TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

Status
Not open for further replies.
Baada ya kukosa nafasi ya kuaga uwanjani nikasema ngoja niwahi uwanja wa ndege. Nilichokiona huku watu ni wengi mno wengine wametoka kwa miguu uwanjani wa Uhuru wakisindikiza msafara. Huzuni imetawala hapa ni vilio tu.
Sifa za kijinga! Corona ipo!
 
Lakini amefanya mambo mengi ndani ya muda mfupi
 
Wala sijapata ahueni,naona watu wanampigia debe Kinana na team yake warudi.Tunarudi kulekule kwa bora hata Magufuli.
Hiyo kauli ya "Bora Magufuli" hautaisikia nchini Tanzania mpaka unaingia akhera.

Kitu ambacho tumekuwa nacho na tumekisikia mara nyingi ni "Bora Kikwete", "Bora Mkapa", "Bora Mwinyi" na "Bora Nyerere".

Kwa sasa tunasikiliza ya mama yetu mpendwa Samia.
 
Kwahiyo na ya Nyerere ifutwe?
 
Mimi nilikuwa anti-Magufuli (kama rais, si kama mwanadamu), lakini mkuu hapo mkuu umeteleza, kumkumbuka mtu ni muda wowote.

Suala la kumkumbuka mtu aliyepita linatokana na matatizo ya aliyepo kwa wakati huo. Tulianza kusema bora Kikwete baada ya Magufuli kuminya demokrasia na kuisigina katiba vya kutosha, vivyo hivyo anayefuata anaweza kukengeuka na kufanya ujinga wa kupita viwango. Hapo itakuwa rahisi sana kusema bora Magufuli kuliko huyu!
 
Apumzike Kwa Amani
Amelala Mauti
Tutamkumbuka Sana
 
Ni kweli mkuu,"wanasema never say never" anaweza kuja mwendawazimu akawa hajali vitu wala watu....maana kwa Magufuli tunamkosoa tu kwa kutojali watu....lakini kwenye vitu aliwajibika siyo siri.
 
Acha upumbavu..!! Unahamasisha watu washerekee kifo. Tukikupwapua tukuhifadhi nyuma ya nondo uanze kulialia?
Mkuu sijachochea ila niliona post zao wakiomba mzee afe wafurahie, so nimeona sala zao zimejibiwa ikabidi niwakumbushe
 
Aisee
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…