Rais Samia: Wenye akili za kawaida ndiyo wananikosoa kusafiri nje

Rais Samia: Wenye akili za kawaida ndiyo wananikosoa kusafiri nje

Wana ka msemo kao kuwa ukiwatoza Kodi MATAJIRI unavuruga Uchumi wa Nchi.

Eti maskini ndo HAKI kulipishwa mikopo iliyokopwa wakapewa MATAJIRI kuinua Uchumi!!!!

Mbona Nchi za MABEBERU matajiri na maskini wanalipa Kodi na wanajivunia kulipa Kodi?

Vituo vya mafuta nw hawatoi tena risiti za EFD.

Ukigusa makontena ya wakubwa bandarini unatumbuliwa.

Hivi sie ni WAJAMAA Uchwara au Mabepari Uchwara?
Kodi yote anakula silent ocean, halafu mnaanza kukuletea maneno ya kejeli, hiyo barabara ya dar mza imejaa matuta matupu, maroli kilasiku yanatoboa boosters
 
"Wenye uwezo wa Kawaida wa Kufikiri ( Nadhani akina GENTAMYCINE ) wanasema kuwa ninasafiri sana Nje ya nchi. Ukweli ni kwamba nikisafiri Mikoani nakuza tu Siasa za Ndani ila nikienda huko Ulaya naenda Kuwaletea Pesa kama hizi"

Rais Samia Mwanao GENTAMYCINE nilikuwa sijui kuwa kumbe Kufanya Ziara za Mikoani kwa Rais wa Tanzania ni kuitia tu Njaa nchi na kuendeleza Umasikini ila kumbe ukienda Ulaya unaenda Kuchota Fedha za Watanzania Masikini walizozihifadhi kwa Wazungu.

Halafu Rais Samia Mwanao GENTAMYCINE nilikuwa sijui kuwa kumbe Kura nyingi tunazowapeni pale mkigombea Urais ni za kuwatumeni tu Kuzurula Ulaya kuomba Pesa na kwamba Shida za Watanzania Masikini wengi tutakuwa tunazimaliza Wenyewe na 'Miungu' yetu tunayoiomba na Maombi ya akina Mitume Mwamposa na Kuhani Richard Mwacha.

Sawa Mama Safiri ukatuletee Fedha.
Total misconception !!
 
"Wenye uwezo wa Kawaida wa Kufikiri ( Nadhani akina GENTAMYCINE ) wanasema kuwa ninasafiri sana Nje ya nchi. Ukweli ni kwamba nikisafiri Mikoani nakuza tu Siasa za Ndani ila nikienda huko Ulaya naenda Kuwaletea Pesa kama hizi"

Rais Samia Mwanao GENTAMYCINE nilikuwa sijui kuwa kumbe Kufanya Ziara za Mikoani kwa Rais wa Tanzania ni kuitia tu Njaa nchi na kuendeleza Umasikini ila kumbe ukienda Ulaya unaenda Kuchota Fedha za Watanzania Masikini walizozihifadhi kwa Wazungu.

Halafu Rais Samia Mwanao GENTAMYCINE nilikuwa sijui kuwa kumbe Kura nyingi tunazowapeni pale mkigombea Urais ni za kuwatumeni tu Kuzurula Ulaya kuomba Pesa na kwamba Shida za Watanzania Masikini wengi tutakuwa tunazimaliza Wenyewe na 'Miungu' yetu tunayoiomba na Maombi ya akina Mitume Mwamposa na Kuhani Richard Mwacha.

Sawa Mama Safiri ukatuletee Fedha.
Unazidi kudhihirisha jinsi ulivyo na akili ndogo kama alivyosema SSH..

Unaweza niambia ni ziara ipi Rais ameifanya ikawa ya hasara? Na Je angebakia anazurura na kudanganya watu mikoani angefikisha investment kubwa kama inayoonekana sasa?

Unajua Tzn ni imesima vyema kuliko Nchi karibu zote za hapa Afrika kwamba licha ya changamoto za uchumi wa Dunia ila tumekuwa na nafuu kwenye Kila kitu?

Nchi za jirani hapo Hali ni mbaya sana Sasa sijui kwamba na wao ni kwa vile wanasafiri sana au hapana..

