Rasmi Putin aonesha sample za noti mpya za BRICS. Je, huu ndio mwisho wa US Dollar?

Rasmi Putin aonesha sample za noti mpya za BRICS. Je, huu ndio mwisho wa US Dollar?

Hata kuishusha thamani US Dollar ni muhimu sana mkuu.Marekani wameionea sana dunia kwa kutumia dola yao,hiyo haikubaliki kabisa.

WHAT DO OTHER BRICS LEADERS THINK?​

South African officials had said a BRICS currency was not on the agenda for the summit.

In July, India's foreign minister said, "there is no idea of a BRICS currency". Its foreign secretary said before departing for the summit that boosting trade in national currencies would be discussed.

 
Wandugu mkae mkijua usd inaenda kuanguka na kupoteza umaarufu katika soko la Dunia.
Nitaeleza Kwa lugha nyepesi ili watu wasio wachumi wenzangu mnielewe.

Pesa kubwa duniani.

Kabla ya Euro kulikua Kuna Paund na USD.
Euro ilianzishwa baadae sana mwishoni mwa miaka ya 90.
Kwa Sasa kwa umaarufu Euro imeifunika Paund ya Uingereza.

Kwa Nini USD inaenda kupoteza nguvu umaarufu na kuanguka baada ya ujio wa fedha ya BRICS?

Haihitaji kua na elimu ya uchumi kuelewa hili.
Iko hivi.

Hakuna asiejua kua, USD ndio fedha pekee inayotumiwa na watu wengi zaidi ama nchi nyingi zaidi hapa duniani kwa ajili ya kubadilishana kati ya fedha na bidhaa.

Sasa iwapo itapatikana fedha nyingine ambayo imeundwa kutoka kwenye nchi zenye idadi kubwa sana ya watu hapa duniani,mfano china ,India, Brazil,Urusi na nchi nyingine.
Na Kuna nchi nyingi zimeonesha kiu ya kujiunga,
Kwa maana hiyo nchi zote hizo zitaachana na matumizi ya USD katika kufanya biashara baina Yao,yaani baina ya nchi wanachama wa BRICS .
Kwa Hali hiyo,dola itakua imepoteza umaarufu na nguvu.

Mfano,mtu akitaka kununua bidhaa kutoka nchi mwanachama wa BRICS,nchi muuzaji itamuambia alipe kwa fedha ya BRICS badala ya USD,
Hapa USD itakua imepeoteza umaarufu na nguvu.
Matumizi ya USD yataenda kupungua kwa sababu nchi nyingi sana zitaacha kuzitumia USD kama chombo Cha kubadilishana bidhaa.
Sasa kama nchi zitaachana na USD kwa Hali ya kawaida haiwezi kubaki na thamani ileile.

Kwa mfano Sasa hivi ukitaka kununua kitu chochote nje ya nchi,kama
vile kununua magari ama bidhaa nyingine kutoka Japan,china,India,Urusi,south Africa,Saudi Arabia,Iran,Dubai, Malaysia, Singapore, Korea kusini, Philippines, Taiwan, Israel,Canada n.k ni lazima ulipie kwa USD,.
Lakini BRICS currency ikija, nchi nyingi zitahamia kwa fedha ya BRICS,
Huo pia utakua ni mwanzo wa kupoteza umaarufuwa USD.

Kwa lugha rahisi kabisa kama fedha ilikua inatumiwa na nchi nyingi,nchi nyingine nyingi zikaamua kuachana nayo hakika thamani yake haiwezi kubaki kama ilivyokua mwanzo.

Hata hivyo kitakachotokea

Nadhani watu wengi hapa wanatakiwa watofautishe kati ya USD kushuka thamani na USD kupoteza umaarufu.
Kwa mtazamo wangu naamini USD haitashuka thamani,Bali itapoteza umaarufu.
USD itabaki na thamani yake,kwa sababu hata Marekani yenyewe itakua inauza bidhaa zake kwa USD,


ingawa nayo italazimika kununua bidhaa kutoka kwa BRICS members kwa kutumia fedha ya BRICS.
Wakati Sasa hivi ukienda kununua bidhaa Marekani utalipa kwa USD na Marekani ikija kununua bidhaa kwako italipa kwa USD .

Anguko lingine la USD ni haitatimika Tena kama fimbo kuzichapia nchi hasimu wa Marekani
Hapa nguvu ya USD itakua imekwisha kabisa.


Hali hii ndio iliikumba Pound ya Uingereza.
Kabla ya kuanzishwa kwa euro,pound ya Uingereza ilikua maarufu sana,lkn Sasa hivi imebaki na thamani yake lkn sio maarufu kama euro.

Mtazamo wangu.
Bora wewe naelewa point yako lkn wengi humu wanachangia hoja wakiwa na ushabiki wa upande wanao upendelea na sio uhalisia.
 
