Rushwa haina madhara yoyote ya maana kwa maendeleo ya nchi

Rushwa haina madhara yoyote ya maana kwa maendeleo ya nchi

San Abacha alikuwa Rais wa Nigeria. Alikuwa corrupt balaa. Aliiba karibu dola bilioni 5. Akatorosha pesa na kwenda kuwekeza Ulaya, leo hata hazijulikani ziliko. Mtoto wa Nguema ni corrupt san. Pesa ameenda kuwekeza Ulaya na Marekani.

Huyo Abacha au Nguema angewekeza hizo pesa nchini mwake ingeboost sana uchumi. Utoroshaji pesa ndiyo adui mkubwa kuliko rushwa na ufisadi. Tuwe na kampeni ya kupambana na utoroshaji pesa, kam tulivyo na kampeni za kupambana na rushwa.
 
hapa tumegusia mahakama,ambayo ni msingi wa kutoa haki ikiwemo business legal cases. Mwekezaji gani atakuja kwenye corrupt
wawekezaji wanaangalia faida. Tena wanapenda sana nchi zenye rushwa, hasa kama kuna bidhaa ina faida kubwa kama madini, mafuta, mazao ya misitu etc.
 
Tumia akili.hayo madeni yanalipwa Kwa kutumia Kodi ya watanzania.
Mimi ninachosema tule kwa urefu wa kamba zetu sio mpaka tuvimbiwe, kama mawaziri wameambia wajipimie na kila mtu akijipimia maisha yataenda...
 
Kupitia rushwa,hata watu wasio qualify,wanapata fursa!We fikiri wapanga maendeleo ya nchi wanakuwa vilaza kisa tu wamepata nafasi hizo Kwa rushwa!
Nchi zilizoendea kazi za sekta binafsi ndio nzuri zaidi, zenye kulipa vizuri na maslahi zaidi na ndizo zinasakwa zaidi na watu smart kuliko za serikali. Hapa kwetu udumavu wa sekta binafsi ndio inasababisha watu watoe rushwa na nepotism kupata ajira serikalini.
 
Tunapiga vita rushwa hadi tumeiundia taasisi. Na wengine wanasema nchi za Africa haziendelei sababu ya rushwa. Hili suala limefanyiwa utafiti na limeonekana halina ukweli. Imeonekana kuwa mtu anapokula rushwa na kuwekeza kwenye uchumi huo huo kunakuwa hakuna madhara yoyote ya maana kwenye uchumi.

Tatizo kubwa kwenye uchumi wa Africa ni utoroshwaji wa fedha. Viongozi wengi wa Africa wamekuwa wakiiba pesa na kwenda kuwekeza huko Ulaya au kuzitunza mabenki ya nje. Hapo wanaenda kukuza uchumi wa nchi hizo na kudhoofisha huku. Hili jambo linaathari kubwa sana kwa uchumi kuliko rushwa.

Matajiri wakubwa nao wamekuwa wakihamisha fedha nyingi kwenda nje ya nchi. Mambi haya yanaathari kubwa kiuchumi kuliko rushwa.

Pengine sasa PCCB waongezewe nguvu kubwa ili waweze kupambana na utoroshaji wa pesa, huo ndio moja ya adui wakubwa wa maendeleo yetu.
Uko sahihi mkuu kwa 90% japo wengi watakupinga.
 
Uelewa wenu unatia mashaka!Watu wafanye ufisadi,kwasababu ni pesa za serikali basi mnasema Haina madhara kwasababu mtu hatafuatwa nyumbani kudaiwa!Hizi ni akili timamu kweli?Pesa ambayo ilipaswa ikajenge Barabara,ikanunue madawa na wananchi tupate maji,eti ndio inakwenda kugharamia matumbo ya watu kujineemesha!
Hivi kweli unaweza kusema Kodi unayolipa watu wajinufaishe na haina tatizo kwasababu haikugusi Moja Kwa Moja?Huu ni Ujinga!
Basi tukafute hizo Sheria tulizoweka juu ya rushwa na ufisadi!
Na hiyo Takukuru ifutwe,goli liwe wazi kila mtu kujipimia an
Mimi ninamwelewa mtoa uzi, unajua mawazirii wameambiwa wale kwa urefu wa kamba zao, wasizidishe kwani wakizidisha wataharibu, polisi nae vivyo hivyo na watoa huduma kadhalika lakini watumie fedha hapa nchini wasiende kuzificha benki za Uswiss hapo uchumi utaendelea. Kama polisi akipokea Kita kisha akaenda kununua bodaboda akampa mtoto wa kaka yake huoni ametoa nafasi ya kazi kwa mtu mmoja. Au akijenga nyumba huoni mafundi kadhaa wamepata kazi ... ndio hivyo!
 
