RC Rose: Mkoa wa Chato utakuwa na wilaya 5 Kakonko, Biharamulo, Ngara, Bukombe na Chato yenyewe

RC Rose: Mkoa wa Chato utakuwa na wilaya 5 Kakonko, Biharamulo, Ngara, Bukombe na Chato yenyewe

Wachukue na wilaya zote zinazovuka maji za Mwanza zihamie huko, Sengerema na Ukerewe, Mwanza ni kubwa sana, waendelee kugawa na mikoa mingine hata dar waigawe mara mbili maana kwa Tanzania maendeleo yanafika vijijini haraka kwa njia hiyo mikoa mipya na kuipa maendeleo ya mikoa.
Duh.....umekasirika sana!
 
Kwa nini walazimishe hivyo mkoa wa Chato kuzaliwa ? Kwa nini uende ukapore Wilaya 3 za mikoa mingine Ili tu kutimiza adhma ya Mwendazake?
 
Naunga mkono kabisa kuundwa kwa mkoa wa Chato kwa sababu kuu moja, ... nayo ni kuisogeza serikali karibu zaidi na ukanda huu uliopakana na chanzo kikuu cha migogoro ya nchi za maziwa makuu (TUTSI/HUTU conflict zone)!
👊 😎✌️💥☠️☠️☠️💀
 
ni sawa tu!!Huchochea maendeleo kwa sehemu ambazo zilikuwa bado duni kimaendeleo!!!Nadhani Ndugu yangu MPANGO atasimamia vema hili!!
 
Hivi bado Kuna wakuu wa mikoa ambao wana hamu sana ya kupigwa mti kimasihara?
Unawezaje kuja na hayo mapendekezo?
Hivi tunajua gharama za kuanzisha mkoa mpya na kuuendesha?

Kabla ya Chato kuwa mkoa, nadhani uindwe kwanza hii mikoa.
1. Butiama.
2. Kisarawe.
3. Lupaso.
4. Msoga.

Itifaki ni muhimu kuzingatiwa kwanza.
Kwa kweli huu ujinga mama asiuendekeze. Tuna mengi ya kufanya, hela hatuna. Sasa ya nn kuongeza gharama za kuendesha serikali kwa kuongeza mkoa?
 
Hivi JPM alienda kwa mganga gani yaani jamaa amekufa huku wazima wana haha kama kondoo
 
Kahama ndiyo inastahili kuwa mkoa na siyo Chato. Hata hizo wilaya za Bukombe na Mbogwe zilimegwa kutoka wilaya ya Kahama. Sasa wameimega tena na kuanzisha wilaya za Ushetu na Ukune. Wilaya hizi zirudishwe kuifanya Kahama kuwa mkoa. Wanaweza kuimegea na wilaya za Ukene na Urambo. Kahama kimaendeleo na kiuchumi iko juu sana ukilinganisha na Chato. Mji tu wa Kahama ni zaidi ya Dodoma! Mzunguko wa fedha Kahama unazidi DSM. Shida ya watu wa Kahama ni wapole sana na hawajui kupiga kelele eg mbunge wao Kishimba yeye kila kitu poa tu. Hata kudai barabara ya kutoka Kahama hadi Urambo kupitia Ukune kujengwa kwa lami hajui wakati barabara hiyo ni ya muhimu sana ku tap utajiri wa eneo hili kwa manufaa ya taifa letu. Lina utajiri wa asali (nyuki), maziwa (ng'ombe), miwa (sukari), mahindi, mchele, mafuta (karanga), mahama, dhahabu na madini mbali mbali.
 
Makabila mseto mangapi ? Waha, wasukuma, wasubi, wahangaza na wasumbwa. Na wasukuma watabaki kabila kubwa katika mkoa huo tarajiwa maana Wilaya hizo karibu zote isipokuwa Ngara na Kakonko wasukuma ndio majority
mkoa wa chato utakua na makabila mseto hadi raha
 
Umemkomesha
Kama za Mkoa wa Mara zilivyokaliwa na wajaluo (Kenya) , Arusha wamasaai (Kenya) Mtwara na Lindi wamakonde (Nchumbiji) - Ruvuma wangoni na wayao (Malawi) - Kilimanjaro pia na Kagera upande wa mpakani na Uganda! Pia Mpanda,Katavi, Sumbawanga (Zambia) - Kigoma wamanyema (DRC).
Kwa hiyo Usishangae warundi na wanyarwandwa kuwapo. Ubaguzi ulishindwa hata Africa ya Kusini wakati wana bomu la nyuklia! Sembuse ubaguzi wako wa chuki tu na ujinga! Shame on you!
 
Mhh ukerewe kuna mapendekezo ya kuunda mkoa wa Bunda na Ukerewe.
Wachukue na wilaya zote zinazovuka maji za Mwanza zihamie huko, Sengerema na Ukerewe, Mwanza ni kubwa sana, waendelee kugawa na mikoa mingine hata dar waigawe mara mbili maana kwa Tanzania maendeleo yanafika vijijini haraka kwa njia hiyo mikoa mipya na kuipa maendeleo ya mikoa.
 
