Rais Samia Suluhu, Waganda wamekupigia 'Salute' kwa Kiingereza chako kizuri japo huna PhD yoyote

Rais Samia Suluhu, Waganda wamekupigia 'Salute' kwa Kiingereza chako kizuri japo huna PhD yoyote

Madame President ameijengea heshima kubwa Nchi yetu ya Tanzania kwa jinsi alivyotumia jukwaa la Kimataifa vizuri hasa kwenye matumizi ya Lugha ya kimataifa -ENGLISH huko Uganda. Kiingerea cha Madam President ni kiwango cha juu, ukimsikiliza kwa umakini, ni English ya akina Obama, Nyerere au Ben Mkapa; Vijana wetu wamehamasika kusoma English kwa manufaa yao na kwa mataifa ya jirani. Itakuwa ni makosa kutaka kuwaaminisha watu kuwa kiingereza sio kizuri au uzalendo ni kukikujua kiswahili tu; Dira ya Taifa ya MAENDELEO ya 2025 inasema kuwa tunakwenda kujenga "middle class society which is very competitive"you can not compete by having a monolanguange instead of multilingua citizens.
Hongera sana Madame President kwa kutujajua juu ya mawingu in East Africa community.
 
Nyie vilaza hamumuwezi kwa hisabati huyo mama.
Ina maana hata Polepole hafui dafu na zile hesabu zake kudiskraibu za madiagram na kumachua 1.5T?? 😂

Everyday is Saturday................................😎
 
Ningeshangaa sana kama Uzi huu usingevamiwa na wasiokijua ' Kiingereza ' na najua mtajitokeza wengi tu.

Ninachojua tu ni kwamba duniani kuna Lugha nyingi na nzuri ila hakuna ambayo hadi hivi leo imeweza kuwa ni Kiungo ' Kikuu ' cha Mataifa yote duniani iwe Kiuchumi na hata Kidiplomasia kama cha Kiingereza.

Kama Mchina, Mrusi, Mjerumani na Mchina pamoja na Jeuri zao zote za kuwa ' Super Powers ' ulimwenguni na Lugha zao pia ni Kubwa lakini bado hao hao wanakizungumza Kiingereza Wewe Mpuuzi Mmoja wa Kiswahili usiye na mbele wala nyuma ni nani ukipinge?

Itatuchukua muda mrefu sana na huenda pia hata isitokee kwa Mataifa mengi duniani Kuachana na Lugha ya Kiingereza kwani kama kuna Mafanikio makubwa ambayo nchi ya Uingereza ilipata tokea Kipindi cha ' Colonialism ' ni kuhakikisha Lugha yao si tu inaendelea kutumika bali pia inapendwa na kuendelea Kuaminiwa na Vizazi na Vizazi.

Kama Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere pamoja na kutowakubali Wazungu ( hasa kwa Sera zao na Matendo yao kwa Waafrika ) lakini Mwenyewe kwa Mdomo wake ( na Clips zipo Mitandaoni ) alikiri kuwa Kiingereza ni Lugha muhimu, siyo ya Kuepukwa duniani na ya Kibiashara zaidi.
Unajiita generalist wakati you are specificity...actually we are not oppose the fact that english lang.is the most popular one and one should atleast understand it. The point is, why should we scorn someone who doesn't know it properly?? You can't compare an english man with the non-english..we should not consider english as a measure of intelligence as you consider it.
Shame on you specificity.
 
Siyo wote wanaoongea Kiingereza wana elimu mkuu,Kiingereza ni lugha na wala siyo elimu.

Ukisema English ni Elimu utaonekana huna elimu

Kuna Warusi, Wataliano, Wafaransa hawazungumzi Kiingereza sio kwamba hawana elimu...KIINGEREZA NI LUGHA
Mkuu sisi ni tofauti kidogo, Sisi tunatumia Kiingeleza kama lugha ya taaluma kwa hiyo ukikuta mtu ana doctorate still hajui kuongoa kiingeleza kwa ufasaha basi ujue ana tatizo, kuna sehemu haiko sawa. Lugha uliyotumia miaka yote kujifunzia toka Form one hadi Doctorate (miaka si chini ya 15) yaani maisha yako yote ya usomi kwa nini ikupe shinda?
 
