RC Mtaka ataka wanafunzi wanaofanya makosa wafukuzwe shule

RC Mtaka ataka wanafunzi wanaofanya makosa wafukuzwe shule

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
Mtaka ni kama ana serikali yake ambayo haiendani na ya CCM na Samia, hivi mtoto unamfukuza shule ili iweje? Kwanza ni mtoto, anahitaji malezi na maangalizi.

Kwa aina ya waalimu tulio nao, hivi unawapa mamlaka yote hayo?

Mtaka ni moja ya members wazuri wa magrupu ya Chadema, na huwa mchangiaji mzuri wa fedha

==========

Mtaka: Mwanafunzi mtukutu afukuzwe shule, asichapwe​

Mtaka.png

Njombe. Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Anthony Mtaka amewaagiza wakuu wa shule za Serikali kuwafukuza wanafunzi watukutu badala ya kuwachapa viboko au kuwarudisha nyumbani.

Mtaka alisema hayo alipozungumza na wanafunzi wa Sekondari ya Wasichana ya Manyunyu, iliyopo Matembwe wilayani Njombe.

Alisema shule si sehemu za watu kufanya mizaha na wazazi wengi wanaheshimu sana shule binafsi lakini za Serikali mambo huwa tofauti.

“Kuna shule za binafsi zikiagiza mwanafunzi aje na nguo mbili wanaenda nazo hizohizo, ukienda na ya tatu unarudishwa, wanakuambia shule hii ni marufuku mtoto kuja na simu ukienda nayo unarudishwa nyumbani, huku kwenye shule zetu za umma tuna mizaha mingi,” alisema.

Mizaha hiyo alisema inasababisha mwanafunzi akifanya vituko na mwalimu akamwadhibu basi mwalimu atajadiliwa hadi kwenye mitandao ya kijamii na polisi watamkamata kuandika maelezo, lakini ujinga huo haufanyiki shule binafsi.

Alisema jamii inapozungumzia maadili ni lazima yasimamiwe na namna ya kuyasimamia ni kuyajenga tangu vijana wakiwa shuleni.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe, Valentino Hongoli alisema “mwaka jana mheshimiwa Rais alitupatia Sh60 milioni ambazo tulijenga madarasa matatu na ofisi shuleni hapa, kama tusingepewa watoto wangeshindwa kusoma.”

Mkuu wa Sekondari ya Wasichana Manyunyu, Advera Bagoka alisema wanafunzi waliotakiwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka huu walikuwa 202, ila walioripoti ni 120 na 51 wamebadilisha shule, huku 31 hawajulikani walipo.

“Shule yetu ina uhaba wa walimu wa sayansi na hisabati,” alisema.
 
Huo utaratibu wa kufukuza shule wanafunzi wanaofanya makosa yaliyo ainishwa kwenye sheria za shule, mbona uko miaka yote! Sasa udikteta wa huyo Mtaka uko wapi?.

Kuwakumbusha watu kuzisimamia sheria za shule ndiyo udikteta!! Yaani unataka wanafunzi wanaovunja sheria za shule, waachwe tu!! Unataka Taifa liwe na kizazi cha aina gani miaka ijayo?

Wewe kama ungeachwa ufanye unavyotaka wakati unasoma, muda huu ungekuwa wapi? Si ungekuwa umeshachomwa moto kwa ujambazi sugu!!
 
Mtaka yupo sahihi maana kaeleza na sababu, wakiadhibiwa wanawashtaki walimu. Ili isiwe tabu na walimu kupotezewa muda wafukuzwe tu, waende wakasome shule za kulipia au wasomeshwe majumbani kwao.
 
Weee jamaa ni aina ya watu wanaopenda mambo ya holela. Sheria za shule ziko wazi, yapo makosa ambayo mwanafunzi akifanya anastahili kufukuzwa.

Kufumbia macho makosa hayo ni kujenga kizazi cha hovyo cha wasioheshimu Sheria. Wewe mkumbushe mwanao kuwa taasisi zinaendeshwa kwa Sheria na kwamba anapaswa kuzizingatia. Mweleze pia kuwa asipotii Sheria Kuna adhabu na mojawapo ni kufukuzwa shule.
 