Rais wa Urusi, Vladimir Putin, wakati yupo kwenye mkutano mkuu wa BRICS uliofanyika Kazan aliwashangaza washiriki kwa kugawa sampuli za noti mpya za Benki ya BRICS, ishara inayodaiwa kuwa mwisho wa enzi kwa Dola ya Marekani kama sarafu ya akiba duniani.

Noti hizo za BRICS, ambazo zimeonekana kwa mara ya kwanza katika hafla hiyo ya kimataifa, zimeibua mjadala mkubwa kuhusu mustakabali wa mfumo wa fedha wa dunia.

Sarafu hiyo mpya inasemekana kuungwa mkono na bidhaa halisi kama dhahabu na mafuta, tofauti na Dola ya Marekani ambayo ni sarafu ya "fiat" isiyo na dhamana ya moja kwa moja ya mali.



Sarafu ya BRICS Kuipiku Dola ya Marekani?

Wachambuzi wanaeleza kuwa uzinduzi wa sarafu ya BRICS huenda ukawa mwanzo wa kipindi kipya cha kutoitegemea Dola ya Marekani katika biashara za kimataifa.


Wanaonya kuwa sarafu hiyo mpya inaweza kupunguza sana ushawishi wa kiuchumi wa Marekani ulimwenguni, hasa kutokana na ukweli kwamba nchi nyingi zinaweza kuacha kutumia Dola kama sarafu ya kibiashara.



Mjinga mjinga China ananunua bond za Marekani kila siku. Huu usanii tu!!
 
Shida miongoni mwao kuna wanafiki, USA akianza crackdown watakaa pembeni na kumuacha Russia peke yake.
Huu muunganiko haujaingiwa kienyeji Russia ana akili sana. Wale founding members wote wanavVETO powers na wamesaini agreement ambayo Kila mmoja lazima aitekeleze ndio maana umeona uturuki amepingwa na India kujoin kwa sababu kwanza Bado yupo NATO na ana ushirika na Pakistan. Kwahiyo huu muungano utashape nchi wanachama na hilo ndio anguko la upande wa pili
 
Una teseka ukiwa wapi !?


Ina maana wewe unajua Sana kuliko Putin na washirika wake !?

Hata kuunda sindano Tu hauwezi halafu unataka uwakosoe watu wanao ipasua kichwa USA na washirika wake

Ila wabongo 🚮🚮🚮😁😁😁😁
Umeongea vizuri sana.
Lakini huyo uliemjibu Yuko upande wako.
Yaani mnaongea lugha moja ila hamjaelewana.
 
Kama US Dollar na upuuzi wote wa US on other nations ilikubalika all that long,the BRICS currency kutumika is just a matter of time.There is urgent need for such a currency,where no country will dictate terms on another.The World is fed up of US bullying.
Sasa ni kwa nini upost thread ya habari ya uongo?
 
Broo umeelewa kwanini nimemjibu hivyo jamaa!??
Jamaa aliuliza kati ya dollar na hela ya Brics ukiambiwa uchague utachukua ipi!?
Ndio nikamjibu Brics bado haijaanza kufanya kazi UNASHINDANISHAJE NA DOLLAR!?
Maana yangu atulie sarafu ya Brics ianze kufanya kazi halafu baadae ndio aulize hilo swali.
Maana ni sawa uanze kushindanisha silaha ambayo China ndio kwanza ametoka kuiunda kiwandani labda na ATACMS ya USA,ilhali ya China bado haijawa operational kama ya USA.
Niuwie radhi
 
Dunia
Rais wa Urusi, Vladimir Putin, wakati yupo kwenye mkutano mkuu wa BRICS uliofanyika Kazan aliwashangaza washiriki kwa kugawa sampuli za noti mpya za Benki ya BRICS, ishara inayodaiwa kuwa mwisho wa enzi kwa Dola ya Marekani kama sarafu ya akiba duniani.

Noti hizo za BRICS, ambazo zimeonekana kwa mara ya kwanza katika hafla hiyo ya kimataifa, zimeibua mjadala mkubwa kuhusu mustakabali wa mfumo wa fedha wa dunia.

Sarafu hiyo mpya inasemekana kuungwa mkono na bidhaa halisi kama dhahabu na mafuta, tofauti na Dola ya Marekani ambayo ni sarafu ya "fiat" isiyo na dhamana ya moja kwa moja ya mali.



Sarafu ya BRICS Kuipiku Dola ya Marekani?

Wachambuzi wanaeleza kuwa uzinduzi wa sarafu ya BRICS huenda ukawa mwanzo wa kipindi kipya cha kutoitegemea Dola ya Marekani katika biashara za kimataifa.


