Quran 112:1
Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.
112:2 - Mwenyezi Mungu Mkusudiwa.
112:3 - Hakuzaa wala hakuzaliwa.
112:4 - wala hana anaye fanana naye hata mmoja.
Infropreneur 14:7
Ulimwengu na vyote vilivyomo except man-made things, Havina na havihitaji kuwa na muumbaji.
14:8- Kama kila kitu kilichopo lazima kiwe na muumbaji wake, Hata muumbaji wa kila kitu lazima awe na muumbaji wake mwingine. Hivyo hivyo pasipo kukoma.
14:9- Pasiwepo kitu chochote kile kilicho jitokeza chenyewe pasipo muumbaji. Maana kitazua maswali ya kiliwezaje kuwepo pasipo muumbaji.
14:10- Na kama si lazima kwamba kila kitu kilichopo kina muumbaji,
Hata Ulimwengu na vyote vilivyomo except man-made things, Havina muumbaji.
Infropreneur;
20:1- Ulimwengu Hauna muumbaji.
20:2- Ulimwengu Hauhitaji kuwa na muumbaji.
20:3- Ulimwengu ulikuwepo, upo na utaendelea kuwepo milele yote.
Hizi Aya nimekuwekea Ili kukuonyesha kile ambacho Mimi nakiamini kuhusu uwepo wa Mungu kiimani
Hizi aya nimekuwekea kukuonyesha vile logic ilivyo kifalsafa.
Wala sijakuambia au kukulazimisha na wewe uamini kama Mimi
Hukatazwi kuwa na imani yako, unaweza kuamini hata mawe, milima mapango, majabali n.k
Lakini ukianza kudai kwamba imani yako ina ukweli lazima uthibitishe.
Ila Mimi nataka wewe uthibishe kile ambacho unakiamini Kwa sababu wewe unasema hauwezi kuamini kitu ambacho hauwezi kukithibisha Kwa akili zako
Sihitaji kuamini.
Nahitaji kujua kwa uhakika, ushahidi na uthibitisho.
Sasa Cha ajabu na wewe tena unaamini kitu ambacho hauwezi kukithibisha Kwa kutumia akili yako
Mimi siamini kwenye kuamini.
Sina imani ya aina yeyote ile.
Na kama Kila unachokiamini unaweza kukithibisha Kwa akili zako haya thibisha Sasa hi kauli yako
Mimi siamini kwenye kuamini.
Sina imani ya aina yeyote ile.
Sihitaji kuamini, Nahitaji kujua kwa uhakika, ushahidi na uthibitisho.
1) Jua halijazuka
2) Jua limekuwepo milele
3) Jua litaendelea kuwepo milele
Hakuna wakati wowote ule ambapo Jua ☀️ halikuwepo, kisha likawepo.
Jua limekuwepo milele yote na wakati wote litaendelea kuwepo.
Na mwisho thibitisha kama wewe unazo akili Kwa kuzipiga picha hizo akili zako uweke picha yake hapa tuzione Ili tujue akili zako zinafananaje
Akili ni dhana ya kufikirika isiyo katika umbo la kuonekana au kushikika.
Akili ni kielelezo cha namna gani ubongo 🧠 hufanya kazi.
Akili ni nomino dhahania. Sawa na nomino kama njaa, kiu, hofu, woga, wasiwasi n.k
Do you get the point?