Pre GE2025 Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Pre GE2025 Rais Samia: Serikali itanunua Umeme nje maalum kwa Mikoa ya Kaskazini

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Mkuu,

Kwani haiwezekami umeme wa ziada ukawepo lakini kukawa na tatizo la kuunganisha sehemu fulani za nchi kiasi kwamba hizo sehemu iwe rahisi kununua umeme wa nje?

Hata mkono wako unapingana na kichwa chako Kwa haya unayoandika
 
Sema kama kuna kitu nawakubali ni timing za kutoa hizi taarifa, kupiga matukio. Hiki kipindi story kubwa itakuwa ni game ya Simba na Yanga, na unaweza kutwa ilihailishwa kitaalamu tu.

Waache kuchezea hela kwenye mambo yayo ya muhimu, wapeleke sehemu husika mambo yatakaa sawa tu. Hakuna nchi imewahi kujengwa kwa uchawa.
 
Vyombo vya usalama wa nchi bado hawaoni sababu tu ya kuwaacha wananchi wachague viongozi kwa njia ya haki kuitia tume huru na katiba mpya.

Huyu aliyepo hajui hata ni kwa nini Aliyepita aliamua kujenga bwawa la Mwalimu Nyerere.

Hajui na hana habari kabisa .
Atatuachia madeni na makesi ya mikataba ya mabilioni kwenye umeme kama ilivyokua miaka yote na ufisadi .

Hapo ndipo hawa wanajeshi na polisi wanapokosea wananchi kwa kuendekeza Watawala wa CCM wanaokaa miaka mitano madarakani kwa ajili ya kujilimbikizia mali wakati polisi kwa mfano wanakaa kazini miaka 40 huku wakiwa hawaewi hata pesa za kuhamisha mizigo yao achilia mbali kikokotoo kinachowapa pesa zisizofikia mil.40.
Mtu anakaa madarakani miaka 10 analiachia taifa likiwa na madeni makubwa na hasara kila kona kutokana na kutaka kuwanufaisha watu wake bila kujali uchumi wa nchi utakua kwenye hali gani.

Tujiulize tu ni Lini mikoa ya Kaskazini wana uhaba wa umeme mpaka kufikia mahali pa kununua umeme kama Mkoa wa Kagera ?

Mikoa ya kaskazini wana chanzo cha Nyumba ya Mungu ,hale na umeme unaotoka Kwenye kiwanda cha sukari ungeweza kuingizwa kwenye gridi na kuongeza ukubwa wa umeme .

CCM imetydharau sana wapiga kura kwa sababu ya mfumo wa tume unaoua maamuzi ya kura za wananchi.

Yaani kweli kabisa Akina majaliwa, Kabudi ,Ndugai ,polepole,Makonda , Jafo, Januari ,Tulia ,Tibaijuka ,Mpina wote wamewakanyagia chini wanatuletea huyu aliyewahi hata kuchukua fomu na kuomba ridhaa kwa haki na kutuambia nini maono yake juu ya vizazi vya watanganyika mil 60 !!!
Yaani Tanzania tutoe fedha za tozo tupeleke nchi za nje kununua umeme wakati tuna gesi na makaa ya mawe ,upepo na joto kubwa la ardhini kwenye mikoa ya Singida ?
Kweli kabisa wanaCCM wanaona ni bora matakwa ya JK na familia yake na Samia wafurahie kwa maumivu makubwa ya Taifa kwa miaka mingi ijayo ?

Hii sio sawa .

Samia atalipeleka kubaya sana Taifa hili hasa Tanganyika atakua na kukiua kabisa chama cha mapinduzi .
Chama cha mapinduzi Mwisho wake ni huu wa utawala wa Samia . Kutakuwa kimechokwa na kuchukiwa sana na wananchi mpaka hivyo vyombo vya dola vitachoka sana kwa sababu wengi na watoto wa maskini ambao wanaona jinsi wanavyotaabika kwa manufaa ya watu wasio na uchungu na nchi hata kidogo. Magufuli aliwashuguulikia wapinzani lakini aliwashuguulikia mafisdi na kukataaichongo yao lakini huyu anawashughulikia wapinzani huku akiwachekea mafisadi na kufurahia michongo yao ya kifisadi
Ila hili la kutokuwepo kwa mwendelezo wa mikakati ya kimaendeleo litatufanya tuendelee kubaki pale pale,maana kila utawala unakuja na yake

Mfano kwenye elimu hakuna miendelezo,kila utawala unakuja na utaratibu wake
 
Huu ni upigaji ndo unaoendelea yaani hamjifunzi katika

Escrow
Richmond

Na sasa mmekuja na huu mchongo Mpya na mlivyo wajanja mmeshamtia mkuu wenu ndani.
 
