Rais Samia: Nilipoingia ofisini tu Mufti alinijia na furushi la migogoro ya mali za BAKWATA, ila tatizo wamelitengeneza wenyewe

Rais Samia: Nilipoingia ofisini tu Mufti alinijia na furushi la migogoro ya mali za BAKWATA, ila tatizo wamelitengeneza wenyewe

Hiyo ndiyo kazi na malengo ya kuundwa Bakwata, palikuwa na viongozi wala hawakuwa waislam mule
Uko sahihi kuamini kuwa kila mtu awe halisi katika mwili, tabia, akili na imani yake kwa Muumba wake, ila kwa bahati mbaya wanadamu hawako hivo toka Mwanza, angalia kwa Adamu na Hawa, waliachiwa Bustani lakini waliuza ile kwa tapeli. Hivyo sio uhalisia wako kaumini waliotangulia wakauza kabla yako hawakuwa waislam, bali ni
 
Bakwata iliasisiwa Iringa mkabala na ilipokuwa Railway Hotel
John...
Hapo Iringa ilikuwa kukamilisha ratiba.
Mambo makubwa na msumari wa mwisho ulipigiliwa Tanga kabla ya kufika Iringa.

Wakati wa vurugu hizi za EAMWS zinaendelea Kamati Kuu ya TANU ilikuwa inafanya kikao chake Tanga.

Saleh Masasi na wenzake waliokuwa wanaipinga EAMWS [1] walipanda ndege hadi Tanga kwenda kushauriana na Kamati Kuu ya TANU jinsi ya kumaliza ''mgogoro'' wa EAMWS.

Ujumbe huu ulikwenda Tanga kuonana na Rais Julius Nyerere ukiwa na orodha ya Waislam ambao walikuwa wanataka serikali wakamatwe na kutiwa kizuizini ili msuguano upate kumalizika kwa haraka kuwezesha serikali kuunda BAKWATA.

Hivi ndivyo walivyofika Iringa baada ya masheikh waliodhaniwa kuwa wanapinga kuvunjwa kwa EAMWS kukamatwa.

Katika orodha ile ya kukamatwa kulikuwa na jina la Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.
 
Elli,
Nitaandikaje kwa bahati mbaya.
Mtu anaandika vipi kwa bahati mbaya?

Maoni yako ni yapi kwa serikali ili kuwafanya waislam wamiliki mali zao? Na kwa nini mpaka sasa inashindikana wakati rais ambaye ndo mkuu wa kila kitu ni muislam? Una history nzuri sana ya nchi na tushasoma mengi kutoka kwako. Kwa sasa tunaomba maoni yako nini kifanyike usiogope kutoa ya moyoni sheikh na uzuri muheshimiwa huwa anapita pita huku anaweza kuchukua mawili matatu kutoka kwako
 
Elli,
Nitaandikaje kwa bahati mbaya.
Mtu anaandika vipi kwa bahati mbaya?
Good, nilitaka nipate hili vizuri Ili tuanzie hapa, naomba sasa tuhamie na lile swali la msingi kuwa Ukristo/Wakristo ndio wanaoshika madaraka tangu uhuru Hadi Sasa.
 
Ndg,kuna changamoto kubwa sana. Nakumbuka kipindi cha Magufuli palikua na kelele nyingi sana kuhusu wale masheikh walio selo. Imani ya wengi ni kuwa wanaonewa sababu ya dini. Ukiwauliza hao masheikh walikamatwa kipindi gani wanatafuta sababu mpya. Ni ngumu sana kuwaelewa
Basi Kuna tatizo kubwa tusilolifahamu
 
Maoni yako ni yapi kwa serikali ili kuwafanya waislam wamiliki mali zao? Na kwa nini mpaka sasa inashindikana wakati rais ambaye ndo mkuu wa kila kitu ni muislam? Una history nzuri sana ya nchi na tushasoma mengi kutoka kwako. Kwa sasa tunaomba maoni yako nini kifanyike usiogope kutoa ya moyoni sheikh na uzuri muheshimiwa huwa anapita pita huku anaweza kuchukua mawili matatu kutoka kwako
Massa,
Maoni yangu hayana maana yoyote kwako.

Hili ni jambo baina ya serikali na Waislam na serikali haihitaji kunisikia mimi.

Serikali inajua kila kitu.
 
Massa,
Maoni yangu hayana maana yoyote kwako.
Hili ni jambo baina ya serikali na Waislam na serikali haihitaji kunisikia mimi.

Serikali inajua kila kitu.

