#COVID19 Rais Samia: Tanzania tuna wagonjwa wa Wimbi la Tatu la Corona

#COVID19 Rais Samia: Tanzania tuna wagonjwa wa Wimbi la Tatu la Corona

Hilo wimbi la tatu liko kwenye magazeti na televisheni, lakini huku mtaani hakuna cha wimbi wala bibi yake na wimbi.

Hizo fedha za wazungu mlizokula hakika mtazitapika majizi nyinyi. Maana hamuishi kuweweseka na makorona kama visungura tope.

Huku Buzza kwanza hatujui hata maana ya corona. Tunaisikiaga tu kwenye mitandao na majarida.

Kwendeni huko na mabarakoa yenu uchwara!

Matapeli wakubwa!
Huko kijijini kwako ni kweli hakuna corona, huku mjini ipo.
 
Hii biashara ya kusema "eti wengi walikufa" walikufa wapi huko ambapo wengine hawafiki?.

Kuna watu humu mnakuwa wanafiki sana.

[emoji1485] Wewe ndiye mmojawapo wa wale waliosema "mlioenda Kilimarathon mjiandae kupukutika" leo kuna nini?.

Kwa kuwa kuna wimbi wa tatu na leo kuna mechi ya Biashara United na Yanga SC huko Tabora, watu waliojazana huko mpaka nafasi hakuna so, ni nini mnaaminisha watu?.

Kuna wakati tumia akili yako badala ya kutumia ya mtu mwingine [emoji850]!.
Kwahio wewe unatakaje?serikali ndio imeshatangaza sasa kwamba kuna wagonjwa wa wimbi la tatu,kila mtu achukue tahadhari,kama unabisha endelea kubisha
 
Si aseme tu
Si ulishangilia Nasari na ‘Lijuha-likali kwenye ule mkeka wa majuzi?! Kula maumivu taratibu sasa! Na kuna uzi, wa hukumu ya kina Mbowe kubatilishwa kule, ma-sukumagang hamjatia mguu kule, tumbo za kuhara litakuwa tatizo lenu mwaka huu, koroboi kabisa!
 
Mungu wa Mbinguni alitushindia mawimbi yote mawili ya awali ndiye atakaye tushindia hili linaloitwa la tatu.Pamoja na kwamba uongozi wake hautilii manani kuhimiza anao waongoza kumtegemea Mungu kwanza lakini bado Mungu wa Mbinguni amemletea Ujumbe, kuwa barako zitavaliwa na wanamzynguka tu si huku mitaani.

Kwa kutumia kutokuvaa barakoa mitaani ajue Mungu wa Mbinguni kampa Ujumbe kwamba Watanzania hawata acha ule msingi walio jengewa na mtangulizi wake 'JPM' wa KUMTEGEMEA na KUMPA KIPAUMBELE CHA KWANZA Mungu wa Mbinguni kwa kila jambo.
Asihadaiwe na anao kutana nao kwenye mikutano wamevaa barakoa uhalisia uko huku mitaani kwenye maisha ya kila siku. Wengine huvaa barakoa kulinda ajira ila nyoo zao hazifurahishwi wala hazihiari.
Una elimu gani ndugu
 
Kwa Nini Baraza la maaskofu katoliko TU?

Wao ndiyo wenye waumini TU??
Misikitini hakuna waumini?
Akina gwajima na makanisa mengine ya kilokole Hakuna waumini?

Waumini ndyo wanahatari ya kuambukizwa na Corona?

Na wasio na dini wahimizwe na Nani kuchukua tahadhari??

Kuna Nini nyuma ya katoliko na wimbi la tatu,?

Hata wimbi la pili katoliki walipiga kelele Sana! Kuna Nini nyuma ya pazia?

Wenye wananchi Ni serikali au Baraza ka katoliki??

Nway ,watu wasioitakia nchi hii mema, wanapenda tahadhari ya lockdown na kuzika watu bila ndugu.

India walikuwa wanachukua viungo vya watu waliokufa kwa kivuli Cha Corona.
 
Na ni bora aliwafokea hao maaskofu uchwara.

