Rais Samia: Nilipoingia ofisini tu Mufti alinijia na furushi la migogoro ya mali za BAKWATA, ila tatizo wamelitengeneza wenyewe

Rais Samia: Nilipoingia ofisini tu Mufti alinijia na furushi la migogoro ya mali za BAKWATA, ila tatizo wamelitengeneza wenyewe

Nilimsikia Rais akihutubia Baraza la Eid alisikika akisema alipoingia madarakani tu Mufti alimjia na lundo la mafaili ya migogoro ya mali za Waisilamu.

Akasema kwa bahati mbaya nilipochunguza mafaili yale yana utata kwa kuwa wahusika wakubwa wa hizo sintofahamu ni wahusika wenyewe.

Naomba kwa mwenye uelewa mzuri kuhusu hii migogoro ya BAKWATA na wahusika anisaidie kuelewa vizuri ili tuwajue wahujumu wa mali za Waisilamu.
Waislam wenyewe
 
Kuna mahali niliwahi kwenda nikawaambia jamaa nataka.ninunue eneo including msikiti wakakubali.
Ndo namna walivyoingia ule msikiti wa pale Mwenge ni wao wenyewe Bakwata wamempa mtu ubia matokeo jamaa kavunja msikiti woote kajenga frem za biashara bila kujenga sehemu ya kusalia. Aliyefanya madudu hayo katumbuliwa ila atakuja ajae atapeleka malalamiko Serikalini kuwa wamedhulumiwa

Na kwa madudu hayo ya Bakwata ndo inapelekea kisiwe chombo kinachoheshimika, kukubaliwa na kupendwa wala kufuatwa na idadi kubwa ya waislamu hapa nchini japo ndo kinajinasibu kuwa ndo msimamizi wa waislam wote hapa nchini.
 
Yawezekana ilikuwa ni deliberate way kufanya wauze mali ili ushawishi upungue. Baada ya kutaifisha kuonekana kigumu, wengine wakinyang'anywa shule na hospitali wakaachiwa kidogo.

Ila nchi ambazo dini ina utajiri mkubwa huwa utengamano wake unasumbua kama ilivyo Uturuki
Uturuki tatizo si dini kuwa na utajiri, uturuki geographically ipo kimkakati Sana,si ulaya si Asia, magharibi wanatamani zaidi iwe kisecular Kama ilivyokua huko nyuma,si unaona walimtumia sheikh kutaka mpindua Erdogan!!
 
Waislam wenyewe
Engineer...

Katika kitabu cha Abdul Sykes nimeeleza jinsi EAMWS iivyovunjwa na serikali na nimeeleza sababu kwa nini ilivunjwa.

Hayo sitayalelza hapa.

Hapa nitaeleza jinsi serikali ilivyoshughulikia mali za Waislam na kuipa BAKWATA:

''Waziri wa Mambo ya Ndani Ali Said Mswanya kwa kuamriwa na Rais Julius Nyerere akatangaza kuwa tawi la Tanzania la East African Muslim Welfare Society na Baraza la Tanzania la East African Muslim Welfare Society ni jumuiya zisizotambulika kisheria chini ya kifungu 6 (i) cha Sheria ya Vyama.[1]

Kwa tangazo hilo la Rais wa Tanzania, Waislam walinyimwa nafasi ya kukutana na kuzungumza kuhusu tatizo ambalo kwa kweli liliwahisu Waislam peke yao.

Kwa ajili hii basi Waislam walinyimwa nafasi ya kujadili na kulitolea uamuzi tatizo la mgogoro wa EAMWS.

Viongozi wa EAMWS wakiongozwa na Rais wa EAMWS Tawi la Tanzania Tewa Said Tewa waliitwa mbele ya Kabidhi Wasii ambae ndiye alikuwa amekabidhiwa na serikali jukumu la kusimamia shughuli za kufunga rasmi shughuli za EAMWS.

Viongozi walifahamishwa kuwa chini ya sheria ya vyama mali zote za EAMWS zitauzwa na madeni yatalipwa kutokana na fedha hizo na fedha zitakazobaki watapewa wanachama.

Serikali ilikuwa haiwezi kufanya kama sheria ilivyokuwa imeelekeza.

