Rais Samia; Urais wa nchi ni mambo makubwa

Rais Samia; Urais wa nchi ni mambo makubwa

Mkuu umeguswa sana manake hilo neno "asikudanganye mtu" umelitumia sijui mara ngapi!! Hahaaaa....

Nikirudi kwenye mada yako, ni kweli nchi hii ina matatizo mengi na mengine ni sugu haswa mpaka wengine hasa yanaowasibu wameamua tu kutokulalamika tena. Wamepoteza tumaini.

Ila naamini SSH anayajua vizuri tu, cha muhimu tukubaliane mzigo wa matatizo uliopo ni mkubwa kuliko hata uwezo wa nchi. Kwahiyo tusirumie muda mwingi kumlaumu/kumlalamikia Rais. Tunapaswa sote tuyabebe matatizo ya nchi hii na kutapatia ufumbuzi.

Watanzania tuna kasumba ya kutupia viongozi mzigo halafu tayari tunajiona kama tumeshatimiza wajibu wetu.

Kila mtu ana wajibu kwake mwenyewe, familia yake na Taifa lake.
Ume-conclude topic
 
alikuwa mkatili kwa nataifa ya nje. ila kwa nchi yake alikuwa mzalendo the same kwa hayati, aliwatimua wapiga bingo mjini ili aijenge nchi watu wake waje wafaidi.
Huna lolote ujualo zaidi ya kupiga siasa mfu hapa jukwaani.
 
Habari wana JF,

Binafsi nafurahia uongozi wako Mh Rais Samia, lakini napenda kutoa mtazamo tofauti ili kuboresha kwa kuwa bado una muda.
Rais wangu, asikudanganye mtu, Uongozi wa Nchi ni mambo makubwa, ni juu ya hatma ya kesho, sio leo tu, ni juu ya leo na vizazi vijavyo.

Nchi hii bado ni maskini sana, askidunganye mtu. Wanachi wetu bado ni fukara wa kutupwa, asikudanganye mtu yeyote.
Ninatembea kila kona ya Tz, wanachi wako bado ni fukara sana. Kupiga siasa pekee hakutawasaidia wananchi wako.

Hivi mheshimiwa Rais unajua zipo wilaya, % kubwa ya watu wake hawawezi hata kulipia hela ya kufungua jalada hospitali?
Ni Elfu 1 tu, lakini hana na hapo ni ugonjwa. Anaumwa kwelikweli!!!

Ngoja nizungumze kidogo kama Nyerere...

1. Tunataka Rais anayejua hali halisi za wanachi wake, kwamba Watanzania bado ni maskini sana.
Bado tu fukara sana. Bahati mbaya ni kwamba mfumo wetu wa kiuongozi unawatenga sana nyinyi mliojuu na sisi wa huku chini.
Ni hakika ukiwa Rais nchi hii huwezi abadani kuhisi shida za watu wako. Shida MFUMO. Shida WAPAMBE.
Watakwambia aaah!, mambo yako sawa Mheshimiwa..

Nitoe mfano halisi kwenye Uongozi wako.

Jana ukiwa na wanawake kwa mara ya pili, binafsi, nimekusikia ukisemea swala la maiti kuzuiwa ktk hospitali za umma ili kulipwa gharama za matibabu.

Ukasema (na uliwahi kusema), Wizara iangalie, labda mgonjwa awe anapewa bili yake kidogo kidogo kadri anavyoendelea na tiba!
MOYO WANGU UNAUMIA SANA.... Hebu Mh Rais yachimbe haya mambo kiundani. Wajue wananchi wako kiundani, itakusaidia. Wananchi wako ni fukara sana, asikudanganye mtu!!

Tatizo sio bili kidogo kidogo! Okay tuseme amelazwa, siku ya pili akapewa bili akashindwa kulipa yote, je madaktari wasitishe huduma ili alipe kwanza?!
Hivi maskini anayevumilia maumivu ya kichwa asiweze kununua panadol, ndiye wakupewa bili kidogo kidogo!

Wapo watakaonishambulia hapa, kwamba unataka Rais asemeje, watibiwe bure?! Okay wasikilize tu...

