Ripoti ya CAG 2021-2022: Rais Samia ataka baadhi ya mashirika yasiyo na tija kufutwa

Ripoti ya CAG 2021-2022: Rais Samia ataka baadhi ya mashirika yasiyo na tija kufutwa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu leo amepokea ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) pamoja na TAKUKURU. Katika ripoti hiyo CAG aliyataja mashirika 14 yanayoendeshwa kwa hasara ikiwemo TRC, ATCL na NDC. Rais Samia alisema kwa muda baadhi ya makampuni yamekuwa yakiendeshwa kwa hasara lakini hayaingizii serikali chochote ni bora yakafutwa ili kutoendelea kuleta hasara.

"Kuna haja ya kufanya tathimini kama baadhi ya mashirika ya umma yanafaa kuendelea kuwa nayo, yale yanayofaa yaendelee na yasiyo na tija yafutwe. Mashirika mengi yanachuma fedha kutoka serikalini lakini yenyewe haileti fedha serikalini" - Rais Samia Suluhu.

Lakini kwa upande wa TTCL, Rais Samia Suluhu anasema "TTCL na biashara ya simu kusema kweli imewashinda, tujiulize hivi kweli wanaweza kuendelea kufanya biashara ya sekta ya simu, kwanza wao wana mkongo, kwa kufanya biashara ya simu hakuleti mazingira sawa ya ushindani katika biashara hiyo na kampuni nyingine."

FsYZILXXoAE0pLd

Namuunga mkono mama
 
Namuunga mkono kwa hili, hakuna haja ya kung'ang'ana na mavitu yanayotafuna pesa za walipa kodi tu bila umuhimu wowote.
Kama mashirika tumeshindwa kuendesha si hata serikali yenyewe tumeshindwa pia? Shirika lililopo chini ya wizara tunasema tumeshindwa, alafu wizara tumeweza? Haiingii akilini
Kama kufuta basi na wizara nazo zifutwe
 
TTCL ni kampuni ya umma, naiona hatari simu nyeti kama za ikulu na Usalama zikipitia kampuni binafsi, ambazo wanahisa ni wale mabeberu.

TTCL wabaki na land line na miundombinu wezeshi ya mawasiliano
Hapa ndiko CCM yenu ya wezi na wavivu ilipotufikisha. Shirika kama hili linashindwaje kuendeshwa kwa faida kama siyo hujuma? Mkurugenzi, bodi na mazagazaga kibao si yanateuliwa na rais?
 
Tanesco walichofanya wameuza madeni yao yote kwa serikali. Hata hayo mashirika yakifanya hivyo hutaona hasara.

Najiuliza ilikuwaje mama samia alikubaliana na hawa kina maharage kuuza madeni ya Tanesco kwa serikali
Wewe umetoa wapi hizo hasara maana leo tanesco hajatajwa kabisa
 
TTCL ni kampuni ya umma, naiona hatari simu nyeti kama za ikulu na Usalama zikipitia kampuni binafsi, ambazo wanahisa ni wale mabeberu.

TTCL wabaki na land line na miundombinu wezeshi ya mawasiliano
Kwani hujui Rais hutumia namba ya Voda?

Serikali ina 49% Airtel
 
Tanesco walichofanya wameuza madeni yao yote kwa serikali. Hata hayo mashirika yakifanya hivyo hutaona hasara.

Najiuliza ilikuwaje mama samia alikubaliana na hawa kina maharage kuuza madeni ya Tanesco kwa serikali
Hana ''kichwa'' cha kuweza kujisimamia chenyewe. Japokuwa sikatai akubali ushauri lakini kuna mambio mengine hata kwa common sense ya mwenyekiti wa kijiji ni upumbavu kukubaliana nayo.
 
Serikali haifanyi biashara, mashirika kama TRC au TTCL waachiwe wawekezaji alafu serikali iwe mbia tu awe anakula tozo na gawio lake
Walishadanya hivyo ikashindikana. Tumesahau ATCL tuliingia ubia na South Africa? Mwisho shirika ndio likawa mfu
Ttcl tulifanya hivyo tena chini ya waziri mwandosya, mwisho wa siku shirika likawa mfu
 
Back
Top Bottom