"Kwa aina ya waalimu tulio nao, hivi unawapa mamlaka yote hayo? "Unamaanisha Nini kwa sentensi hii? Kwamba walimu waliopo hawajafunzwa namna ya kulea wanafunzi, au hawawezi kutafasiri Sheria za shule hivyo una wasiwasi hawatatenda haki? Mfunze mwanao kuzingatia Sheria au la atafukuzwa na arudi nyumbani kwako maana mchuma majanga hula na wakwao
 
mpwayungu village pls njoo huku mwalimu mwenzangu, hivi waalimu wa kitanzania wanafeli wapi? Why ubora wa elimu ya Zimbabwe, Botswana ni mkubwa mno kuliko wa kwetu sisi? Why upper class wanasomesha watoto wao western europe (hakuna kufukuzana wala copral punishment), SA, au Zimbos wakati watoto wa walala hoi ndio wasome hapa Mtwivila sec school?

Please POLITICIANS STAY AWAY kwenye mada hii, ninyi ndio mmevuruga foundation ambayo nchi ilitaka kuwa nayo, Makweta commission kuhusu elimu ndio ilitakiwa ituwekee mfumo mzuri wa kielimu nchi hii, yaani muda huu tungekua tunajenga kwenye msingi imara, watoto wangekuwa wanafundishwa coding &programing maana hii ndio future, sisi bado tupo kwenye history ya akina Dr. Livingstone ambayo haitusaidii chochote, mwanafunzi kufukuzwa shule kwangu it's a NO, copral punishment also its a NO.
 
mpwayungu village pls njoo huku mwalimu mwenzangu, hivi waalimu wa kitanzania wanafeli wapi? Why ubora wa elimu ya Zimbabwe, Botswana ni mkubwa mno kuliko wa kwetu sisi? Why upper class wanasomesha watoto wao western europe (hakuna kufukuzana wala copral punishment), SA, au Zimbos wakati watoto wa walala hoi ndio wasome hapa Mtwivila sec school?

Please POLITICIANS STAY AWAY kwenye mada hii, ninyi ndio mmevuruga foundation ambayo nchi ilitaka kuwa nayo, Makweta commission kuhusu elimu ndio ilitakiwa ituwekee mfumo mzuri wa kielimu nchi hii, yaani muda huu tungekua tunajenga kwenye msingi imara, watoto wangekuwa wanafundishwa coding &programing maana hii ndio future, sisi bado tupo kwenye history ya akina Dr. Livingstone ambayo haitusaidii chochote, mwanafunzi kufukuzwa shule kwangu it's a NO, copral punishment also its a NO.
Mwingine huyu hapa wa ajabu ajabu! Kweli nchi yetu Ina watu wanao umwa
 
mpwayungu village pls njoo huku mwalimu mwenzangu, hivi waalimu wa kitanzania wanafeli wapi?,why ubora wa elimu ya Zimbabwe, Botswana ni mkubwa mno kuliko wa kwetu sisi?,why upper class wanasomesha watoto wao western europe (hakuna kufukuzana wala copral punishment),SA,au Zimbos wakati watoto wa walala hoi ndio wasome hapa Mtwivila sec school?,pls POLITICIANS STAY AWAY kwenye mada hii,ninyi ndio mmevuruga foundation ambayo nchi ilitaka kuwa nayo, Makweta commission kuhusu elimu ndio ilitakiwa ituwekee mfumo mzuri wa kielimu nchi hii, yaani muda huu tungekua tunajenga kwenye msingi imara, watoto wangekuwa wanafundishwa coding &programing maana hii ndio future, sisi bado tupo kwenye history ya akina Dr.Livingstone ambayo haitusaidii chochote, mwanafunzi kufukuzwa shule kwangu it's a NO, copral punishment also its a NO
Sasa wewe ndoo umeandika nini? Hii nchi ina balaaa

Sent from my TECNO KA7O using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom