Rais Tshisekedi siku zake zinahesabika

Rais Tshisekedi siku zake zinahesabika

Pamoja na hayo, sioni Rwanda inaishindaje DRC wakipigana sasa hivi. Nasisitiza endapo hakuna external influence kwa yeyote
Mpaka Sasa Rwanda imeshaishinda Drc, kitendo cha Drc kuwashindwa M23 ni udhaifu tayari.....Rwanda ya Sasa ni imara mno kuliko ya miaka ile na imekuwa na nguvu Sana kwenye hilo eneo.
 
nini lengo kuu la m23?
Wanaikumbusha serikali ya Drc (hasa Tshekedi ) kutopuuza umuhimu wa Rwanda kwenye eneo hilo.

Huo ni mkono wa nchi jirani kujaribu kuishinikiza Drc kutimiza matakwa yao, kitendo cha Drc kuzialika Burundi na Uganda kupambana na waasi wao waliopo huko na kuitenga Rwanda kumechangia hili.

zitto junior JokaKuu Count Capone
 
Wanaikumbusha serikali ya Drc (hasa Tshekedi ) kutopuuza umuhimu wa Rwanda kwenye eneo hilo.

Huo ni mkono wa nchi jirani kujaribu kuishinikiza Drc kutimiza matakwa yao, kitendo cha Drc kuzialika Burundi na Uganda kupambana na waasi wao waliopo huko na kuitenga Rwanda kumechangia hili.

zitto junior JokaKuu Count Capone
means hawana lengo la kuitoa serikali ya kinshansa,zaidi ya kuzuia juhudi za fdlr
 
Ukiniuliza mimi kwenye vita kamili isiyo ya kujificha kati ya Rwanda na DRC nani anashinda nasema ni DRC endapo hakuna external influence baina ya pande zote mbili.

Congo ukitaka kuipima kwa kuangalia eneo lake la Mashariki utapotea, itazame nchi nzima hadi kule Magharibi. Mashariki ni kama imepotezewa na ina waasi wengi wanaojificha na kusumbua kila wakijisikia. Wakipigwa wanavaa kiraia wanalima, wakipata support wanaanza mapigano. Ukija kwenye vita ya nchi na nchi hapo hujifichi, madaraja tunajua yalipo, kambi zilipo, airbase ilipo, HQ, defensive lines na mambo mengine.

Congo sio wazembe kuliko nchi nyingi za Kiafrika, tatizo lao wana rasilimali nyingi na bahati mbaya ya kunyonywa na mataifa ya nje, ila nchi nyingi za Afrika hazina unafuu kijeshi kuwazidi. Hakuna nchi ina makundi ya waasi hadi 10 kama Congo ilivyo, logistics za kuipiga Congo kuanzia mpakani kwa Rwanda mpaka katikati ya nchi kule ni gharama kwa Rwanda. Rwanda kuipiga Congo sio rahisi hata kidogo
Kijeshi CONGO ina nguvu kuliko rwanda !! lakini kimbinu Rwanda ameizidi DRC mbali sana. So kama ni vita ya ana kwa ana Rwanda haiwezi kufua dafu kwa DRC !! ila kwa vita za siku izi hazipo hivo sikuizi vita zake ni za kuchekeana machoni na kupigana kimya kimya ,kupigana kimifumo na kupandikiziana magaidi na waasi kitu ambacho drc haijabobea!!

rwanda ina marafiki wengi nje kuliko DRC!!
Drc inashindwa hata kujihusisha na nchi marafiki kupata msaada kijeshi na kitechnologia
 
means hawana lengo la kuitoa serikali ya kinshansa,zaidi ya kuzuia juhudi za fdlr
Naweza kukubaliana na wewe kwa sehemu tu, ila unadhani fdlr ina uwezo wowote wa kuiangusha serikali ya Kagame ?...

Huoni kwa Sasa Fdlr inatumika tu kama sababu ya kuhakikisha 'balance of power' kati ya Rwanda na mahasimu wake wa Kikanda yaani Uganda na Burundi inaendelea kuwepo huko Drc.

Unadhani fdlr ikiondoka huko Drc, Rwanda inaweza kuendeleza ushawishi wake huko Drc hata kuipiku Uganda na Burundi ?

