Rais Samia Suluhu amepokea hundi ya Dola Milioni 30 kutoka kwa Barick Gold Mine

Rais Samia Suluhu amepokea hundi ya Dola Milioni 30 kutoka kwa Barick Gold Mine

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Rais Samia Suluhu amepokea hundi ya Dola Milioni 30 (Bilioni 70) kutoka kwa Barick Gold Mine kwa ajili ya ujenzi madarasa nchi nzima hasa kwa ajili ya Wanafunzi wa kidato cha 5 na 6 watakaoanza masomo katika muhula ujao wa masomo

Rais Samia ameeleza kuwa kwa sasa wanafunzi watakaomaliza masomo mwezi Juni ni 72000 lakini wale wanaotarajiwa kuanza kidato cha 5 wakiwa ni zaidi ya 192000 hivyo kuwa na ongezeko la wanafunzi zaidi ya 120000

Rais Samia amewaomba watanzania wengine kuunga mkono jitihada za serikali huku akisisitiza kuwa kwa sasa suala la madarasa watakayosoma watoto wa Kitanzania wa kidato cha 5 kwa muhula ujao wa masomo ndilo suala linalomnyima usingizi kwa sasa.

Katika mchango walioutoa Barick utawasilishwa kwa awamu tatu tofauti wakianza na kutoa Dola Milioni 10.
 
Rais Samia Suluhu amepokea hundi ya Dola Milioni 30 (Bilioni 70) kutoka kwa Barick Gold Mine kwa ajili ya ujenzi madarasa nchi nzima hasa kwa ajili ya Wanafunzi wa kidato cha 5 na 6 watakaoanza masomo katika muhula ujao wa masomo
Mwambie hakuna kitu kama hicho na hasitafute huruma kwa watanzania anaowanyonya kila siku kupitia viongozi waka hasa M.Rameck Ester big stars, Anakosaje hela ya kujenga madarasa wakati anapata hela ya kununua gori moja 5mln?

Akikujibu, mijadala ianzie hapo.
 
Mwambie hakuna kitu kama hicho na hasitafute huruma kwa watanzania anaowanyonya kila siku kupitia viongozi waka hasa M.Rameck Ester big stars,Anakosaje hela ya kujenga madarasa wakati anapata hela ya kununua gori moja 5mln?

Akikujibu, mijadala ianzie hapo.
Hebu tulia, andika vizuri kwa mtiririko sahihi ueleweke
 
Net income XXX
Less C.A XXX
Add T. I XXX
Less
Qualified C.D. XXX
Taxable income. XXX

Hiyo hela na wao wanaitoa kwenye kodi kama ‘qualified charitable donation’ halafu kwanini waseme watatoa kwa awamu, kiasi gani watandika kwenye hesabu zao mwaka huu $10m au $30m?

Serikali inatakiwa kuwa makini hayo mambo yana mbinu zake kwenye kutengeneza losses na kutafuta tax rebate; hasa kwa nchi kama Tanzania ambapo taasisi nyingi hazifuati IFRS kwenye kuandaa financial statement zao.

Inasikitisha sana nchi inapoelekea ni wazi hapo kuna sarakasi za kukwepa kodi.
 
Rais Samia Suluhu amepokea hundi ya Dola Milioni 30 (Bilioni 70) kutoka kwa Barick Gold Mine kwa ajili ya ujenzi madarasa nchi nzima hasa kwa ajili ya Wanafunzi wa kidato cha 5 na 6 watakaoanza masomo katika muhula ujao wa masomo

Rais Samia ameeleza kuwa kwa sasa wanafunzi watakaomaliza masomo mwezi Juni ni 72000 lakini wale wanaotarajiwa kuanza kidato cha 5 wakiwa ni zaidi ya 192000 hivyo kuwa na upungufu wa madarasa zaidi 120000

Rais Samia amewaomba watanzania wengine kuunga mkono jitihada za serikali huku akisisitiza kuwa kwa sasa suala la madarasa watakayosoma watoto wa Kitanzania wa kidato cha 5 kwa muhula ujao wa masomo ndilo suala linalomnyima usingizi kwa sasa.

