Mkuu,
Kwani haiwezekami umeme wa ziada ukawepo lakini kukawa na tatizo la kuunganisha sehemu fulani za nchi kiasi kwamba hizo sehemu iwe rahisi kununua umeme wa nje?
Ila hili la kutokuwepo kwa mwendelezo wa mikakati ya kimaendeleo litatufanya tuendelee kubaki pale pale,maana kila utawala unakuja na yakeVyombo vya usalama wa nchi bado hawaoni sababu tu ya kuwaacha wananchi wachague viongozi kwa njia ya haki kuitia tume huru na katiba mpya.
Huyu aliyepo hajui hata ni kwa nini Aliyepita aliamua kujenga bwawa la Mwalimu Nyerere.
Hajui na hana habari kabisa .
Atatuachia madeni na makesi ya mikataba ya mabilioni kwenye umeme kama ilivyokua miaka yote na ufisadi .
Hapo ndipo hawa wanajeshi na polisi wanapokosea wananchi kwa kuendekeza Watawala wa CCM wanaokaa miaka mitano madarakani kwa ajili ya kujilimbikizia mali wakati polisi kwa mfano wanakaa kazini miaka 40 huku wakiwa hawaewi hata pesa za kuhamisha mizigo yao achilia mbali kikokotoo kinachowapa pesa zisizofikia mil.40.
Mtu anakaa madarakani miaka 10 analiachia taifa likiwa na madeni makubwa na hasara kila kona kutokana na kutaka kuwanufaisha watu wake bila kujali uchumi wa nchi utakua kwenye hali gani.
Tujiulize tu ni Lini mikoa ya Kaskazini wana uhaba wa umeme mpaka kufikia mahali pa kununua umeme kama Mkoa wa Kagera ?
Mikoa ya kaskazini wana chanzo cha Nyumba ya Mungu ,hale na umeme unaotoka Kwenye kiwanda cha sukari ungeweza kuingizwa kwenye gridi na kuongeza ukubwa wa umeme .
CCM imetydharau sana wapiga kura kwa sababu ya mfumo wa tume unaoua maamuzi ya kura za wananchi.
Yaani kweli kabisa Akina majaliwa, Kabudi ,Ndugai ,polepole,Makonda , Jafo, Januari ,Tulia ,Tibaijuka ,Mpina wote wamewakanyagia chini wanatuletea huyu aliyewahi hata kuchukua fomu na kuomba ridhaa kwa haki na kutuambia nini maono yake juu ya vizazi vya watanganyika mil 60 !!!
Yaani Tanzania tutoe fedha za tozo tupeleke nchi za nje kununua umeme wakati tuna gesi na makaa ya mawe ,upepo na joto kubwa la ardhini kwenye mikoa ya Singida ?
Kweli kabisa wanaCCM wanaona ni bora matakwa ya JK na familia yake na Samia wafurahie kwa maumivu makubwa ya Taifa kwa miaka mingi ijayo ?
Hii sio sawa .
Samia atalipeleka kubaya sana Taifa hili hasa Tanganyika atakua na kukiua kabisa chama cha mapinduzi .
Chama cha mapinduzi Mwisho wake ni huu wa utawala wa Samia . Kutakuwa kimechokwa na kuchukiwa sana na wananchi mpaka hivyo vyombo vya dola vitachoka sana kwa sababu wengi na watoto wa maskini ambao wanaona jinsi wanavyotaabika kwa manufaa ya watu wasio na uchungu na nchi hata kidogo. Magufuli aliwashuguulikia wapinzani lakini aliwashuguulikia mafisdi na kukataaichongo yao lakini huyu anawashughulikia wapinzani huku akiwachekea mafisadi na kufurahia michongo yao ya kifisadi
Mkuu Unaelewa Maana ya Grid?Ww hakika ni zero brain....kwaiyo hiyo back up unayoisemea itakua special kwa ukanda wa kaskazini tu, kanda ya kaskazini pekee ndio Tanzania?
Mkuu Hili ni dili tu kama yalivo madili mengine hata wanao craft izi Contract watakuwa sehemu ya dili tu''Something is terribly wrong''
Tumeambiwa umeme wa JNHP unatosheleza nchi na kuuza nje
Tukaambiwa hata mvua isponyesha miaka 3 hatuna shida ya umeme
Kaskazini kuna Nyumba ya Munga na Hale Tanga zinazochangia grid ya Taifa
Tuna Upepo na Jua katika uwanda wa kuanzia Same hadi Singida
Tumejenga ''line' kuunganisha na Kenya ili tuweze kuwauzia umeme wa ziada tulio nao.
Leo tunasikia eti tunataka kuagiza umeme.
Huu mkanganyiko una mambo mawili kwa Wananchi. Ima wakae kimya kwasababu hawaelewi, na wale wanaoelewa wakae kimya kwasababu ya kuchanganyika. Kuna tatizo kubwa sana!
