Rais Samia: Simba alikuwa hatulii kama ‘Mwanangu Lissu’, ndio maana nikasema apewe jina hilo

Rais Samia: Simba alikuwa hatulii kama ‘Mwanangu Lissu’, ndio maana nikasema apewe jina hilo

Anachoweza kukumbukwa lisuu ni
lisuu ni nani kwanza ??
mimameno yake ya ubaguzi, uchochezi na matusi tu.
Lissu kachochea nini?

Lissu kambagua nani?

Mbaguzi ni nani kama sio Samia anayefukuza watu kwenye ardhi yao ya asili huku Lissu akikemea wazi ubaguzi huo sasa hapo mbaguzi nani?

Naungana na mchangiaji mmoja aliyeomba machawa mjengewe uwezo [capacity building] kwenye kujibu hoja baada ya kupandisha mabandiko na mpunguze hizo lullabies.
Lakini Rais wetu amefanya mambo mengi ambayo hayawezi kufutika wala kufutwa na yeyote yule katika Taifa letu.
Yapi ?

Hebu orodhesha 10 tu!
Ni Mama Samia Rais wetu mpendwa ndiye amefanya Elimu kuwa bure kabisa hadi kidato cha sita.ambapo sasa watoto wanasoma kwa furaha na matumaini makubwa sana ya kutimiza ndoto zao.
Elimu bure sio kigezo mmechelewa sana na sikulaumu wewe sababu watanzania wengi exposure ni ndogo.

Mimi nimewahi kutembelea nchi kadhaa elimu ni bure sababu inagharamiwa na kodi za wananchi na si kitu cha kumpa heko mtawala.

Usikute wewe licha ya kuwa Mbeya hujawahi hata kufika nchi jirani kama Malawi na Zambia tu .
Ni Mama Samia Rais wetu mpendwa ambaye ametoa maelfu kwa maelfu ya ajira kwa vijana kila mwaka tangia
Ajira zipi ?

Unaweza kuweka takwimu hapa?

Maana vijana hao hao ndio tunaona humu wamegeuka kujiita "maafisa ubashiri" je kamari ni ajira rasmi,?

Malalamiko ya ajira yamo lukuki humu.
ameingia madarakani.ni Mama Samia amepandisha bajeti ya kilimo kutoka Billion 250 hadi Trilioni 1.2.
Hizi pesa anatoa wapi yeye kama rais?

Hizo ni kodi na tozo wanazolipa wananchi ,rais hana hizo pesa na sio zake hivyo hastahili sifa yoyote hapo wapongezwe watu kwa kulipa kodi sio mtawala.
ni Rais Samia Mama yetu Mpendwa ameweka rekodi ya kuzindua mradi wa treni ya mwendo kasi ,kukamilisha bwawa la mwalimu Nyerere ambalo alilikuta likiwa 34% .
Kuzindua mradi nacho ni kitu cha kujisifia ?

Hizo pesa za kugharamia mradi zimetoka wapi?

Nani watalipia gharama za huo mkopo wa kujenga hiyo miradi kama sio watumiaji wa mwisho ambao ni wananchi?

Samia tangu amezindua hiyo treni kapanda lini tena , mfano huko Kizimkazi alipokuwepo wiki nzima kwenye bonanza alienda na treni ?

Kuzindua sio jambo la kupongezwa hakuna sifa yoyote kwenye kuzindua bali wanaotakiwa kujipongeza ni wanachi kodi zao ndio zimejenga mradi huo uwanufaishe wao.

Je Samia mbona ameshindwa kudhibiti wizi ambao magenge ya wezi yanachepusha makusanyo ya kodi kwenda katika njia zisizo rasmi?

Au kwenye mambo ya wizi , ubadhirifu,matumizi mabaya ya ofisi sio uongozi wa Samia au huko Tanzania ni ya rais mwingine na sio Samia?
IMG_20240611_163734.jpg
 
..Ni Simba wa Tanganyika.

..Zanzibar na Kizimkazi hakuna Simba.

