Rais Samia; Urais wa nchi ni mambo makubwa

Rais Samia; Urais wa nchi ni mambo makubwa

Tuongeze vyanzo vya mapato hapo ndipo tutaweza kusema wazee na watoto wote matibabu bure.....umasikini mkubwa sana vijijini huko hata buku kwa siku mtu hapati...ni shida sasa Rais atafanyeje ? Kwa sasa hana ubavu wowote hata aje nani ....labda siku tukipata pesa za mafuta uganda zitasaidia sana mno boast revenue ....kupunguza makali umasikini ....masna watalipa pesa kubwa sana mwaka 75% bajeti yetu sasa....hapo tutajidai kidogo kupambana umasikini lakini sio kwa bajeti hii 65% tunasaidiwa donors.....
 
Tuongeze vyanzo vya mapato hapo ndipo tutaweza kusema wazee na watoto wote matibabu bure.....umasikini mkubwa sana vijijini huko hata buku kwa siku mtu hapati...ni shida sasa Rais atafanyeje ? Kwa sasa hana ubavu wowote hata aje nani ....labda siku tukipata pesa za mafuta uganda zitasaidia sana mno boast revenue ....kupunguza makali umasikini ....masna watalipa pesa kubwa sana mwaka 75% bajeti yetu sasa....hapo tutajidai kidogo kupambana umasikini lakini sio kwa bajeti hii 65% tunasaidiwa donors.....
MKUU PESA ZIPO TENA NYINGI SANA.
Tazama huko bungeni na BOT wanavyokula helza zetu kwa kulipana mabilioni....
 
Naungana na wewe nchi ina matatizo makubwa sana hasa ukishuka wilayani kwa wananchi wa hali ya chini. Isipowekwa mikakati madhubuti na ufuatiliaji makini hali itakua mbaya sana huku chini. Wiki mbili zilizopita nimepita kijiji kimoja nimekuta zahanati imefungwa muuguzi na tabibu wote wameenda semina nilijiuliza maswali mengi sana hela za dawa hakuna ila hela za semina zipo na niliambiwa wanakimbizana kumaliza hela kabla mwaka wa serikali haujaisha.
Lakini si JPM alitupeleka uchumi wa kati?,huyu SAMIA anatupeleka wapi wakuu?
 
Huyu mama amechemka mapema sn hii kazi ni ngumu haiwezi
Hii kazi ilikua ya JPM,kuteka teka watu,kuongopa data,kuvunja katiba,kutoajili raia........kuua upinzani.......JK na Samia hii nchi wameonesha kufeli......viva JPM
 
Nilishangaa, halafu anasema eti kidogo kidogo tunaenda.

Na hii ya kujenga shule moja ya Bweni ya Wasichana kila mkoa.

SERIOUS?

Ni kama anafanya 'favour' au anatoa zawadi.

Tunawezaje kupaka rangi tatizo kubwa tena ktk 'level' ya Urais?

Mambo mengin hata washauri wake waone aibu.

Hiyo ya mashuka 200 haikutakiwa hata kutangazwa in public.
Nzuri ni ile ya kuchota mahela ikulu halafu kila anayelalamika njiani unamgawia burungutu.....viva JPM[emoji16][emoji122]
 
Inasikitisha sana kuona fedha za matumizi ya kawaida kuliko zinazotengwa Kwa miradi ya maendeleo,

Halafu Bado tunawapa maskini hao hao mzigo wa mikopo kwa miradi isiyokuwa na faida za kuonekana.

Nadhani ipo haja Kwa serikali kupunguza Matumizi makubwa yasiyokuwa na tija na kuelekeza fedha kwa miradi itakayolenga kubadili maisha ya watanzania wenye hali za chini.
Samia ndio kaleta hii mikopo,JPM alikua anatumia vyanzo vya ndani .
Note:Nyerere hadi kikwete Deni la taifa trillioni 40,JPM Deni la taifa trillioni 37[emoji16][emoji16][emoji16]
 
Afya ni eneo nyeti Sana Watanzania wengi wanapoteza maisha na kudhalilika Sana hospitali hata za umma kwa kukosa pesa.
JPM si akiingia hii nchi uchumi wa kati?......imekuaje tena wakuu?,huyu Samia anatupeleka wapi?[emoji16]
 
Tumpe muda gani zaidi? Tangu March Hadi Sasa hajamaliza kuteua . Bado madc,maded wa halmashauri,,makatibu tawala. Speed yake ni ndogo sana sana. Songwe na kigoma atafika lini?
Huko JPM alishaipeleka.nchi uchumi wa kati.......nchi hii ni tajiri sana,sisi ni Tanzania mpya A+,[emoji16][emoji16]
 
Watanzania tumebakia kuimba tu mapambio ya kauli mbiu za viongozi wao wakiendelea kurithishana nafasi zenye neema na familia zao.

