Rais Samia Suluhu ahutubia Mabunge ya Kenya: Biashara kushamiri, Vikwazo Mipakani kutatuliwa, Udugu kudumishwa

Rais Samia Suluhu ahutubia Mabunge ya Kenya: Biashara kushamiri, Vikwazo Mipakani kutatuliwa, Udugu kudumishwa

Ayubu (Job) anune lakini ni kweli kuwa ukilinganisha mabunge haya mawili - uhuru wa Bunge unaonekana kuwa mkubwa Kenya kuliko hapa. Kenya kila jambo linaweza kusemwa Bungeni na mbunge kupata kinga stahiki. Hapa kwetu utasikia “futa kauli” au “maneno ya kuudhi” au “hotuba ya upinzani haitasomwa kwa sababu ina maneno yasiyotakiwa”!!

Bunge la Kenya ninaihoji na kuibana serikali kwa sababu mawaziri (secretaries) hawatoki miongoni mwa wabunge. Hapa nyumbani, mawaziri wanaogopwa na wabunge kwa sababu nao ni wabunge pia!! Kila mbunge anapalilia siku moja kuteuliwa kuwa waziri kwa hiyo anakosa hari na moyo wa kuikosoa serikali!!
This must change.Ministers must not come from among members of the parliament.
 
Rais Samia amemshukuru Spika wa Bunge la Kenya kwa kumpa heshima ya kuhutubia Mabunge mawili ya nchi hiyo kwa pamoja.

Rais Samia amesema yeye ni Rais wa pili kutoka Tanzania kupewa heshima ya kuhutubia bunge hilo linaloheshimika duniani akiwa ametanguliwa na Mstaafu Jakaya Kikwete.

Rais Samia amesema Bunge la Kenya linavutia kwa upana wa demokrasia yake.

Kazi Iendelee!
Ukiona vyaelea, vimeundwa. Wenzetu Kenya walipambana sana mpaka wakapata katiba mpya. Ukiwa na Katiba nzuri, unaondoa ujinga, upumbavu na upuuzi mwingi tu. Mfano, Kenya mbunge anaweza kabisa kuondolewa bungeni na wapigakura wake. Hapa kwetu chama tawala tu ndio kinaweza kumtoa mbunge awe wa ccm ama hata wa upinzani, kwa kumtumia spika ambaye ni kada mwandamizi wa ccm.

Tumeona kina Mwambe wakirejeshwa bungeni kwa ubabe tu. Sasa katika hali hiyo mbunge lazima anyenyekee kwa spika.

Mama Samia ndio mtu sahihi wa kutuletea Katiba mpya, sio Magu. Huyo angetuletea Magumashi tu ya katiba pendekezwa
 
Hana jipya zaidi ya kujipendekeza huko, yuko katika fast track ya kuuza na kuruhusu kila ujinga nchini.
We ni Timu Jiwe naona bado unaota ndoto za alnacha!!!
Hayati hatorudi tena keshaenda zake kwa muumba wake....!!!
 
Yaani mtu akipata cheo anafikiri yeye anajua kuliko wote na mamlaka ni yake tu
Bunge letu linaongozwa na kichaa mmoja hivi. Mhe. SSH anapaswa kumshauri Spukali Ndugai arudi tena India kwa matibabu zaidi....!!!!
 
Ukiona vyaelea, vimeundwa. Wenzetu Kenya walipambana sana mpaka wakapata katiba mpya. Ukiwa na Katiba nzuri, unaondoa ujinga, upumbavu na upuuzi mwingi tu. Mfano, Kenya mbunge anaweza kabisa kuondolewa bungeni na wapigakura wake. Hapa kwetu chama tawala tu ndio kinaweza kumtoa mbunge awe wa ccm ama hata wa upinzani, kwa kumtumia spika ambaye ni kada mwandamizi wa ccm.

Tumeona kina Mwambe wakirejeshwa bungeni kwa ubabe tu. Sasa katika hali hiyo mbunge lazima anyenyekee kwa spika.

Mama Samia ndio mtu sahihi wa kutuletea Katiba mpya, sio Magu. Huyo angetuletea Magumashi tu ya katiba pendekezwa
Ndugai ni mgonjwa na bado hajamwelewa Rais Madame Suluhu......ni shidaaaa!!!
Ndugai ni saloon bovu kabisa la hayati Jiwe!!!
Mfumo dume hewa... Analazimisha tuone kitu ambacho hakipo😂🤣
Msimulaumu mama wa Watu, Katiba ndo imemwingiza siyo mfumo Jike. Nyie lieni na Hayati Jiwe ndiye aliyewachomekea Makamu Jike....!!!
 
Hebu nikuulize jambo, baada ya sifa kemkem hizi:

Hujasahau kitu (jambo) hapo, au ni siri ya baadae, hapo unaposema "Mungu ampe miaka mingi...", ili atawale 10, au mitano zaidi?
Hata hiyo 10 anayostahili anatakiwa kuombewa. Mwingine miaka 5 na miezi hivyo ni lazima tumuombee. Kila awamu ni 10 yrs. Au wewe unataka muda gani wa kwako?
 
Hata hiyo 10 anayostahili anatakiwa kuombewa. Mwingine miaka 5 na miezi hivyo ni lazima tumuombee. Kila awamu ni 10 yrs. Au wewe unataka muda gani wa kwako?
Hapana, sio "muda wa kwangu", ni wa kwako, uliyemwaga sifa. Mi nilidhani 20, au 30 hivi kama sio zaidi ndiyo ingeendana na sifa nyingi ulizommwagia!
Au unasemaje?
 