Sawa mkuu nimekupata vizuri Kwa hiyo na maandiko yako nayo hayana umuhimu kwangu sio? Ila usiwe na shaka sheikh. Cha muhimu jaribuni kuiga kwa wakatoliki jengeni umoja mukaonane na serikali ili muweke sawa madai ya waislam na kipindi kizuri ndo hiki cha kiongozi muislam. Vinginevyo mtaendelea kulalamika wakati mna madai ya msingi sana kwa ustawi wa waislam. Mungu awe nanyi mpate mnachotaka umoja ni nguvu
 
Nilimsikia Rais akihutubia Baraza la Eid alisikika akisema alipoingia madarakani tu Mufti alimjia na lundo la mafaili ya migogoro ya mali za Waislamu.

Akasema kwa bahati mbaya alipochunguza mafaili yale yana utata kwa kuwa wahusika wakubwa wa hizo sintofahamu ni wahusika wenyewe.

Naomba kwa mwenye uelewa mzuri kuhusu hii migogoro ya BAKWATA na wahusika anisaidie kuelewa vizuri ili tuwajue wahujumu wa mali za Waislamu.
tatizo kubwa la ndugu zetu waislamu wanaamini wakristu na wengine wasio waislamu ndiyo adui yao mkuu, jambo ambalo siyo sahihi hata kidogo
 
Kama maeneo ya BAKWATA, viongozi wanawauzia waislam wenzao matajiri, wanajenga vituo vya mafuta, viongozi wanagawana pesa, wanakuja viongozi wapya wanadai eneo mgogoro Apo tayari mfano huo
Lile Eneo la Chang'ombe Kibasila, la Ekari 26 walilo mwuzia Kanji kwa millioni 500, limeniuma sana ingawa mimi sio Muislamu.
Kuanzia pale nimewadharau sana
Bin-Bakwata.
 
Sawa mkuu nimekupata vizuri Kwa hiyo na maandiko yako nayo hayana umuhimu kwangu sio? Ila usiwe na shaka sheikh. Cha muhimu jaribuni kuiga kwa wakatoliki jengeni umoja mukaonane na serikali ili muweke sawa madai ya waislam na kipindi kizuri ndo hiki cha kiongozi muislam. Vinginevyo mtaendelea kulalamika wakati mna madai ya msingi sana kwa ustawi wa waislam. Mungu awe nanyi mpate mnachotaka umoja ni nguvu
Massa,
Waislam walipounda African Association 1929 na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933 hadi kuunganisha wananchi wote kupigania uhuru wa Tanganyika waliiga kutoka kwa nani?

Ali Mnjale na Salum Mpunga waliposafiri kutoka Lindi kuja Dar es Salaam kushawishi viongozi wa TANU kumleta Nyerere Lindi, Southern Province kuvunja propaganda kutoka Peramiho wakiwazuia waumini wao kujiunga na TANU wakiwatisha kuwa harakati za uhuru zilikuwa Maji Maji nyingine Waislam wanataka kupambana na Waingereza mipango hii waliiga kutoka wapi?

Haiyumkiniki kuwa waliwaiga Wakatoliki.

Nani aliyekuambia Waislam hatuna umoja?

Nyerere kafika Dar-es-Salaam 1952 nani walimpokea na kuishinae hadi uhuru ukapatikana?

Waislam wangekuwa hawana umoja Nyerere angechaguliwa vipi na Waislam wa Dar-es-Salaam kuongoza TAA 1953 na TANU 1954?

Nani aliyekuambia kuwa haki ya Waislam inaweza kutolewa na Rais Muislam peke yake?
 
Massa,
Waislam walipounda African Association 1929 na Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933 hadi kuunganisha wananchi wote kupigania uhuru wa Tanganyika waliiga kutoka kwa nani?

Ali Mnjale na Salum Mpunga waliposafiri kutoka Lindi kuja Dar es Salaam kushawishi viongozi wa TANU kumleta Nyerere Lindi, Southern Province kuvunja propaganda kutoka Peramiho wakiwazuia waumini wao kujiunga na TANU wakiwatisha kuwa harakati za uhuru zilikuwa Maji Maji nyingine Waislam wanataka kupambana na Waingereza mipango hii waliiga kutoka wapi?

Haiyumkiniki kuwa waliwaiga Wakatoliki.

Nani aliyekuambia Waislam hatuna umoja?

Nyerere kafika Dar-es-Salaam 1952 nani walimpokea na kuishinae hadi uhuru ukapatikana?

Waislam wangekuwa hawana umoja Nyerere angechaguliwa vipi na Waislam wa Dar-es-Salaam kuongoza TAA 1953 na TANU 1954?