..Jina lingine ambalo Lissu amepewa na Wazanzibari ni "Ronaldo."
Lissu amekosa ushawishi kwa watanzania na ndio maana mpaka leo anahangaika na michango ya kununua gari .wakati angekuwa anakubalika kwa watanzania angekuwa amepata hata billion moja mpaka muda huu.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan ni mwanasayansi wa sayansi ya siasa kiasili.

Ni kiongozi anayeijuwa vyema sana sayansi ya siasa.ni kiongozi ambaye anajuwa kucheza na lugha na maneno Utafikiri magwiji na mafundi ya mpira aina ya christian Ronaldo,Lionel Messi ,Ronaldinyo ,Pele ,JJ OKocha walivyokuwa wanajuwa kuuchezea mpira mpaka mpira wenyewe unatulia katika miguu yao kwa heshima na adabu na kutoa salute .

Sasa hapo jana baada ya Rais Huyu nguli na jabali wa siasa kutamka kuwa Simba aliyekuwa anaruka ruka na kushindwa kutulia utafikiri karatasi inayopulizwa na upepo apewe jina la Lissu ,wafuasi kiduchu wa Lissu wakaanza kuvimba vichwa Utafikiri wameng'atwa na nyigu au nyuki Juani. Kuwa RAIS Samia anamuwaza sana Lissu na kumuogopa kuelekea uchaguzi Mkuu hapo Mwakani.

Wengine wakafikia hatua hadi ya kuanza eti kutoa tafsiri zao kuhusu Simba na maana yake kibiblia ilimradi tu wapooze na kupata faraja ya kujifariji hasa baada ya kujuwa kuwa Lissu kwa kiasi kikubwa hakubaliki kwa watanzania wala kuungwa mkono.

Hii ni kutokana na tabia yake mbaya ya uropokaji,mihemuko na lugha zake mbaya na zenye kuchocheo ubaguzi katika Taifa letu.lakini kubwa zaidi ni kukosa kwake adabu kama ambavyo tulishuhudia akitukana viongozi wetu wengi sana wenye heshima katika Taifa letu akiwepo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliyetukanwa kwa mdomo huohuo wa Lissu ambao umekuwa na maneno ya ukigeugeu kama kinyonga.

Na hapa mnaweza pia kukumbuka namna pia alivyomdhalilishaga Hayati Edward lowassa kabla ya kuja CHADEMA na kugombea Uraisi .

Sasa Rais wetu amesema kuwa Simba yule alisema apewe jina la Lissu kwa sababu aliona Simba yule hajatulia hata kidogo.kama ambavyo Mliona simba yule alikuwa anaruka ruka na hajatulia.

Nami Mwashambwa namuunga kabisa mkono Mheshimiwa Rais kuwa Lissu hajatulia kabisa na ndio maana anakosa Busara na hekima hata katika kuzungumza kwake ,maana utulivu wa mtu ukiwa mzuri inapelekea hata kauli na maneno yake kujaa kwa hekima na Busara.lakini mtu ambaye hajatulia aina ya Lissu ndio sababu huona akitoa neno lolote linalomjia mdomoni pake bila hata kulichuja wala kufikiria Kabla ya kulitoa.

Mwisho ni kuwa kamwe na katu Lissu hawezi kupata kura hata nusu tu ya kura za Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan mgombea Urais wa CCM hapo Mwakani.kamwe lisuu hawezi kuwa Rais wa Taifa hili hata kama angekuwa ndani ya CCM hawezi kupewa nafasi ya kugombea Uraisi.View attachment 3079010

Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Kuna ubaguzi mbaya kama mama aliowafanyia Massai? Avae kijola aende kwenye...... Hastaili kuwa ikulu
 
..wanaohangaika nchi hii wako wengi sana nini kimemfanya Samia amkumbuke Tundu Lissu na kuwaacha wengine?

..Samia, Nchimbi, Makalla, na viongozi kadha wa kadha wa serikali na Ccm wote hawaishi kumtaja Tundu Lissu. Kwanini?

..Kwa maoni yangu, kipaji cha siasa, na ujasiri ktk kutetea wananchi, ndio sababu ya Lissu kuwa ktk kichwa, na kinywa cha Samia Suluhu, na wengi hapa nchini.
Ni usajili ambao CCM wanautaka leo, kesho na keshokutwa……
 
Yani Mh kila mtu nchi hii anamuona kama mwanae.

