Rais Samia; Urais wa nchi ni mambo makubwa

Rais Samia; Urais wa nchi ni mambo makubwa

Mashuka 200, hiyo siyo hata level ya mkuu wa Kata. Mashuka inabidi siku zote yawepo hospitalini.

Level ya Urais at very least ni kuzungumzia madawa, vitendea kazi, Mishahara, Budget ya wizara ya Afya, kusimamia manunuzi ya vifaa, madawa, ujenzi wa hospitali kwamba hatupigwi.
Mashuka hata mimi nyoka naweza kupeleka
 
Habari wana JF,

Binafsi nafurahia uongozi wako Mh Rais Samia, lakini napenda kutoa mtazamo tofauti ili kuboresha kwa kuwa bado una muda.
Rais wangu, asikudanganye mtu, Uongozi wa Nchi ni mambo makubwa, ni juu ya hatma ya kesho, sio leo tu, ni juu ya leo na vizazi vijavyo.

Nchi hii bado ni maskini sana, askidunganye mtu. Wanachi wetu bado ni fukara wa kutupwa, asikudanganye mtu yeyote.
Ninatembea kila kona ya Tz, wanachi wako bado ni fukara sana. Kupiga siasa pekee hakutawasaidia wananchi wako.

Hivi mheshimiwa Rais unajua zipo wilaya, % kubwa ya watu wake hawawezi hata kulipia hela ya kufungua jalada hospitali?
Ni Elfu 1 tu, lakini hana na hapo ni ugonjwa. Anaumwa kwelikweli!!!

Ngoja nizungumze kidogo kama Nyerere...

1. Tunataka Rais anayejua hali halisi za wanachi wake, kwamba Watanzania bado ni maskini sana.
Bado tu fukara sana. Bahati mbaya ni kwamba mfumo wetu wa kiuongozi unawatenga sana nyinyi mliojuu na sisi wa huku chini.
Ni hakika ukiwa Rais nchi hii huwezi abadani kuhisi shida za watu wako. Shida MFUMO. Shida WAPAMBE.
Watakwambia aaah!, mambo yako sawa Mheshimiwa..

Nitoe mfano halisi kwenye Uongozi wako.

Jana ukiwa na wanawake kwa mara ya pili, binafsi, nimekusikia ukisemea swala la maiti kuzuiwa ktk hospitali za umma ili kulipwa gharama za matibabu.

Ukasema (na uliwahi kusema), Wizara iangalie, labda mgonjwa awe anapewa bili yake kidogo kidogo kadri anavyoendelea na tiba!
MOYO WANGU UNAUMIA SANA.... Hebu Mh Rais yachimbe haya mambo kiundani. Wajue wananchi wako kiundani, itakusaidia. Wananchi wako ni fukara sana, asikudanganye mtu!!

Tatizo sio bili kidogo kidogo! Okay tuseme amelazwa, siku ya pili akapewa bili akashindwa kulipa yote, je madaktari wasitishe huduma ili alipe kwanza?!
Hivi maskini anayevumilia maumivu ya kichwa asiweze kununua panadol, ndiye wakupewa bili kidogo kidogo!

Wapo watakaonishambulia hapa, kwamba unataka Rais asemeje, watibiwe bure?! Okay wasikilize tu...

2. Tunataka Rais anayejua kwamba UJINGA, UMASKINI na MARADHI sasa ni maadui waliokubuhu.
Unaogopa nini kuvunja-vunja mfumo wa elimu yetu huu, uutengeneze upya?!
Tuna elimu ya ajabu, hata vitabu wanavyosoma watoto wetu leo havichangamshi akili hata kidogo.
Halafu hii ya kujenga shule moja ya wasichana kila mkoa, kwamba tunajaribu au? Hebu Mama acha Legacy, usijaribu-jaribu.

Tunahitaji Rais anayewajua Watanzania wote, kuanzia Machinga, Wakulima, Matajiri, Wafanyabiashara, Wafanyakazi, Wawekezaji, Rika zote, Rangi zote, Jinsi zote, Kabila zote, n.k.

Tunataka Rais anayejua kwa dhati kuwa huu ni "uzandiki" na huu ndio "ukweli", na akatae waziwazi uzandiki wowote ule hata kama umeletwa na rafiki/ndugu yake.

