Rais Samia: Ukinikuna Vizuri, mimi nakukuna huku nnakupapasa na kukupuliza. Lakini "Ukinipara...Nakuparura!

Rais Samia: Ukinikuna Vizuri, mimi nakukuna huku nnakupapasa na kukupuliza. Lakini "Ukinipara...Nakuparura!

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi

Rais Samia ambaye ni Rais Mwanamke wa Kizanzibari mwenye lugha tamu laini na lafudhi ya Kizanzibari, yenye maneno na vineno, vitamu hadi raha kumsikiliza haku ukitamani asimalize kuzungumza.

Leo kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uhuru wa habari, Rais Samia katamka maneno haya


"Ukinikuna Vizuri, mimi nakukuna huku nnakupapasa tena na kukupuliza ufu ufu ". Lakini "Ukinipara...Nakuparura!" - Hivi Vijineno!, Japo Vitamu Hadi Raha Kusikiliza!.

Hili ni onyo la kiana kwa vyombo vya habari, tujitahidi kumkuna Mama ili na yeye atukune, na atupapase. Tuepuke kumpara, asije kutuparura!. Ikitokea Mwandishi wa habari akampara Mama, no one knows huko kumparura, style ya Mama ya kumparura ikoje!. Kule nyuma aliwahi kutoa onyo kama hilo kuwa "ukimzengua, tutazenguana", Leo ni "ukinipara, nitakuparua!. Kwa vile no one knows uparuaji wake, unaweza kuwa mchungu kuliko Shubiri, hivyo natoa wito kwa waandishi wenzangu wa habari
1. Waandishi wanaopenda kukunwa na kupapaswa, waendelee kumkuna ili awakune na kuwapapasa.

2. Sisi waandishi wapara, tujitahidi sana kumpara kwa taratibu sana ili alone ni unamkuna, tusije mpara kwa nguvu Mama, akatupara hivyo Shubiri, tutaionja.

3. Wale waandishi ma konki ambao hawaogopi shubiri, ikitokea jambo la kumkuna, tutamkuna, lakini likitokea la kumpara, tutampara kwasababu ni waandishi wanao mpara ndio watamsaidia kuliko wanao mkuna!. Tulifanya hivyo kwa watangulizi wake, tutafanya hivyo kwake ili kumsaidia!. Kumuenzi Magufuli: Tujikumbushe 'spana' za JF zilivyomsaidia Hayati Magufuli na Taifa. Je, Samia pia tumsaidie kwa 'spana' au tumkune tu tusimpare?

Happy Press Freedom Day.
Paskali

Mabandiko mwendelezo
 
Vipi mkuu, bila shaka utapendwa kukunwa kupapaswa na kupilizwa pruuuuu na Mama, kuanzia leo uwe wazi mambo ya kuniandika nyuzi zako kwa mafumbo huku ukimteta Mama iwe mwisho 😀

Ukifanya hivyo utapata reward ya kukunwa na kupapaswa huku ukipulizwa pruuu na Mama yetu kipenzi Chifu Hangaya..
 
Wanabodi

Rais Samia ambaye ni Rais Mwanamke wa Kizanzibari mwenye lugha tamu laini na lafudhi ya Kizanzibari, yenye maneno na vineno, vitamu hadi raha kumsikiliza haku ukitamani asimalize kuzungumza.

Leo kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uhuru wa habari, Rais Samia katamka maneno haya


"Ukinikuna Vizuri, mimi nakukuna huku nnakupapasa tena na kukupuliza ufu ufu ". Lakini "Ukinipara...Nakuparura!" - Hivi Vijineno!, Japo Vitamu Hadi Raha Kusikiliza!.

Hili ni onyo la kiana kwa vyombo vya habari, tujitahidi kumkuna Mama ili na yeye atukune, na atupapase. Tuepuke kumpara, asije kutuparura!. Ikitokea Mwandishi wa habari akampara Mama, no one knows huko kumparura, style ya Mama ya kumparura ikoje!. Kule nyuma aliwahi kutoa onyo kama hilo kuwa "ukimzengua, tutazenguana", Leo ni "ukinipara, nitakuparua!. Kwa vile no one knows uparuaji wake, unaweza kuwa mchungu kuliko Shubiri, hivyo natoa wito kwa waandishi wenzangu wa habari tujitahidi sana tusije mpara Mama, Shubiri, tutaionja.

Happy Press Freedom Day.
Paskali
Nani kama mama?
9YuV-t8gibNX29HdbyNWD_JWnaZegc9DVx7x5mJnVBg.jpg
 
Amepeleka ujumbe mfupi kwa waandishi anataka kusifiwa, so wakimsifia hatayafungia magazeti yao, ila wakimponda wajiandae kwa litakalowapata.

Chakushangaza baada ya kauli yake hiyo amesisitiza utii wa sheria, lakini mbona naye ameshindwa kutii sheria kama za mikutano ya siasa?

Muhimu atambue utii wa sheria hauhusiani na kumfurahisha yeye kama mkuu wa nchi, awaache waandishi watimize majukumu yao kwa uhuru kisheria bila kufuata hisia/mawazo yake.
 
Wanabodi

Rais Samia ambaye ni Rais Mwanamke wa Kizanzibari mwenye lugha tamu laini na lafudhi ya Kizanzibari, yenye maneno na vineno, vitamu hadi raha kumsikiliza haku ukitamani asimalize kuzungumza.

Leo kwenye maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uhuru wa habari, Rais Samia katamka maneno haya


"Ukinikuna Vizuri, mimi nakukuna huku nnakupapasa tena na kukupuliza ufu ufu ". Lakini "Ukinipara...Nakuparura!" - Hivi Vijineno!, Japo Vitamu Hadi Raha Kusikiliza!.

Hili ni onyo la kiana kwa vyombo vya habari, tujitahidi kumkuna Mama ili na yeye atukune, na atupapase. Tuepuke kumpara, asije kutuparura!. Ikitokea Mwandishi wa habari akampara Mama, no one knows huko kumparura, style ya Mama ya kumparura ikoje!. Kule nyuma aliwahi kutoa onyo kama hilo kuwa "ukimzengua, tutazenguana", Leo ni "ukinipara, nitakuparua!. Kwa vile no one knows uparuaji wake, unaweza kuwa mchungu kuliko Shubiri, hivyo natoa wito kwa waandishi wenzangu wa habari tujitahidi sana tusije mpara Mama, Shubiri, tutaionja.

Happy Press Freedom Day.
Paskali

Pascal Mayalla:

Maneno kama "kuparura" , "kudemka" naweza kusema yanachagiza katika ukuaji wa misamiati ya kiswahili ingawa mpaka sasa Mh. Rais hatujaweza kuona misamiati hiyo ikitumika katika utekelezaji wake !!
 
Back
Top Bottom