JokaKuu Pascal Mayalla
Sasa Mzee kama una ushahidi kama mafarao wamepoka bwawa sii tuipeleke serikali kwa courtUmeme ushauzwa hautoshi nani kakwambia Bwawa la kwenu lile wakati lishauzwa km ilivyouzwa Gesi
Umetoa maelezo vizuri kabisa kuliko Gerson msigwa.Wakuu Mama ni kama amepewa taarifa Sio wame mislead Sijapenda kabisa, Kwasasa Total Capacity ya Uzalishaji wa Umeme Countywide ni 3040MW against matumizi ambayo hayafiki ata 2500MW kitu ambacho tunaweza Kusema kwa Sasa tuna Surplus
Issue ya Kukatika Kwa umeme sidhani kama Ni scarcity isipokuwa Miundo Mbinu ya Usambazaji na Usafirishaji ndio sio rafiki Ministry of Energy ime take ilo onboard na Kuna Miradi ya Usafirishaji Inafanyika Kuongeza Expansion ya Grid mfano wanajenga Mradi Wa 400KV kutoka Chalinze mpaka dodoma Ili umeme unaotoka Bwawa la Mwalimu Nyerere uwe distributed Vyema.
Mwezi uliopita walifanikiwa Kuunganisha Line za Msongo wa 400KV kutoka isenye Kenya Mpaka Singida Via Arusha Na Kujenga Kituo Kikubwa cha Kupooza umeme Substation Arusha Namuguru (400KV) Kiasi kwamba Muunganiko Huo utasaidia Cross-border trading ya Umeme kati yetu sisi Kenya kupitia (Ketraco) na Ethiopia ambaye Ethiopia ndio giant kwenye Ukanda Huu Muunganiko huo Uko guided na Kitu kinaitwa Eastern African power pool Power(EAPP) chenye wanachama Mataifa 13 to date
Ivo issue ya Kusema sisi tununue umeme hakuna sababu kabisa ya msingi ya Kufanya Ivo unless tupate scarcity kitu ambacho kwa sasa hatuna ujenzi wa Line ya msongo 400Kv chalinze dodoma utasaidia Vituo Vinne Kuwa interconnected vya 400Kv ambacho ni Chalinze, Zuzu pamoja Kituo kikubwa cha Singida na Namguru Arusha Ivo izo infrastructure zikishakuwa Constructed tutakuwa na Usafirishaji mzuri na Kaskazini itaenda Kuwa Stable upande wa Nishati
Mheshimiwa Naibu waziri Mkuu ni zaidi ya Mara Moja Tumesikia Ukisema Kuwa Kwa sasa nchi ina Kiwango cha Ziada(Surplus) upande wa uzalishaji ila tu Changamoto Ni Miundo Mbinu ya Usafirishaji na Usambazaji ambalo ni swala wote tunaelewa kuwa Linarekebishwa kwa Muda na ni swala Progressive hii Policy ya kusema tununue Umeme Kenya au Ethiopia sana sana Ethiopia ila Tupitishie kenya Naona Haijakaa Vizuri kabisa
Wakenya kwa sasa tumewapita Upande wa Capacity ya Grid zetu.
Fuatilia mada mwanzo mwisho. Bila kuhemuka.Hata mkono wako unapingana na kichwa chako Kwa haya unayoandika
Court ipi wakati Court yenyewe ipo mfukoni mwa Serikali? Unazungumzia Court ipi?Sasa Mzee kama una ushahidi kama mafarao wamepoka bwawa sii tuipeleke serikali kwa court
Acheni wivu wa kike! Nyie wengine si mnapata umeme usiokatikakatika kutoka stigla goji na kinyerezi 1,2,3,4,5...12?Ww hakika ni zero brain....kwaiyo hiyo back up unayoisemea itakua special kwa ukanda wa kaskazini tu, kanda ya kaskazini pekee ndio Tanzania?
Zambia hii hii ya Hichelema au Zambia ipi? Maana hapa Lusaka hatuna umeme hii ni siku ya nne sasa.Sisi tunaotumia wa Zambia ni uhakika
Hiyo hiyo na ndio faida ya mikataba ya Kimataifa.Zambia hii hii ya Hichelema au Zambia ipi? Maana hapa Lusaka hatuna umeme hii ni siku ya nne sasa.
Serikali iuze na sgr yetu dubai ili tupate pesa ya kuwanunua wapinzani kwenye uchaguzi ujao.Kumbe huu wimbo ya kuuza umeme nje ya nchi tumekuwa tunachezeshwa toka enzi za mzee wa “mitaji yenu niya kujenga viwanda vya juisi”!
Tangu ipigwe ile K. O ya bandar za tz bara na bado watu wakasifu na kuabudu kwamba ni maamuz sahihi bhas sioni lolote la kupingwa.Hivi ni kwann masuala kama haya wananchi huwa hatushirikishwi kabisa kwenye kutoa maoni na maamuzi pia na badala yake tunakuja kupewa taarifa mwishoni ambapo tayari watu wachache wapumbavu wameshakaa na kufanya maamuzi.
Hii katiba yetu kwakweli ni yakipumbavu sana.
Halafu huo umeme wa bwawa la Nyerere la huko Rufiji watakuja waiuzie Kenya na Uganda ambapo kuna umbali zaidi kuliko Kanda ya kaskazini!Sababu umbali, cha kujiuliza umeme siyo mawe useme ni bora ununue mpakani mwa Kenya kuliko kuyafata mawe Rufiji kuyapelela Same, Kwanii umeme wasinunue kutoka Moshi kuliko kwenda kununua Ethiopia