Pre GE2025 Rais Samia: Sijawahi kuua mtu labda sisimizi, jibuni hoja zao msikae kimya

Pre GE2025 Rais Samia: Sijawahi kuua mtu labda sisimizi, jibuni hoja zao msikae kimya

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Madhara ya kurithisha madaraka mtu mwenye upeo mdogo ndiyo haya sasa.yeye ndiyo amri jeshi mkuu,chochote kitakachofanyika mhusika ni yeye na kama halijui Hilo Bora ajiuzulu maana inaonesha hajui majukumu yake.yeye anataka awe anasifiwa tu lakini akikosolewa anachukia
 
Tunataka report ya kifo cha Meddy kibao.
Hutokuja kuiona hiyo, umesikia hata wakitoa mrejesho! wangapi wamekamatwa kusaidia uchunguzi? {unakumbuka alipotekwa Mo walivyokuwa wanatoa mrejesho}
sasa kwa kisa hiki ilitakiwa mrejesho na mikwala ya police iwe vile , ukimya huu jiongeze ndio imepita hiyo. Nilitegemea huyu mama kuwa kazi itakamilika soon na lipoti itawekwa wazi, ila kamfananisha alieuawa na sisiminzi. Yaani yeye kaua sisiminzi asisakamwe... mwee
 
Huko ndio kuishiwa kwenyewe. Uliweza kufunguwa domo lako wakati wake?

Au ulikuwa gizani?
We msimamo mkali embu acha kutetea mauaji... Hao watu wasiojulikana wanajulikana na wanapewa vyeo usijidai mwehu kamavile huelewielewi!!
Mungu huona vya ndani kabisa rohoni,kama unamwabudu katika kweli tubu tuu LAKINI kama unazugazuga tuu basi zuga uje hapa Torokauje bar tupige kitimoto na konyagi afu twende pale Kajificheni gestihausi tukapige pushapu😘
 
Naunga mkono hoja, mtu mwenye wajihi kama huu, Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth!” hawezi hata kuua panya!, kama ni kuua labda mbu, mende na sisimizi.

Ila kwa vile yuko serikalini na yeye ndie mkuu wa serikali, na anajua kuna mazingira fulani, serikali zote duniani huwa zina waua watu hatarishi kwa usalama wa nchi, dissidents, na kabla hawa dissidents hawajauliwa lazima CinC asaini ile death warrant, then death warrant yoyote ikisainiwa, aliyeua ni aliyesaini death warrant na sio wale watekelezaji.

Ikitokea makosa ya watu wake kumuua kwa makosa mtu safi kwa kudhaniwa ni dissident, then the blood of that person is upon aliyetoa hiyo order kwa niaba yake.

Na kunapotokea vifo ambavyo vingezuilika kwa kufanya kitu lakini hakikufanyika, then damu iliyomwagika is upon yule ambaye angezuia lakini hakuzuia.

Hivyo tumeshauri Kama Walioua ni "Wasiojulikana" Then Karma, Albadir Itawahusu, ila kama ni 'Wasiojulikana', Hata Albadir Haisaidii Kitu, Wametimiza Tuu Wajibu Wao!
P

Vipi kuhusu Hawa Askari ambao wanaotuhumiwa kila siku kuua raia ?
Vipi kuhusu hao raia ambao wamekuwa wakifa wakiwa mikononi mwa Jeshi la Polisi katika Vituo vya Polisi ?? Nao hawamhusu?
Vipi hao mateka ambao baadhi yao wameokotwa wakiwa tayari wameuawa kinyama? Nao hawamhusu??

Akumbuke kwamba yeye binafsi akiwa Kama Mkuu wa nchi hii kwa mikono yake ndiye aliyewateua hao Viongozi wote wa Serikali hii iliyopo, wakiwamo na Wakuu wa Majeshi ambayo wa-Tanzania wanayatuhumu kwamba yamekuwa yakihusika katika kuwateka raia na kisha kuwaua. Matendo yote yanayofanywa na hao Watu Wateule wake ni sawa sawa kabisa kwamba ameyafanya yeye mwenyewe Mteuaji binafsi. Kushindwa kwa hao Watu ambao amewateua ndio kushindwa kwake yeye Mteuaji. Kwa hiyo kwa namna yoyote ile kamwe hawezi akajitenga na matendo mazuri au mabaya yanayofanywa na Wateule wake.

Aidha, hata tuhuma anazotupiwa za kuhusika na tukio la jaribio la mauaji ya Tundu Lissu kule Dodoma yeye pia tuhuma hizo zinamhusu Moja kwa Moja. Rais Magufuli siyo Mtuhumiwa pekee wa shambulizi lililofanywa dhidi ya Tundu Lissu, hata yeye pia anahusika kwa sababu Serikali ya 'MaguSami' (i.e. Magufuli+Samia) ndio iliyokuwa madarakani wakati ule tukio hilo lilipotokea.
 
Mungu wa Mbinguni azidi kukubariki mh Rais Samia 🌹


Tatizo ni hawa akina Mwagito Chalamila maelezo yao hawayanyooshi Sawa Sawa

Ila kiukweli hili swala la kushambuliwa Mwenyekiti ambaye ni Rais wa JMT halikubaliki kabisa!
Wewe nawe ni hueldweki tu.
 
Maza hajui kama anaua indirectly kwa kuwajibika au kutowajibika kama Amir Mkuu na Rais wa JMT!
 
We msimamo mkali embu acha kutetea mauaji... Hao watu wasiojulikana wanajulikana na wanapewa vyeo usijidai mwehu kamavile huelewielewi!!
Mungu huona vya ndani kabisa rohoni,kama unamwabudu katika kweli tubu tuu LAKINI kama unazugazuga tuu basi zuga uje hapa Torokauje bar tupige kitimoto na konyagi afu twende pale Kajificheni gestihausi tukapige pushapu😘
Anabugia sana Kitimoto huyo
 
Hutokuja kuiona hiyo, umesikia hata wakitoa mrejesho! wangapi wamekamatwa kusaidia uchunvuzi? {unakumbuka alipotekwa Mo walivyokuwa wanatoa mrejesho}
sasa kwa kisa hiki ilitakiwa mrejesho na mikwala ya police iwe vile , ukimya huu jiongeze ndio imepita hiyo. Nilitegemea huyu mama kuwa kazi itakamilika soon na lipoti itawekwa wazi, ila kamfananisha alieuawa na sisiminzi. Yaani yeye kaua sisiminzi asisakamwe... mwee
Ukimya means waliofanya ni "WATU WASIOJULIKANA".
 
Mungu wa Mbinguni azidi kukubariki mh Rais Samia 🌹


Tatizo ni hawa akina Mwagito Chalamila maelezo yao hawayanyooshi Sawa Sawa

Ila kiukweli hili swala la kushambuliwa Mwenyekiti ambaye ni Rais wa JMT halikubaliki kabisa!
Mwagito ndaule
 
Back
Top Bottom