Tunapiga vita rushwa hadi tumeiundia taasisi. Na wengine wanasema nchi za Africa haziendelei sababu ya rushwa. Hili suala limefanyiwa utafiti na limeonekana halina ukweli. Imeonekana kuwa mtu anapokula rushwa na kuwekeza kwenye uchumi huo huo kunakuwa hakuna madhara yoyote ya maana kwenye uchumi.

Tatizo kubwa kwenye uchumi wa Africa ni utoroshwaji wa fedha. Viongozi wengi wa Africa wamekuwa wakiiba pesa na kwenda kuwekeza huko Ulaya au kuzitunza mabenki ya nje. Hapo wanaenda kukuza uchumi wa nchi hizo na kudhoofisha huku. Hili jambo linaathari kubwa sana kwa uchumi kuliko rushwa.

Matajiri wakubwa nao wamekuwa wakihamisha fedha nyingi kwenda nje ya nchi. Mambi haya yanaathari kubwa kiuchumi kuliko rushwa.

Pengine sasa PCCB waongezewe nguvu kubwa ili waweze kupambana na utoroshaji wa pesa, huo ndio moja ya adui wakubwa wa maendeleo yetu.
Kama yule askari
 
Utakapo hitaji kitu muhimu au huduma muhimu ambayo ni haki yako afu uulizwe umejipangaje . Ndo utakapo elewa
Mojawapo ya nchi yenye viwango vikubwa vya rushwa kubwa duniani ni Urusi ila bado ni mojawapo ya nchi kumi tajiri duniani ambazo wananchi wake wengi wana maisha mazuri ya maendeleo makubwa na raha mustarehe.
 
Since tunaongelea Uchumi na sio matatizo mengine ya Haki n.k. ngoja tuongelee Uchumi
How Corruption affects emerging economies
Inefficiently Allocated Resources
Uneven Distribution of Wealth
High Prices for Low Quality
Low Stimulus for Innovation
A Shadow Economy Exists
Low Foreign Investment and Trade
Poor Education and Healthcare
Russia ni mojawapo ya mataifa yenye viwango vikubwa vya Rushwa duniani ila bado ni Taifa Tajiri na lenye maendeleo makubwa sana.
 
Tufanye serikali inakopa trillions 6 kwa ajili ya barabara ya dar mpaka dodoma halafu mkandarasi ana jenga ya bajeti ya trillion moja baada ya miaka mitatu inaharibika unaenda kukopa tena ukarabati barabara ile ile iliyojengwa chini ya kiwango hapo si kutiana umasikini mkuu.

Kitu kimoja kinakopewa hela mara tatu na bado hakina ubora halafu unasema rushwa haina madhara we utakuwa askari bila shaka.
 
Mbona hata kununua bidhaa nje ya nchi NI sawa na kutorosha pesa nje...labda kabla ya masuala ya rushwa tupige Vita uagizwaji wa ndege,madawa,magari,n.k ili pesa zibaki hapa tu kuzunguka nchini [emoji1787][emoji1787]
Hawana huo ubavu vyoo tu wameshindwa kujenga leo hii ndege na madawa subutuu
 
Mimi ninamwelewa mtoa uzi, unajua mawazirii wameambiwa wale kwa urefu wa kamba zao, wasizidishe kwani wakizidisha wataharibu, polisi nae vivyo hivyo na watoa huduma kadhalika lakini watumie fedha hapa nchini wasiende kuzificha benki za Uswiss hapo uchumi utaendelea. Kama polisi akipokea Kita kisha akaenda kununua bodaboda akampa mtoto wa kaka yake huoni ametoa nafasi ya kazi kwa mtu mmoja. Au akijenga nyumba huoni mafundi kadhaa wamepata kazi ... ndio hivyo!
Duuuh,kweli akili zetu zimechoka!Sioni shida kama mkibariki na wizi,kwamba ukimuona tajiri,mvamie muibie then nunua boda boda mpe nduguyo,utakuwa umetengeneza ajira!!!
Nikuleleze tu,ikifika huko kwamba kila mtu apige basi hata miradi ya maendeleo haitamalizika!Fikiri mradi labda wa maji wa Bilioni 1,kuanzia Waziri mpaka mtendaji mdogo idara ya maji alijinyofolea kutabaki Nini?Acheni kushabikia rushwa na ufisadi!
 
hapa tumegusia mahakama,ambayo ni msingi wa kutoa haki ikiwemo business legal cases. Mwekezaji gani atakuja kwenye corrupt
Tatizo kubwa la mhimili wa mahakama kwa nchi nyingi za bara la Africa ni kuingiliwa na mhimili wa Executive/serikali sio rushwa ndio maana unaona hata kwenye nchi yenye kiwango kikubwa cha rushwa kama Kenya wawekezaji wanamiminika tu, sababu ni uhuru wa mhimili wa mahakama sio kwa sababu hakuna rushwa.
 
Wee jamaa naona umekula maharage mabovu tuu na unaonekana umekata tamaa ya maisha mpaka huwezi kufikiria vizuri tena
 
Back
Top Bottom