RC Rose: Mkoa wa Chato utakuwa na wilaya 5 Kakonko, Biharamulo, Ngara, Bukombe na Chato yenyewe

RC Rose: Mkoa wa Chato utakuwa na wilaya 5 Kakonko, Biharamulo, Ngara, Bukombe na Chato yenyewe

Kama za Mkoa wa Mara zilivyokaliwa na wajaluo (Kenya) , Arusha wamasaai (Kenya) Mtwara na Lindi wamakonde (Nchumbiji) - Ruvuma wangoni na wayao (Malawi) - Kilimanjaro pia na Kagera upande wa mpakani na Uganda! Pia Mpanda,Katavi, Sumbawanga (Zambia) - Kigoma wamanyema (DRC).
Kwa hiyo Usishangae warundi na wanyarwandwa kuwapo. Ubaguzi ulishindwa hata Africa ya Kusini wakati wana bomu la nyuklia! Sembuse ubaguzi wako wa chuki tu na ujinga! Shame on you!
Muwe mnakaa kimya wakubwa wakiwa wanaongea vitoto vya siku hizi hamna adabu kabisa.
 
Unaunda mkoa mpya kwa kumega ardhi toka mikoa mingine isiyotaka kumegwa!!!!
 
objectively, kuimega Chato kutoka Geita (ilikuwa Kagera kabla), Ngara-kutoka Kagera, Kakonko kutoka Kigoma, Bukombe na Biharamulo kuwa mkoa ni jambo jema. Kwa sasa wanaofaidi matunda ya mkoa Kagera ni Bukoba, Muleba na Karagwe. waiache Ngara iondoke tuu. mfano Ngara ilichangia sana kujenga miundo mbinu ya shule za Bukoba miaka ya nyuma....mda si mrefu wakaambiwa kila wilaya ijitegemee kwa kujenga miundombinu yake. Mpaka leo Ngara haija recover. ni miaka ya juzi tuu imeanza kupata shule zake. Ndo maana hata wana ngara waliopata elimu kupitia shule za bukoba ni wachache. Pia kutoka Ngara kwenda Bukoba ni mbali.

Chato utakuwa mkoa wenye coherence. Ngara na Kakonko lugha yao ni almost ile ile. Biharamulo na Chato zamani ilikuwa wilaya moja. imagine mtu kutoka Kakonko kwenda Kigoma kutafuta huduma. kwa raslimali walizonazo...utakuwa mkoa wenye potential sana. Ngara kuna madini ya kutosha...Chato uvuvi nk....Hata kikanisa..Ngara, Chato, baadhi ya sehemu za Kakonko, na Biharamulo ziko chini ya Jimbo moja la Rulenge-Ngara......(ingawa hili kiuhalisia halina uzito-maana imani za kidini na serikali ni tofauti)

Sema, kurahisisha maisha na huduma kwa wananchi....huu mkoa ungewekwa katikati pale Biharamulo. Ila hata makao makuu yakiwekwa Chato sioni shida...

Changamoto hapa ni kwamba wengi wanamchukia Hayati kwa hiyo hata swala la huu mkoa wanaliangalia kwa miwani ya mwendazake. ila kiukweli Chato na hizo wilaya tajwa.. unastahili kuwa mkoa.

Ingawa nashauri kuondoa au kupunguza hizi chuki dhidi ya mwendazake....tunaweza kuuita jina lingine ila isiwe Chato. Mf. mkoa wa Rubondo au mkoa wa Nyabugombe...au Burigi....nawaza tuu.

Ingawa nimalizie kwa kusema kwamba ingawa Hayati alikuwa anatokea Chato, Chato na hizo wilaya kuna watanzania wengine pia. Wathaminiwe na kuheshimiwa pia. sioni kwa nini mwananchi wa Ngara au Kakonko awe penalized kwa sababu tuu hizi wilaya ziko karibu na Chato.
Na ni kweli bukoba,misenyi,muleba,karagwe na kyerwa zina maendeleo makubwa hasa ya vijijini na Hali ya maisha kiujumla tofauti na biharamulo na ngara.
Imagine Biharamulo ilikuwa wilaya ya pili Kwa umaskini nchini.

Pia wahaya wameachiwa mkoa wao sasa maana walitofautiana mno na biharamulo na ngara .


Mkoa usiitwe chato mkoa uitwe biharamulo na makao makuu yawe biharamulo.