Ilikuwa jambo zito sana kwa serikali na Nyerere kuonekana anasimamia kuuzwa kwa mali za Waislam.

Viongozi wa EAMWS walipoitwa kwa Kabidhi Wasii mara ya pili walifahamishwa kuwa serikali imebadilisha mawazo yake kutekeleza amri kama sheria inavyosema kwa ajili hiyo basi imefanya mabadiliko ya sheria ya vyama ambayo yanaiwezesha sasa kutoa mali ya EAMWS na kukabidhi BAKWATA.

Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyochukuliwa na kupewa BAKWATA bila ya ridhaa ya Waislam wenyewe.

Hivi ndivyo shule zote zilizojengwa na EAMWS pamoja na mradi wa Chuo Kikuu cha Kiislam kilipoanguka katika mikono ya kundi la Adam Nasibu lililokuwa likishirikiana na serikali na vyombo vyake vyote vya usalama.

BAKWATA haikuwa na uwezo wa kuendesha mipango yoyote na taratibu shule na miradi yote ya elimu ikafifia na mwishowe kufa kabisa.''

Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyopotea mali ambazo BAKWATA leo inadai ni mali zao.

Hata hapo Kinondoni ulipojengwa msikiti mkubwa wa Mfalme Hassan wa VI wa Morocco hicho kiwanja pamoja na shule ys Sekondari ya Kinondoni vimejengwa katika ardhi ya EAMWS na shule ilijengwa na EAMWS.

1682366984110.jpeg

File la Tewa Said Tewa lenye taarifa za mgogoro wa EAMWS

1682367256306.jpeg

Tewa Said Tewa akisalimiana na Waislam
wakati alipokuwa kiongozi wa EAMWS
Inatakiwa umakini sana pale BAKWATA inapounganishwa na Waislam kwa kuwa BAKWATA haikuundwa na Waislam.

Tafuta muhtasari wa mkutano ambao Waislam walikutana na kuamua kuwa hawaitaki EAMWS.

Haupo.

Waislam wengi wako kimya kuhusu BAKWATA kwa ajili ya kuweka staha ya hawa viongozi waliokuwapo madarakani hivi sasa ili wapate utulivu na waendeshe shughuli zao.
 
Mufti alibugi kweli kumpelekea Sa100 kesi za aina hii, mama anayaogopa sana mafisadi...sanasana angeyaomba YAMPISHE halafu shughuli ingekuwa imeisha!.
 
Uturuki tatizo si dini kuwa na utajiri, uturuki geographically ipo kimkakati Sana,si ulaya si Asia, magharibi wanatamani zaidi iwe kisecular Kama ilivyokua huko nyuma,si unaona walimtumia sheikh kutaka mpindua Erdogan!!
Dini kuwa na nguvu sio tatizo kwa Uturuki, tatizo ni makundi ya kidini kuwa na utajiri. Gulenists wanakuwa na jeuri kwa kuwa ni matajiri wanamiliki uwekezaji mkubwa. Na haohao ndio walimsaidia Erdogan kuingia madarakani mwaka sijui 2001 ule.

Mpinzani mkuu yule Kemal Kılıçdaroğlu na chama chake cha Nationalists siwaelewi ni secularists au non-secular. Sipendi Uturuki iwe non-secular kama Kemal Ataturk angewafanya vile wasingefanya maendeleo makubwa hivi.

Sijaona nchi non-secular ina maendeleo makubwa hata iwe na mapato kiasi gani. Tena nchi ikiwa theocratic ndio kabisaa matatizo unless muwe na dini moja yenye kama 90% ya population hao 10% mtanyanyasa wajilipue.

Uturuki naona itabaki kuwa secular na raia wanapenda hivyo.
 
Engineer...

Katika kitabu cha Abdul Sykes nimeeleza jinsi EAMWS iivyovunjwa na serikali na nimeeleza sababu kwa nini ilivunjwa.

Hayo sitayalelza hapa.
Hapa nitaeleza jinsi serikali ilivyoshughulikia mali za Waislam na kuipa BAKWATA:

''Waziri wa Mambo ya Ndani Ali Said Mswanya kwa kuamriwa na Rais Julius Nyerere akatangaza kuwa tawi la Tanzania la East African Muslim Welfare Society na Baraza la Tanzania la la East African Muslim Welfare Society ni jumuiya zisizotambulika kisheria chini ya kifungu 6 (i) cha Sheria ya Vyama.[1]

Kwa tangazo hilo la Rais wa Tanzania, Waislam walinyimwa nafasi ya kukutana na kuzungumza kuhusu tatizo ambalo kwa kweli liliwahisu Waislam peke yao.