Huoni kama ushirikiano kati ya Burundi, Uganda, Kenya, Tz na Drc ni mzuri mno hata wakaruhusiwa kupeleka askari wao huko, huku Rwanda ikizuiwa huoni hilo jambo ni kitisho na hatari kwa Rwanda?
zitto junior JokaKuu
 
Kijeshi CONGO ina nguvu kuliko rwanda !! lakini kimbinu Rwanda ameizidi DRC mbali sana. So kama ni vita ya ana kwa ana Rwanda haiwezi kufua dafu kwa DRC !! ila kwa vita za siku izi hazipo hivo sikuizi vita zake ni za kuchekeana machoni na kupigana kimya kimya ,kupigana kimifumo na kupandikiziana magaidi na waasi kitu ambacho drc haijabobea!!

rwanda ina marafiki wengi nje kuliko DRC!!
Drc inashindwa hata kujihusisha na nchi marafiki kupata msaada kijeshi na kitechnologia
Ndio maana nikasema Rwanda apigane na Congo kwenye vita halisi, na kusiwepo third party. Sioni Rwanda anashindaje vita hiyo
 
Naweza kukubaliana na wewe kwa sehemu tu, ila unadhani fdlr ina uwezo wowote wa kuiangusha serikali ya Kagame ?...

Huoni kwa Sasa Fdlr inatumika tu kama sababu ya kuhakikisha 'balance of power' kati ya Rwanda na mahasimu wake wa Kikanda yaani Uganda na Burundi inaendelea kuwepo huko Drc.

Unadhani fdlr ikiondoka Rwanda inaweza kuendeleza ushawishi wake huko Drc hata kuipiku Uganda na Burundi ?
zitto junior JokaKuu

..eastern congo isipotawalika rwanda nayo haitakuwa salama.

..pia rwanda iache kuchochea na kufadhili makundi ya waasi wa congo.

..lingine ni suala la DEMOKRASIA Rwanda. Kagame atatawala mpaka lini?
 
Naweza kukubaliana na wewe kwa sehemu tu, ila unadhani fdlr ina uwezo wowote wa kuiangusha serikali ya Kagame ?...

Huoni kwa Sasa Fdlr inatumika tu kama sababu ya kuhakikisha 'balance of power' kati ya Rwanda na mahasimu wake wa Kikanda yaani Uganda na Burundi inaendelea kuwepo huko Drc.

Unadhani fdlr ikiondoka huko Drc, Rwanda inaweza kuendeleza ushawishi wake huko Drc hata kuipiku Uganda na Burundi ?

Huoni kama ushirikiano kati ya Burundi, Uganda, Kenya, Tz na Drc ni mzuri mno hata wakaruhusiwa kupeleka askari wao huko, huku Rwanda ikizuiwa huoni hilo jambo ni kitisho na hatari kwa Rwanda?
zitto junior JokaKuu
hao fdr walishaambiwa km wanaweza wakafanye siasa kigali,huko porini hawashindi ht kwa nn

Nami nakubaliana na wewe,ila chaka analoingia felix ni kuanzisha hivyo vikundi km huo mpango anao
 
Ndio maana mkuu nikakuuliza kama hao waasi sio competent why wanawachapa jeshi la serikali Kila siku? Yaani sio Nkunda, Ntaganda, Makenga n.k Ina maana askari wasio na mafunzo Wala elimu ni Bora kuliko jeshi la DRC!!

Kumbuka hata Kabila Senior alipindua Mobutu kutumia "vitoto" Sasa kwa namna hii unadhani Hilo jeshi ambalo linazidiwa Competence na rebels ndio Lina uwezo wa kutandika sio jeshi tu Bali Battle-hardened army kama RDF?

Embi tuweni serious, msimuingize Fatshi mkenge
Sasa mkuu, Marekani imepigana na Taliban miaka 20, ikapiganana na al Qaeda miaka mingi, ikapigana na wanamgambo na magaidi wengine miaka na miaka. Hatuwezi sema Marekani itashindwa vita na Switzerland kwa kuwa hawajawahi teswa na wahuni.