Tunataka Rais anayejua shida za watu wake, 'Matajiri na Maskini', maana wote tajiri na maskini wana shida/mahitaji.
Anayejua kuwa wote wanatakiwa kusaidiwa bila upendeleo, wala kukanyaga mgongo wa mwingine.

Naomba hii iwe part 1...

Asante Mh Rais kwa usikivu wako..
Sikia hakuna atakachofanya,kikawaridhisha watu wote,na hata akufanya hayo unayataka wewe,bado watatokea watu wamlaumu tu,hivyo afanye aonavyo yeye basi
 
Sikia hakuna atakachofanya,kikawaridhisha watu wote,na hata akufanya hayo unayataka wewe,bado watatokea watu wamlaumu tu,hivyo afanye aonavyo yeye basi
Hatuhitaji kuridhishwa, hapo ndio mnapopuyanga!
 
Mleta mada pole sana! Japo una mawazo mazuri sana lakini utasubiri sana.
Kwanini... Hayo yote ni matokeo ya mfumo tulioukumbatia na kuuweka madarakani. Ifahamike kuwa ccm kwa sasa haina dira, mwelekeo na itikadi rasmi!
ccm ishajitenga mbali sana na jembe na nyundo. Hivyo ni rahisi sana kwa serikali na viongozi watokanao na ccm kujitenga mbali sana na wananchi!!
Asante,
Kwa hiyo tuiache CCM ijiendee inavyoona, sio?!
 
Habari wana JF,

Binafsi nafurahia uongozi wako Mh Rais Samia, lakini napenda kutoa mtazamo tofauti ili kuboresha kwa kuwa bado una muda.
Rais wangu, asikudanganye mtu, Uongozi wa Nchi ni mambo makubwa, ni juu ya hatma ya kesho, sio leo tu, ni juu ya leo na vizazi vijavyo.

Nchi hii bado ni maskini sana, askidunganye mtu. Wanachi wetu bado ni fukara wa kutupwa, asikudanganye mtu yeyote.
Ninatembea kila kona ya Tz, wanachi wako bado ni fukara sana. Kupiga siasa pekee hakutawasaidia wananchi wako.

Hivi mheshimiwa Rais unajua zipo wilaya, % kubwa ya watu wake hawawezi hata kulipia hela ya kufungua jalada hospitali?
Ni Elfu 1 tu, lakini hana na hapo ni ugonjwa. Anaumwa kwelikweli!!!

Ngoja nizungumze kidogo kama Nyerere...

1. Tunataka Rais anayejua hali halisi za wanachi wake, kwamba Watanzania bado ni maskini sana.
Bado tu fukara sana. Bahati mbaya ni kwamba mfumo wetu wa kiuongozi unawatenga sana nyinyi mliojuu na sisi wa huku chini.
Ni hakika ukiwa Rais nchi hii huwezi abadani kuhisi shida za watu wako. Shida MFUMO. Shida WAPAMBE.
Watakwambia aaah!, mambo yako sawa Mheshimiwa..

Nitoe mfano halisi kwenye Uongozi wako.

Jana ukiwa na wanawake kwa mara ya pili, binafsi, nimekusikia ukisemea swala la maiti kuzuiwa ktk hospitali za umma ili kulipwa gharama za matibabu.

Ukasema (na uliwahi kusema), Wizara iangalie, labda mgonjwa awe anapewa bili yake kidogo kidogo kadri anavyoendelea na tiba!
MOYO WANGU UNAUMIA SANA.... Hebu Mh Rais yachimbe haya mambo kiundani. Wajue wananchi wako kiundani, itakusaidia. Wananchi wako ni fukara sana, asikudanganye mtu!!

Tatizo sio bili kidogo kidogo! Okay tuseme amelazwa, siku ya pili akapewa bili akashindwa kulipa yote, je madaktari wasitishe huduma ili alipe kwanza?!
Hivi maskini anayevumilia maumivu ya kichwa asiweze kununua panadol, ndiye wakupewa bili kidogo kidogo!

Wapo watakaonishambulia hapa, kwamba unataka Rais asemeje, watibiwe bure?! Okay wasikilize tu...

2. Tunataka Rais anayejua kwamba UJINGA, UMASKINI na MARADHI sasa ni maadui waliokubuhu.
Unaogopa nini kuvunja-vunja mfumo wa elimu yetu huu, uutengeneze upya?!
Tuna elimu ya ajabu, hata vitabu wanavyosoma watoto wetu leo havichangamshi akili hata kidogo.
Halafu hii ya kujenga shule moja ya wasichana kila mkoa, kwamba tunajaribu au? Hebu Mama acha Legacy, usijaribu-jaribu.