Mhh. Uitoe Kahama Shinyanga ibaki na nini ?
Kahama ndiyo inastahili kuwa mkoa na siyo Chato. Hata hizo wilaya za Bukombe na Mbogwe zilimegwa kutoka wilaya ya Kahama. Sasa wameimega tena na kuanzisha wilaya za Ushetu na Ukune. Wilaya hizi zirudishwe kuifanya Kahama kuwa mkoa. Wanaweza kuimegea na wilaya za Ukene na Urambo. Kahama kimaendeleo na kiuchumi iko juu sana ukilinganisha na Chato. Mji tu wa Kahama ni zaidi ya Dodoma! Mzunguko wa fedha Kahama unazidi DSM. Shida ya watu wa Kahama ni wapole sana na hawajui kupiga kelele eg mbunge wao Kishimba yeye kila kitu poa tu. Hata kudai barabara ya kutoka Kahama hadi Urambo kupitia Ukune kujengwa kwa lami hajui wakati barabara hiyo ni ya muhimu sana ku tap utajiri wa eneo hili kwa manufaa ya taifa letu. Lina utajiri wa asali (nyuki), maziwa (ng'ombe), miwa (sukari), mahindi, mchele, mafuta (karanga), mahama, dhahabu na madini mbali mbali.
 
Mkuu wa mkoa wa Geita mh Rose amesema ombi la kuunda mkoa wa Chato likipita basu mkoa wa Geita utabakiwa na wilaya za Busanda, Nyang'wale na Geita yenyewe na Mbogwe

RC Rose amesema mkoa mpya wa Chato utapokea wilaya 1 kutoka Kigoma na 2 kutoka Kagera.

Kwa maana hiyo mkoa mpya wa Chato unaopendekezwa utakuwa na wilaya 5 ambazo ni Kakonko kutoka Kigoma, Bihalamuro na Ngara kutoka Kagera na Bukombe na Chato yenyewe kutoka Geita.

Chanzo: ITV habari!

Kazi Iendelee
Hiyo wilaya ya chato iunganishwe na mkoa wa Bukoba ili uwanja wa ndege wa kimataifa wa chato uwe kwetu sisi wahaya wenye pesa, wasomi, wenye mapesa ya kutumia usafiri wa ndege tufwaidi. Vinginevyo hapo chato patakuwa magofu kama kule badolite nyumbani kwa marehemu tajiri dictator mobutu seseko wa zaire bhoojo.
 
objectively, kuimega Chato kutoka Geita (ilikuwa Kagera kabla), Ngara-kutoka Kagera, Kakonko kutoka Kigoma, Bukombe na Biharamulo kuwa mkoa ni jambo jema. Kwa sasa wanaofaidi matunda ya mkoa Kagera ni Bukoba, Muleba na Karagwe. waiache Ngara iondoke tuu. mfano Ngara ilichangia sana kujenga miundo mbinu ya shule za Bukoba miaka ya nyuma....mda si mrefu wakaambiwa kila wilaya ijitegemee kwa kujenga miundombinu yake. Mpaka leo Ngara haija recover. ni miaka ya juzi tuu imeanza kupata shule zake. Ndo maana hata wana ngara waliopata elimu kupitia shule za bukoba ni wachache. Pia kutoka Ngara kwenda Bukoba ni mbali.

Chato utakuwa mkoa wenye coherence. Ngara na Kakonko lugha yao ni almost ile ile. Biharamulo na Chato zamani ilikuwa wilaya moja. imagine mtu kutoka Kakonko kwenda Kigoma kutafuta huduma. kwa raslimali walizonazo...utakuwa mkoa wenye potential sana. Ngara kuna madini ya kutosha...Chato uvuvi nk....Hata kikanisa..Ngara, Chato, baadhi ya sehemu za Kakonko, na Biharamulo ziko chini ya Jimbo moja la Rulenge-Ngara......(ingawa hili kiuhalisia halina uzito-maana imani za kidini na serikali ni tofauti)

Sema, kurahisisha maisha na huduma kwa wananchi....huu mkoa ungewekwa katikati pale Biharamulo. Ila hata makao makuu yakiwekwa Chato sioni shida...

Changamoto hapa ni kwamba wengi wanamchukia Hayati kwa hiyo hata swala la huu mkoa wanaliangalia kwa miwani ya mwendazake. ila kiukweli Chato na hizo wilaya tajwa.. unastahili kuwa mkoa.

Ingawa nashauri kuondoa au kupunguza hizi chuki dhidi ya mwendazake....tunaweza kuuita jina lingine ila isiwe Chato. Mf. mkoa wa Rubondo au mkoa wa Nyabugombe...au Burigi....nawaza tuu.

Ingawa nimalizie kwa kusema kwamba ingawa Hayati alikuwa anatokea Chato, Chato na hizo wilaya kuna watanzania wengine pia. Wathaminiwe na kuheshimiwa pia. sioni kwa nini mwananchi wa Ngara au Kakonko awe penalized kwa sababu tuu hizi wilaya ziko karibu na Chato.
 
Back
Top Bottom