Rais Samia: Nilipoingia ofisini tu Mufti alinijia na furushi la migogoro ya mali za BAKWATA, ila tatizo wamelitengeneza wenyewe

Rais Samia: Nilipoingia ofisini tu Mufti alinijia na furushi la migogoro ya mali za BAKWATA, ila tatizo wamelitengeneza wenyewe

Hivi Kuna wakati wakatoliki walimpelekea Nyerere migogoro au Mimi ndio sielewi.serikali ijitenge na dini la sivyo watakuja waumini wa dini zote huko ikulu

Sent from my Infinix X665B using JamiiForums mobile app
Modest...
Soma kitabu, "Development and Religion in Tanzania," (1981) cha Jan P van Bergen kinaeleza mikutano ya Nyerere na viongozi wa Kanisa Katoliki Ikulu.

Mimi hujizuia sana kuandika haya lau kama nayajua mengi.

Lakini kwa kuwa hukuwa unayajua hayo nimekupa rejea hiyo ili uijue nchi yetu na matatizo yake.

Kitabu hiki kilikuwa kinauzwa Cathedral Bookshop lakini kwa unyeti wa yaliyokuwa ndani ya kitabu hicho kimya kimya kiliondolewa sokoni kisiuzwe.

Hiki kitabu kilikuwa maarufu sana kwa Waislam katika miaka ya 1980.

Taarifa hizo zilizokuwa katika kitabu hicho ziliandikwa katika kitabu cha Prof. Njozi, "Mwembechai Killings..." (2002)na serikali ya Rais Mkapa ikapiga marufuku kitabu hicho.

Kuitaka serikali ijitenge na dini kwa maana yake kwa Tanzania ni kulitaka Kanisa likae nje ya serikali.

Huu ni muhali mkubwa kwani Kanisa limehodhi uendeshaji wa nchi kwa asilimia 80:20.

Hii ni kama vile Waislam hawapo.

Hili la waumini wa dini zote halipo Tanzania.

Dini kubwa zenye maslahi na serikali ni Uislam na Ukristo.

Waislam maslahi yao katika serikali ni historia yao katika kupigania uhuru wa Tanganyika.

Wakristo maslahi yao ni kuwa ndiyo walioshika madaraka ya kuendesha nchi toka uhuru upatikane mwaka wa 1961 hadi hivi sasa.

Vipi leo utawataka waachie madaraka haya?

Busara ni walioshika madaraka yote ya serikali wawe tayari kuona na wengine wanapata fursa walizopata wao za elimu nk na wanaingi serikalini bila wao kuwa pingamizi.

1682385173860.jpeg
 
Ile chang'ombe karibia nusu vimeuzwa viwanja vya waislamu .ila wahusika ni hao hao viongozi wanaoneana aibu.

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
Shehe mkuu anajua fika hizo mali zimeuzwa kihalali na wenzake waliomtangulia, kwa hiyo anatafuta huruma ili Mh Rais apore haki za wengine wapewe wao, kwa kuwa Rais anayo mamlaka ya kufanya hivyo ili awafurahishe wao, hiyo nia yao mbaya Rais kaishtukia kaikwepa.
 
Yaani
Kuna mahali niliwahi kwenda nikawaambia jamaa nataka.ninunue eneo including msikiti wakakubali.
[/QUOTE Yaani wewe jamaa huwa sikupendi skabisaa. Wakati Mwendazake anatuhujumu wewe ilikuwa ukifurahia sana
 
NYUMBA YA MAMA YAKE SHEIKH HAIDAR MWINYIMVUA BI.MWAMTORO BINT CHUMA NDIYO ILIYOBAKIA NA HISTORIA YA UHURU WA TANGANYIKA
Angalia picha ya Bi. Mwamtoro bint Chuma mama yake Sheikh Haidar Mwinyimvua akipiga kura Uchaguzi Mkuu 1970.

Bila ya shaka yoyote kura yake ilikwenda kwa Julius Kambarage Nyerere na chama chao cha TANU.