Watu wasichangie kisiasa maana hata kuumega mkoa wa kagera ni Sawa Sana maana mkoa Una population density na population kubwa pia zaidi million 3 na density ya 120 per km.
Wanaoagalia umbali Tu ili ianzishwe mikoa ya kutoka tabora na Lindi wanakosea maana mikoa hiyo ina population ndogo na density pia
 
Mkuu wa mkoa wa Geita mh Rose amesema ombi la kuunda mkoa wa Chato likipita basu mkoa wa Geita utabakiwa na wilaya za Busanda, Nyang'wale na Geita yenyewe na Mbogwe

RC Rose amesema mkoa mpya wa Chato utapokea wilaya 1 kutoka Kigoma na 2 kutoka Kagera.

Kwa maana hiyo mkoa mpya wa Chato unaopendekezwa utakuwa na wilaya 5 ambazo ni Kakonko kutoka Kigoma, Bihalamuro na Ngara kutoka Kagera na Bukombe na Chato yenyewe kutoka Geita.

Chanzo: ITV habari!

Kazi Iendelee
Ikiwa hivyo, namhurumia Marehemu maana ndoto zake tangu tupo primary school zilikuwa kuondoa chato kutoka kwa ‘wahaya’ ili ikaungane na wasukuma wenzao!
 
Sawa Mkuu, ila ukitazama kwenye ramani hata hivyo mtu wa kutoka Bukombe ni kama Chato kwake ni mbali zaidi kuliko Geita
Nadhani ishu wabongo wengi wanaangalia kugawanywa mikoa Kwa umbali Tu sio population density na population.

Mkoa wa Dar ni mdogo kigiographia lakin Una wilaya nchini hivyo hivyo Kwa Kilimanjaro.


Kagera ambayo imemegwa wilaya mbili kulingana na makadirio ya idadi ya watu ina population ya 3.2 million people na population density ya 120 per km nyuma ya mkoa wa Dar na mwanza tu yaan hata Kilimanjaro inaziwa na kagera Kwa population density na population na kijiografia ni makubwa na mrefu. Kutoka ngara Hadi bk ni 400 km .

So nashangaa watu wanasema sijui mikoa ya Lindi, tabora igawanye.
Just imagine mkoa wa Lindi Una watu million Tu na population density ya 12 people per km. Sawa ni mkubwa sasa wakianzisha mkoa watu watatoka wap.
 
Na ni kweli bukoba,misenyi,muleba,karagwe na kyerwa zina maendeleo makubwa hasa ya vijijini na Hali ya maisha kiujumla tofauti na biharamulo na ngara.
Imagine Biharamulo ilikuwa wilaya ya pili Kwa umaskini nchini.

Pia wahaya wameachiwa mkoa wao sasa maana walitofautiana mno na biharamulo na ngara .


Mkoa usiitwe chato mkoa uitwe biharamulo na makao makuu yawe biharamulo.


Watu wasichangie kisiasa maana hata kuumega mkoa wa kagera ni Sawa Sana maana mkoa Una population density na population kubwa pia zaidi million 3 na density ya 120 per km.
Wanaoagalia umbali Tu ili ianzishwe mikoa ya kutoka tabora na Lindi wanakosea maana mikoa hiyo ina population ndogo na density pia

Asante mkuu. Hivi vitu ukiviangalia bila kujifunza historia yake utakwama. Biharamulo na Ngara wamenyanyasika sana uwepo wao Kagera. kiuhalisia sidhani kama Ngara na Biharamulo wamefaidika kwa lolote kuwepo Bukoba.

mnyonge mnyongeni...JPM hili alilijua siku nyingi na alijitahidi kupambana. Bila juhudi za JPM sidhani kama Ngara, Biharamulo na Chato zingetoboa siku za hivi karibuni. Bukoba ilimeza kila kitu!

Ungeniuliza mimi ningeshauri makao makuu yawekwe Biharamulo.
 
Ni kweli kama watakuwa fair Bihalamuro pana deserve kumpunguzia umbali mtu wa Ngara na Kakonko nadhani na Bukombe
Ili mama Samia aliangalie sana.

Makao makuu yawe biharamulo
 
Ikiwa hivyo, namhurumia Marehemu maana ndoto zake tangu tupo primary school zilikuwa kuondoa chato kutoka kwa ‘wahaya’ ili ikaungane na wasukuma wenzao!
Mbona wakiufanya mkoa watafanikiwa mno .

