Rais Samia: Watu 13 wamefariki kwenye jengo lililoporomoka Kariakoo. Serikali kugharamia matibabu ya majeruhi na kuhakikisha waliofariki wanasitiriwa

Rais Samia: Watu 13 wamefariki kwenye jengo lililoporomoka Kariakoo. Serikali kugharamia matibabu ya majeruhi na kuhakikisha waliofariki wanasitiriwa

Loh
 

Attachments

  • IMG-20241117-WA0032.jpg
    IMG-20241117-WA0032.jpg
    118.5 KB · Views: 3
Rais Samia ambaye amesafiri kwenda Jijini Rio de Janeiro nchini Brazil 16 Novemba, 2024 kwa mwaliko wa Rais wa Brazil, Luiz Inácio Lula da Silva kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa nchi Wanachama wa Kundi la G20, amezungumza na Wananchi kufuatia kuporomoka kwa ghorofa Kariakoo Jijini Dar es Salaam.


Rais Samia amesema “Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kuporomoka kwa ghorofa katika eneo la Kariakoo Jijini Dar es Salaam. Nimekuwa nikipata taarifa za mara kwa mara kuhusu zoezi la uokoaji kutoka kwa Waziri Mkuu na nimekuwa nikifuatilia zoezi hilo kwa karibu zaidi.”

Pia soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Amesema “Hadi saa nne asubuhi leo, jumla ya watu 84 wameokolewa na kufikishwa hospitalini kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Kati ya hao majeruhi 26 bado wanaendelea na matibabu. Pamoja na hao kwa huzuni kubwa tumepoteza wenzetu 13 katika tukio hilo.”

Aidha ameongeza kuwa “Serikali itabeba gharama za matibabu kwa wote waliojeruhiwa, na kuhakikisha waliofariki wanastiriwa ipasavyo. Nitoe pole kwa ndugu, jamaa na marafiki walioguswa na tukio hili. Niwaombe watanzania wote tuwaweke kwenye maombi wote walioathirika na tukio hili na kuwaweka kwenye maombi waliotangulia mbele za haki.”

Salamu za Pole za Awali za Rais Samia: Rais Samia atoa pole kwa waathirika Kariakoo. Aagiza kufanywa kila linalowezekana kufanikisha zoezi la uokoaji na tiba kwa majeruhi

“Serikali itaendelea kutoa taarifa zaido kuhusu zoezi la uokoaji hadi hapo zoezi hilo litakapokamilika. Hadi sasa sababu za kitaalamu za jengo hilo kuporomoka bado hazijachunguzwa na kubainishwa, kwani kipaumbele chetu kwanza ni kuwaokoa wenzetu waliokuwa ndani ya jengo hilo.”

“Nashukuru mashirika binafsi na wananchi wote waliojitolea na waliotoa ushirikiano katika zoezi hilo. Nashukuru pia Madaktari wanaoendelea kuhudumia majeruhi. Nampongeza Waziri Mkuu, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na timu zao kwa kusimamia kazi kubwa ya uokozi.”

“Baada ya uokozi kukamilia, namtaka Waziri mkuu kuongoza timu ya Wakaguzi majengo, kukagua majengo yote ya eneo la Kariakoo na tupate taarifa kamili ya hali ya majengo ya Kariakoo yalivyo.”

Soma taarifa ya mwaka 2013: Magorofa 64 hatarini kuanguka Kariakoo

Aidha, Rais Samia ameagiza Jeshi la Polisi kupata taarifa kamili kutoka kwa Mmiliki wa Jengo lililoporomoka, kuhusu ujenzi ulivyokuwa unafanyika. Aidha, amesema taarifa zote za uchunguzi zitakapopatikana zitawekwa wazi kwa wananchi wote
Ahsante raisi kwa kujali.
 
Jpm hakuwa anajali kulipotokea maafa.
Hapana ndugu,
Alijali sana,isipokuwa kuna baadhi ya watu hakumwelewa,walikuwa na usiasa zaidi kuliko uhalisia,hata hivyo, kujali kwake kuliwafanya watendaji wake kuwajibika usiku na mchana, tofauti na awamu hii yenye laana, kiongozi anathubutu kusema hadharani,''sasa ni usiku sana,tusitishe zoezi la uokoaji, tutaendelea tena asubuhi ''bila kujali kuwa sekunde/dakika chache baadae zinaweza kuleta matokeo gani kwa mhanga/wahanga ambao ungeweza kuwaokoa!
Ni fedheha sana.
 
Unadhani Rais akienda Kariakoo au akiahirisha safari ndio walio chini ya vifusi watapona? Wacha ujinga na upumbavu.

Mara nyingi nasema kama huna Msaada usiense eneo la tukio na Wala business wanaovuja jasho kuokoa watu.