Ww hakika ni zero brain....kwaiyo hiyo back up unayoisemea itakua special kwa ukanda wa kaskazini tu, kanda ya kaskazini pekee ndio Tanzania?
Mkuu Unaelewa Maana ya Grid?
Grid ni Interconnection of Power plants and Transmission infrastructures
Arusha hana Hata Chanzo Kimoja cha Umeme lakini anatumia Umeme unaotoka Kidatu au Mtera hio ndio maana ya Interconnection

Kuunga na Kenya kwetu au option ya Kununua umeme iwe kama back up tu leo tumeungana na Kenya kupitia arusha kwa vile Arusha Nimpakani haimaanishi Umeme huo utatumika Arusha tu no utakuwa distributed Countrywide kutegemea na Kiasi chake

Yani iko Ivi Arusha imekuwa kama Gateway tu ila Ikitokea Total blackout tunaweza kwa haraka kuchukua Umeme kenya na Tukasema umeme huo usitumike Arusha uje moja kwa Moja dar es salam au Dodoma Kwenye Maeneo strategic ili operation ziendelee
 
''Something is terribly wrong''
Tumeambiwa umeme wa JNHP unatosheleza nchi na kuuza nje
Tukaambiwa hata mvua isponyesha miaka 3 hatuna shida ya umeme

Kaskazini kuna Nyumba ya Munga na Hale Tanga zinazochangia grid ya Taifa
Tuna Upepo na Jua katika uwanda wa kuanzia Same hadi Singida

Tumejenga ''line' kuunganisha na Kenya ili tuweze kuwauzia umeme wa ziada tulio nao.

Leo tunasikia eti tunataka kuagiza umeme.

Huu mkanganyiko una mambo mawili kwa Wananchi. Ima wakae kimya kwasababu hawaelewi, na wale wanaoelewa wakae kimya kwasababu ya kuchanganyika. Kuna tatizo kubwa sana!

JokaKuu Pascal Mayalla
Mkuu Hili ni dili tu kama yalivo madili mengine hata wanao craft izi Contract watakuwa sehemu ya dili tu

Kwa akili ya kawaida huwezi kuwa na Surplus Then ukaenda tena Kununua nje Umeme
It doesn't make sense kabisa hio hela ya kwenda Kununulia umeme Nje kwanini usifanye facilitation tu Ukajenga Transmission Line yenye uhakika kabisa badala ya Kwenda kununua Umeme nje

Hii ni dili tu
 
Hii ni DP world nyingine,inaingiziwa mikoa ya Kaskazini mwa Tanzania,kuliko zaliwa Chadema!
 
Wakuu Mama ni kama amepewa taarifa Sio wame mislead Sijapenda kabisa, Kwasasa Total Capacity ya Uzalishaji wa Umeme Countywide ni 3040MW against matumizi ambayo hayafiki ata 2500MW kitu ambacho tunaweza Kusema kwa Sasa tuna Surplus

Issue ya Kukatika Kwa umeme sidhani kama Ni scarcity isipokuwa Miundo Mbinu ya Usambazaji na Usafirishaji ndio sio rafiki Ministry of Energy ime take ilo onboard na Kuna Miradi ya Usafirishaji Inafanyika Kuongeza Expansion ya Grid mfano wanajenga Mradi Wa 400KV kutoka Chalinze mpaka dodoma Ili umeme unaotoka Bwawa la Mwalimu Nyerere uwe distributed Vyema.