Tulianza kusikia nyimbo za Kilimo Kwanza, Tanzania ya Viwanda na Sasa 50/50.

Nadhani ni Hofu tu ya watawala kwamba wakitukwamua kiuchumi watakosa wa kuwatawala woga usiokuwa na mantiki yeyote.
Rais anayejenga uwanja wa ndege kijijini kwao,ilhali akiacha sehemu zenye potential yakitalii na kibiashara bila hio huduma,atakukwamua wewe kiuchumi.......umerogwa wewe[emoji16][emoji3]
 
Inashangaza sana kumsikia huyo mama eti deni lilipwe kidogo kidogo! Kwa vipato gani walivyo navyo asilimia kubwa ya Watanzania kuweza kulipa deni la milioni na ushee wakati hata mlo mmoja tu wa siku wataupata vipi hawajui. The so called Viongozi hawajui lolote kuhusu ufukara wa kutisha unaowakabili Watanzania wengi sana.
Wananchi si mafukara,sisi ni matajiri,sisi tupo uchumi wa kati,sisi hatukopi.....JPM aliingiza hii nchi kwenye uchumi wa kati
 
  • Kicheko
Reactions: BAK
Binafsi hii nchi aliiweza magufuli peke ake, ili maendeleo yawepo uvunjifu wa mfumo wa kidemokrasia lazima uwepo. hivi viatu alivyovaa mama etu mpendwa ni vigumu na vinahitaji utulivu wa mwili na akili, kwa mwanamke ambaye ameumbwa kuongozwa hawezi kutufikisha popote. unajua hayati hakuwa akimsikiliza kila mtu alifanya vile akili yake ilivyomtuma maana alijua miluzi mingi humpoteza mbwa pia alijua kuwa nchi haijengwi kwa siasa bali kwa jasho na damu na ndo maana alikuwa tayari kupoteza damu yake ili kuleta maendeleo yenye tija, tuache kuwa wabinafsi richa ya kuwa wananchi wengi ni fukara ila hayati alipambana kuijenga nchi kuwaacha wananchi wanaumia ili vizazi vyao vije vifurahie matunda ya jasho za baba zao, ila watanzania wengi hatupo tayari kujitoa kwaajili ya future ya watoto wetu, kila mmoja ana roho ya ubinafsi anaona ni bora aje ateseke mtoto wake ila yeye ale matunda ya nchi. na ndo maana hatukusita kumpinga. Ok turudi kwenye mada, katika kitu cha umuhimu ambacho raisi anatakiwa kukifanya ni kuhakikisha anabadilisha mfumo wa elimu na kuongeza idadi ya technical schools and colleges ili kutengeneza watu wanaoweza kujiajili, pia angewekeza katika kuwapa sapoti local inovators ili kuikuza teknolojia yetu maana hili litapunguza cost burden kwenye foreign importation, huenda maraisi waliopita wangewasapoti local inovators sasa ivi tungekuwa tunatengeneza magari yetu wenyewe, viwanda vingekua, un employment rate ingepungua, kilimo kingebadirika na watu wangevuna mpaka wasingekuwa na mahali pa kuvipeleka vyakula, ila kwa sababu mawazo yao yamefungwa ndo maana akitokea mtu amegundua kitu anasainiwa na mataifa ya kibeberu ili wakawanufaishe wazungu waje watunyonye wakati sisi tunamuona mpuuzi eti hakina quality kitahatarisha maisha ya watu ivii mmesahau kuwa hata britain iliyosumbua kuwa na viwanda vikubwa karne ya 16 walianza na mfumo mdogo (stem engine)?. nchi yetu inahitaji raisi mwenye fikra za kujilisha wenyewe na sio kuombaomba maana hata marekani inapasua vichwa kwa kuwa ba uchumi mkubwa duniani kwa sababu ilipata maraisi wenye akili, wenye kushindana kuiondoa nchi kutoka kwenye umasikini na sio kushindana kwa kiki, tukiendelea kukaza vichwa tutabaki nyumanyuma kama koti la babu msizilo, wazungu wataendelea kututafuna vichwa wakati sisi tukiendelea kuwachekea.
yangu ni hayo tu wakuu.[emoji120][emoji120]
JPM aliiweza hii nchi.......Nyerere hadi Kikwete walikopa trillioni 40,JPM pekee yake alikopa Trillioni 27........JK alitoa ajira kwa kada ya elimu na afya kila wanaomaliza shule......JPM hata waliokuepo aliwafukiza........JK alijenga miundombinu bila upendeleo.......JPM alijenga kijijini kwake chato tu......
Ni kweli....JPM aliiweza hii nchi hadi kufika uchumi wa kati[emoji3][emoji16][emoji122][emoji122]
 
Hapaka, mpaka Juni 2015 deni la taifa lilikuwa 38.2 Trilioni. Magufuli kaondoka deni likiwa 57 Trilioni. Ni ongezeko la 19 Trilioni.