Tunahitaji Rais anayewajua Watanzania wote, kuanzia Machinga, Wakulima, Matajiri, Wafanyabiashara, Wafanyakazi, Wawekezaji, Rika zote, Rangi zote, Jinsi zote, Kabila zote, n.k.

Tunataka Rais anayejua kwa dhati kuwa huu ni "uzandiki" na huu ndio "ukweli", na akatae waziwazi uzandiki wowote ule hata kama umeletwa na rafiki/ndugu yake.

Tunataka Rais anayejua shida za watu wake, 'Matajiri na Maskini', maana wote tajiri na maskini wana shida/mahitaji.
Anayejua kuwa wote wanatakiwa kusaidiwa bila upendeleo, wala kukanyaga mgongo wa mwingine.

Naomba hii iwe part 1...

Asante Mh Rais kwa usikivu wako..

Maneno mazito haya:

" Rais wangu, asikudanganye mtu, Uongozi wa Nchi ni mambo makubwa, ni juu ya hatma ya kesho, sio leo tu, ni juu ya leo na vizazi vijavyo."

aliwahi kukimbiwa mwendazake hata siku moja?

Kiulinganifu mama yuko vizuri mno kuliko bwana yule ambaye hakukitendea haki cheo kile.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Maneno mazito haya:

" Rais wangu, asikudanganye mtu, Uongozi wa Nchi ni mambo makubwa, ni juu ya hatma ya kesho, sio leo tu, ni juu ya leo na vizazi vijavyo."

aliwahi kukimbiwa mwendazake hata siku moja?

Kiulinganifu mama yuko vizuri mno kuliko bwana yule ambaye hakukitendea haki cheo kile.

Au nasema uongo ndugu zangu?
hii nchi ilikuwa INANUKA ufisadi wa kutisha!!
kila Mteule ktk nafasi yoyote ile serikalini alikuwa anakwapua fedha za umma bila aibu!!
kulikuwa na matumizi ya ovyo, kila kiongozi akiumwa mafua alikuwa anaenda kutibiwa ulaya!!!
kila kiongozi alikuwa dalali wa rasilimali zetu.

Rais wetu wa sasa Mama Samia anapita ktk njia zile zile za kuziba myanya na kutunza rasilimali zetu.Hongera sana Mama Samia kwa msimamo madhubuti, tunakuamini na tunaimani sana.
 
hii nchi ilikuwa INANUKA ufisadi wa kutisha!!
kila Mteule ktk nafasi yoyote ile serikalini alikuwa anakwapua fedha za umma bila aibu!!
kulikuwa na matumizi ya ovyo, kila kiongozi akiumwa mafua alikuwa anaenda kutibiwa ulaya!!!
kila kiongozi alikuwa dalali wa rasilimali zetu.

Rais wetu wa sasa Mama Samia anapita ktk njia zile zile za kuziba myanya na kutunza rasilimali zetu.Hongera sana Mama Samia kwa msimamo madhubuti, tunakuamini na tunaimani sana.

Nchi hii ilikuwa imechezewa sana. Kila mteuliwa alikuwa design ya Ole, Kondakta nk. Wadhwalimu na wa haja waongo wa kupitiliza kama kina Wajaliwa.

Watu wakanyaswa nyaswa, wakatekwa, wakapotea nk. Achilia mbali waliotelekezewa Corona iwafutilie mbali.

Vipaumbele vilikuwa hamna. Ikawepo mipango ya kujenga hadi mabarabara ya ringi kupendezesha majiji na majizi wakati barabara kuu ambazo ni msingi wa uchumi zikiwa hoi.

Yakanunuliwa madege, hivi sasa yame paki jknia hayana kazi. CAG akawa hana ruhusa kuyakagua hayo wala tanroads, bot, TPA na ya namna hiyo.

Ya Corona nayo kuna asiyejua ilikuwa je?

Hakika nchi ikichezewa sana kama shamba la bibi tu. Mengine kama haya yangalipo leo kama mabaki mabaki ya utawala huo uliokuwa dhwalimu mno:


Vipi niendelee kuwataja hadi majina yao?
 