Nigeria hii inateswa na Boko Haram magaidi, achana na zile suicide missions zao za mabomu nasema ile kubwa na vikosi vya mafunzo, kupiga kambi za jeshi, kumiliki Sambisa forest na kuteka maelfu ya watu humo wakiwemo mamia ya wanafunzi. Mtu akitumia kigezo hicho kudai Nigeria inaweza pigwa na Tanzania kisa inashindwa na Boko Haram ujue hajui kitu kwenye majeshi, hajui kitu kabisa.

Kuteswa na waasi sio kipimo cha jeshi kuwa dhaifu. Nchi za Afrika ambayo ilipambana na usumbufu wa hivyo ni the mighty South Africa ya apartheid pekee kupigana na kina SWAPO kule Angola na kupigana na resistance fighters wa Namibia. Hadi leo Misri ina magaidi pale Sinai na Turkey inasumbuliwa na vikundi vya Wakurdi na nchi hizo mbili hata ujumlishe majeshi ya Afrika Mashariki nzima hayawezi ipiga mojawapo
 
..eastern congo isipotawalika rwanda nayo haitakuwa salama.

..pia rwanda iache kuchochea na kufadhili makundi ya waasi wa congo.

..lingine ni suala la DEMOKRASIA Rwanda. Kagame atatawala mpaka lini?
Rwanda ni ticking bomb, muda wowote Kagame akidondoka ujue ni vita ya utawala. Dalili ya kwanza ya kutambua hilo tuulizane ni nani mrithi wa Kagame aliyeandaliwa mpaka sasa?

Maana kawaida ya totalitarian leaders hawapendi kutaja mrithi kuepuka mapinduzi. Unamjua mkubwa ila second in command mmoja wa uhakika hajulikani, unakuta watu kama watatu wenye influence sawasawa. Sasa kati yao kila mmoja akiamua apambane ndio tunarudi kupokea wakimbizi
 
Wakuu inakuaje? sasa twende kazi.

Siku mbili tatu hizi kumekuwa na hali ya sintofahamu kati ya serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo na ile ya Rwanda, kila mmoja akimtupia lawama mwenzake na kutishia kuvunjilia mbali uhusiano wao wa kidiplomasia nk.

Kwa upande wa Congo ndio wanaonekana kuwa wamechukia zaidi hadi kupelekea serikali yao kumfukuza nchini kwao balozi wa Rwanda, na pia kumwata balozi wao aliekuwa nchini Rwanda.

Kwa upande wa Rwanda yenyew haioneshi kupanic wala kuchukizwa kivile, inaonekana ime relax ikisubiria kuona kingine kitachojiri kutoka katika serikali ya jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Sasa basi... Rwanda ina uwezo wa kuichakaza na kuisambaratisha Congo kijeshi kwa njia zote, iwe kwa angani, majini au ardhini tena kwa muda mfupi sana.

Congo inaweza kuishinda Rwanda kwa maneno tu, maana wakongomani ni waimba miziki na wachezaji wakubwa, ila linapokuja swala la mapambano ya kijeshi na weupe sana wanashindwa hata na Burundi.

Kwanza toka Congo ilipopata uhuru jeshi lake halikuwahi kushinda vita yoyote ile. Wakati wa Mobutu jeshi la Congo lilichakazwa vibaya na waasi waliokuwa wanaongozwa na hayati Desire Kabila (father) na baadae jeshi hilo limeendelea kuchakazwa na makundi mbali mbali ya waasi wengi wao ni kutoka nchi jirani.

Sasa jiulize ikiwa nchi yenye raia zaidi ya milioni 1 inachakazwa na waasi wasiozidi elfu 5, huku waasi hao wakiwa na silaha za kuunga unga na mazoezi ya msituni yasiokuwa rasmi. Je watakapoingia kwenye vita na nchi yenyewe si ndo yatakuja kutokea yale ya Mobutu na Idi Amini!!

Hivi kweli Tshisekedi anaamini kuwa nchi yake inaweza kuipiga Rwanda au ndo kifo kinamwita, au wazee wa kazi (Kabila's team) wanamshauri ujinga ili akipigwa akikimbia Kabila arudi kuongoza Congo?

Maana katika hali ya kawaida haiwezekani nchi inayoshindwa vita na waasi elfu 3, ijidanganye kuwa inaweza kupambana na nchi yenye wanajeshi zaidi ya laki, wenye ueledi mkubwa wa kivita, silaha za kisasa na wanajeshi wa kutosha.