Kambuka juzi tu World Bank wamekubali kitukopesha 2.3 Trilioni wakati mama ana miezi 3 tu. Kama tunaangalia ukuaji wa deni, tusibiri miaka 5 tuone.
Muda ndio utaweza kumfananisha JPM na Samia......kama tu ulivoweza kumtofautisha kati ya JK na JPM......................msomi yeyote hupima Takwimu katika muda kama factor muhimu[emoji120][emoji3578][emoji419]
 
Habari wana JF,

Binafsi nafurahia uongozi wako Mh Rais Samia, lakini napenda kutoa mtazamo tofauti ili kuboresha kwa kuwa bado una muda.
Rais wangu, asikudanganye mtu, Uongozi wa Nchi ni mambo makubwa, ni juu ya hatma ya kesho, sio leo tu, ni juu ya leo na vizazi vijavyo.

Nchi hii bado ni maskini sana, askidunganye mtu. Wanachi wetu bado ni fukara wa kutupwa, asikudanganye mtu yeyote.
Ninatembea kila kona ya Tz, wanachi wako bado ni fukara sana. Kupiga siasa pekee hakutawasaidia wananchi wako.

Hivi mheshimiwa Rais unajua zipo wilaya, % kubwa ya watu wake hawawezi hata kulipia hela ya kufungua jalada hospitali?
Ni Elfu 1 tu, lakini hana na hapo ni ugonjwa. Anaumwa kwelikweli!

Ngoja nizungumze kidogo kama Nyerere.

1. Tunataka Rais anayejua hali halisi za wanachi wake, kwamba Watanzania bado ni maskini sana.
Bado tu fukara sana. Bahati mbaya ni kwamba mfumo wetu wa kiuongozi unawatenga sana nyinyi mliojuu na sisi wa huku chini.
Ni hakika ukiwa Rais nchi hii huwezi abadani kuhisi shida za watu wako. Shida MFUMO. Shida WAPAMBE.
Watakwambia aaah!, mambo yako sawa Mheshimiwa.

Nitoe mfano halisi kwenye Uongozi wako.

Jana ukiwa na wanawake kwa mara ya pili, binafsi, nimekusikia ukisemea swala la maiti kuzuiwa ktk hospitali za umma ili kulipwa gharama za matibabu.

Ukasema (na uliwahi kusema), Wizara iangalie, labda mgonjwa awe anapewa bili yake kidogo kidogo kadri anavyoendelea na tiba!
MOYO WANGU UNAUMIA SANA.

Hebu Mh Rais yachimbe haya mambo kiundani. Wajue wananchi wako kiundani, itakusaidia. Wananchi wako ni fukara sana, asikudanganye mtu!!

Tatizo sio bili kidogo kidogo! Okay tuseme amelazwa, siku ya pili akapewa bili akashindwa kulipa yote, je madaktari wasitishe huduma ili alipe kwanza?

Hivi maskini anayevumilia maumivu ya kichwa asiweze kununua panadol, ndiye wakupewa bili kidogo kidogo!

Wapo watakaonishambulia hapa, kwamba unataka Rais asemeje, watibiwe bure?! Okay wasikilize tu.

2. Tunataka Rais anayejua kwamba UJINGA, UMASKINI na MARADHI sasa ni maadui waliokubuhu.

Unaogopa nini kuvunja-vunja mfumo wa elimu yetu huu, uutengeneze upya?

Tuna elimu ya ajabu, hata vitabu wanavyosoma watoto wetu leo havichangamshi akili hata kidogo.

Halafu hii ya kujenga shule moja ya wasichana kila mkoa, kwamba tunajaribu au? Hebu Mama acha Legacy, usijaribu-jaribu.

Tunahitaji Rais anayewajua Watanzania wote, kuanzia Machinga, Wakulima, Matajiri, Wafanyabiashara, Wafanyakazi, Wawekezaji, Rika zote, Rangi zote, Jinsi zote, Kabila zote, n.k.

Tunataka Rais anayejua kwa dhati kuwa huu ni "uzandiki" na huu ndio "ukweli", na akatae waziwazi uzandiki wowote ule hata kama umeletwa na rafiki/ndugu yake.

Tunataka Rais anayejua shida za watu wake, 'Matajiri na Maskini', maana wote tajiri na maskini wana shida/mahitaji.
Anayejua kuwa wote wanatakiwa kusaidiwa bila upendeleo, wala kukanyaga mgongo wa mwingine.

Naomba hii iwe part 1

Asante Mh Rais kwa usikivu wako.
We must highlight all issues we need our President to put them right. This must not be restricted to her, we shall extend it to the next Presidents . Never should we be hindered by many good for nothing imbeciles.
 