Mkoa kagera unaachiwa na wahaya Tu peke Yao.

Biharamulo na ngara hazikuwa wilaya za wahaya Bali wasubi, wasukuma na wahangaza
 
Ama kweli kutangulia sio kufika! Hapo kabla, Chato ilikuwa ipo wilaya ya Biharamulo... leo hii Biharamulo inataka kuwa Mkoa wa Chato!

Hakika Everything happens for a reason!
Chige ukitaka kuwa fair, bila mihemuko ya kisiasa, Biharamulo would be ideal makao makuu. Ingawa na wenyewe ile jiografia yao ya barabara kuu kupita nje ya mji..inawatesa sana!
 
Chige ukitaka kuwa fair, bila mihemuko ya kisiasa, Biharamulo would be ideal makao makuu. Ingawa na wenyewe ile jiografia yao ya barabara kuu kupita nje ya mji..inawatesa sana!
Wala kupita nje ya sio tatizo .mji utapanuka kuifata hiyo barabara.kama ulivyo mji wa bukoba. Barabara kuu imepita rwamishenye 4km kutoka bukoba town centre lakin mji umepanuka na kupitiliza rwamishenye na kueleka katoma 10 km kutoka cente. Na rwamishenye inachangamka zaidi kuliko huko katikati.
 
Chige ukitaka kuwa fair, bila mihemuko ya kisiasa, Biharamulo would be ideal makao makuu. Ingawa na wenyewe ile jiografia yao ya barabara kuu kupita nje ya mji..inawatesa sana!
Sasa kwavile wanalipenda sana neno "Chato" labda kwavile ni fupi kuliandika, basi wanaweza kuanzisha Mkoa wa Chato wenye Makao Makuu Biharamulo!

Unless kama kulikuwa na sababu za msingi za kupitisha barabara nje ya mji, lakini kama hakuna basi baada ya Biharamulo kuwa ndio Makao Makuu ya Mkoa wa Chato, ofisi za mkoa zingeifuata barabara, and eventually mji ungeendelea kupanuka kuelekea zilikojengwa ofisi kadhaa za mkoa, na hivyo kumaliza changamoto ya barabara kujengwa nje ya mji!
 
Hizo wilaya zinazounda mkoa wa Chato ni wilaya zilizokaliwa na warundi na wanyarwanda kuanzia Lafudhi hadi mila na desturi.
Umeishia darasa la ngapi? Unafaham historia ya Nchi yako? Tz kuna mijinga mingiiiii sanaaaaa haijiewi, by the way kwa concept hyo watz n akina ndugai tuu nyie wakaskazin n Wakenya🤨🤨🤨
 
Mkuu wa mkoa wa Geita mh Rose amesema ombi la kuunda mkoa wa Chato likipita basu mkoa wa Geita utabakiwa na wilaya za Busanda, Nyang'wale na Geita yenyewe na Mbogwe

RC Rose amesema mkoa mpya wa Chato utapokea wilaya 1 kutoka Kigoma na 2 kutoka Kagera.

Kwa maana hiyo mkoa mpya wa Chato unaopendekezwa utakuwa na wilaya 5 ambazo ni Kakonko kutoka Kigoma, Bihalamuro na Ngara kutoka Kagera na Bukombe na Chato yenyewe kutoka Geita.

Chanzo: ITV habari!

Kazi Iendelee
Hii nchi ya hovyo sana kuongeza maeneo ya utawala kunatatua vipi tatizo kubwa kama la ajira?
Kwanini kipaumbele isiwe kujenga hospitari kama Muhimbili,Kagera,au Mtwara,au chuo kikuu kama UD au Udom?kwanini tunakimbilia kuigawa nchi kama vile Kuna tija yoyote,zaidi ya kuongeza gharama za uendeshaji,RC,RAS,RPC,?
 
Umeishia darasa la ngapi? Unafaham historia ya Nchi yako? Tz kuna mijinga mingiiiii sanaaaaa haijiewi, by the way kwa concept hyo watz n akina ndugai tuu nyie wakaskazin n Wakenya[emoji2955][emoji2955][emoji2955]
Mi sijaishia darasa lolote afu mi ndo Ndugai mwenyew kuwa na adabu we Sadala.
 
Back
Top Bottom