Rais Samia this will haunt you for the rest of your life

Rais Samia this will haunt you for the rest of your life

Inashangaza sana, kwamba hadi sasa hivi kwenye uzi huu hamna yeyote yule aliyeitaja Kenya, wala wakenya. Nuksi zitakuwa za nini, waliojeruhiwa na kuhamishwa si walikuwa wakenya? Sio haki tena kwa rais wa Tanzania kuwakanyaga kanyaga mamluki wa Kenya na kuwaondoa kabisa kwenye ardhi ya Tanzania?
 
Kuwahamisha wamasai toka ardhi yao ya kurithi inaweza kuwa amri rahisi kabisa uliyowahi kuitoa ila jambo hili limeumiza wengi na litakuhusu kwa kipindi chako chote.

Napenda nikuambie kwamba hili hukufanya sawa.

Umekosea.
Kwa Loliondo ipo kwa kuwanufaisha wakenya kuleta mifugo yao kulisha, kwa sababu tu ni wamasai?


Duniani, nchi nyingi zimehamisha watu wao ndao kwa manufaa makubwa ya nchi. Eg: USA, Canada (red indians), Brazil, Botswana (Basarwa), n.k. Kama raia hawatakiwi kuachwa porini bila huduma muhimu kama; maji Safi, hospital services, schools, and many other social services.
 
Hakuna asiyotaka hayo mazuri uliyoorodhesha hapo wewe, lakini umejiuliza sababu zinazosababisha hizi kelele nyingi kuwepo ni za nini?
Wewe unadhani hao wasiotaka kwenda huko kwenye neema ni vichaa?
Kwa nini usichukue muda kujiridhisha kwa nini serikali iwe na uongo mwingi kiasi hiki, huku ikiwa na maslahi ya wananchi wake!
Ni human nature tu ya ku resist any changes. Katika jamii huwezi kupata watu wote wakakubaliana na kitu flani. Hata jangwani walipinga kuhama na walipata watetezi wengi tu. Hao watu wangehamishwa enzi ya JPM, wangehama bila hata nyumba moja na no one would dare to speak shit or loud.
 
My friend you have a very low IQ,

Can't argue with you.

Wakati nilikua nampigania Magufuli awe Rais nilifanya hivyo kwa Samia pia.

Wewe hukuwepo.

You are just a plastic fan.

So you better shut your mouth.
Mtu akiwa na maoni tofauti na yako haina maana lazima awe na low IQ.
 
My friend you have a very low IQ,

Can't argue with you.

Wakati nilikua nampigania Magufuli awe Rais nilifanya hivyo kwa Samia pia.

Wewe hukuwepo.

You are just a plastic fan.

So you better shut your mouth.
Very shallow reply
Have you ever taken an IQ test?
 
Ukweli uliojificha. Jambo hili lina pande mbili: Mosi, ongezeko la watu na mifugo ni hatari kwa uhifadhi, hii nadhani inatokana na wenyeji kutokuwa waminifu na wazalendo.

Wamekaribisha mifugo ya Wakenya na wanafanya siasa hifadhini, na ndiyo unaona leo kelele zinapigwa sana Kenya. Kenya wanamuomba Mh Uhuru aje aongee na Rais Samia. Kwa lipi? Wote tujiulize.

Pili, uhifadhi wa mazingira wa Ngorongoro ni mkubwa sana, na ndiyo maana kila mfugaji tajiri awe Kenya au Tanzania atapeleka mifugo kule kwani nyasi ni nyingi sana kwa ajili ya wanyama pori na maji yapo throughout the year, na ndiyo ugomvi, wameharibu mazingira katika maeneo yao wanaingiza mifugo yao kwenye hifadhi.

Hifadhi ni km 1,500 za mraba, eneo la wamasai wamepewa km 2,500 za mraba kwa ajili yao na mifugo. Sasa wanataka zile km 1,500 za mraba na wao wawepo! Kama umefuatilia jana yupo Mkenya ametoa kauli ya serikali kuacha mara moja uwekaji wa alama za mawe kuzunguka hifadhi.
 