“ Tena nyie watu hapa wazuri mnitafutie mke hapa”
 
H” hivi mmesema inaitwa enterpretetua sijui enter nini eeehee basi hiyohyo”
 
“ wewe Mbunge ulikua unamwandikia meseji huyu mkuu wa wilaya usiku tena meseji zenyewe sii nzuri “
 
What's the logic behind this comment?
Kwann wamuone bora tu kisa kaongea english language ? Kwann wasione kama ni privillage wao ku host trip ya kwanza wa rais mwanamama ktk ukanda wa EAC ...
 
Bado tunasafari ndefu kama nchi.

Yaani mtu kuzungumza Kingereza kizuri nalo ni swala la kujisifia?
Aisee, Mungu atuhurumietu safari nindefusana mkuu.

Unapokuwa na watu wenye akili za kitumwa kama huyojamaa anaesifia kingereza tunahitaji kufanya maombi sana.
 
Ningeshangaa sana kama Uzi huu usingevamiwa na wasiokijua ' Kiingereza ' na najua mtajitokeza wengi tu.

Ninachojua tu ni kwamba duniani kuna Lugha nyingi na nzuri ila hakuna ambayo hadi hivi leo imeweza kuwa ni Kiungo ' Kikuu ' cha Mataifa yote duniani iwe Kiuchumi na hata Kidiplomasia kama cha Kiingereza.

Kama Mchina, Mrusi, Mjerumani na Mchina pamoja na Jeuri zao zote za kuwa ' Super Powers ' ulimwenguni na Lugha zao pia ni Kubwa lakini bado hao hao wanakizungumza Kiingereza Wewe Mpuuzi Mmoja wa Kiswahili usiye na mbele wala nyuma ni nani ukipinge?

Itatuchukua muda mrefu sana na huenda pia hata isitokee kwa Mataifa mengi duniani Kuachana na Lugha ya Kiingereza kwani kama kuna Mafanikio makubwa ambayo nchi ya Uingereza ilipata tokea Kipindi cha ' Colonialism ' ni kuhakikisha Lugha yao si tu inaendelea kutumika bali pia inapendwa na kuendelea Kuaminiwa na Vizazi na Vizazi.

Kama Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere pamoja na kutowakubali Wazungu ( hasa kwa Sera zao na Matendo yao kwa Waafrika ) lakini Mwenyewe kwa Mdomo wake ( na Clips zipo Mitandaoni ) alikiri kuwa Kiingereza ni Lugha muhimu, siyo ya Kuepukwa duniani na ya Kibiashara zaidi.
Sawa uliyosema lakini SIYO KWELI kuwa mtu ambaye haongei kiingereza kwa ufasaha HANA ELIMU. Kiingereza ni lugha tu sawa na lugha nyingine yoyote. Vile vile ukumbuke kuwa watu wanatofautiana vipaji katika masomo mbalimbali ndiyo maana wengine ni wazuri kwenye lugha wengine ni wazuri kwenye numbers.

Pia kiingereza kilitapakaa duniani kwa sababu Waingereza walikuwa na makoloni mengi zaidi kuliko nchi nyingine yoyote duniani. Kwa hiyo usiwakandie watu wasioweza kuzungumza kiingereza vizuri ukadhani hawana akili au hawana elimu.

Ukienda Uingereza au hata hapa Tanzania kwa watoto wa darasa la tano wanaosoma shule zinazofundisha kiingereza tu utawakuta wanaongea kiingereza kizuri sana tofauti na wazazi wao waliosoma shule za Kayumba, sasa unataka kutuambia kuwa hao watoto wana elimu zaidi kuliko hao wazazi? Au ni wa maana zaidi kuliko wengine wasiozungumza kiingereza?
 
Jana Usiku nilipokea Meseji moja kutoka kwa Rafiki mkubwa kutoka Uganda akielezea Kufurahishwa Kwake na 'Kiingereza ' kizuri alichonacho Rais wa Tanzania Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan.

