RUGE tuamuangalie upande wa pili

RUGE tuamuangalie upande wa pili

muda mrefu nilikua natafta uzi kama huu.
.
uzuri wa mtu haujulikan akifa hata siku moja, mema ya mtu yanaonekana akiwa hai, qangu m ruge is nothing maana wakat yupo hai waliolaumu juu yake walikua weng kuliko walimsifia kam hivi sasa.
.
so naungana na vinega tu..


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Masaki alipokuwa anaishi amepanga? Kama hana Nyumba Basi ni Hatari Faya!!!

Nyumba bila mke inapwaya!
Penye msiba watu wanakula, wanakunywa !
Mfano hata mnahitaji vifaa flani mtajua vinakaaga wapi humo ndani?
Ama mtamuuliza nani? Na mwenyewe ndo huyo hayupo?!

Nazani amesema hana nyumba akimaanisha kuwa hakuwa na mke/familia !


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamani ambao umri umeenda na bado hamjaoa nawashauri mkaoe [emoji3][emoji3][emoji3]!
Kama uko na uwezo wa kutunza mke na watoto kaoe bana!

Unajua wengine wanatafuta visingizio na wengine kutafuta justifications lakini niwaambie ukweli wengine ni sababu ya vifungo!

Wengine wamerogwa [emoji108][emoji108][emoji108]

Kwa hiyo tafuteni ufumbuzi muoe bana!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi niulize Yule Nandy ni mmoja wa wanafamilia ya mutahaba au ni mmoja ya wajane?
Maana karemjee alikua ndani ukimbini akiwa ameketi sehemu ya familiyana Amelia sana hata kushindwa kuimba hii imeleta utata

Sent using Jamii Forums mobile app
Hizi ndio shida za mtu mzima kufa hujaoa. Unaacha michepuko inagombania high table
 
Inatakiwa ufungwe jela maana umetoa bandiko linaloudhi watu. Wewe jifikirie had rais kaumia kwa kifo cha ruge wewe ni nan usiumie nawaagiza polisi ufungwe jela maana hujaumia kwa kifo cha Mwana ccm ruge

Sent using Jamii Forums mobile app
Mzee kwani Rais ni malaika,mtume au Mungu? Acha fikra za karne 16 hii ni karne 21 si lazima anachoguswa nacho Rais na wewe uguswe,,,yeye ameguswa kwa kuwa ana maslahi nae moja kwa moja na si wote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tangu kutokea msiba wake sifa lukuki zimekuwa zikitolewa kuhusu maisha na kazi zake ambazo nyingi ni za kweli. Lakini kama tujuavyo hakuna binadamu aliye mkamilifu hivyo ukitaka kumuelezea mtu halisi lazima na upande wa mapungufu yake uyagusie.

Kwangu mimi Ruge licha sifa zote , hakuwa mfano wa kuigwa kwa maisha ya kijana na nitaeleza sababu zaangu.

Ruge amefariki akiwa na umri wa miaka 49 lakini hakuwa na maisha ya familia, kwa maana ya mke na watoto.

Ameishi maisha ya kihuni yasiyofaa kuigwa kwa vijana wanaotafuta kuishi vizuri. Ruge angekuwa ni mtu aliyefanikiwa kimaisha, msiba wake ungekuwa nyumbani kwake na sio kwa wazazi wake.

Vijana wengi alioibua vipaji vyao japo wengi wamefanikiwa kupata pesa lakini wengi wao wanaishi maisha ya kihuni.

Ndoa zao zimeshindikana na wamekuwa watu wa kuonyesha vitendo vya aibu katika jamii. Hili nalo naweza kulihusisha na Ruge kwani mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu wake.

Zipo pia tetesi kuwa hata pale Clouds wafanyakazi wengi wanajihusisha na vitendo vya kishoga na kwa msemo wa kiswahili kuwa lisemwalo lipo, huenda likawa na ukweli ndani yake na Ruge akawa ni sehemu ya jamii hiyo.

Nimalize tu kwa kusema Ruge amejitahidi katika sehemu moja ya maisha na kufanikiwa, kiuchumi, ila upande wa pili wa maisha , kimaadili, hakufanikiwa hata kidogo.

Kama binadamu mwenye imani kiasi, namwombea kwa muumba wake aipumzishe roho yake mahali zinakopumzishwa roho zote , Amen

Du we jamaa si bure aliyoyafanya ni makubwa hata angekuwa na familia leo ingemlilia peke yao ila alichowekeza kitabaki Milele kwa watu
 
Du we jamaa si bure aliyoyafanya ni makubwa hata angekuwa na familia leo ingemlilia peke yao ila alichowekeza kitabaki Milele kwa watu
Hakuna kinachoweza kudumu milele ila Mungu pekee, media imemkuza sana kuliko alivyostahili. Sioni makubwa aliyoyafanya zaidi ya kuinua vipaji vichache vya mashoga na wahuni kadhaa
 
Back
Top Bottom