2. Tunataka Rais anayejua kwamba UJINGA, UMASKINI na MARADHI sasa ni maadui waliokubuhu.
Unaogopa nini kuvunja-vunja mfumo wa elimu yetu huu, uutengeneze upya?!
Tuna elimu ya ajabu, hata vitabu wanavyosoma watoto wetu leo havichangamshi akili hata kidogo.
Halafu hii ya kujenga shule moja ya wasichana kila mkoa, kwamba tunajaribu au? Hebu Mama acha Legacy, usijaribu-jaribu.

Tunahitaji Rais anayewajua Watanzania wote, kuanzia Machinga, Wakulima, Matajiri, Wafanyabiashara, Wafanyakazi, Wawekezaji, Rika zote, Rangi zote, Jinsi zote, Kabila zote, n.k.

Tunataka Rais anayejua kwa dhati kuwa huu ni "uzandiki" na huu ndio "ukweli", na akatae waziwazi uzandiki wowote ule hata kama umeletwa na rafiki/ndugu yake.

Tunataka Rais anayejua shida za watu wake, 'Matajiri na Maskini', maana wote tajiri na maskini wana shida/mahitaji.
Anayejua kuwa wote wanatakiwa kusaidiwa bila upendeleo, wala kukanyaga mgongo wa mwingine.

Naomba hii iwe part 1...

Asante Mh Rais kwa usikivu wako..
Equation ya hiki unachokisema hapa hakiwezi kuwa triggered na mtu mmoja bali collective efforts.

Kuna makundi mawili ambayo haya hayawezi kubadili mentality zao kwakua wamejinasibu kama injini ya mambo kusonga.

Kundi la kwanza la play makers hawa wanajulikana kama watu wa system ambao ni TISS, JUDGES NA JWTZ top ranking official.

Kundi hilo hapo juu ndio moyo wa mambo kwenda au kukwama nchi hii na hawa wanakula 30% ya keki ya Taifa na nitakuambia kitu. They deserve kwakua a single mistake we are all doomed.

Kundi la pili ni la Wanasiasa na wakurugenzi hawa hawapitishi tu maslahi ya kundi la kwanza bali wanajiweka nao hapo na kwakua kundi la kwanza maslahi yao yanalindwa na kundi hili hawana muda wa kuhoji kwakua huzibwa midomo kwa kuongezewa ambacho hawajaomba.

Tatizo la kundi hili la pili hawastahili wanachopata wakiwa madarakani na hata baada ya kuondoka. Kwakua they are just matairi ambayo hayahitaji kutizamwa baada ya kuondolewa kwenye gari.

TATIZO LINAPOANZIA:
Kundi la pili linatakiwa kuja na mikakati ya kukusanya zaidi ili waweze kupeleka kwa wananchi baada ya kutenga fungu la kundi la kwanza.

Sasa hawa Wanasiasa na Wakurugenzi wanaishia kuuza nyago tu na hawana la maana wanalofanya.

Mfano:
TRA/BANDARI/HALMASHAURI NA MANISPAA hawana weledi katika majukumu yao ambapo ndipo fedha inapopotelea...

Hivi unadhani ni kiasi gani cha fedha serikali itakusanya iwapo itatoa kwa kila mfanyabiashara mwenye eneo shilingi 364,000/_ kwa mwaka kwa biashara anayofanya ambayo ni Sawa na shilingi 1000 tu kwa siku?

Manispaa/Halmashauri zikiamua kukusanya kodi ya majengo tu Tanzania nzima kila jengi shilingi 364,000/- kwa mwaka ambayo ni Sawa na hilo 1000 kwa siku?

Hivi TPA wakiamua kutoza 100,000 kwa kila contena ya 40ft inayopita bandarini pale?

Mambo ni mengi sema kundi la pili ndio kikwazo

Wasalaam
 
Equation ya hiki unachokisema hapa hakiwezi kuwa triggered na mtu mmoja bali collective efforts.

Kuna makundi mawili ambayo haya hayawezi kubadili mentality zao kwakua wamejinasibu kama injini ya mambo kusonga.