"Mr. Generalist are sure that this President of yours Mama Samia she's not a Briton? She speaks fluent English, very articulate, attractive and comfortable with it unlike other so called intellectuals with their doctorates on hand "

Na Waganda hawakuishia hapa tu kwa huyu Rafiki yangu Kunitumia hiyo Meseji bali hata ukienda huko Ugandans On Twitter ( UOT ) Wachangiaji wengi wamevutiwa na Uwezo mkubwa wa Kuongea Kiingereza ' kilichonyooka ' cha Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan.

Wameenda mbali zaidi na Kuhoji inakuwa Marais wengine (hasa Barani Afrika) wana Elimu Kubwa lakini walipokuwa wakiwasikiliza (wanapowasikiliza) huwa wanaongea Viingereza 'vibovu vibovu' tu wakati Makabatini mwao wamehifadhi Vyeti vya ' PhD ' zao.

Kongole sana Kwako Rais Mama Samia.
Rest easy Ben Saanane
 
Ina maana hata Polepole hafui dafu na zile hesabu zake kudiskraibu za madiagram na kumachua 1.5T?? 😂

Everyday is Saturday................................😎
Kila mtu na karama yake.
 
Kiingereza cha rais wetu ni kizuri zaidi ya kile cha Angela Merkel, hahaha!
 
Sina hakika kama kujua kingereza ndio kipimo cha kusoma; Magufuli na "mabaya" yake but kwenye issue ya Corona kawa outsmart hadi WHO na sasa hivi mataifa mengi makubwa (including UK ) wana copy from Magufuli, Magufuli kweli hakuakijua vizuri Kingereza but jamaa shule yake imeonekana kwenye mambo mengi ukiachilia mbali tabia za ubabe ambazo sidhani kama shule inaweza ku unlock.
Kingine, wazee wenzangu, tusijitoe ufahamu, wasomi wengi wa masomo ya sayansi wale wa zamani, na of course hata sasa hivi baadhi wapo, kingereza kwao kuongea ni shida sana, tena sana. Tafuta Engineer yeyote au msomi hata wa Hesabu kama mama Ndalichako, nuongee nae Kingereza kwa dakika 5 tu, atachemsha vibaya sana, why, Science ina deal zaidi na symbols, maneno kama therefore, etc, so nk yote yana alama, chemicals zote alama, sentensi inaweza kua ndefu, engineer atatumia alama tu na engineer mwenzie akaelewa jamaa anataka kusema nini; watu hao hao sasa, wapeni kazi ndio utajua kama alisoma au hakusoma.

Ningeshangaa sana kama Uzi huu usingevamiwa na wasiokijua ' Kiingereza ' na najua mtajitokeza wengi tu.

Ninachojua tu ni kwamba duniani kuna Lugha nyingi na nzuri ila hakuna ambayo hadi hivi leo imeweza kuwa ni Kiungo ' Kikuu ' cha Mataifa yote duniani iwe Kiuchumi na hata Kidiplomasia kama cha Kiingereza.

Kama Mchina, Mrusi, Mjerumani na Mchina pamoja na Jeuri zao zote za kuwa ' Super Powers ' ulimwenguni na Lugha zao pia ni Kubwa lakini bado hao hao wanakizungumza Kiingereza Wewe Mpuuzi Mmoja wa Kiswahili usiye na mbele wala nyuma ni nani ukipinge?

Itatuchukua muda mrefu sana na huenda pia hata isitokee kwa Mataifa mengi duniani Kuachana na Lugha ya Kiingereza kwani kama kuna Mafanikio makubwa ambayo nchi ya Uingereza ilipata tokea Kipindi cha ' Colonialism ' ni kuhakikisha Lugha yao si tu inaendelea kutumika bali pia inapendwa na kuendelea Kuaminiwa na Vizazi na Vizazi.

Kama Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere pamoja na kutowakubali Wazungu ( hasa kwa Sera zao na Matendo yao kwa Waafrika ) lakini Mwenyewe kwa Mdomo wake ( na Clips zipo Mitandaoni ) alikiri kuwa Kiingereza ni Lugha muhimu, siyo ya Kuepukwa duniani na ya Kibiashara zaidi.
 
Back
Top Bottom