Katika EAC nzima, nchi ambazo Rwanda inaweza kuhofia kwa namna fulani kupambana nazo ni Tanzania na Kenya tu ambazo majeshi yao yameshafanya mambo makubwa ndani na nje ya mipaka yao Tanzania ikiwa inaongoza kwa kufanikiwa oparation mbali mbali katika nchi za Msumbiji, Zimbabwe, Angola, Namibia, Comoros nk. Ila hizo zingine Rwanda inaziona kama vile ni nchi zinazolindwa na makundi ya sungu sungu tu na sio wanajeshi kamili.

So chonde chonde Tshisekedi watu bado wanakuhitaji uendelee kuwa raisi wao. Usije kuingia kwenye mtego ambao utashindwa kujinasua. Kagame alimhofia Kikwete tu mjeshi mwenzake na anajua watu wa kicheka cheka kama JK maamuzi yao yanakuwaga na athari kubwa kwa wengine. Lakini nyinyi wengine anawaona vikaragosi wake.

Tena kwa Congo ndo kabisa hawezi kutuma jeshi lake kupoteza muda wao. Sana sana ataajiri vijana kutoka katika makampuni mbali mbali ya ulinzi waje kumaliza kazi.

Pichani juu ni jeshi la Rwanda na picha ya chini ni jeshi la Congo.

Siku njema kwa wasomaji na wachangiaji wote. Asanteni.
Jambo la kwanza lazima utofautishe vita baina ya nchi na nchi na vita ya waasi,au vikundi vya kigaidi ambao wana kuwa ndani ya nchini vita ngumu sana kwani huwa wanajificha ndani ya jamii humo humo,na mifano ipo mingi,Kenya,msumbiji,Uganda,Burundi na hata Rwanda,zimeshawahi kukutana na hali hii,na viliwasumbua sana.Na vingi hupotea pale milija ya ufadhiri inapokatwa ,hivyo huwa ni ngumu kujua nani hasa ndiye unayegombana naye,lakini vita ya nchi kwa nchi,hiyo ni rahisi sana kwani adui yako unamfahamu,ni nani.Hao M23 nguvu inatoka Kigari tu,na ndio maana siku hizi lile kundi la ADF,lililokuwa likileta vulugu Rwanda,ni kama halipo tena,baada ya Uganda kuamua kulitokomeza ,na kukosa misaada ya kifedha,u lile la LRA la joseph koni.Ninachokiona mbeleni huko KAGAME,atakuja kuanza kuilaumu EAC,kuwa inampendelea DRC,kwani wao wanapeleka majeshi kulinda mipaka ya DRC,na RWANDA,sasa kama kuna michezo inafanywa na Rwanda ndani ya DRC,itafikia mwisho,na majeshi ya EAC,yapo huko under chapter 6,lakini yanataka ikibidi yapewe majukumu ya under chapter 7(hapo yatakuwa na uwezo wa kushambulia sio kulinda tu wananchi)hao M23 baada ya kudhibitiwa huko mashariki mwa congo,vifaa vitakuwa vinapitia wapi kuwafikia.Na kiuchumi DRC,kila mtu ana muhitaji sana kuliko RWANDA.Na rwanda hawezi kukosana na TZ na Kenya kwa wakati mmoja kwani atapata shida sana kiuchumi.
 
Umejitahidi kujifichia kwenye utanzania lakini imeshindikana.Utawajua tu banyamulenge kwa maandishi yao
Haya anza sasa kumsifia mungu wenu PAKA maana ndiyo kazi muiwezayo
Mkuu Nyamizi wanyamulenge ni wakongoman, Paka ni mnyarwanda na mimi mleta mada ni mtanzania. Kwahiyo tuna utofauti wa utaifa.

Usiniaminishe kuwa kila anaeitetea Congo humu ni mkongomani na anaezungumzia tofauti ni mnyarwanda.

Siku zote mtu anaekupenda ni yule anaekwambia ukweli wa hatari iliyopo mbele yako ili uchukue tahadhari mapema kabla hatari hiyo haijakufikia. Ukiona mtu anaficha kukueleza ukweli wa hatari hiyo wakati anaifahamu huwa huyo sio mwema kwako. Sasa kwahiyo hapa nimekuja kutoa tahadhari kwa raisi wa ndugu zetu wakongomani ili wale vijana wake waliopo humu wamfikishie taarifa mapema kabla hajaingia kichwa kichwa vitani na Rwanda.
 