Ni human nature tu ya ku resist any changes. Katika jamii huwezi kupata watu wote wakakubaliana na kitu flani. Hata jangwani walipinga kuhama na walipata watetezi wengi tu. Hao watu wangehamishwa enzi ya JPM, wangehama bila hata nyumba moja na no one would dare to speak shit or loud.
Mkuu samahani sana, unazungumzia binaadam kama mifugo?

Utashi aliokupa Mungu wewe unadhani wengine hawana utashi kama wako?

Sasa unasema hilo la kutumia nguvu, kwa hiyo nchi hii isiwe ya maelewano bali iwe ya kila mwenye maguvu afanye atakavyo, na serikali ndiyo basi tena wakiamua chochote pasiwepo mtu wa kuhoji?

Hivi wewe huelewi kwamba wakoloni nao walikuwepo hapa, tena na nguvu nyingi zaidi hata kuwashinda hawa unaowashangilia sasa.

Maana ya kuwa na serikali inayoheshimu matakwa ya wananchi ni nini?

Haya unamzungumzia Magufuli, yupo wapi sasa?

Hawa nao wakati wao unakuja. Vuta subira tu.
Kama umewekeza huko, hakikisha usipoteze kila kitu.
 
Ukweli uliojificha. Jambo hili lina pande mbili: Mosi, ongezeko la watu na mifugo ni hatari kwa uhifadhi, hii nadhani inatokana na wenyeji kutokuwa waminifu na wazalendo.

Wamekaribisha mifugo ya Wakenya na wanafanya siasa hifadhini, na ndiyo unaona leo kelele zinapigwa sana Kenya. Kenya wanamuomba Mh Uhuru aje aongee na Rais Samia. Kwa lipi? Wote tujiulize.

Pili, uhifadhi wa mazingira wa Ngorongoro ni mkubwa sana, na ndiyo maana kila mfugaji tajiri awe Kenya au Tanzania atapeleka mifugo kule kwani nyasi ni nyingi sana kwa ajili ya wanyama pori na maji yapo throughout the year, na ndiyo ugomvi, wameharibu mazingira katika maeneo yao wanaingiza mifugo yao kwenye hifadhi.

Hifadhi ni km 1,500 za mraba, eneo la wamasai wamepewa km 2,500 za mraba kwa ajili yao na mifugo. Sasa wanataka zile km 1,500 za mraba na wao wawepo! Kama umefuatilia jana yupo Mkenya ametoa kauli ya serikali kuacha mara moja uwekaji wa alama za mawe kuzunguka hifadhi.
Heshima mkuu Huihui,

Haya unayoeleza hapa umeeleza upande mmoja, ingawaje mwanzo ulisema pande mbili.
Haya hapa ninakubaliana nawe, isipokuwa anayebeba lawama kubwa ni serikali yenyewe kushindwa kusimamia kazi yake ipasavyo.

Kwa nini mifugo itoke Kenya ije kulishwa Tanzania, huoni kasoro hii. Kwa hiyo makosa haya ni ya kuwalaumu wakazi wa Loliondo, na siyo serikali kushindwa kazi ya kulinda mipaka ya nchi yetu?

Uhifadhi ni muhimu, na kama kuna uharibifu ni udhaifu wa serikali hiyo hiyo. Wakazi wa eneo hilo wao wenyewe ndio wangekuwa wanahimiza uhifadhi kama wange elimishwa faida za uhifadhi huo, faida ambazo wao wenyewe ndio wangekuwa wanufaika wakubwa.
Unamlaumu mtu ambaye hata siku moja hujamuelimisha chochote, na wala kumwonyesha faida zinazotokana na yeye kuwa mwangalifu na mazingira yake asitaharibu?