Kundi la kwanza la play makers hawa wanajulikana kama watu wa system ambao ni TISS, JUDGES NA JWTZ top ranking official.

Kundi hilo hapo juu ndio moyo wa mambo kwenda au kukwama nchi hii na hawa wanakula 30% ya keki ya Taifa na nitakuambia kitu. They deserve kwakua a single mistake we are all doomed.

Kundi la pili ni la Wanasiasa na wakurugenzi hawa hawapitishi tu maslahi ya kundi la kwanza bali wanajiweka nao hapo na kwakua kundi la kwanza maslahi yao yanalindwa na kundi hili hawana muda wa kuhoji kwakua huzibwa midomo kwa kuongezewa ambacho hawajaomba.

Tatizo la kundi hili la pili hawastahili wanachopata wakiwa madarakani na hata baada ya kuondoka. Kwakua they are just matairi ambayo hayahitaji kutizamwa baada ya kuondolewa kwenye gari.

TATIZO LINAPOANZIA:
Kundi la pili linatakiwa kuja na mikakati ya kukusanya zaidi ili waweze kupeleka kwa wananchi baada ya kutenga fungu la kundi la kwanza.

Sasa hawa Wanasiasa na Wakurugenzi wanaishia kuuza nyago tu na hawana la maana wanalofanya.

Mfano:
TRA/BANDARI/HALMASHAURI NA MANISPAA hawana weledi katika majukumu yao ambapo ndipo fedha inapopotelea...

Hivi unadhani ni kiasi gani cha fedha serikali itakusanya iwapo itatoa kwa kila mfanyabiashara mwenye eneo shilingi 364,000/_ kwa mwaka kwa biashara anayofanya ambayo ni Sawa na shilingi 1000 tu kwa siku?

Manispaa/Halmashauri zikiamua kukusanya kodi ya majengo tu Tanzania nzima kila jengi shilingi 364,000/- kwa mwaka ambayo ni Sawa na hilo 1000 kwa siku?

Hivi TPA wakiamua kutoza 100,000 kwa kila contena ya 40ft inayopita bandarini pale?

Mambo ni mengi sema kundi la pili ndio kikwazo

Wasalaam
Kaazi kweli kweli..
 
Naungana na wewe nchi ina matatizo makubwa sana hasa ukishuka wilayani kwa wananchi wa hali ya chini. Isipowekwa mikakati madhubuti na ufuatiliaji makini hali itakua mbaya sana huku chini. Wiki mbili zilizopita nimepita kijiji kimoja nimekuta zahanati imefungwa muuguzi na tabibu wote wameenda semina nilijiuliza maswali mengi sana hela za dawa hakuna ila hela za semina zipo na niliambiwa wanakimbizana kumaliza hela kabla mwaka wa serikali haujaisha.
Nchi imefunguliwa mkuu.

Tusubirie zile semina za kufanyika Dubai zitafunguliwa pia....
 
Nilishangaa, halafu anasema eti kidogo kidogo tunaenda.
Na hii ya kujenga shule moja ya Bweni ya Wasichana kila mkoa.
SERIOUS!??
Ni kama anafanya 'favour' au anatoa zawadi.
Tunawezaje kupaka rangi tatizo kubwa tena ktk 'level' ya Urais?!

Mambo mengin hata washauri wake waone aibu.

Hiyo ya mashuka 200 haikutakiwa hata kutangazwa in public.
Binafsi nilishangaa Rais wa nchi mashuka 200???!!!
 
Umeelezea vizuri. Hilo la elimu ni kweli kabisa. Lakini siyo elimu tu. Tanzania inahitaji kujitathmini upya. Tujiulize mbona kila rais anayeingia hafanikiwi na akimaliza muda anayeingia anakuwa kama anaanza upya? Jibu ni kuwa system yetu ya uongozi siyo nzuri kabisa. Tunatakiwa tufumue fumue kila kitu tuweke mfumo mzuri zaidi. Wanasiasi wamekuwa wengi na wako kila mahali. Ndiyo wanafanya kila jambo na mbaya zaidi wengi ni vilaza na matapeli waliokimbilia huko kwa sababu tu ni mabingwa wa kupiga gumzo. Tufumue mfumo wetu viongozi wawe wachache na asilimia ndogo tu wateuliwe na rais. Bila kufanya hivyo mama Samia hatakuwa na jipya tena atachokwa haraka sana.
Labda tupate serikali ya kijeshi!
 
