Rais Samia: Tutaendelea kukopa tumalizie miradi inayoendelea

TRA kule zanzibar wanazileta bara ndio mnakula huko milo 3.,
 
Hatuwezi kukamilisha miradi hii kwa pesa za ndani wala pesa za tozo, hivyo ni lazima tukope kuliko kuwakamua wananchi" aliongeza Rais SSH.[emoji3064][emoji3064][emoji3064][emoji3064] KWAHIYO TOZO ZITAFUTWA?
Samia anatufanya sisi vifaranga vya kuku
 
Tanzania's debt cycle is weird. Being in a strategic debt is not bad, but seeing the Government and its mates getting fatter with it hapo ndo you get to know these people are really BadAss 😂😂

John Adams alipata kusema, "Two ways to conquer and enslave a country. One is by sword the other is by debt"
 
Kaanza Mipasho ?

Hao wapiga ramli hawalipi Kodi ?, Kama wanalipa sio wabezwe bali tujaribu kuwaelewesha na kama bado wanapinga tujiulize kwanini na tushindane nao kwa hoja...
Anayeambiwa ni Job & co, sasa job analipa kodi gani na wapi?
 
Mama Samia
Na andika kukuomba hao kina Supika na wenzake uwachinjie baharini kwani wana lao jambo na tunajua umewavumilia kwa muda mrefu sasa.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Rais yuko sahihi hapa. Kukopa ukala ni kosa, lakini kukopa ukawekeza kwenye miradi yenye uwezo wa kurudisha deni ni sawa sana.

Mfano mzuri ni reli mpya ya Nairobi hadi Mombasa. Kenya walikopa wakaijenga. Sasa direct benefits na spin off businesses zake zinachangia sana kuinua uchumi wa Kenya, na ina uwezo wa kulipa deni.

Mtu asifikirie kujenga reli ya kisasa Dar hadi Mwanza kipato chake kwa nchi ni nauli zitakazokusanywa na malipo ya kusafirisha mizigo tu. Kuna spin off businesses nyingi zitakua. Hilo litainua kiwango cha uchumi na makusanyo ya kodi za serikali. Mkopo utalipika vizuri sana na kuacha faida kubwa.

Pamoja na kwamba namshutumu sana Mama kwa kosa lake la kutokubali mchakato wa katiba mpya sasa (I posted some advice on this, right from the beginning. Nilisizitiza kwa kuandika the catch words : MAMA SEMA NENO MOJA TU NA NCHI ITAPONA), lakini yuko sahihi kwenye hili la mikopo.

Kwa mfano, kama unatafiti mapato na matumizi ya kuwa na basi la kusafirisha abiria kati ya Dar na Dodoma, na ukagundua kwamba gharama za kununua basi la kufanya kazi hiyo zinaweza kurudishwa baada ya miaka 3 na kisha ukaogopa mkopo wa kufanya huo uwekezaji basi wewe ni mbumbumbu. Inatakiwa ukae kimya uache watu wajenge nchi.
 

Jiulize huu mzigo wote upo wapi mkuu!!! Daaah masikini Tanzania yangu..... hawa viongozi wanatuona wajinga sana
 
 
Kama anakopa na speed ya ukamilishaji miradi ionekane,kwa maana miradi ikamilike kwa wakati!! Hapo hatutakuwa na nongwa!!, kwanza huko dar wanamdanganya Sana,arudi huku ikulu ya nchi iliko Dodoma,mbona anang'ng'ana na daisalama!!??, kituo Cha kazi yake Kiko Dodoma,yeye anang'ang'ania kukaa nje ya kituo chake Cha kazi, si utovu wa nidhamu ya kazi huu!!!

yeye ni mtumishi ,sawa na watumishi wengine,mbona waalimu, ma nesi n.k wanalazimishwa kubaki kwenye vituo vyao vya kazi!!?, arudi kituo chake Cha kazi,aachane na huo mji wa daisalama!! Ebo!!
 
Taarifa ni kuwa Dodoma bado haijakamilika ujenzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…