Bibi huyu aliishi zaidi ya miaka 100 na alifariki tarehe 11 May 1981.

Nyumba yake ilikuwa Mtaa wa Kariakoo na New Street No. 69 nyuma ya ofisi ya TAA miaka ya 1930 na TANU katika miaka ya 1950.

Hii nyumba bado ipo katika mikono ya familia ya Mzee Haidar Mwinyimvua na sasa iko nyuma ya Ofisi Ndogo ya CCM.

Nyuma ya nyumba hii kwa upande wa Mtaa wa Udoe Mzee Haidar Mwinyimvua mtoto wa Bi. Mwamtoro alikuwa na nyumba yake mwenyewe ambayo ikitumiwa zaidi kama mlango wa kutokea wanawake waliohudhuria mikutano ya TANU ya ndani kwenye nyumba hiyo ya mama yake, Bi. Mwamtoro bint Chuma iliyopakana na ofisi ya TANU.

Siku zile ua wa makuti ndiyo uliokuwa unatenganisha ofisi ya TANU na nyumba ya Bi. Mwamtoro.

Siku ya mkutano wa ndani wa TANU haya makuti yakiondolewa hivyo kuunganisha nyua hizi mbili kuwa ua mmoja.

Wanawake wakikaa nyuma na wanaume wakiwa mbele katika ua wa nyumba ya TANU New Street sasa Lumumba Avenue na akina mama wao wakiwa uani kwa Bi. Mwamtoro.

Huo ndiyo ulikuwa uwanja wao akina Bi. Titi Mohamed, Bi. Hawa bint Maftah, Bi. Tatu bint Mzee, Bi. Chiku bint Said Kisusa kwa kuwataja wachache.

Wakimaliza mkutano wanawake walikuwa wanaingia kwenye nyumba ya Haidar Mwinyimvua ambayo mlango wake uko Mtaa wa Udoe kuondoka kuepuka kupishana na wanaume.

Wakati wa uhai wake marehemu Rashid Mfaume Kawawa aliwaambia ndugu zake Sheikh Haidar Mwinyimvua kuwa nyumba yao hii imebeba kumbukumbu nyingi ya harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na endapo watataka kuiuza basi wakifikirie chama kwanza kabla ya mnunuzi mwingine.

Picha ya kwanza ni Bi. Mwamtoro bint Chuma na ya pili ni mwanae Haidar Mwinyimvua wote wapigania uhuru wa Tanganyika.

Picha zifuatazo ni nyumba hiyo pamoja na jengo la CCM Mtaa wa Kariakoo.




johnthebaptist umesikia maneno hayo?
 
Engineer...

Katika kitabu cha Abdul Sykes nimeeleza jinsi EAMWS iivyovunjwa na serikali na nimeeleza sababu kwa nini ilivunjwa.

Hayo sitayalelza hapa.

Hapa nitaeleza jinsi serikali ilivyoshughulikia mali za Waislam na kuipa BAKWATA:

''Waziri wa Mambo ya Ndani Ali Said Mswanya kwa kuamriwa na Rais Julius Nyerere akatangaza kuwa tawi la Tanzania la East African Muslim Welfare Society na Baraza la Tanzania la East African Muslim Welfare Society ni jumuiya zisizotambulika kisheria chini ya kifungu 6 (i) cha Sheria ya Vyama.[1]

Kwa tangazo hilo la Rais wa Tanzania, Waislam walinyimwa nafasi ya kukutana na kuzungumza kuhusu tatizo ambalo kwa kweli liliwahisu Waislam peke yao.

Kwa ajili hii basi Waislam walinyimwa nafasi ya kujadili na kulitolea uamuzi tatizo la mgogoro wa EAMWS.

Viongozi wa EAMWS wakiongozwa na Rais wa EAMWS Tawi la Tanzania Tewa Said Tewa waliitwa mbele ya Kabidhi Wasii ambae ndiye alikuwa amekabidhiwa na serikali jukumu la kusimamia shughuli za kufunga rasmi shughuli za EAMWS.

