RC Rose: Mkoa wa Chato utakuwa na wilaya 5 Kakonko, Biharamulo, Ngara, Bukombe na Chato yenyewe

RC Rose: Mkoa wa Chato utakuwa na wilaya 5 Kakonko, Biharamulo, Ngara, Bukombe na Chato yenyewe

Sasa unataka umaskini usogezwe Biharamulo makao makuu badala ya kuuvutia pengine ukapunguzwe! Kumbuka pia Kakonko alikua wa kwanza kwa umaskini kwa hiyo kiujumla ni mkoa mpya wenye changamoto na inatakiwa wananchi wachangamke kuukwamua. Anzeni na kuchagua wawakilishi wenye akili za kuwakwamua wananchi na maeneo yao. Wabunge na madiwani, halafu mpewe viongozi wasimamizi wenye uthubutu. Hilo ni eneo potentials sana hasa katika kilimo na ufugaj.

Mkuu tusidanganyane...set up ya utawala wa nchi yetu..Rais ndo mwenye mamlaka na sauti ya mwisho fungu liende wapi! Hukuona JPM alikuwa anawasimanga waliojaribu kuchagua wapinzani wake kisiasa?

Hakuna mbunge anayeleta maendeleo Tanzania!

Ukweli ni kwamba kuanzisha mkoa mpya..angalau itasaidia watu wagawane kidogo kilichopo. Ila kiuhalisia wilaya kama Kakonko, Ngara zilisahauliwa kabisa. Maybe wakipata mkoa..wananchi wanaweza pata fursa kidogo.
 
Hakuna umbali huo kati ya Ngara na Bukoba. Ukipita Karagwe ni KM 270 na ukipita Biharamulo ni KM 300. Pili KM haziwezi kuwa sababu ya kugawa kwa sasa, dunia inaelekea kuwa ya kidijitali na umbali wa kimawasiliano unazidi kupungua siku hadi siku.

Tunatumia sababu zisizo na mashiko kuongeza gharama za uendeshaji.
Lakin bado ni mbali Sana. Yaan ushafika morogoro tayari ukitoka Dar.


Population density na population zinamata imagine kagera ina 3 million people,na density ya 120 people per square km. So ni sahihi Sana kuugawa.

Mkoa kama Dar ni mdogo na unawilaya nyingi sababu ni population density na population.

Ni upumbavu kutengeneza mkoa mpya Kwa sababu ya umbali Tu bila kuangalia population utakuwa mkoa wa nyasi Tu na mbuga mfano kama Lindi yenye density ndogo
 
Watz wengi sana ukisoma comments unaona ni wajinga, wana wivu na maendeleo ya nchi yao as if sehemu fulani ikiendelea sio ndani ya Jamhuri...wengine with very poor analytical skills wana compare mikoa yenye mapori kama Tabora na Morogoro wanq sahau Geita ni kati ya mikoa yenye population density kubwa per square kilometers. Unataka waanzishe mikoa ku service miti na mapori?
Hata kagera pia.

Hiv hawajiulizi Kwa nini mkoa wa Dar na Kilimanjaro ni midogo lakin ina wilaya nyingi.
Sababu kuu ni population density na population.


Mkoa kama kagera Una density ya 120 na population above 3million ukiwa wa tatu nchi nyuma ya Dar na mwanza so ni Bora ugawanywe ili watu wawe managed vzr.

Tofauti na mikoa kama Lindi wenye density ya 13 per km
 
Biharamulo vichwa maji tia maji tia maji sana. Wakipewa makao makuu ya mkoa haifumi pale. Hawana ali ya maendeleo pale. Majungu ndiyo yao, ndio maana kamebaki vile vile toka enzi za mjerumani mpaka leo. Ki wilaya ka wajuaji wasiojua kama hawajui. I rest my case.
Hakuna kinachoshindikana Kwa serikali
 