Sasa una utendaji wa serikali ulivyo mbovu. Kama wamefanya tathmini na kuona kuwa uharibifu umetokea, taarifa hiyo ilifika kwa wananchi?
Wananchi wanapewa amri tu, kuhama miezi sita, na hapo hapo wanaanza kupewa vitisho wasipotii amri?

Na kama bado huelewi ninachoandika hapa, wananchi hawa hawa wanaijua historia chafu na ovu ya serikali yao, kwani walishatendewa uovu huo kupitia kwa mwekezaji aliyeletwa na kuwanyanyasa wananchi ndani ya nchi yao.

Wanachoelewa wananchi sasa hivi na serikali hii ni mwendelezo huo huo wa unyanyasaji. Mwekezaji, ambaye hata siku moja hawajawanufaisha chochote na uwekezaji wake, bali uonevu, sasa analindwa zaidi na serikali kuliko serikali kulinda maslahi ya wananchi wake..

Hatukutafuta uhuru wetu, halafu miaka michache tu tuwe tumechoka na kuwa huru na kuanza kutafuta wakoloni wengine waje kutunyanyasa ndani ya nchi yetu, kwa vipande vya rushwa wanavyopewa hawa wasaliti wa uhuru wetu.
 
Kuwahamisha wamasai toka ardhi yao ya kurithi inaweza kuwa amri rahisi kabisa uliyowahi kuitoa ila jambo hili limeumiza wengi na litakuhusu kwa kipindi chako chote.

Napenda nikuambie kwamba hili hukufanya sawa.

Umekosea.
Kwani kawahamisha? Yeye kawapunguza tu kwa kua eneo wanaloishi una umuhimu kwa shughuli za kitalii na uhifadhi wa wanyama pori. Wanyama pori na utalii ni muhimu kwa uchumi wa nchi.
Zaidi ya hapo wamasai sio wageni kuishi sehemu zingine za nchi. Wametapakaa kote wakiendesha maisha yao ya kifugaji huku mara nyingi wakiwahangaisha wakulima sehemu nyingi za nchi kwa mifugo kula mazao yao.
 
Mkuu samahani sana, unazungumzia binaadam kama mifugo?

Utashi aliokupa Mungu wewe unadhani wengine hawana utashi kama wako?

Sasa unasema hilo la kutumia nguvu, kwa hiyo nchi hii isiwe ya maelewano bali iwe ya kila mwenye maguvu afanye atakavyo, na serikali ndiyo basi tena wakiamua chochote pasiwepo mtu wa kuhoji?

Hivi wewe huelewi kwamba wakoloni nao walikuwepo hapa, tena na nguvu nyingi zaidi hata kuwashinda hawa unaowashangilia sasa.

Maana ya kuwa na serikali inayoheshimu matakwa ya wananchi ni nini?

Haya unamzungumzia Magufuli, yupo wapi sasa?

Hawa nao wakati wao unakuja. Vuta subira tu.
Kama umewekeza huko, hakikisha usipoteze kila kitu.
Point yako nini mbona hueleweki? Ni wapi Serikali imetumia nguvu kuwahamisha? Shida iko wapi kwa jamii moja kuhama kutoka sehemu moja kwenda nyingine iwapo mazingira wezeshi yamewekwa huko wanakohamia. Mbona Serikali imewahamisha watumishi wake kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma, au huu sio kuwahamisha watu kutoka maeneo yako. Kuna watu wamehamishwa kutoka maeneo yao ya asili kwa ajili ya kulinda vyanzo vya maji, na hili limefanyika karibu mikoa mingi tu Tanzania. Shida ni nini kwa wamasai? Watanzania mnatengenezewa agenda nanyi mnakubali. Amkeni.

Natamani nionyeshwe wapi Serikali ilipokosea katika hili?
 
Kuwahamisha wamasai toka ardhi yao ya kurithi inaweza kuwa amri rahisi kabisa uliyowahi kuitoa ila jambo hili limeumiza wengi na litakuhusu kwa kipindi chako chote.

Napenda nikuambie kwamba hili hukufanya sawa.