Kwa ajili hii basi Waislam walinyimwa nafasi ya kujadili na kulitolea uamuzi tatizo la mgogoro wa EAMWS.

Viongozi wa EAMWS waliitwa mbele ya Kabidhi Wasii ambae ndiye alikuwa amekabidhiwa na serikali jukumu la kusimamia shughuli za kufunga rasmi shughuli za EAMWS.

Viongozi walifahamishwa kuwa chini ya sheria ya vyama mali zote za EAMWS zitauzwa na madeni yatalipwa kutokana na fedha hizo na fedha zitakazobaki watapewa wanachama.

Serikali ilikuwa haiwezi kufanya kama sheria ilivyokuwa imeelekeza.

Ilikuwa jambo zito sana kwa serikali ya Nyerere kuonekana anasimamia kuuzwa kwa mali za Waislam.

Viongozi wa EAMWS walipoitwa kwa Kabidhi Wasii mara ya pili walifahamishwa kuwa serikali imebadilisha mawazo yake kutekeleza amri kama sheria inavyosema kwa ajili hiyo basi imefanya mabadiliko ya sheria ya vyama ambayo yanaiwezesha sasa kutoa mali ya EAMWS na kukabidhi BAKWATA.

Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyochukuliwa na kupewa BAKWATA bila ya ridhaa ya Waislam wenyewe.

Hivi ndivyo shule zote zilizojengwa na EAMWS pamoja na mradi wa Chuo Kikuu cha Kiislam kilipoanguka katika mikono ya kundi la Adam Nasibu lililokuwa kikishirikiana na serikali na vyombo vyake vyote vya usalama.

BAKWATA haikuwa na uwezo wa kuendesha mipango yoyote na taratibu shule na miradi yote ya elimu ikafifia na mwishowe kufa kabisa.''

Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyopotea mali ambazo BAKWATA leo inadai ni mali zao.

Hata hapo Kinondoni ulipojengwa msikiti mkubwa Mfalme Hassan wa Morocco hicho kiwanja pamoja na shule ys Sekondari ya Kinondoni vimejengwa katika ardhi ya EAMWS.
Napitia andiko lako kwa makini kisha ntakurehea mkuu
 
Pale Lumumba ni nyumba ya Muislam jamaa yake na Mohamed Said
NYUMBA YA MAMA YAKE SHEIKH HAIDAR MWINYIMVUA BI.MWAMTORO BINT CHUMA NDIYO ILIYOBAKIA NA HISTORIA YA UHURU WA TANGANYIKA
Angalia picha ya Bi. Mwamtoro bint Chuma mama yake Sheikh Haidar Mwinyimvua akipiga kura Uchaguzi Mkuu 1970.

Bila ya shaka yoyote kura yake ilikwenda kwa Julius Kambarage Nyerere na chama chao cha TANU.

Bibi huyu aliishi zaidi ya miaka 100 na alifariki tarehe 11 May 1981.

Nyumba yake ilikuwa Mtaa wa Kariakoo na New Street No. 69 nyuma ya ofisi ya TAA miaka ya 1930 na TANU katika miaka ya 1950.

Hii nyumba bado ipo katika mikono ya familia ya Mzee Haidar Mwinyimvua na sasa iko nyuma ya Ofisi Ndogo ya CCM.

Nyuma ya nyumba hii kwa upande wa Mtaa wa Udoe Mzee Haidar Mwinyimvua mtoto wa Bi. Mwamtoro alikuwa na nyumba yake mwenyewe ambayo ikitumiwa zaidi kama mlango wa kutokea wanawake waliohudhuria mikutano ya TANU ya ndani kwenye nyumba hiyo ya mama yake, Bi. Mwamtoro bint Chuma iliyopakana na ofisi ya TANU.

Siku zile ua wa makuti ndiyo uliokuwa unatenganisha ofisi ya TANU na nyumba ya Bi. Mwamtoro.