View: https://x.com/ortamisemitz/status/1858178289744961727?t=0vuOFgP8wYZb3Hz80yJ3Og&s=19

Jitahidi kuficha upuuzi wako na hao ccm wenzako.Unatuonyesha picha na taarifa kuwa hao ccm walienda eneo la tukio,kisha wamekaa na kupiga picha ya pamoja,hebu tuambie uwepo wao ulikuwa na tija gani kwenye zoezi la uokoaji?

Kipindi mz.Lowasa alipokuwa Waziri Mkuu,jengo la chang'ombe village [keko]lilianguka,Mz.Lowasa alisimamia zoezi la uokoaji pamoja na wahusika wa hilo jengo kuwajibishwa, tofauti na hawa jamaa zako walienda kupiga picha ya pamoja ili tuone kuwa walikuwepo hapo,,Hivi hamna aibu hata kidogo?Tuondoleeni upumbavu wenu.
 
Rais Samia ambaye amesafiri kwenda Jijini Rio de Janeiro nchini Brazil 16 Novemba, 2024 kwa mwaliko wa Rais wa Brazil, Luiz Inácio Lula da Silva kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa nchi Wanachama wa Kundi la G20, amezungumza na Wananchi kufuatia kuporomoka kwa ghorofa Kariakoo Jijini Dar es Salaam.


Rais Samia amesema “Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kuporomoka kwa ghorofa katika eneo la Kariakoo Jijini Dar es Salaam. Nimekuwa nikipata taarifa za mara kwa mara kuhusu zoezi la uokoaji kutoka kwa Waziri Mkuu na nimekuwa nikifuatilia zoezi hilo kwa karibu zaidi.”

Pia soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Amesema “Hadi saa nne asubuhi leo, jumla ya watu 84 wameokolewa na kufikishwa hospitalini kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Kati ya hao majeruhi 26 bado wanaendelea na matibabu. Pamoja na hao kwa huzuni kubwa tumepoteza wenzetu 13 katika tukio hilo.”

Aidha ameongeza kuwa “Serikali itabeba gharama za matibabu kwa wote waliojeruhiwa, na kuhakikisha waliofariki wanastiriwa ipasavyo. Nitoe pole kwa ndugu, jamaa na marafiki walioguswa na tukio hili. Niwaombe watanzania wote tuwaweke kwenye maombi wote walioathirika na tukio hili na kuwaweka kwenye maombi waliotangulia mbele za haki.”

Salamu za Pole za Awali za Rais Samia: Rais Samia atoa pole kwa waathirika Kariakoo. Aagiza kufanywa kila linalowezekana kufanikisha zoezi la uokoaji na tiba kwa majeruhi

“Serikali itaendelea kutoa taarifa zaido kuhusu zoezi la uokoaji hadi hapo zoezi hilo litakapokamilika. Hadi sasa sababu za kitaalamu za jengo hilo kuporomoka bado hazijachunguzwa na kubainishwa, kwani kipaumbele chetu kwanza ni kuwaokoa wenzetu waliokuwa ndani ya jengo hilo.”

“Nashukuru mashirika binafsi na wananchi wote waliojitolea na waliotoa ushirikiano katika zoezi hilo. Nashukuru pia Madaktari wanaoendelea kuhudumia majeruhi. Nampongeza Waziri Mkuu, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na timu zao kwa kusimamia kazi kubwa ya uokozi.”

“Baada ya uokozi kukamilia, namtaka Waziri mkuu kuongoza timu ya Wakaguzi majengo, kukagua majengo yote ya eneo la Kariakoo na tupate taarifa kamili ya hali ya majengo ya Kariakoo yalivyo.”

Soma taarifa ya mwaka 2013: Magorofa 64 hatarini kuanguka Kariakoo

Aidha, Rais Samia ameagiza Jeshi la Polisi kupata taarifa kamili kutoka kwa Mmiliki wa Jengo lililoporomoka, kuhusu ujenzi ulivyokuwa unafanyika. Aidha, amesema taarifa zote za uchunguzi zitakapopatikana zitawekwa wazi kwa wananchi wote

Mama unatoa bilioni 100 kwa polisi kununua washawasha za uchaguzi na unatoka milioni 300 mpaka 400 kununua magari ya wakurugenzi wa wilaya wanao engua wagombea. Lakini huwezi kutoa pesa za kununua vifaa vya uokoaji. Hakuna mtu anafukuzwa TZ hata watu wakifa siku hizi. Ripoti unazoomba ni fake kila siku unaomba ripoti fake ambazo hazitoki na hazitatoka. Mnajali chama, ndugu zenu na marafiki . Wananchi mnawajali ili tu wawaweseshe kuendelea kuiba na kujinufaisha nyie na ndugu zenu. Wananchi wamekuwa mbumbumbu hawawezi hata kulalamika tena kama vile wafanyakazi wenu na sio nyie wafanyakazi wao. Hii nchi ni Mungu tu ndiyo anaeeza kuiokoa kwasasa na tukiweka imani atafanya hivyo
 