Hapana, sio "muda wa kwangu", ni wa kwako, uliyemwaga sifa. Mi nilidhani 20, au 30 hivi kama sio zaidi ndiyo ingeendana na sifa nyingi ulizommwagia!
Au unasemaje?
Hata akiwa Rais wa maisha kwangu ni sawa tu ili mradi tunakuwa na Amani, Uhuru na uchumi usio na matabaka. Sitaki kuongea mengi hapa ila acha Mungu aitwe Mungu na Mungu ni fundi na si Fundi Mchundo. Tuishie hapa
 
Hata akiwa Rais wa maisha kwangu ni sawa tu ili mradi tunakuwa na Amani, Uhuru na uchumi usio na matabaka. Sitaki kuongea mengi hapa ila acha Mungu aitwe Mungu na Mungu ni fundi na si Fundi Mchundo. Tuishie hapa
Hata angekuwa kiongozi mzuri kiasi gani, hawezi kuendelea kuwa mzuri kama atasubiri hadi kifo kimchukue.

Hiyo sehemu ya sentensi yako inayohusu "kuwa na uhuru na amani, uhuru na uchumi (usio na matabaka?)"; hata mimi hayo ningeyapenda sana, ingawaje kukosekana matabaka ni ngumu sana popote pale.

Lakini mkuu 'Zogwale' kwa matakwa yako haya, unasahau haya mapya ya "kufungua nchi"?

Utawezaje kupata hayo unayoyatamani kama tutakuwa watu wa kunyang'anyana hata hicho kidogo kitakachopatikana, ambacho sehemu yake kubwa hutakiona kwa vile waliofunguliwa njia ndio watakaokuwa wanafaidika nacho?

Umesikia mahali popote akieleza njia atakazotumia kuhakikisha kwamba hata majambazi hayaji kutunyang'anya kidogo tunachotakiwa kubaki nacho ili na sisi kitufaidishe?
Hili ndilo ninalolisubiri kwa hamu kulisikia toka kwake.

Akifanya hivyo, huenda nami nitakuwa naomba sana kama unavyofanya wewe.
 
Hata angekuwa kiongozi mzuri kiasi gani, hawezi kuendelea kuwa mzuri kama atasubiri hadi kifo kimchukue.

Hiyo sehemu ya sentensi yako inayohusu "kuwa na uhuru na amani, uhuru na uchumi (usio na matabaka?)"; hata mimi hayo ningeyapenda sana, ingawaje kukosekana matabaka ni ngumu sana popote pale.

Lakini mkuu 'Zogwale' kwa matakwa yako haya, unasahau haya mapya ya "kufungua nchi"?

Utawezaje kupata hayo unayoyatamani kama tutakuwa watu wa kunyang'anyana hata hicho kidogo kitakachopatikana, ambacho sehemu yake kubwa hutakiona kwa vile waliofunguliwa njia ndio watakaokuwa wanafaidika nacho?

Umesikia mahali popote akieleza njia atakazotumia kuhakikisha kwamba hata majambazi hayaji kutunyang'anya kidogo tunachotakiwa kubaki nacho ili na sisi kitufaidishe?
Hili ndilo ninalolisubiri kwa hamu kulisikia toka kwake.

Akifanya hivyo, huenda nami nitakuwa naomba sana kama unavyofanya wewe.
Ningekuwa mmoja wa washauri wa Rais hakika ningetumia brain yangu mpaka mwisho katika kumshauri kuhusu uwekezaji unaoshirikisha wananchi wenye uwezo. Yaani suala la Local content. Nchi za Falme za Kiarabu walifanikiwa sana kwenye hili. Na open up ya uchumi inatakiwa ifanye kwa uangalifu na kwa hatua ili kujifunza from the past phase ili uboreshe the next. Sasa kwa kuwa mambo ya nchi hii ni kitendawili sana huwa anapenda focus ya maisha yangu kwa kupambana. Kifupi I hate poverty so personally I do fight as most collective policies have failed. Tumelogwa na nani Mkuu Kalamu1
 
kuhusu uwekezaji unaoshirikisha wananchi wenye uwezo. Yaani suala la Local content. Nchi za Falme za Kiarabu walifanikiwa sana kwenye hili. Na open up ya uchumi inatakiwa ifanye kwa uangalifu na kwa hatua ili kujifunza from the past phase ili uboreshe the next
Usisahau, utakapokuwa unamwombea, omba haya uliyoandika hapa juu yamwingie akilini mwake na ayatimize kwa umakini mkubwa.

Hahitaji kufanya mambo makubwa sana kujiwekea sifa ya kuwa kiongozi mzuri.
 
Ndugai ni mgonjwa na bado hajamwelewa Rais Madame Suluhu......ni shidaaaa!!!
Ndugai ni saloon bovu kabisa la hayati Jiwe!!!

Msimulaumu mama wa Watu, Katiba ndo imemwingiza siyo mfumo Jike. Nyie lieni na Hayati Jiwe ndiye aliyewachomekea Makamu Jike....!!!
Binafsi sina shida na mama...

Ninampenda na kumuombea sana kwa Mungu... Kwa sasa bado ana kazi ya kufagia kivuli cha jiwe na hatuwezi kujua mwelekeo wake kwa sasa kwani ni mapema mno... Tutakuwa kwenye nafasi ya kum-judge kuanzia mwakani muda kana huu baada ya kuona maneno na matendo yake.
 
Back
Top Bottom