Wanaonya kuwa sarafu hiyo mpya inaweza kupunguza sana ushawishi wa kiuchumi wa Marekani ulimwenguni, hasa kutokana na ukweli kwamba nchi nyingi zinaweza kuacha kutumia Dola kama sarafu ya kibiashara.

Dola itaanguka, brics currency itaanguka, na sarafu zingine zoooote zitaanguka very soon kutakuwa na currency moja dunia nzima asikiaye na afahamu
 
Hata kuishusha thamani US Dollar ni muhimu sana mkuu.Marekani wameionea sana dunia kwa kutumia dola yao,hiyo haikubaliki kabisa.
USD itashuka thaman at least kwa nusu au chini ya nusu ni suala la muda tu uchumi wa US unacollapse na USD inaisha kuwa global currency mwakani kipindi kama hiki tutakuwa tunajionea dhahiri hiki nilichoandika.
 
Unajua marekani itabaki kuwa taifa kubwa na hakuna mtu wakuitoa katika ramani ya hii dunia. Nasema hivi nikiwa mtu neutral ila huo ndio ukweli

Dola imeanza kutumika dunia hii lini? Unazani itachukua muda gani kwa hiyo ela ya brics kuja ku dominate dola.

Online shopping zote kubwa kama alibaba na wengineo wanauza bidhaa zao kwa dola wala hawatumii sarafu ya china.

Angalia waasisi wa taifa hili ni kina nani na jaribu kufanya tafiti ya kusoma historia yao.... Hawa watu walikuwa ni vichwa na hawakuibuka kama kina Hitler .
 
Unajua Marekani na ulaya wote Bado wanafanya Biashara na Urusi pamoja na kuweka vikwazo vyao vyote!?? Na unajue kuwa hawatumii dollar kama medium of exchange!? .... Unajua Hilo Kwanza kuwa Marekani na ulaya Bado Wanafanya Biashara na Urusi Ili tuendelee!??
Najua.

Biashara kati ya Marekani na Urusi ama Ulaya/EU na Urusi ni biashara zenye thamani ndogo sana kidunia ukilinganisha na biashara kati ya Marekani na China au Marekani na Ulaya.

Urusi sio mshirika mkuu wa kibiashara wa Marekani na Ulaya/EU hivyo medium of exchange haina impact yoyote ya maana yenye kuathiri thamani ya Dollar kwenye international trade. Medium of exchange kati ya Marekani na Urusi ama Ulaya/EU na Urusi inategemeana na mikataba iliyopo au kanuni za kibiashara kati ya pande mbili husika.
 
Wabongo Kwa ujuaji hakuna binadamu anatuweza hapa duniani.
Yaani unataka kubishana Hadi na akina Ramaphosa.
Aisee uko vizuri.
Hata wakati euro inaanzishwa Kuna watu kama wewe walikuaja na ngonjera zao lkn euro Leo IPO na inadunda.
Mimi Kila siku hua nasema ,wewe Mtanzania hauwezi kuwa na akili kuliko viongozi, wasomi,wachumi na wataalamu na wabunge kutoka nchi za BRICS na wa nchi zinazotaka kujiunga na BRICS.
Hao wote hawawezi kua wajinga ila wewe Msimbiti ukawa na akili kuwazidi wao.
Ramaphosa na chama chake [ANC] anaongoza serikali ya nusu mkate South Africa. Aliyebishana na Ramaphosa si mimi pekee bali hata washirika wao kwenye serikali ya nusu mkate [DA] wameipinga kauli yake kwa facts.

Urusi haipo hata kwenye top 10 ya washirika wa karibu wa South Africa kibiashara. Ushirika wa Urusi na South Africa unatokana na historia ya itikadi kati ya chama cha ANC na Urusi. Ukija kwenye biashara (trade ties) kati ya Urusi na South Africa hakuna cha maana.
 
Hata kuishusha thamani US Dollar ni muhimu sana mkuu.Marekani wameionea sana dunia kwa kutumia dola yao,hiyo haikubaliki kabisa.
Itakuwa mshindani lakin sio kwa kiwango hicho au kwa haraka hiyo. Maana nakumbuka wakati wa euro inatoka kulikuwa na stor kama hiz pia. Nachojiuliza pia hiv kwa upande wa soft payed itakuwaje
 
Itakuwa mshindani lakin sio kwa kiwango hicho au kwa haraka hiyo. Maana nakumbuka wakati wa euro inatoka kulikuwa na stor kama hiz pia. Nachojiuliza pia hiv kwa upande wa soft payed itakuwaje
Mkuu don't mix things.Kwenye Euro hapakua na issue ya replacement of a currency.Now nations are seeking to replace a currency in their transactions,which is still a legal tender in the US.What does this mean,this means that the currency will crumble in terms of value worldwide and even in the US itself.
 
Back
Top Bottom