Nakuunga mkono Mkuu akifanya hivyo atajijengea legacy kubwa sana, lakini sioni akisimamia ajenda kubwa au kutokana na kushauriwa na waliomzunguka au matakwa yake binafsi. Tukumbuke huyo mama alikuwa ni mmoja wa waliokuwa vizingiti vikubwa katika lile bunge la katiba aliyesababisha tusiipate Katiba mpya ya rasimu ya Warioba.
Na wewe leo unaunga mkono aanze kufanya vitu vikubwa vikubwa?!!!, unweza kuvitaja, maana mwendazake alifanya hivyo vikubwa , lakini kila siku unamtukana.

hebu tutajie hivyo vitu vikubwa zaidi ya alivyofanya mwendazake.
 
  • Thanks
Reactions: nao
Kwani Magufuli alikuwa ana akili au alikithiri kwa kutumia mabavu? Ndani ya miaka 5+ aliyokaa madarakani deni la taifa limepaa kwa 30t+. Ukiambiwa uonyeshe hiyo miradi ya 30t wala hutoweza. Usichanganye akili na kiburi cha madaraka.
Hayo manufaa ya 30 tr utayaona ndani ya miaka 15 ijayo wakati miradi yake itakapokuwa imekamilika,

miradi bado inawndelea kujengwa, hapo ndio utakuwa na sababu ya kulilia hizo tr30 zako.
Au unajifanya hujui lengo la kukopa hizo pesa?
 
Hayo manufaa ya 30 tr utayaona ndani ya miaka 15 ijayo wakati miradi yake itakapokuwa imekamilika,

miradi bado inawndelea kujengwa, hapo ndio utakuwa na sababu ya kulilia hizo tr30 zako.
Au unajifanya hujui lengo la kukopa hizo pesa?

Kwa taarifa yako hizo 30t ilipaswa hiyo miradi iwe imeisha. Mradi wa SG ni 6.5t, na SGR ni 10t, na hakuna hata mradi mmoja kati ya hiyo uliofika nusu. Sasa hiyo 30t imeingia kwenye nini?
 
Mkuu sitaki kupinga ulichoeleza hapa. Hilo deni la taifa ukitaka kusikia raha sikiliza waziri Mkuu akilisema atataja figure yake, waziri wa fedha atataja figure yake na rais pia atataja figure yake. Ngoja tubaki kwenye hiyo figure yako ya 57t. Ukiangalia vizuri, hilo deni 1/3 ni kipindi cha miaka mitano tu, linganisha na miaka 54 ya marais wengine wote wanne waliopita. Je unaweza kunitajia miradi iliyopelekea deni kuwa kubwa hivyo, wakati serikali ya Magufuli ilikuwa inajinasibu kukusanya 1.3t@month?
Ndio maana tunasema Magufuli ni mwanaume, hivi hiyo miaka 54 unayoitaja kwa akili yako ni nini kilifanyika?

kulijengwa reli mpya, kulinunuliwa ndege mpya 12, kulijengwa meli mpya, kulijengwa vivuko, kulijengwa madaraja haya yanayojengwa leo,
Vipi mahospitari yalijengwa,

mastandi ya mabasi yalikuwepo, vipi vituo vya afya ktk hiyo miaka mitano tu.

tukikuambia una chuki mbaya na mwendazake unachukia mpaka unaziba macho kujifanya huoni chochote.
 
Habari wana JF,

Binafsi nafurahia uongozi wako Mh Rais Samia, lakini napenda kutoa mtazamo tofauti ili kuboresha kwa kuwa bado una muda.
Rais wangu, asikudanganye mtu, Uongozi wa Nchi ni mambo makubwa, ni juu ya hatma ya kesho, sio leo tu, ni juu ya leo na vizazi vijavyo.

Nchi hii bado ni maskini sana, askidunganye mtu. Wanachi wetu bado ni fukara wa kutupwa, asikudanganye mtu yeyote.
Ninatembea kila kona ya Tz, wanachi wako bado ni fukara sana. Kupiga siasa pekee hakutawasaidia wananchi wako.

Hivi mheshimiwa Rais unajua zipo wilaya, % kubwa ya watu wake hawawezi hata kulipia hela ya kufungua jalada hospitali?
Ni Elfu 1 tu, lakini hana na hapo ni ugonjwa. Anaumwa kwelikweli!

Ngoja nizungumze kidogo kama Nyerere.