Katika mchango walioutoa Barick utawasilishwa kwa awamu tatu tofauti wakianza na kutoa Dola Milioni 10.
Hao 72000 wanamaliza kidato gani?
 
Kwenye ujenzi wa vyumba vya madarasa kuna 'upigaji'mwingi sana.
Nadhani wahusika wameshajua udhaifu wa serikali yao.
Ni afadhali kujenga viwanda hata kama wanafunzi wakisomea chini ya mti, wakimaliza wapate ajira.

Kila fedha kuelekezwa kwenye ujenzi wa vyumba vya madarasa kuna tatizo mahali
 
Rais Samia Suluhu amepokea hundi ya Dola Milioni 30 (Bilioni 70) kutoka kwa Barick Gold Mine kwa ajili ya ujenzi madarasa nchi nzima hasa kwa ajili ya Wanafunzi wa kidato cha 5 na 6 watakaoanza masomo katika muhula ujao wa masomo

Rais Samia ameeleza kuwa kwa sasa wanafunzi watakaomaliza masomo mwezi Juni ni 72000 lakini wale wanaotarajiwa kuanza kidato cha 5 wakiwa ni zaidi ya 192000 hivyo kuwa na upungufu wa madarasa zaidi 120000

Rais Samia amewaomba watanzania wengine kuunga mkono jitihada za serikali huku akisisitiza kuwa kwa sasa suala la madarasa watakayosoma watoto wa Kitanzania wa kidato cha 5 kwa muhula ujao wa masomo ndilo suala linalomnyima usingizi kwa sasa.

Katika mchango walioutoa Barick utawasilishwa kwa awamu tatu tofauti wakianza na kutoa Dola Milioni 10.
Barrick Gold ni nani mpaka watoe hizo hela kwa ajili ya ujenzi wa madarasa! Kama ni mgao wa faida si inatolewa halafu serikali inaamua kiasi gani kitumike kwenye hili ama lile? Inakuwa kama vile tunapewa msaada na Barrick wakati ni gawio tena la kiwizi mkubwa. Dah!
 
Ndio hivyo kodi zetu zinakwenda kujenga madarasa kwa wanafunzi wa watoto wa Kitanzania
Hujawai kulipa kodi na hautokuja lipa kodi,hiyo simu unatumia humu umenunuliwa,vocha unawekewa so hujui lolote.
Ssh hajafanya lolote mnamsifia bure.
 
Sio mchango. Ni pesa yetu kupitia kampuni yetu ya twiga. Hayo ni moja ya matunda ya Magufuli na Kabudi. Ila hawatasema.

..Magufuli aliwasamehe wizi wa usd 191 billion.

..leo Barrick wanatupa usd 10 million tena kwa awamu!!

..tukisema Magufuli alikuwa KIBARAKA tutakuwa tumekosea?
 
Zamani vyumba vya madarasa vilijengwa kwa nguvu za wananchi na serikali ilijikita kwenye kupaua na finishing pamoja na kuajiri walimu.

Leo hii kila fedha ni kujenga vyumba vya madarasa. Hao wanafunzi wakimaliza wanakosa hata pa kujishikiza angalau kupata kipato, matokeo yake wanakuwa 'maafisa usafirishaji'

Tumeshuhudia mahali pengine vyumba vimejengwa vingi lakini hakuna wanafunzi. Matokeo yake yanakuwa kama maghofu. Huu ni ubadhilifu wa mali ya umma.
 
Barrick Gold ni nani mpaka watoe hizo hela kwa ajili ya ujenzi wa madarasa! Kama ni mgao wa faida si inatolewa halafu serikali inaamua kiasi gani kitumike kwenye hili ama lile? Inakuwa kama vile tunapewa msaada na Barrick wakati ni gawio tena la kiwizi mkubwa. Dah!
Gawio lako au kodi ya serikali unapangiwa utumie vipi?

Hiyo ni donation ndio maana inaenda mahala maalum, na wanaitoa kwenye faida yao kabla ya kodi huko mbele its legal expenses before taxation.

Hakuna serikali makini inaweza pokea charity kama hiyo ni kuchochea ukwepaji kodi.

Halafu watu wanakwambia Nehemia ni financier ‘my foot’ yaani amepelekwa hazina kushauri ujinga.
 
Back
Top Bottom