Mwisho ,laiti kama Jiwe angekuwa hai leo hii,Tanzania tungekuwa kama Zimbabwe au Sri Lanka..Kwa miaka ya Jiwe madarakani bidhaa ya sukari iliwahi adimika mara 3,saruji mara 2 na mafuta ya mitambo mara 2 pia.
 
lakini ulishaanza na umekamilika kwa asilimia kubwa sana kama sioa silimia 90... maana mpaka wanafanya testing. hata ndugai alikuwa anajua hali halisi ya miradi kuwa haiitaji kukopa kopa kila siku

..SGR kipande cha Dar to Moro ndio kimekamilika kwa asilimia 90.

..SGR ni zaidi ya km 1800 na kipande cha Dar Moro ni km 300+.

..Zaidi, SGR imelenga kusafirisha shehena kubwa za nchi majirani.

..Bila reli hiyo kufika mpakani na nchi jirani, au Isaka Dry Port, haitaweza kukidhi malengo iliyowekewa.
 
Wana ka msemo kao kuwa ukiwatoza Kodi MATAJIRI unavuruga Uchumi wa Nchi.

Eti maskini ndo HAKI kulipishwa mikopo iliyokopwa wakapewa MATAJIRI kuinua Uchumi!!!!

Mbona Nchi za MABEBERU matajiri na maskini wanalipa Kodi na wanajivunia kulipa Kodi?

Vituo vya mafuta nw hawatoi tena risiti za EFD.

Ukigusa makontena ya wakubwa bandarini unatumbuliwa.

Hivi sie ni WAJAMAA Uchwara au Mabepari Uchwara?
Kwa akili yako kodi za nchi hii zinalipwa na watu gani? Machinga na mama nitilie? Bodaboda? Au wakulima huko vijijini?
Unajua makampuni kama TBL, Vidacom, Metl, Azam wanalipa kodi kiasi gani?
 
Kama wapi? Utalii hatupati kodi na fedha za kigeni? Madini hatupati kodi na mirabaha, kuwa wanachimba bure? Uvuvi hatupati mapato? Japo ni madogo sababu hakuna uwekezaji..

..tatizo letu ni kwamba tunadharau kilimo, ufugaji, na uvuvi.

..kwa mfano, fedha tulizofuja kununua midege toka kwa mabeberu zingeweza kufanya transformation kubwa kama zingewekezwa kwenye kilimo.

..katika safari zote za Raisi za kutafuta wawekezaji, sijasikia kama amepatikana muwekezaji ktk kilimo, au viwanda, ambaye analeta fedha sawa, au kuzidi, zile tulizowekeza kwenye viwanda vya mabeberu vya kutengeneza ndege.

..Majuzi tulisikia habari za Uganda kutuuzia sukari. Hii ni aibu kwasababu viwanda vya sukari vya Tz vilikuwa operational wakati ambapo viwanda vya Uganda vilikuwa vimekufa. Sasa Uganda wameweza kufufua viwanda vyao na sasa wanaweza hata ku export ktk soko letu.

..Jambo lingine la kusikitisha na kuonyesha uzembe wa miaka mingi wa serikali zetu ni kile kilichoonekana ktk ziara ya Waziri wetu wa Kilimo kwenda Uganda kujifunza kuhusu zao la Chikichi.

..Nchi yetu haiwezi kuendelea bila Watz kuongeza uzalishaji ktk kilimo ambacho kinaajiri asilimia kubwa ya wananchi wetu.
 
Madini inachangia 7% tu ya GDP yetu, Botswana wao madini 35% ya GDP. Alafu sisi tunawazidi Botswana kwa uzalishaji madini.

Ingekua hata 20% au 30%, leo hii GDP yetu ingekua sawa au zaidi ya kenya

..Watz tuko milioni 50++.

..Botswana wako milioni 2 [ sina uhakika].

..kutokana na idadi yao ndogo lazima Botswana watafaidi zaidi madini yao kulinganisha na Tz.

..Hata ukiangalia mafuta ya Nigeria vs ya nchi za Kiarabu.

..Ni kweli kuna rushwa na ubadhirifu Nigeria, lakini kwa idadi kubwa ya watu wao sio rahisi kuona manufaa ya mafuta ukilinganisha na Saudia, Kuwait, etc.

