Rais Samia: Sekta binafsi ndiyo itakayotutoa kiuchumi, Serikali hatufanyi biashara

Rais Samia: Sekta binafsi ndiyo itakayotutoa kiuchumi, Serikali hatufanyi biashara

Mbona Serikali ya Emirate Dubai inafanya Biashara kwani hao mliowauzia Bandari ni Kampuni ya Serikaki DP Dubai hata Kampuni za China mlizowapa Bagamoyo ni za Serikali pia, huyu raisi wenu aisee, duh, mnakodisha Qatar Airways Serikali nzima kwenda USA Qatar Airways ni za Serikali pia, …
Serikali ya Emirates inafanya biashara ktk mfumo wa kibinafsi, na wanajielewa, watz mashirika ya kibiashara yote mmeua na bado mnangangania kuyaendesha ili muendelee kuiba na kutafuna jasho la watz majizi makubwa nyie.
 
Rais Samia Suluhu leo Juni 09, 2023 amesema sekta binafsi ndiyo itakayoitoa Tanzania kiuchumi, ameyasema hayo wakati akishiriki Mkutano wa 14 wa Baraza la Taifa la Biashara(TNBC).

Rais Samia amesema wajibu wa Serikali ni kutengeza mazingira bora ya kufanya biashara jambo ambalo pia litatanua wigo wa kukusanya kodi.

Hivi huyu ni binadamu kweli? Isije kuwa tunaongozwa na jini jamani.., mazingira bora ni kuuza bandari zote za Tanganyika kwa kipindi kisicho na kikomo?
 
Akili yako kama ya Samia, unadhani muhimu ni kutoa kila kitu kwa sekta binafsi bila hata kuangalia mkataba unaoingia nao unasema nini!.
Aliyekwambia hatuangalii mkataba ni Nani we unaiona serikali ya Samia ni ya kipumbavu mpaka ishindwe kufanya mikataba mizuri? Hivi nyie majizi mnataka hiyo bandari iendelee kudumaa mpaka lini?
 
Rais Samia Suluhu leo Juni 09, 2023 amesema sekta binafsi ndiyo itakayoitoa Tanzania kiuchumi, ameyasema hayo wakati akishiriki Mkutano wa 14 wa Baraza la Taifa la Biashara(TNBC).

Rais Samia amesema wajibu wa Serikali ni kutengeza mazingira bora ya kufanya biashara jambo ambalo pia litatanua wigo wa kukusanya kodi.

Sawa nakubali lakini sio ubinafsishaji horela wa bandari kwa kisingizio Cha sekta binafsi
 
Aliyekwambia hatuangalii mkataba ni Nani we unaiona serikali ya Samia ni ya kipumbavu mpaka ishindwe kufanya mikataba mizuri? Hivi nyie majizi mnataka hiyo bandari iendelee kudumaa mpaka lini?
Kama mnaitazama hiyo mikataba halafu mnaweka saini zenu baada ya kusoma terms za kijinga na kinyonyaji kama zile, basi nyie ni wapumbavu, hamfai kutuongoza.
 
Hilo la serikali kutofanya biashara lipo katika kifungu gani cha katiba na sheria za nchi?, Au ni maamuzi binafsi tu ya Samia Suluhu Hassan?

Mbona wakati wa Nyerere na Magufuli serikali ilifanya biashara. Ina maana hao walikuwa wanaongoza kwa katiba tofauti na hii?
 

Attachments

  • 43E4195C-193D-4570-8CB9-0CBA0F603DBD.jpeg
    43E4195C-193D-4570-8CB9-0CBA0F603DBD.jpeg
    26.6 KB · Views: 1
Back
Top Bottom