Baada ya Nyerere wamepita marais wangapi,
Nampenda sana Nyerere, lakini Nyerere ndio alijenga reli ya kati, hiyo TAZARA inaprogress vipi mpaka leo,
Unajua hayo mabwawa ya Nyerere yanatoa MEGAWATTS ngapi kuendana na populations ya leo ( hazifiki hata 600), compare na Mwendazake,
Hizo ndege zipo wapi sasa hivi!

hivi unakumbuka kama Taifa tulifikia kukodisha ndege kama national carrier ALLIANCE AIR) na tukaishia kupigwa tu,

leo taifa lina ndege zake unaishia kubeza,,!!

MSWAHILI BWANA ni shida tu,

Hebu twende taratibu kisha ujipime. 2014 kabla ya Magufuli kuwa rais tulikuwa tunaimbishwa kama watoto wadogo kuhusu umeme wa gas, wakati huo Magufuli alikuwa waziri na yeye alibariki suala la umeme wa gas. Tukakopa $1.3b sawa na 3t kujenga bomba la gas toka Mtwara, tuliambiwa kwenye umeme wa Gas tutazalisha 5,000m, na kweli bomba liko hapa Dar na uzalishaji umeanza kiwango 450mg kama sikosei, ukichanganya na umeme wa vyanzo vingine tuna umeme 1,500m+. Inakuwaje Magufuli awe rais aanze mradi mpya wa maji wa 6.5t utakaozalisha 2,115m aache wa gas utakaozalisha 5,000? Tena anatumia maji, ambapo akiwa waziri alikuwa ni mmoja ya waliotumanisha tatizo la umeme wa maji ni mabadiliko ya tabia nchi? Je angeweka 2.5t asingeweza kuzalisha 2,115m hapo kwenye gas ambapo tayari bomba liko hapa Dar, na fedha zinazobaki zikiingia kwingine? Hilo ni moja.

Tuje kwenye hilo la ndege, sina popote ninapobeza kuwa na ndege, ila ndege zilipaswa kuwa kipaombele cha mwisho dhidi ya vipaombele vingine. Ama ni bora angenunua ndege nyingi ndogo za ndani kuwezesha safari za ndani, kuliko hizo za masafa marefu wakati ushindani wa biashara hiyo kimataifa kwetu ni mdogo. Kuliko kuwekeza 1.8t kwenye ndege alizonunua, angeweza kujenga viwanda vya kimkakati kwenye maeneo yalimayo pamba, korosho, kahawa, tumbaku nk vya wangalua 50b@, kisha atoe ajira. Ama basi angejeja shule za VETA kila mkoa ymza 10b@ vijana wapate ujuzi. Kama una akili nzuri ulipaswa kujiuliza mambo hayo, na sio kusubiri kulishwa propaganda na kuanza kusifia kama kipofu.
 
Hahahahahahaha eti dhalimu alifanya vitu vikubwa 🤣🤣🤣🤣🤣🤣 vitu vikubwa vipi hivyo? Bomoa bomoa? Kuteka na kubambikia kesi? Kununua ndege zilizoingiza hasara ya karibu bilioni 400? Kudharau katiba, mahakama na Bunge? Kufanya mauaji dhidi ya raia wasio na hatia? Kujichotea trillions hazina kinyemela? Hebu acha kuandika UPUUZI!!!!
Na wewe leo unaunga mkono aanze kufanya vitu vikubwa vikubwa?!!!, unweza kuvitaja, maana mwendazake alifanya hivyo vikubwa , lakini kila siku unamtukana.

hebu tutajie hivyo vitu vikubwa zaidi ya alivyofanya mwendazake.
 
Hapaka, mpaka Juni 2015 deni la taifa lilikuwa 38.2 Trilioni. Magufuli kaondoka deni likiwa 57 Trilioni. Ni ongezeko la 19 Trilioni.

Kambuka juzi tu World Bank wamekubali kitukopesha 2.3 Trilioni wakati mama ana miezi 3 tu. Kama tunaangalia ukuaji wa deni, tusibiri miaka 5 tuone.
Naomba kueleweshwa kidogo kuhusu ukubwa wa deni la taifa.
Hili deni huwa linathaminishwa kwa Tsh au USD?
Hoja yangu iko hapa; mwaka 2015 wakati JPM anaingia madarakani thamani ya tsh ilikuwa 1800+ kwa dola moja ya marekani na kufikia 2021 thamani imepanda hadi 2300+. Je,kama 2015 mlidaiwa tsh 38T za kitanzani,thamani yake itaendelea kuwa hiyo hiyo au itabadilika kulingana na kupanda ama kushuka kwa dola ya marekani?
Samahani kama niko nje kidogo ya mada ila kuna utata kuhusu nani amelikuza hili deni parefu kati ya marais 3 waliopita.
 
Back
Top Bottom