Rais Samia uliomba ripoti ya "haraka" kuhusu utekaji nchini! Haraka ni muda gani?

Rais Samia uliomba ripoti ya "haraka" kuhusu utekaji nchini! Haraka ni muda gani?

We ni nani hasa mpaka umpangie mh Rais nini afanye na kwa muda gani??? Who are you??
Acha ufala, huyo ndio mwajiri wake ebo!
Lakini ile kesi ya Tigo kule London imesha toa majibu kuwa wauaji, watekaji na wafanya mipango hiyo ni kina nani.
Ila watambue tuu, utawala mwingine ukiingia madarakani eitha kwa uchaguzi au nguvu ya kijeshi kuna watu mnawaheshimu leo mtawaona Ukonga au Isanga wakisubiri kitanzi.
Taratibu tutafika!
 
Ili uchunguzi kwa kifo cha Ally Kibao majibu yapatikane haraka ni lazima mnyika akamatwe mara moja kuhojiwa
 
Kumekuwa na utamaduni wa kudanganywa hata na uongozi wa juu. Mama Samia aliomba riport ya kutekwa tekwa kwa watu nchini. Cha ajabu hakuna mtu anaongelea ripoti na wengi kujisahaulisha. Isije ikawa tena tunadanganya danganywa na uongozi wa juu. Chunguzi nyingi za utekaji hazifanyiki maana watekaji wengi wa watu hasa mashuhuri ni hao hao Polisi na usalama. Mo alitekwa , Lussu alipigwa risasi hatujawahi kuona ripoti yeyote.

Swali kuna mtu hata mmoja anajua Mama anaposema ripoti apewa haraka ni hasa kwa muda gani? Mwezi, Mwaka, siku au ...... ukweli ni kwamba ni siasa tu hakuna ripoti. Ikifika sehemu maneno ya Raisi yanapuuzwa na iwe danganya toto iko siku hao hao Polisi na usalama watamgeuka na wataona powa.
Acha hiyo ile ripoti ya Mtwara ya Askari kuua raia na yenyewe mpaka leo kimnya. Hii ni danganya toto kwamba yatapita watasahau
 
Ni muhimu mno pakawepo na ustahimilivu na subra kwenye hilo,

Nadhani sote ni mashuhuda kwa jinsi ambavyo mashahidi muhimu hususani kutoka vyama vya siasa nchini , wanavyokaidi na kudinda kutoa ushirikiano kwa vyombo vya uchunguzi mpaka walazimishwe. Huo ni miongoni mwa ucheleweshaji wa makusudi wa muafaka wa jambo hilo..

Na hilo nadhani linaweza kuibua mashaka zaidi na na kuonyesha picha halisi ya ugumu wa kufikia muafaka wa mapema kuhusu jambo hilo baya zaidi kutokea Tanzania.

Nachelea kutoa rai kwa wananchi wenzangu wote, kuwa watulivu, wakati uchunguzi ukiendelea, ili hatimae ukweli wa mambo na wahusika waweze kujulikana na kuchukuliwa hatua mujarabu za kisheria, kwa dhuluma waliyoifanya kwa mwanadamu mwezao 🐒
Damu ya mtu sio bia wee jamaa. Maandiko yanasema Kwenye Ulimi kuna uzima na mauti na waupendao watashiba matunda yake. Acha kufanya spining openely ili haki ya watu ibakie ardhini na wewe ufurahie kisa tu mmetofautiana itikadi. When it is your turn hutakua na wa kulian nae, jiepushe sana ndugu it is a friendly reminder
 
Damu ya mtu sio bia wee jamaa. Maandiko yanasema Kwenye Ulimi kuna uzima na mauti na waupendao watashiba matunda yake. Acha kufanya spining openely ili haki ya watu ibakie ardhini na wewe ufurahie kisa tu mmetofautiana itikadi. When it is your turn hutakua na wa kulian nae, jiepushe sana ndugu it is a friendly reminder
nikireply kwa maandiko nadhani ntakuchanganya zadi,

Ni muhimu zaidi wanatakiwa kutoa ushahidi wa wanachojua dhidi ya mauaji ya mTanzania yeyote ni vema wakatoa ushirikiano bila ukaidi wala ujeuri,wanaogopa nini mbona taarifa za mwanzo wa utekaji na zile za mauti ya mtekwaji, walikua wakiripoti kwa mbwembwe sana mitandaoni?

kweli hawana report za hapo katikati palitendeka nini kwa mwendazake kamanda Ally Kibao? 🤭

halafu gentleman,
ni muhimu kua serious kwenye mambo muhimu. Hisia, muhemko na kutegemea huruma ni useless na nonsense katika kutafuta ukweli 🐒
 
Aya za Qur'an kuhusu hukumu bila kupendelea:Surah An-Nisa (4:135):

"Enyi mlioamini! Kuweni wenye kusimama kwa haki, mkiwa mashahidi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ijapokuwa ni juu ya nafsi zenu au wazazi wawili na jamaa zenu, ikiwa (yule mnayemshuhudia) ni tajiri au maskini, basi Mwenyezi Mungu anawastahiki zaidi. Basi msifuate matamanio ili muweze kutenda haki. Na mkiupotoa (ushahidi) au mkakataa kutoa, basi hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za mnayoyatenda."


(Qur'an 4:135)Aya hii inawataka waumini kutoa hukumu bila kupendelea, hata kama ni dhidi yao wenyewe au dhidi ya watu wa familia yao. Waislamu wanatakiwa kuepuka matamanio au hisia binafsi ili kuhakikisha haki inatendeka.
 
Aya za Qur'an kuhusu hukumu bila kupendelea:Surah An-Nisa (4:135): "Enyi mlioamini! Kuweni wenye kusimama kwa haki, mkiwa mashahidi kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, ijapokuwa ni juu ya nafsi zenu au wazazi wawili na jamaa zenu, ikiwa (yule mnayemshuhudia) ni tajiri au maskini, basi Mwenyezi Mungu anawastahiki zaidi. Basi msifuate matamanio ili muweze kutenda haki. Na mkiupotoa (ushahidi) au mkakataa kutoa, basi hakika Mwenyezi Mungu anazo khabari za mnayoyatenda."
(Qur'an 4:135)Aya hii inawataka waumini kutoa hukumu bila kupendelea, hata kama ni dhidi yao wenyewe au dhidi ya watu wa familia yao. Waislamu wanatakiwa kuepuka matamanio au hisia binafsi ili kuhakikisha haki inatendeka.
 
Back
Top Bottom