Tena Wawili uko nao katika Serikali yako ya sasa, Mmoja ni Mstaafu mkubwa mno na Wawili ni Wanawake ambao wanashirikiana na Wakubwa fulani pamoja na Wachina kadhaa.
Mheshimiwa Rais Samia Mimi Mwanao GENTAMYCINE napinga na nakataa kata kata kuwa Mgao wa Maji ulionza katika Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani na Morogoro ni kutokana na Ukame uliosababisha kina cha Maji ya Mto Ruvu kupungua Kina chake.
Mheshimiwa Rais Samia kuna Mteule wako Mmoja huko Mkoa wa Pwani ana Shamba Kubwa halina Mfano na Mabwawa Sita ya Kufuga Samaki aina ya Sato na Sangara ambapo nae ameyachepusha Maji ya Mto Ruvu na kutusababishia sasa akina GENTAMYCINE tutoke na Ndoo zetu Tegeta hadi Mbagala Kuu kutafuta hii Precious Liquid ( Water ) ili tusinuke hovyo 'Vikwapa' na 'Vizalisha Binadamu' vyetu vya Kutukuka.
Wadadisi Sie hatudanganyiki hovyo.
Cc:
Bujibuji Simba Nyamaume,
adriz,
Bila bila,
Daudi Mchambuzi etc.
Rais Samia alisema suala la uhaba wa upatikanaji wa maji Mkoa wa Dar es Salaam lina sura mbili - za asili na zinazosababishwa na wanadamu.
"Kwa kiasi kikubwa kupungua maji Mto Ruvu ni matendo yetu wenyewe, tumeambiwa hapa mkoa ule unakata miti kwa kiasi kikubwa, ardhi inakauka. Vyanzo vidogo vinakauka, maji hayaendi, na yale yanayokwenda unakuta njiani watu wameweka vizuizi maji hayawezi kwenda," "Unakuta mashine kubwa zimewekwa, 'wanapampu' maji kwenda kwenye mashamba, mashamba ya wageni wala siyo mashamba ya wenyeji wa eneo lile, unakuta vizuizi kadhaa watu wamejenga mabwawa humo ndani wanafuga samaki humo," alisema.
Kutokana na kadhia hiyo, Rais Samia aliwaagiza wakuu hao wa mikoa Dar es Salaam na Pwani pamoja na DAWASA kuhakikisha wanakwenda kuondoa vizuizi vyote Mto Ruvu.
"Nilizungumza na DAWASA wakasema wamefanya operesheni mwezi uliopita, binadamu ni mzito sana inawezekana mmepita mwezi uliopita mlipoondoka tayari wameweka vizuizi, ninaomba mwende kuzunguka, kama ni kupita kwa helkopta au miguu kama mtakwenda kwa magari yenu, ninataka msafishe mto maji yaende yakachangie upatikanaji wa maji," aliagiza.
Rais Samia pia alimtaka Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kwenda kuhakikisha maagizo aliyotoa ya kuunganisha lita 70,000 za maji kutoka Kigamboni kwenda Dar es Salaam yanafanyiwa kazi kwa kuwa fedha tayari zimeshatoka ili kupunguza makali ya uhaba wa maji uliopo.
Alisema Dar es Salaam ina miundombinu mikongwe ya usambazaji maji na mingine ilijengwa wakati mkoa huo ukiwa na watu milioni tatu lakini sasa una wakazi milioni tano.
"Wanaohusika na maji, DAWASA na Wizara ya Maji waangalie pia muunganisho wa maji ndani ya jiji hili kwa sababu ukisoma kazi iliyofanywa, Dar es Salaam ina uwezo wa kupata maji kwa asilimia 100 kuanzia mwaka 2023 lakini bado maeneo mengine wanalia.
"Sababu nyingine ni ujenzi holela, ndani ya Dar es Salaam watu wamejijengea tu kiasi ambacho mabomba hayawezi kupita, mfumo wowote hauwezi, bali ni kuchimba tu visima na kutoa maji kwa watu. Mkuu wa Mkoa wa sekta husika ninataka myasimamie hayo na Waziri Mkuu atawasimamia," aliagiza.
Mkuu wa Nchi alisema utatuzi wa muda mrefu wa uhaba wa maji mkoani humo ni kujenga Bwawa la Kidunda ambalo mkataba wake ulitiwa saini juzi na serikali imeshatenga fedha za kuanza ujenzi wake.
Alisema bwana hilo litachukua muda mrefu kukamilika na itachukua miaka miwili kujaa maji kutegemea mvua itakavyonyesha.
"Lakini, miaka minne mitano, sita mbele Dar es Salaam itakuwa na akiba kubwa ya maji ya kutosha," Rais Samia alisema. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla, akitoa salamu za mkoa huo, alimweleza Rais kazi ambayo walielekezwa kuhusu Kigamboni wameitekeleza.
Source : Nipashe