Umekosea.
Hao wamasai wameathirika vipi?
Wewe umeathirika vipi?
 
Tunakujua wewe masikini!
Kama wew ni masikini usidhani kila mtu ni masikini. Hata huyo jiwe alikuwa anawadanganya mjivunie unyonge wakati yeye anapiga pesa. Pole sana mnyonge
 
Hapana.
Hapa sioni msukumo ukiwa maslahi ya kitaifa zaidi ya maslahi binafsi ya wahusika.
Maslahi ya kitaifa, hata hao masai nina hakika wangeyaunga mkono kwa moyo safi kabisa kama serikali ingekuwa na nia njema ya kufanya kazi hiyo kwa ufanisi kuliko inavyofanya sasa..
Haya siyo maslahi ya taifa. Huo ni uongo.
So wale wa kimara ilikuwa ni maslai ya kitaifa na waliyaunga mkono hao walio vunjiwa nyumba?
 
Hao sukumagang" unaowasema hapo, na wao enzi zao walikuwa wakishangilia kama unavyoshangilia wewe sasa hivi!
Basi kama sis tulivumilia kwanini na wao wasivumilie wakati tunaleta maendelea ya kitaifa kama wao walivyosema enzi zao? Kikubwa kila mtu ashinde mechi zake
 
Hapana.
Hapa sioni msukumo ukiwa maslahi ya kitaifa zaidi ya maslahi binafsi ya wahusika.
Maslahi ya kitaifa, hata hao masai nina hakika wangeyaunga mkono kwa moyo safi kabisa kama serikali ingekuwa na nia njema ya kufanya kazi hiyo kwa ufanisi kuliko inavyofanya sasa..
Haya siyo maslahi ya taifa. Huo ni uongo.
Boss! Nchi hii masai siyo wa kwanza kuhamishwa. Wakati wa Kikwete na Mkapa, kanda ya ziwa imeathirika sana na hama hama hizi kwa kuwapisha wachimba madini. Pale Geita kuna familia waliishi darasani kwa miaka zaidi ya miwili; bila fidia, bila kujemgewa nyumba. Miaka ya 70 wananchi wa Ukara walihamishiwa wilaya ya Sengerema. Walichopewa ni usafiri tu; bila kujengewa chochote! Kwa nini Maasai waonekane ni special?

Hisia mbaya nio hiyo kwamba eneo anapewa mwarabu. Hili sitashangaa maana rais wetu anaonekana ni mpenda uarabu. na haonekani kujiul;iza mara mbili kabla ya kuzungumza.
 
Boss! Nchi hii masai siyo wa kwanza kuhamishwa. Wakati wa Kikwete na Mkapa, kanda ya ziwa imeathirika sana na hama hama hizi kwa kuwapisha wachimba madini. Pale Geita kuna familia waliishi darasani kwa miaka zaidi ya miwili; bila fidia, bila kujemgewa nyumba. Miaka ya 70 wananchi wa Ukara walihamishiwa wilaya ya Sengerema. Walichopewa ni usafiri tu; bila kujengewa chochote! Kwa nini Maasai waonekane ni special?

Hisia mbaya nio hiyo kwamba eneo anapewa mwarabu. Hili sitashangaa maana rais wetu anaonekana ni mpenda uarabu. na haonekani kujiul;iza mara mbili kabla ya kuzungumza.
Mkuu, Patriot', sidhani kwamba kinachohojiwa hapa ni watu (wamasai) kuhamishwa; na mwishowe nashukuru umepata sehemu ya jibu, hata kama si jibu kamili kwa nini watu wanahoji.
Nijuavyo mimi, watu wa Ukara walipohama, sidhani kuwa kulikuwa na kelele zozote za kupinga, kwa sababu watu tayari walishaandaliwa na kupewa elimu juu ya sababu hizo za kuhama.

Hili la leo, la hawa wamasai, nalo lingekuwa rahisi zaidi kama lingetekelezwa kwa umakini na hao wanaolitekeleza.
 
Back
Top Bottom