Hakuna dini inayofundisha kutapeli watu kwa magonjwa ya kuigiza.

Nyinyi madalali na vibaraka wa wazungu kiama chenu hakipo mbali.

Hatuwezi kuruhusu mliangamize taifa kwa machanjo yenye sumu.
Umechanjwa mara ngapi na kula vingapi vya wazungu hadi leo ndiyo uwaogope?
 
Mithali 10:24 ,Aogopacho mtu asiye haki ndicho kitakachomjilia,na wenye haki watapewa matakwa yao.

Hivyo bado tunaimani na Mungu wetu juu ya uponyaji wa janga hili atatuponya hakika yeye anasema tujapopita kati ya maji mengi hayatatugharikisha,tujapo pita katikati ya moto na kujaribiwa kwa namna hii hakika hatutateketea kamwe.

Sent from my SM-A307FN using JamiiForums mobile app
 
“Tanzania tuna wagonjwa wa wimbi la Tatu la Corona. Hili jambo bado lipo, tuchukue hadhari zote na tunawaomba viongozi wa dini mseme hili kwa sauti kubwa"

Rais Samia Suluhu Hassan wakati akizungumza na baraza la maaskofu katoliki (TEC) #Tanzania #COVID19

=========

Rais Samia Suluhu: Wahashamu, baba Maaskofu kama mnavyofahamu, dunia kwasasa inakabiliwa na mlipuko wa Covid-19 na nafahamu kanisa tangu mwanzo limekuwa na msimamo Thabit katika kupambana na ugonjwa huu hivyo basi niwaombe sana Maaskofu msisahau kuwakumbusha waumini kuhusu wa kujikinga na kuchukua Tahadhari zote zinazoelekewa na wataalam wa Afya dhidi ya ugonjwa wa Corona.

Kwakuwa Kinga ni Bora kuliko Tiba, tusiache kutumia kila kitakachotukinga na maradhi haya ili kuepesha vifo vya makundi.

Kama tunavyojua, duniani sasa hivi kuna wimbi la tatu la Corona, tumetoka kwenye wimbi la kwanza Tanzania tumeingia, limekwenda limepungua kidogo, tumeingia Wimbi la Pili tumekwenda nalo na sasa kuna Wimbi la Tatu.

Ishara ndani ya nchi tayari zinaonekana, tayari tuna wagonjwa ambao wameshaonekana katika kwenye wimbi hili la Tatu. Kama mnakumbuka siku nilitembelea hospitali ya Mwananyamala, kuna wodi daktari mfawidhi alikuwa ananiingiza akaniambia humu kuna wagonjwa wenye matatizo ya kupumua, nikamwambia hebu kuwa muwazi, ni covid, akaniambia ndio Covid wakati wapiga picha wangu tayari wameshatangulia, nikawaambia nyie tokeni haraka huko.

Kwahiyo ni kusema kwamba hili jambo bado lipo, tusijiche, bado lipo tuchukue hadhari zote na tunawaomba sana viongozi wa Dini mliseme hili kwa sauti kubwa, kwa waumini wetu ili tujiepushe na vile vifo vya makundi.

Pamoja na yote hato, ni vyema pia tumuombe Mungu kwa kiasi kikubwa aendelee kutuepusha na kutupa hifadhi yake kutokana na maradhi hasa Janga hili la Corona kwakuwa yeye ndio Muweza wa Yote.


Baada ya Raisi kutaka ukweli kutoka kwa daktari na kuambiwa ukweli, ni hatua gani zilichukuliwa na serikali kupitia wizara husika? Kama Raisi aliwatoa haraka wapiga picha wake walio tangulia wodini kwa nini Raisi aendeleze mikutano yenye kukusanya watu wengi bila kuwepo tahadhari ya kutosha wakati alisha ujua ukweli? Baada ya kuujua ukweli kuhusu wimbi la 3 kuingia nchini kwa nini adi sasa serikali (wizara ya afya) haija toa tamko rasmi kwa Taifa? Yaani maswali ni mengi mno.
 
Back
Top Bottom