingizio vya kikao ambavyo hufanya Maamuzi vikiwa na Chuki Binafsi na Mitazamo hasi uliogandana na Uelewa finyu .
Katiba Kanuni Miongozo na Taratibu zetu zinaelekeza wazi na ziko wazi ila zinasiginwa kwa sababu ya baadhi ya Viongozi wetu walio na Uelewa finyu ambao baadhi yao walipata Uongozi huo kwa Rushwa na walio kosa lishe kwenye ubongo wao.
Watu wameelekezwa Sana watende haki kwa kufuata katiba Kanuni Miongozo na Taratibu ila kwa ukosefu wa lishe baadhi wamekuwa wakifikiri kwa kuwaza matumbo yao. NA faida wajipatazo kwa Rushwa ya kuwapitisha Wagombea Maboya kwa Maelekezo ya Viongozi wenye Fedha na kuwakata wote wenye Uelewa Mpana na ambao wangukuwa chachu ya kukiimarisha Chama.
Nakumbuka Tarehe 30/09/2022
Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan
Katika Mkutano wa Mwaka wa Tathmin ya Sita ya mkataba wa lishe September 30, 2022
Alisema,

" Ndiyo Yale aliyoyasema , nadhani Waziri Ummy, tunagombana huko TAMISEMI huko Chini, hata huko juu Serikalini.
Unamuelekeza mtu kitu mara nne , mara tano,hata hakimuingii.
Unamuuliza Dharau !?,
Jeuri !?, Hutaki !?
Kumbe Maskini hujuwi historia yake.
History yake imefichwa na suti na tai aliyoivaa.
Inawezekana kabisa maanake unasema ahaa, mbona mi naona hapa Kuna tatizo!?"
"Naona (Matatizo) moja , mbili, tatu, hivi inakuwaje huyu niliyemuamini hapa (Yeye haoni )!?"
"Haoni"
"Haiwezekani"
" Kumbe Kuna hayo ( ya Uelewa Mdogo na ukosefu wa lishe)"
"Tuna watu lakini sio Raslimali watu."

Mwisho wa kunukuu

Naye Pastor Mmbaga
Wa Mahubiri TV
Tarehe 26/12/2020
Aliwahi kusema,

"Sasa mnisamehe Sana Kama hii sentence itawakwaza"
" Kuna watu mtaishia kuwa Wapishi wa (watu) wengine (kwa) maana hamjiongezi
"(Kwa sababu ya ) Ufahamu (Mdogo)"
" Pata Maarifa , na kinachozuia tusipate Ufahamu ni ka Roho kale ka Nini!?
"Wivu , korosho "
" Yaani korosho ilivyo tamu lakini watu wakasema eti ( mtu) ana Roho ya korosho wakati korosho NI tamu!?"
Tubadilishe TU , tuite (Roho) ya ndoano ".

Mwisho wa kunukuu

Tuzaliwe Upya Kifikra Uongozi sio kuvaa nguo zilizo kolea kijani na nyeusi huku tukiwa hatujielewi tunatumikishwa na kujionyesha kuwaponda wanaotupatia Uelewa ili tukalipwe vihera kwa wenye hela za Rushwa.

Tusome Kitabu cha Katiba ya CCM 1977 Toleo 2020 ibara 15(3)(4)(6)(7) , Ibara 12(1)(a) ili tukasome uk 151 vifungu 1,3,6 na 8.

Nakumbuka Tarehe 28/10/2021
Comrade Humphrey Polepole
Akiwa Mbunge
Aliwahi kusema,

" Leadership is the ability to develop a Vision that motivate others to move with a passion towards a common goal."
Mwisho wa kunukuu.

Tuache kucheka check kwenye Mambo yanayoweza kuathiri jitihada za kulisongesha Taifa letu mbele.





Kidumu Chama Cha Mapinduzi






Mathias Mugerwa Kahinga
 
Rafiki unazungumza maneno yenye mantiki sana. Ila kiukweli kwa navyomjua mtu wa kupenda siasa basi huyu bwana anapenda sana. Hizo kazi ulizo zielezea hapo kwa navyomwelewa japo nimekaa naye kwa muda mfupi hazimtoshi. Huyu ni mtu wa kupenda kusaidia kutatua matatizo ya jamii yake. Moyo wake ndio umekaa hivyo. Hivyo anatakiwa kukaa mahali ambapo atatatua shida za watu wa jamii yake moja kwa moja. Akiwa kwenye hizo kazi za professional anafanya kazi na machines tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…