..Kwa hapa Tanzania hatuwezi kuwakwepa WAKULIMA kama tunataka kujikwamua kiuchumi.
 
..Watz tuko milioni 50++.

..Botswana wako milioni 2 [ sina uhakika].

..kutokana na idadi yao ndogo lazima Botswana watafaidi zaidi madini yao kulinganisha na Tz.

..Hata ukiangalia mafuta ya Nigeria vs ya nchi za Kiarabu.

..Ni kweli kuna rushwa na ubadhirifu Nigeria, lakini kwa idadi kubwa ya watu wao sio rahisi kuona manufaa ya mafuta ukilinganisha na Saudia, Kuwait, etc.

..Kwa hapa Tanzania hatuwezi kuwakwepa WAKULIMA kama tunataka kujikwamua kiuchumi.
Hii ni justification ya tunachopata tunastahili?
 
..Watz tuko milioni 50++.

..Botswana wako milioni 2 [ sina uhakika].

..kutokana na idadi yao ndogo lazima Botswana watafaidi zaidi madini yao kulinganisha na Tz.

..Hata ukiangalia mafuta ya Nigeria vs ya nchi za Kiarabu.

..Ni kweli kuna rushwa na ubadhirifu Nigeria, lakini kwa idadi kubwa ya watu wao sio rahisi kuona manufaa ya mafuta ukilinganisha na Saudia, Kuwait, etc.

..Kwa hapa Tanzania hatuwezi kuwakwepa WAKULIMA kama tunataka kujikwamua kiuchumi.
Huo uwingi Wenu usio na faida mlilazimishwa mzaane hovyo kama Sungura na Panya wakati mkijua hamna Akili?
 
Rais lazima atengeneze deals zitakazoiingizia nchi mapato, iwe ni deal za biashara na uwekezaji, au mikopo ama misaada

Sio jambo la kuficha kuwa nchi yetu ni maskini, wananchi wazawa hatuna mitaji ya kuwekeza kwenye miradi mikubwa, uwezo wetu wa kulipa kodi pia ni mdogo

Kufanya zuara za mikoani tu utaishia kuambiwa tuna shida ya maji, barabara, hospitali n.k lakini fedha hakuna, utatatua vipi hizo shida?

Magufuli yeye alikuwa akikopa mikopo kutoka benki za kibiashara, ambayo riba ni kubwa na muda wa kulipa ni mfupi, so unataka Samia afabya hivyo?

Wewe unaenlaumu Samia wewe mchango wako ni upi kuhakikisha nchi inajitegemea kwenye mapato hasa ya kufanya miradi mikubwa? Kulalamikia kodi na tozo?
Hawakutegemea Samia awe rais na hatukuona rais akifariki madarakani tangu uhuru hivyo maneno mengi wanayoongea ni kuchanganyikiwa.

Hawa ni wale waliokuwa wanafaidika na awamu ya JPM hawakuiona leo hii yenye mabadiliko ya uongozi kuanzia juu kabisa pale ikulu.

Kelele na malalamiko yao ni kwa SSH ambaye ni mrithi wa JPM kwa mujibu wa katiba sio kwa kuingizwa na watu fulani. Wanaishi na maumivu ya moyo yasiyoweza kutibika mahospitalini wala kwa waganga wa kienyeji. Pole inawahusu.
 
Madini inachangia 7% tu ya GDP yetu, Botswana wao madini 35% ya GDP. Alafu sisi tunawazidi Botswana kwa uzalishaji madini.

Ingekua hata 20% au 30%, leo hii GDP yetu ingekua sawa au zaidi ya kenya
Mkuu unajua GDP ya Botswana ni ngapi? Ni 15 Bilion USD, Tanzania ni 62 Bilioni USD,
Sijui hicho kipimo cha kuwa madini yanachangia 7% ya gdp umetoa wapi ila mimi takwimu ninazijua madini yanachangia 10% ya gdp, na inaonyesha 35% ya 15 ni ndogo kuliko na 10% ya 62
 
Pesa zitatafutwa sana ila bila kudhibiti matumizi hakuna kitakachobadilika.
 
Back
Top Bottom