Siku ya mkutano wa ndani wa TANU haya makuti yakiondolewa hivyo kuunganisha nyua hizi mbili kuwa ua mmoja.

Wanawake wakikaa nyuma na wanaume wakiwa mbele katika ua wa nyumba ya TANU New Street sasa Lumumba Avenue na akina mama wao wakiwa uani kwa Bi. Mwamtoro.

Huo ndiyo ulikuwa uwanja wao akina Bi. Titi Mohamed, Bi. Hawa bint Maftah, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Chiku bint Said Kisusa kwa kuwataja wachache.

Wakimaliza mkutano wanawake walikuwa wanaingia kwenye nyumba ya Haidar Mwinyimvua ambayo mlango wake uko Mtaa wa Udoe kuondoka kuepuka kupishana na wanaume.

Wakati wa uhai wake marehemu Rashid Mfaume Kawawa aliwaambia ndugu zake Sheikh Haidar Mwinyimvua kuwa nyumba yao hii imebeba kumbukumbu nyingi ya harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na endapo watataka kuiuza basi wakifikirie chama kwanza kabla ya mnunuzi mwingine.

Picha ya kwanza ni Bi. Mwamtoro bint Chuma na ya pili ni mwanae Haidar Mwinyimvua wote wapigania uhuru wa Tanganyika.

Picha zifuatazo ni nyumba hiyo pamoja na jengo la CCM Mtaa wa Kariakoo.


Bi. Mwamtoro Bint Chuma 1970



Sheikh Haidar Mwinyimvua​






Nyumba ya Bi. Mwamtoro bint Chuma inaonekana nyuma ya Ofisi Ndogo ya CCM Lumumba Avenue​

 
Ndo namna walivyoingia ule msikiti wa pale Mwenge ni wao wenyewe Bakwata wamempa mtu ubia matokeo jamaa kavunja msikiti woote kajenga frem za biashara bila kujenga sehemu ya kusalia. Aliyefanya madudu hayo katumbuliwa ila atakuja ajae atapeleka malalamiko Serikalini kuwa wamedhulumiwa

Na kwa madudu hayo ya Bakwata ndo inapelekea kisiwe chombo kinachoheshimika, kukubaliwa na kupendwa wala kufuatwa na idadi kubwa ya waislamu hapa nchini japo ndo kinajinasibu kuwa ndo msimamizi wa waislam wote hapa nchini.
Ukimkamata mmoja tu ,

Anakuambia hii kazi niachie hao wengine nawamudu.

Hawachelewi aisee.
 
Bakwata na ccm ni kulwa na doto , bakwata Kaiga kwa ccm tabia hiyo.
Kwakweli archbishop Tutu, maCCM baada ya kujiita chama cha Mapinduko yalijimilikisha viwanja vingi vya wazi hasa vile vilivyokuwa vya Mahakama ya Liwali, baadhi yao baadae yakavipiga bei hahah mfano wako unaelewaka zaidi
 
Rais ni Mlezi wa dini zote, hata Magufuli utakumbuka alikuwa karibu na Muft Abubakary, kuhusu Nyerere soma hapo juu andiko la Mohamed Said akieleza alivyoasisi kuchanganya Dini na siasa hadi kufikia kuwavunjia waislam chombo imara "EAMWS" na kuwaundia chombo dhaifu "BAKWATA", hata wakatoliki walichorewa mpango wao mzuri Enzi za Ben na Prof Mahalu hadi Leo unawalipa
 
Nilimsikia Rais akihutubia Baraza la Eid alisikika akisema alipoingia madarakani tu Mufti alimjia na lundo la mafaili ya migogoro ya mali za Waislamu.

Akasema kwa bahati mbaya alipochunguza mafaili yale yana utata kwa kuwa wahusika wakubwa wa hizo sintofahamu ni wahusika wenyewe.

Naomba kwa mwenye uelewa mzuri kuhusu hii migogoro ya BAKWATA na wahusika anisaidie kuelewa vizuri ili tuwajue wahujumu wa mali za Waislamu.
Ndio maana alipomwomba afute kesi ya Mbowe wala hakuwaza akamwamuru DPP aifute mara moja. Hiyo ni baada ya mahakama kuu kuamua kuwa Mbowe ana kesi ya kujibu kwenye mashatska ya ugaidi.
 
Back
Top Bottom