Umeelezea vizuri. Hilo la elimu ni kweli kabisa. Lakini siyo elimu tu. Tanzania inahitaji kujitathmini upya. Tujiulize mbona kila rais anayeingia hafanikiwi na akimaliza muda anayeingia anakuwa kama anaanza upya? Jibu ni kuwa system yetu ya uongozi siyo nzuri kabisa. Tunatakiwa tufumue fumue kila kitu tuweke mfumo mzuri zaidi. Wanasiasi wamekuwa wengi na wako kila mahali. Ndiyo wanafanya kila jambo na mbaya zaidi wengi ni vilaza na matapeli waliokimbilia huko kwa sababu tu ni mabingwa wa kupiga gumzo. Tufumue mfumo wetu viongozi wawe wachache na asilimia ndogo tu wateuliwe na rais. Bila kufanya hivyo mama Samia hatakuwa na jipya tena atachokwa haraka sana.
Mkuu nakubaliana nawe kabisa juu ya matatizo yetu ya kiuchumi. Tatizo ni kwamba nani wa kufumua huo MFUMO? maana wanapaswa kuufumua ni wanufaika wa huo MFUMO.
 
Juzi mara baada ya mama kumaliza kikao nilimwambia wife, " kuanzisha shule moja ya wasichana kila mkoa ni wazo zuri lakini bado wazo hili la mheshimiwa Mama yetu lina njaa ya kutosha", akaniuliza kwa nini?

Unapoanzisha shule moja ya sayansi kwa wasichana maana yake umeangalia upande wa advance ambayo inategemea wasichana watoke huku O level waje kuilisha hii ya advance, sasa swali linakuja je vipi kuhusu usalama wa msichana anaetoka huku chini upoje?

Kumbuka shule nyingi za kata ambazo tunaziona mkombozi hazina mazingira salama. Ziko mbali sana na watoto wanatembea umbali mrefu hadi huruma. Wabunge wetu sijui michango yao juu ya suala la elimu huwa upoje, wamejikita kutoa shukrani na kupambia ngazi za juu kulingana na upepo unapobadilika yaani.
Kwa maoni yangu namshauri mama shule zote za kata ambazo wanafunzi wake hutembea umbali mrefu (hapa wataalamu wainishe ni kuanzia umbali upi) zijengewe mabweni kwa ajili ya watoto wote wa kike.
Na sheria zisimamiwe haswa na mtoto kipindi anaporipoti shule awe na sare peke tu ili kila mahali aendako awe na sare zitapunguza tatizo kwa kiasi kikubwa
 
Mleta mada pole sana! Japo una mawazo mazuri sana lakini utasubiri sana.
Kwanini... Hayo yote ni matokeo ya mfumo tulioukumbatia na kuuweka madarakani. Ifahamike kuwa ccm kwa sasa haina dira, mwelekeo na itikadi rasmi!
ccm ishajitenga mbali sana na jembe na nyundo. Hivyo ni rahisi sana kwa serikali na viongozi watokanao na ccm kujitenga mbali sana na wananchi!!
 
Habari wana JF,

Binafsi nafurahia uongozi wako Mh Rais Samia, lakini napenda kutoa mtazamo tofauti ili kuboresha kwa kuwa bado una muda.
Rais wangu, asikudanganye mtu, Uongozi wa Nchi ni mambo makubwa, ni juu ya hatma ya kesho, sio leo tu, ni juu ya leo na vizazi vijavyo.

Nchi hii bado ni maskini sana, askidunganye mtu. Wanachi wetu bado ni fukara wa kutupwa, asikudanganye mtu yeyote.
Ninatembea kila kona ya Tz, wanachi wako bado ni fukara sana. Kupiga siasa pekee hakutawasaidia wananchi wako.

