Rais Samia Suluhu aitaka Wizara ya Habari kuvifungulia Vyombo vya Habari vilivyofungiwa. Avitaka kufuata Sheria na Kanuni

Rais Samia Suluhu aitaka Wizara ya Habari kuvifungulia Vyombo vya Habari vilivyofungiwa. Avitaka kufuata Sheria na Kanuni

Tanzania ya amani, uhuru, upendo na kuthamini utu imerejea tena. Mungu aliamua mwanadamu hawezi kupinga. Tanzania ni taifa la Mungu na hakuna yeyote ataliyumbisha abaki salama. Iwe fundisho atakayekuja baada ya Rais wetu Mpendwa Mh. Samia S. Hassan asilete mchezo.
 
Mara paap Maxence Melo naye kafungulia Majukwaa yake na kusisitiza Sheria zifuatwe adhabu zitafuta tukizinguana.
Huyu jamaa yetu aliteseka sana kwa ajili ya kucover majina yetu, alikuwa na kesi nyingi kuliko za Tundu Lissu akitetea uhuru wa Habari
 
Upinzani umeshakufa Tanzania. Kupitia haya anayofanya mama yetu,Sijui watakosoa nini tena.
 
Mwanahalisi, Mawio na TanzaniaDaima navyo vitafunguliwa kweli
 
Vifunguliwe na wafuate taratibu

Habari na taarifa ni muhimu sana kwa jamii

Wakianza kuandika tena habari za uchochezi na kuhamasisha hujuma kwa nchi yetu washughulikiwe ipasavyo
Wanaanzia wapi kumfanyia mama hujuma, mama ni msafi hana mawaa.

Wazanzibari wana utu sana.sio kina sir buyer.
 
Huyu mama tangu siku ya kwanza nilijua tu atakuja kuiharibu nchi.
Screenshot_20210406-123928.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Rais Samia Suluhu ameiagiza Wizara ya Habari kuvifungulia vyombo vya habari vilivyofungiwa, na kuhakikisha vinafuata sheria. Aidha, ameagiza sheria kanuni na adhabu ziwe wazi, ifahamike kosa fulani adhabu yake ni fulani, ili isionekane kuwa serikali inaminya uhuru wa habari.

Rais Samia amesema haya...

Wizara ya habari, mnapaswa kusimamia vyombo vya habari, nasikia kuna vyombo vya habari mmevifungia, vifungulieni lakini vifuate sheria na kanuni. Tusiwape mdomo mdomo wa kusema tunabinya uhuru wa habari na nataka kanuni ziwe wazi. Tusifungie tu kibabe

Hallelujah!!
 
Back
Top Bottom