Viongozi walifahamishwa kuwa chini ya sheria ya vyama mali zote za EAMWS zitauzwa na madeni yatalipwa kutokana na fedha hizo na fedha zitakazobaki watapewa wanachama.

Serikali ilikuwa haiwezi kufanya kama sheria ilivyokuwa imeelekeza.

Ilikuwa jambo zito sana kwa serikali na Nyerere kuonekana anasimamia kuuzwa kwa mali za Waislam.

Viongozi wa EAMWS walipoitwa kwa Kabidhi Wasii mara ya pili walifahamishwa kuwa serikali imebadilisha mawazo yake kutekeleza amri kama sheria inavyosema kwa ajili hiyo basi imefanya mabadiliko ya sheria ya vyama ambayo yanaiwezesha sasa kutoa mali ya EAMWS na kukabidhi BAKWATA.

Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyochukuliwa na kupewa BAKWATA bila ya ridhaa ya Waislam wenyewe.

Hivi ndivyo shule zote zilizojengwa na EAMWS pamoja na mradi wa Chuo Kikuu cha Kiislam kilipoanguka katika mikono ya kundi la Adam Nasibu lililokuwa likishirikiana na serikali na vyombo vyake vyote vya usalama.

BAKWATA haikuwa na uwezo wa kuendesha mipango yoyote na taratibu shule na miradi yote ya elimu ikafifia na mwishowe kufa kabisa.''

Hivi ndivyo mali za EAMWS zilivyopotea mali ambazo BAKWATA leo inadai ni mali zao.

Hata hapo Kinondoni ulipojengwa msikiti mkubwa wa Mfalme Hassan wa VI wa Morocco hicho kiwanja pamoja na shule ys Sekondari ya Kinondoni vimejengwa katika ardhi ya EAMWS na shule ilijengwa na EAMWS.

View attachment 2598803
File la Tewa Said Tewa lenye taarifa za mgogoro wa EAMWS

View attachment 2598808
Tewa Said Tewa akisalimiana na Waislam
wakati alipokuwa kiongozi wa EAMWS
Inatakiwa umakini sana pale BAKWATA inapounganishwa na Waislam kwa kuwa BAKWATA haikuundwa na Waislam.

Tafuta muhtasari wa mkutano ambao Waislam walikutana na kuamua kuwa hawaitaki EAMWS.

Haupo.

Waislam wengi wako kimya kuhusu BAKWATA kwa ajili ya kuweka staha ya hawa viongozi waliokuwapo madarakani hivi sasa ili wapate utulivu na waendeshe shughuli zao.
BAKWATA ni serikali au ni waislamu ?
Tatizo mnapokwepa kuwajibishana na kulazimisha kuonekana mnaonewa ndio shida inapoanzia.
Pokeeni changamoto zenu zishughulikieni itasaidia kuliko kulazimisha kila siku.
 
Mufti alibugi kweli kumpelekea Sa100 kesi za aina hii, mama anayaogopa sana mafisadi...sanasana angeyaomba YAMPISHE halafu shughuli ingekuwa imeisha!.
Mufti alijua kwa kuwa ni mwislamu mwenzake basi atashughulikia mgogoro vizuri.
 
johnthebaptist umesikia maneno hayo?
Kinyungu,
Katika miaka ya 1970 Rashid Mfaume Kawawa alimwambia Sheikh Haidar Mwinyimvua kuwa endapo iko siku watataka kuuza nyumba hiyo basi wawauzie TANU kwani hiyo nyumba imebeba historia kubwa ya Mwalimu Nyerere na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.
 