1. Tunataka Rais anayejua hali halisi za wanachi wake, kwamba Watanzania bado ni maskini sana.
Bado tu fukara sana. Bahati mbaya ni kwamba mfumo wetu wa kiuongozi unawatenga sana nyinyi mliojuu na sisi wa huku chini.
Ni hakika ukiwa Rais nchi hii huwezi abadani kuhisi shida za watu wako. Shida MFUMO. Shida WAPAMBE.
Watakwambia aaah!, mambo yako sawa Mheshimiwa.

Nitoe mfano halisi kwenye Uongozi wako.

Jana ukiwa na wanawake kwa mara ya pili, binafsi, nimekusikia ukisemea swala la maiti kuzuiwa ktk hospitali za umma ili kulipwa gharama za matibabu.

Ukasema (na uliwahi kusema), Wizara iangalie, labda mgonjwa awe anapewa bili yake kidogo kidogo kadri anavyoendelea na tiba!
MOYO WANGU UNAUMIA SANA.

Hebu Mh Rais yachimbe haya mambo kiundani. Wajue wananchi wako kiundani, itakusaidia. Wananchi wako ni fukara sana, asikudanganye mtu!!

Tatizo sio bili kidogo kidogo! Okay tuseme amelazwa, siku ya pili akapewa bili akashindwa kulipa yote, je madaktari wasitishe huduma ili alipe kwanza?

Hivi maskini anayevumilia maumivu ya kichwa asiweze kununua panadol, ndiye wakupewa bili kidogo kidogo!

Wapo watakaonishambulia hapa, kwamba unataka Rais asemeje, watibiwe bure?! Okay wasikilize tu.

2. Tunataka Rais anayejua kwamba UJINGA, UMASKINI na MARADHI sasa ni maadui waliokubuhu.

Unaogopa nini kuvunja-vunja mfumo wa elimu yetu huu, uutengeneze upya?

Tuna elimu ya ajabu, hata vitabu wanavyosoma watoto wetu leo havichangamshi akili hata kidogo.

Halafu hii ya kujenga shule moja ya wasichana kila mkoa, kwamba tunajaribu au? Hebu Mama acha Legacy, usijaribu-jaribu.

Tunahitaji Rais anayewajua Watanzania wote, kuanzia Machinga, Wakulima, Matajiri, Wafanyabiashara, Wafanyakazi, Wawekezaji, Rika zote, Rangi zote, Jinsi zote, Kabila zote, n.k.

Tunataka Rais anayejua kwa dhati kuwa huu ni "uzandiki" na huu ndio "ukweli", na akatae waziwazi uzandiki wowote ule hata kama umeletwa na rafiki/ndugu yake.

Tunataka Rais anayejua shida za watu wake, 'Matajiri na Maskini', maana wote tajiri na maskini wana shida/mahitaji.
Anayejua kuwa wote wanatakiwa kusaidiwa bila upendeleo, wala kukanyaga mgongo wa mwingine.

Naomba hii iwe part 1

Asante Mh Rais kwa usikivu wako.
Asante comrade napata hisia ya kwamba ungependekeza mambo makubwa kadhaa yenye national inclusivity na longterm. Umeeleweka barikiwa
 
Kwa taarifa yako hizo 30t ilipaswa hiyo miradi iwe imeisha. Mradi wa SG ni 6.5t, na SGR ni 10t, na hakuna hata mradi mmoja kati ya hiyo uliofika nusu. Sasa hiyo 30t imeingia kwenye nini?
Unafikiri kujenga reli ni sawasawa na kujenga choo,
Umeona mradi wowote umesimama,
Au unafikiri hizo tr30 zinatolewa kwa mkupuo.
Ngoja nikueleweshe, hizo tr 30 zako inawezekana mpaka sasa zimetolewa tr 10,

hizo zilizobakia uje uziulize utakapoona miradi kama ya umeme wa rufiji imekamilika
 
Sasa hivi ni vigumu kutofautisha uzalendo na ujinga. Sema hivi, siku nikikubali kuwa mjinga kama utakavyo, nije unilishe Matango pori. Kimsingi nilijua huna jipya zaidi ya kuleta mawazo ya fuata mkumbo.
Tindo, mwombe Mwenyeji Mungu sana akusaidie kujijua jinsi ulivyo mjinga na roho mbaya, yaani kiufupi ujitambue
 
Back
Top Bottom