Mwezi uliopita walifanikiwa Kuunganisha Line za Msongo wa 400KV kutoka isenye Kenya Mpaka Singida Via Arusha Na Kujenga Kituo Kikubwa cha Kupooza umeme Substation Arusha Namuguru (400KV) Kiasi kwamba Muunganiko Huo utasaidia Cross-border trading ya Umeme kati yetu sisi Kenya kupitia (Ketraco) na Ethiopia ambaye Ethiopia ndio giant kwenye Ukanda Huu Muunganiko huo Uko guided na Kitu kinaitwa Eastern African power pool Power(EAPP) chenye wanachama Mataifa 13 to date

Ivo issue ya Kusema sisi tununue umeme hakuna sababu kabisa ya msingi ya Kufanya Ivo unless tupate scarcity kitu ambacho kwa sasa hatuna ujenzi wa Line ya msongo 400Kv chalinze dodoma utasaidia Vituo Vinne Kuwa interconnected vya 400Kv ambacho ni Chalinze, Zuzu pamoja Kituo kikubwa cha Singida na Namguru Arusha Ivo izo infrastructure zikishakuwa Constructed tutakuwa na Usafirishaji mzuri na Kaskazini itaenda Kuwa Stable upande wa Nishati

Mheshimiwa Naibu waziri Mkuu ni zaidi ya Mara Moja Tumesikia Ukisema Kuwa Kwa sasa nchi ina Kiwango cha Ziada(Surplus) upande wa uzalishaji ila tu Changamoto Ni Miundo Mbinu ya Usafirishaji na Usambazaji ambalo ni swala wote tunaelewa kuwa Linarekebishwa kwa Muda na ni swala Progressive hii Policy ya kusema tununue Umeme Kenya au Ethiopia sana sana Ethiopia ila Tupitishie kenya Naona Haijakaa Vizuri kabisa
Wakenya kwa sasa tumewapita Upande wa Capacity ya Grid zetu.
Umetoa maelezo vizuri kabisa kuliko Gerson msigwa.
 
Hata mkono wako unapingana na kichwa chako Kwa haya unayoandika
Fuatilia mada mwanzo mwisho. Bila kuhemuka.

Halafu elewa kuwa kuna hoja za kidhahania zaidi.

Swali langu hujajibu.
 
N
Ww hakika ni zero brain....kwaiyo hiyo back up unayoisemea itakua special kwa ukanda wa kaskazini tu, kanda ya kaskazini pekee ndio Tanzania?
Acheni wivu wa kike! Nyie wengine si mnapata umeme usiokatikakatika kutoka stigla goji na kinyerezi 1,2,3,4,5...12?
 
Zambia hii hii ya Hichelema au Zambia ipi? Maana hapa Lusaka hatuna umeme hii ni siku ya nne sasa.
Hiyo hiyo na ndio faida ya mikataba ya Kimataifa.

Kwa taarifa Yako tuu Rukwa na Katavi wanatumia umeme wa Zambia.

Nyie mtakaosa umeme hata wiki ila huku lazima walete.
 
Kumbe huu wimbo ya kuuza umeme nje ya nchi tumekuwa tunachezeshwa toka enzi za mzee wa “mitaji yenu niya kujenga viwanda vya juisi”!
Serikali iuze na sgr yetu dubai ili tupate pesa ya kuwanunua wapinzani kwenye uchaguzi ujao.
 
Hivi ni kwann masuala kama haya wananchi huwa hatushirikishwi kabisa kwenye kutoa maoni na maamuzi pia na badala yake tunakuja kupewa taarifa mwishoni ambapo tayari watu wachache wapumbavu wameshakaa na kufanya maamuzi.

Hii katiba yetu kwakweli ni yakipumbavu sana.
Tangu ipigwe ile K. O ya bandar za tz bara na bado watu wakasifu na kuabudu kwamba ni maamuz sahihi bhas sioni lolote la kupingwa.

Labda tutangaziwe kodi ya pumzi.
 
Sababu umbali, cha kujiuliza umeme siyo mawe useme ni bora ununue mpakani mwa Kenya kuliko kuyafata mawe Rufiji kuyapelela Same, Kwanii umeme wasinunue kutoka Moshi kuliko kwenda kununua Ethiopia
Halafu huo umeme wa bwawa la Nyerere la huko Rufiji watakuja waiuzie Kenya na Uganda ambapo kuna umbali zaidi kuliko Kanda ya kaskazini!
 
Back
Top Bottom