Shkamoo Mzee Moh'd, hili umeliandika kwa bahati mbaya au kwa kumaanisha? Au ni madaraka yapi tunayoyazungumzia?
Ndg,kuna changamoto kubwa sana. Nakumbuka kipindi cha Magufuli palikua na kelele nyingi sana kuhusu wale masheikh walio selo. Imani ya wengi ni kuwa wanaonewa sababu ya dini. Ukiwauliza hao masheikh walikamatwa kipindi gani wanatafuta sababu mpya. Ni ngumu sana kuwaelewa
 
BAKWATA ni serikali au ni waislamu ?
Tatizo mnapokwepa kuwajibishana na kulazimisha kuonekana mnaonewa ndio shida inapoanzia.
Pokeeni changamoto zenu zishughulikieni itasaidia kuliko kulazimisha kila siku.
Dingi...
Kuna haya maneno ambayo siyaelewi vyema: ''mnapokwepa kuwajibishana na kulazimisha mnaonewa.''

Sijui unaposema kwa kujumuisha ''mnapokwepa...'' sijui unawakusudia nani hao?
Nani amuwajibishe nani?

Naamini huwakusudii Waislam kuwaingilia BAKWATA katika taasisi yao.

Ama kuhusu ''changamoto,'' Waislam baada ya kuvunjwa kwa EAMWS walipokea changamoto hiyo kwa mikono miwili na hawakukata tamaa.

Katika utawala wa Julius Nyerere Waislam hawakuruhusiwa kusajili taasisi yeyote ya Kiislam kwa maendeleo yao.

Hata hivyo kulikuwa na harakati za chini kwa chini dhidi ya BAKWATA kupitia Warsha taasisi ya vijana wasomi waliofanya kazi kubwa sana ya kuwaamsha Waislam kujitambua.

Harakati hizi zilizaa matunda kipindi cha utawala wa Rais Mwinyi aliporuhusu Waislam kusajili taasisi huru kwa ajili ya maendeleo yao.

Waislam hawajapata kulazimisha chochote ndiyo maana leo utaona kuna BAKWATA na kuna Shura ya Maimam Tanzania na taasisi nyingi huru nchi nzima.

Hizi hazina ugomvi na BAKWATA kila taasisi inajitahidi kuutumikia Uislam kwa lile wanalolimudu.

Wanaoweza kujenga shule wanajenga, wanaoweza kufungua stesheni za tv na radio wanafanya hivyo nk.

Wanaoweza kuandika vitabu vya kuwaelimisha Waislam wanafanya hivyo nk.
 
Ndg,kuna changamoto kubwa sana. Nakumbuka kipindi cha Magufuli palikua na kelele nyingi sana kuhusu wale masheikh walio selo. Imani ya wengi ni kuwa wanaonewa sababu ya dini. Ukiwauliza hao masheikh walikamatwa kipindi gani wanatafuta sababu mpya. Ni ngumu sana kuwaelewa
Dingi...
Tatizo la kukamatwa Waislam ni tatizo kubwa sana.
Waislam wanakamatwa lakini kesi ikifika mahakamani hakuna ushahidi.
 
Rais ni Mlezi wa dini zote, hata Magufuli utakumbuka alikuwa karibu na Muft Abubakary, kuhusu Nyerere soma hapo juu andiko la Mohamed Said akieleza alivyoasisi kuchanganya Dini na siasa hadi kufikia kuwavunjia waislam chombo imara "EAMWS" na kuwaundia chombo dhaifu "BAKWATA", hata wakatoliki walichorewa mpango wao mzuri Enzi za Ben na Prof Mahalu hadi Leo unawalipa
Shukuru...
Serikali ya Tanzania mwaka wa 1993 ilitiliana sahihi mkataba na makanisa, mkataba uliokuja kujulikana kama Memorandum of Understanding makubaliano ambayo yalikuwa serikali kuidhinisha elimu, huduma za jamii na afya ziendeshwe na Christian Council of Tanzania (CCT) and Tanzania Episcopal Conference (TEC) kwa kushirikiana na serikali.

Mkataba huu ulitayarishwa kwa siri na Dr. Costa Mahalu, wa Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na ukatiwa sahihi na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Mkataba huu ulitiwa sahihi bila ya kuwashirikisha au kuwafahamisha Waislam.

Ili makubaliano haya yaweze kutekelezeka, serikali ilibidi ifanye marekebisho kifungu 30 cha Education Act No. 25, 1978.
 
Back
Top Bottom