Inashangaza kidogo rais anahutubua taifa lake akiwa nje ya taifa lake.
Ni kheri angekaa kimya tu au angemwambia dr mpango atoe hiyo taarifa .
Tuna Rais ambaye hajali ila eti anajifanya anajali
 
hebu tuambie uwepo wao ulikuwa na tija gani kwenye zoezi la uokoaji?
Kwa sababu msingi wa hoja zote hizi ni chuki, swali hili hili lingeulizwa pia kama kama angeghairisha safari na kwenda pale. Watu wana agenda zao bwana........
 
Inashangaza kidogo rais anahutubua taifa lake akiwa nje ya taifa lake.
Ni kheri angekaa kimya tu au angemwambia dr mpango atoe hiyo taarifa .
Tuna Rais ambaye hajali ila eti anajifanya anajali
Hivi ndivyo uwezo wa chadema wa kufikiri ulipofikia.
Acha mbowe aendelee tu kujichotea mabilioni ya ruzuku
 
Yaan mama umeeleweka 100% kweli ww ni mfariji mkuu
 
Rais Samia ambaye amesafiri kwenda Jijini Rio de Janeiro nchini Brazil 16 Novemba, 2024 kwa mwaliko wa Rais wa Brazil, Luiz Inácio Lula da Silva kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa nchi Wanachama wa Kundi la G20, amezungumza na Wananchi kufuatia kuporomoka kwa ghorofa Kariakoo Jijini Dar es Salaam.


Rais Samia amesema “Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kuporomoka kwa ghorofa katika eneo la Kariakoo Jijini Dar es Salaam. Nimekuwa nikipata taarifa za mara kwa mara kuhusu zoezi la uokoaji kutoka kwa Waziri Mkuu na nimekuwa nikifuatilia zoezi hilo kwa karibu zaidi.”

Pia soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Amesema “Hadi saa nne asubuhi leo, jumla ya watu 84 wameokolewa na kufikishwa hospitalini kwa ajili ya kupatiwa matibabu. Kati ya hao majeruhi 26 bado wanaendelea na matibabu. Pamoja na hao kwa huzuni kubwa tumepoteza wenzetu 13 katika tukio hilo.”

Aidha ameongeza kuwa “Serikali itabeba gharama za matibabu kwa wote waliojeruhiwa, na kuhakikisha waliofariki wanastiriwa ipasavyo. Nitoe pole kwa ndugu, jamaa na marafiki walioguswa na tukio hili. Niwaombe watanzania wote tuwaweke kwenye maombi wote walioathirika na tukio hili na kuwaweka kwenye maombi waliotangulia mbele za haki.”

Salamu za Pole za Awali za Rais Samia: Rais Samia atoa pole kwa waathirika Kariakoo. Aagiza kufanywa kila linalowezekana kufanikisha zoezi la uokoaji na tiba kwa majeruhi

“Serikali itaendelea kutoa taarifa zaido kuhusu zoezi la uokoaji hadi hapo zoezi hilo litakapokamilika. Hadi sasa sababu za kitaalamu za jengo hilo kuporomoka bado hazijachunguzwa na kubainishwa, kwani kipaumbele chetu kwanza ni kuwaokoa wenzetu waliokuwa ndani ya jengo hilo.”

“Nashukuru mashirika binafsi na wananchi wote waliojitolea na waliotoa ushirikiano katika zoezi hilo. Nashukuru pia Madaktari wanaoendelea kuhudumia majeruhi. Nampongeza Waziri Mkuu, Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam na timu zao kwa kusimamia kazi kubwa ya uokozi.”

“Baada ya uokozi kukamilia, namtaka Waziri mkuu kuongoza timu ya Wakaguzi majengo, kukagua majengo yote ya eneo la Kariakoo na tupate taarifa kamili ya hali ya majengo ya Kariakoo yalivyo.”

Soma taarifa ya mwaka 2013: Magorofa 64 hatarini kuanguka Kariakoo

Aidha, Rais Samia ameagiza Jeshi la Polisi kupata taarifa kamili kutoka kwa Mmiliki wa Jengo lililoporomoka, kuhusu ujenzi ulivyokuwa unafanyika. Aidha, amesema taarifa zote za uchunguzi zitakapopatikana zitawekwa wazi kwa wananchi wote
Mama huku nyumbani tumepata msiba mzito! Na wewe umetutelekeza ukijua hatuna baba. Mungu atakulipa?
 
Back
Top Bottom