Hivi mheshimiwa Rais unajua zipo wilaya, % kubwa ya watu wake hawawezi hata kulipia hela ya kufungua jalada hospitali?
Ni Elfu 1 tu, lakini hana na hapo ni ugonjwa. Anaumwa kwelikweli!!!

Ngoja nizungumze kidogo kama Nyerere...

1. Tunataka Rais anayejua hali halisi za wanachi wake, kwamba Watanzania bado ni maskini sana.
Bado tu fukara sana. Bahati mbaya ni kwamba mfumo wetu wa kiuongozi unawatenga sana nyinyi mliojuu na sisi wa huku chini.
Ni hakika ukiwa Rais nchi hii huwezi abadani kuhisi shida za watu wako. Shida MFUMO. Shida WAPAMBE.
Watakwambia aaah!, mambo yako sawa Mheshimiwa..

Nitoe mfano halisi kwenye Uongozi wako.

Jana ukiwa na wanawake kwa mara ya pili, binafsi, nimekusikia ukisemea swala la maiti kuzuiwa ktk hospitali za umma ili kulipwa gharama za matibabu.

Ukasema (na uliwahi kusema), Wizara iangalie, labda mgonjwa awe anapewa bili yake kidogo kidogo kadri anavyoendelea na tiba!
MOYO WANGU UNAUMIA SANA.... Hebu Mh Rais yachimbe haya mambo kiundani. Wajue wananchi wako kiundani, itakusaidia. Wananchi wako ni fukara sana, asikudanganye mtu!!

Tatizo sio bili kidogo kidogo! Okay tuseme amelazwa, siku ya pili akapewa bili akashindwa kulipa yote, je madaktari wasitishe huduma ili alipe kwanza?!
Hivi maskini anayevumilia maumivu ya kichwa asiweze kununua panadol, ndiye wakupewa bili kidogo kidogo!

Wapo watakaonishambulia hapa, kwamba unataka Rais asemeje, watibiwe bure?! Okay wasikilize tu...

2. Tunataka Rais anayejua kwamba UJINGA, UMASKINI na MARADHI sasa ni maadui waliokubuhu.
Unaogopa nini kuvunja-vunja mfumo wa elimu yetu huu, uutengeneze upya?!
Tuna elimu ya ajabu, hata vitabu wanavyosoma watoto wetu leo havichangamshi akili hata kidogo.
Halafu hii ya kujenga shule moja ya wasichana kila mkoa, kwamba tunajaribu au? Hebu Mama acha Legacy, usijaribu-jaribu.

Tunahitaji Rais anayewajua Watanzania wote, kuanzia Machinga, Wakulima, Matajiri, Wafanyabiashara, Wafanyakazi, Wawekezaji, Rika zote, Rangi zote, Jinsi zote, Kabila zote, n.k.

Tunataka Rais anayejua kwa dhati kuwa huu ni "uzandiki" na huu ndio "ukweli", na akatae waziwazi uzandiki wowote ule hata kama umeletwa na rafiki/ndugu yake.

Tunataka Rais anayejua shida za watu wake, 'Matajiri na Maskini', maana wote tajiri na maskini wana shida/mahitaji.
Anayejua kuwa wote wanatakiwa kusaidiwa bila upendeleo, wala kukanyaga mgongo wa mwingine.

Naomba hii iwe part 1...

Asante Mh Rais kwa usikivu wako..
Magufuli ndo aliturudisha nyuma kwa kusema nchi hii ni tajiri na inaweza kuwa donor country
 
Umewahi kuona wapi Rais wa nchi kwenda kugawa mashuka 200 hospitali serious?

Mashuka 200, hiyo siyo hata level ya mkuu wa Kata. Mashuka inabidi siku zote yawepo hospitalini.

Level ya Urais at very least ni kuzungumzia madawa, vitendea kazi, Mishahara, Budget ya wizara ya Afya, kusimamia manunuzi ya vifaa, madawa, ujenzi wa hospitali kwamba hatupigwi.
 
Rais Samia jana kamwaga yai la Malkia Elizabeth kwa kujiamini.

Inaonekana lile neno maarufu entrepreneur haliwezi kumsumbua namna ya kulitamka.
 
Back
Top Bottom