Nadhani gharama unayomaanisha wewe ni kuikalia (occupation) ila kama ni kuipiga ilishafanya hayo kwa mafanikio mwaka 1996 japo ilishirikiana na waasi wa Zaire na nchi nyingine kama Uganda ,Angola kwa kiasi Eritrea na hata Zimbabwe zilisaidia hayo mafanikio.

Hata mwaka 1998 ilifanikiwa kukalia maeneo makubwa ya huko mashariki kwa ushirikiano na waasi wa huko japo walishindwa kuchukua mji mkuu kwa kuzuiliwa na Angola, Zimbabwe.

Nadhani gharama za kuikalia ndio hawataziweza, hata hawa M23 sidhani kama wana nia ya kuiangusha serikali ya Drc ila watajaribu tu kuteka maeneo mengi kama njia ya kushinikiza muafaka wa kisiasa.
zitto junior JokaKuu mtu chake Richard
Lengo la M23 ni kuchukua Goma mida hii washachukua miji ya Kiwanja na Rutshiru na wajongelea ndani zaidi.

Tatizo kubwa n kwamba M23 wazungumza kinywarwanda na hiyo ni sababu kubwa inotumiwa (kwa makusudi na malengo maalum) kuendelea kuchochea mgogoro.

Tayari kelele za kuomba msaada wa Russia zimeanza na ni kama zile kelele za kule Mali na Burkina Faso ambako majeshi ya Ufaransa yameondolewa katika nchi hizo.

Hapa ni wazi kuwa mgogoro wa Ukraine unasababisha vita ya rasilimali kati ya mataifa makubwa kugombea sehemu zenye maliasili ya kutosha.

M23 waulizwe mafunzo, silaha na vifaa vyote vya kivita wazitoa wapi na nini gharama zake na nani azilipa?

Tukipata majibu hapo ndipo twaweza kuja na kusimamia hoja kikamilifu kwamba siku za Tshisekedi zahesabika.
 
M23 waulizwe mafunzo, silaha na vifaa vyote vya kivita wazitoa wapi na nini gharama zake na nani azilipa?
Wanadai wao walikuwa sehemu ya jeshi la Congo ila waliondoka jeshini na silaha zao na kuasi baada ya serikali ya Drc kutotimiza makubaliano baina yao.
 
Wanadai wao walikuwa sehemu ya jeshi la Congo ila waliondoka jeshini na silaha zao na kuasi baada ya serikali ya Drc kutotimiza makubaliano baina yao.
Mkuu, fuatilia hii zipo taarifa kuwa kuna "contractor" wa kuaminika kutoka Western Europe atoa mafunzo na kila kitu kwa M23.

KP ana influence kubwa sana katika Commonwealth kwa sasa na hii inampa access kwa mambo mengi.

Kuna masuala mengi sana yapo nyuma ya pazia ila kwa sasa Tshisekedi atumika tu.

Ila Sultani Makenga hawezi kuondoka jeshini (Congolese Army) na vifaa vyote yakiwemo "armour vehicles" ambayo mida hii yafagia kule Eastern Congo DRC.
 
Mkuu

Proved


Usishangae yapo mambo mengi sana ya kijasusi yaendelea kwa sasa duniani ni mazito sana.
Inawezekana mkuu, ushindi wanaoendelea kuupata M23 dhidi ya jeshi la Drc unashangaza Sana, huenda kuna mkono mzito nyuma yao.
 
Kagame ana uhakika wa kuitandika Congo wakati wowote na sehem yoyote ndomaana unamuona ana kiburi. Laiti Congo wangekuwa vizuri kijeshi na ki silaha basi kitambo angekuwa ashanywea.

Congo wamejaza wacheza ndombolo yasolo jeshini, wakati Rwanda wamejaza wapiganaji wa vita wenye weledi wa mapigano. So Kagame atakosaje jeuri?
Hii ni fedheha kwa nchi kubwa kwa idadi ya watu, raslimali na eneo kama DRC kudharauliwa na ka nchi kadogo!
 
Back
Top Bottom