Kazaliwa 1960, Lissu 1968, ni mwanae kivipi?
Huyo ni mkuu wa nchi ni mama wa nchi hii, hata uwe mzee kiasi gani automatically anakuwa ni mama yako.
 
Ni usajili ambao CCM wanautaka leo, kesho na keshokutwa……

..Nchi hii inahitaji USHINDANI baina ya vyama vya siasa.

..Tunahitaji kufika mahali ambapo uchaguzi ukiitishwa hakutakuwa na uhakika chama kipi kitashinda.

..Sasa hivi kila sehemu wameshika Ccm ndio maana wanachezea pesa kurubuni wapinzani.
 
Tundu anaweza kuwa mtoto wa Samia,I mean kiumri kwamba anaweza kumzaa?
 
..Nchi hii inahitaji USHINDANI baina ya vyama vya siasa.

..Tunahitaji kufika mahali ambapo uchaguzi ukiitishwa hakutakuwa na uhakika chama kipi kitashinda.

..Sasa hivi kila sehemu wameshika Ccm ndio maana wanachezea pesa kurubuni wapinzani.
Hakuna mwenye akili Timamu na anayejitambua vizuri anayeweza kupoteza muda wake kushabikia upinzani. Upinzani na wapinzani ni wasaka Tonge tu na wachumia tumbo.ndio maana wenye akili Timamu na wanaojitambua wanaondoka CHADEMA kila siku kuja CCM
 
lisuu ni nani kwanza ??

Lissu kachochea nini?

Lissu kambagua nani?

Mbaguzi ni nani kama sio Samia anayefukuza watu kwenye ardhi yao ya asili huku Lissu akikemea wazi ubaguzi huo sasa hapo mbaguzi nani?

Naungana na mchangiaji mmoja aliyeomba machawa mjengewe uwezo [capacity building] kwenye kujibu hoja baada ya kupandisha mabandiko na mpunguze hizo lullabies.

Yapi ?

Hebu orodhesha 10 tu!

Elimu bure sio kigezo mmechelewa sana na sikulaumu wewe sababu watanzania wengi exposure ni ndogo.

Mimi nimewahi kutembelea nchi kadhaa elimu ni bure sababu inagharamiwa na kodi za wananchi na si kitu cha kumpa heko mtawala.

Usikute wewe licha ya kuwa Mbeya hujawahi hata kufika nchi jirani kama Malawi na Zambia tu .

Ajira zipi ?

Unaweza kuweka takwimu hapa?

Maana vijana hao hao ndio tunaona humu wamegeuka kujiita "maafisa ubashiri" je kamari ni ajira rasmi,?

Malalamiko ya ajira yamo lukuki humu.

Hizi pesa anatoa wapi yeye kama rais?

Hizo ni kodi na tozo wanazolipa wananchi ,rais hana hizo pesa na sio zake hivyo hastahili sifa yoyote hapo wapongezwe watu kwa kulipa kodi sio mtawala.

Kuzindua mradi nacho ni kitu cha kujisifia ?

Hizo pesa za kugharamia mradi zimetoka wapi?

Nani watalipia gharama za huo mkopo wa kujenga hiyo miradi kama sio watumiaji wa mwisho ambao ni wananchi?

Samia tangu amezindua hiyo treni kapanda lini tena , mfano huko Kizimkazi alipokuwepo wiki nzima kwenye bonanza alienda na treni ?

Kuzindua sio jambo la kupongezwa hakuna sifa yoyote kwenye kuzindua bali wanaotakiwa kujipongeza ni wanachi kodi zao ndio zimejenga mradi huo uwanufaishe wao.

Je Samia mbona ameshindwa kudhibiti wizi ambao magenge ya wezi yanachepusha makusanyo ya kodi kwenda katika njia zisizo rasmi?

Au kwenye mambo ya wizi , ubadhirifu,matumizi mabaya ya ofisi sio uongozi wa Samia au huko Tanzania ni ya rais mwingine na sio Samia?View attachment 3079078
Haya mambo uliyomuuliza huyu chawa hawezi kukujibu kwa ufasaha. Huwa hawezi kujenga hoja bali anasifia tu.
 
Back
Top Bottom