Nani aliyekuambia kuwa haki ya Waislam inaweza kutolewa na Rais Muislam peke yake?
Nyerere hakuchaguliwa kwa huruma za waisilamu waliona kawapita mbali sana Kwa mengi
 
Nyerere hakuchaguliwa kwa huruma za waisilamu waliona kawapita mbali sana Kwa mengi
The Phylosopher...
Hakika Nyerere alikuwa hodari sana katika kundi lao lote lile lakini si wote walikuwa wanaujua uhodari wake.

Kweli hakuchaguliwa kwa kuonewa huruma kwani huruma haikuwa na nafasi katika harakati za ukombozi.

Hamza Mwapachu ndiye aliyekuwa anaujua uwezo wa Nyerere na ndiye aliyemfikisha kwa Abdul Sykes amtie katika uongozi wa TAA iundwe TANU.

Abdul Sykes yeye alimtaka Chief David Kidaha Makwaia wa Siha ashike nafasi ile waunde TANU na hii ilikuwa 1951.

Lakini kubwa katika hoja ya Hamza Mwapachu ilikuwa nafasi ya kiongozi wa kudai uhuru ishikwe na Mkristo ili kujenga umoja na kuondoa dhana ya kuwa harakati za TAA zimehodhiwa na Waislam.

Angalia picha za kupigania uhuru wa Tanganyika Nyerere kazungukwa na watu gani?

Historia ya Nyerere nimeieleza kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.
 
John...
Hapo Iringa ilikuwa kukamilisha ratiba.
Mambo makubwa na msumari wa mwisho ulipigiliwa Tanga kabla ya kufika Iringa.

Wakati wa vurugu hizi za EAMWS zinaendelea Kamati Kuu ya TANU ilikuwa inafanya kikao chake Tanga.

Saleh Masasi na wenzake waliokuwa wanaipinga EAMWS [1] walipanda ndege hadi Tanga kwenda kushauriana na Kamati Kuu ya TANU jinsi ya kumaliza ''mgogoro'' wa EAMWS.

Ujumbe huu ulikwenda Tanga kuonana na Rais Julius Nyerere ukiwa na orodha ya Waislam ambao walikuwa wanataka serikali wakamatwe na kutiwa kizuizini ili msuguano upate kumalizika kwa haraka kuwezesha serikali kuunda BAKWATA.

Hivi ndivyo walivyofika Iringa baada ya masheikh waliodhaniwa kuwa wanapinga kuvunjwa kwa EAMWS kukamatwa.

Katika orodha ile ya kukamatwa kulikuwa na jina la Mufti Sheikh Hassan bin Ameir.
Ahsante kwa ufafanuzi mzuri

Saleh Masasi na Nyerere walikuwa na ukaribu sana!
 
kwanini baadhi ya waislam hawampendi Sheikh Ponda
Uko sahihi, Kuna wengine ambao wanamuunga mkono na kumwona kama kiongozi wa haki na mtetezi wa maslahi ya Waislamu nchini Tanzania.

Ila Wengine wanamtuhumu kwa kujihusisha na siasa, ambayo inapingwa na baadhi ya Waislamu kama jambo lisilofaa kufanywa na viongozi wa kidini.

NB: maoni haya ni ya baadhi ya Waislamu tu na hayawakilishi maoni ya Waislamu wote kuhusu Sheikh Ponda.
 
Kinyungu,
Katika miaka ya 1970 Rashid Mfaume Kawawa alimwambia Sheikh Haidar Mwinyimvua kuwa endapo iko siku watataka kuuza nyumba hiyo basi wawauzie TANU kwani hiyo nyumba imebeba historia kubwa ya Mwalimu Nyerere na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.
Shukrani sana mkuu kwa kuhifadhi historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika. Hawa wanaokula matunda ya uhuru kina johnthebaptist hawajui chochote kuhusu haya unayoandika ila wana maneno kama radio
 
Shukrani sana mkuu kwa kuhifadhi historia ya kweli ya uhuru wa Tanganyika. Hawa wanaokula matunda ya uhuru kina johnthebaptist hawajui chochote kuhusu haya unayoandika ila wana maneno kama radio
Amenijubu Vizuri sana na kwamba niko sahihi

Mimi nimesoma Shule Bora kabisa ya Bakwata Wakati hii ikiwa na Walimu kutoka Iran akina Hushan na Farid nk, Walimu kutoka Pakistan akina Sheikh, Walimu kutoka India akina Choudry, Mrs Venogopa, Mr and Mrs Abdi nk...nk

The Highlands Sec School

So naielewa Bakwata na naelewa Uhusiano wa karibu sana wa Saleh Masasi na Nyerere

Hata mchungaji Lusekelo mzee wa Upako ameishi sana hapo Jengo la Bakwata Mjini papokuwa na hospitali yao
 
Back
Top Bottom