Hujanipata sawia, alitaka Chato isichanganyike na wasio wasukuma. Kwake wasubi aliwaita wahaya; wanyambo pia aliwaita kuwa ni wahaya nao. Isipokuwa alipokuwa Katoke seminari alichangamana na wahangaza ambao kwake hawakuwa wahaya. Kwake ilimradi lugha yako inasikilizana na wahaya basi ni mhaya na tuseme ukweli hakuwapenda! Hivyo kitendo cha kuingiza biharamulo kuwa part ya chato inaua dhamira yake maana lugha yao inasabihiana na kihaya.
Tuambie sababu ya JPM kuwachukia wahaya
 
Wengi wanaopinga humu ni wale wanatumia nauli sh 400/=kwenda kupata huduma mkoani. Hivi imagine mtu wa ngara ana kesi Bukoba mjini na anaudhuria karibia kila wiki au mara mbili kwa mwezi, huyu mtanzania wa hali ya chini ataweza??
Kiukwwli hizi wilaya zinahitaji kusogezewa kiuduma karibu
 
Watz wengi sana ukisoma comments unaona ni wajinga, wana wivu na maendeleo ya nchi yao as if sehemu fulani ikiendelea sio ndani ya Jamhuri...wengine with very poor analytical skills wana compare mikoa yenye mapori kama Tabora na Morogoro wanq sahau Geita ni kati ya mikoa yenye population density kubwa per square kilometers. Unataka waanzishe mikoa ku service miti na mapori?
[emoji3][emoji3][emoji3]mtu anasema eti na Lindi itengwe!!! Hebu tuwe serious kidogo penye ukweli tuuseme, hili wazo ni zuri
 
Mhh. Uitoe Kahama Shinyanga ibaki na nini ?
Shinyanga si itabaki na wasukuma wa Maswa, Kishapu, Lohumbo na Shinyanga yenyewe: zenye utajiri wa almasi na ng'ombe. Kahama iungane na wanyamwezi wenzao kuunda mkoa wao wa mahama, zao linalopatikana kahama pekee hapa duniani lakini halitambuliki na sasa hivi karibu litapotea kwenye uso wa dunia.
 
Moshi ingeshakuwa mkoa na Kilimanjaro Jiji. zamaaaani sana aisee.hembu angalieniangalieni

Yaani tungekuwa na wilaya ya
1. Pasua
2. Marengo
3. Himo
4. Mwaga
5. Kilema
6. Dar west KLM
7. Uru
8. Kishumundu
9. Rombo
10. Ugweno
 
Ni kweli kama watakuwa fair Bihalamuro pana deserve kumpunguzia umbali mtu wa Ngara na Kakonko nadhani na Bukombe
Makao makuu hayaangalii ukatikati wa eneo, Kuna factor nyingi ikiwemo miundombinu ya ku accommodate huduma na hadhi ya mkoa. Wilaya zingine walikua wanajipanga wakati Biharamulo inapiga porojo. Yaani hata kama B'mulo ingekua ina miundombinu ya kupokea makao makuu sawa tu, hata Kakonko au Ngara ingekua inajitosheleza ingekua vema tu lakini katika wilaya zote pendekezwa,

Wenzenu walikua wanafanya mapokeo kuanzia majengo ya mahakama, vyuo, hospital zenye level ya kanda ukiacha ya wilaya ambayo ipo siku mingi, mahotels, traffic lights, international airport (sio airstrip kama ya katoke) miradi chungu mzima yenye levels ya kikanda na wala si ya kitaifa halafu leo unasema makao makuu yapelekwe Biharamulo ambako hata hospital ya wilaya tu haipo mnang'ang'ana kuijenga pale barabarani like serious mnaomba makao makuu wilaya kongwe Afrika Mashariki tangu enzi za Mjeruman lakini bado unasema ni ya pili kwa umaskini. Kwanini watoto wenu Chato waliendelea kwa kasi hata baada ya kujikata kuliko Biharamulo ?!

Hii Chenga ya mwili ilishapigwa kitambo hakuna namna ni kuwa wapole tu.
 
Back
Top Bottom