Rwanda yafunga Parokia 47 za Kanisa Katoliki

Rwanda yafunga Parokia 47 za Kanisa Katoliki

Ninacheka kama mazuri, Rwanda Makanisa yameacha kuhubiri habari za Yesu, sasa ni mwendo wa kuhubiri, amani na mshikamano. Kama Tanzania tu, sasa hivi, usiposifia chama na mama, watakusativa tu. Afrika bara letu...
Mbona huko dubei kwa wakina ami wanamswalia hadi mfalme mda wa swala.....sio geni hilo
 
Kagame anajua anachokifanya ila hata hivyo muda wake umekaribia atapita na utawala wake utapita. Kila zama na kitabu chake. Anamalizia kuandika kurasa za mwisho katika kitabu chake.
 
Wakati walokole wanafungiwa sisi waumini wa "cult" tulipiga vigelegele, kumbe sisi ndio wachafu kuliko hao walokole, sema tu jamaa alikuwa anatuvutia kasi.
Acha ujinga wewe. Wachafu kwa vigezo vya nani? Yaani mtu mmoja anaamua kuwa hiki kinafaa na hiki hakifai, halafu wewe unakuja hapa kukenua meno? Kagame yeye ni Mungu?
 
Unaweza ukaifananisha Rwanda na mitaa ya Nonde, mabatini, Meta, Ghana? Pamija na maeneo hayo kuwa ni mitaa tu, iliwahi kufikisha idadi zaidi ya makanisa 100.
Kila familia ni kanisa
 
Serikali ya Rwanda chini ya Paul Kagame imezifunga Parokia 47 za Kanisa Katoliki kwa madai ya kukiuka kanuni na sheria za nchi hiyo. Kwa mujibu wa ripoti ambayo imetolewa na Maaskofu wa Kanisa Katoliki, inasema kuwa suala la uhuru wa kuabudu limekuwa changamoto kubwa nchini Rwanda.

Ripoti hiyo inasema kuwa kati ya Parokia 231 zilizopo nchini humo, 47 tu ndizo ambazo zimefungwa kutoka katika Dayosisi tisa.

Hadi kufikia mwanzano mwa mwezi wa Septemba mwaka huu, Serikali ya Rais Paul Kagame ilikuwa imeyafunga Madhehebu na Misikiti takribani 10,000 kwa kile ilichokiita kukiuka sheria za nchi hiyo.


Misikiti mingi haina vyoo, ni michafu na makosa mbalimbali huku wakufunzi wake wakiwa hawana elimu dunia kitu ambacho utawala wa Kagame unasema ndio unasababisha kupotosha watu na kuleta machafuko. Ikumbukwe ilianza na walokole wote walikuwa wachungajinna manabii ambao hawana digrii ya dini walifungiwa na makanisa yao yakafungiwa.

65% ni Wakatoliki
9% Walokole
1% Waislamu

Uislamu ndio cult inayokuwa kwa kasi hapo Rwanda.

Wakati kagame anafunga makanisa ya walokole, baadhi ya Cult zilifurahia sana, zikafanya sherehe , sasa nazo cult zimefikiwa huku Makanisa yanayomwamini Yesu yakiwa yamejirekebisha na kuhubiri amani na mshikamano tofauti na cult!
Ni kuyapiga pin yote sio wagalatia wala wazee wa makubazii...dini zenye asili ya Africa ndo ziruhusiwe tuu.
Haya madini yenye utamaduni wa kiarabu na kizungu ndo changamoto ya mtu mweusi.
 
Serikali ya Rwanda chini ya Paul Kagame imezifunga Parokia 47 za Kanisa Katoliki kwa madai ya kukiuka kanuni na sheria za nchi hiyo. Kwa mujibu wa ripoti ambayo imetolewa na Maaskofu wa Kanisa Katoliki, inasema kuwa suala la uhuru wa kuabudu limekuwa changamoto kubwa nchini Rwanda.

Ripoti hiyo inasema kuwa kati ya Parokia 231 zilizopo nchini humo, 47 tu ndizo ambazo zimefungwa kutoka katika Dayosisi tisa.

Hadi kufikia mwanzano mwa mwezi wa Septemba mwaka huu, Serikali ya Rais Paul Kagame ilikuwa imeyafunga Madhehebu na Misikiti takribani 10,000 kwa kile ilichokiita kukiuka sheria za nchi hiyo.


Misikiti mingi haina vyoo, ni michafu na makosa mbalimbali huku wakufunzi wake wakiwa hawana elimu dunia kitu ambacho utawala wa Kagame unasema ndio unasababisha kupotosha watu na kuleta machafuko. Ikumbukwe ilianza na walokole wote walikuwa wachungajinna manabii ambao hawana digrii ya dini walifungiwa na makanisa yao yakafungiwa.

65% ni Wakatoliki
9% Walokole
1% Waislamu

Uislamu ndio cult inayokuwa kwa kasi hapo Rwanda.

Wakati kagame anafunga makanisa ya walokole, baadhi ya Cult zilifurahia sana, zikafanya sherehe , sasa nazo cult zimefikiwa huku Makanisa yanayomwamini Yesu yakiwa yamejirekebisha na kuhubiri amani na mshikamano tofauti na cult!
Safi sana. Huwa simkubali kabisa Kagame isipokuwa kwenye hili.
Ila taarifa ingeelezea hayo yaliyokiukwa na Kanisa la RC ingependeza
 
Huo utaratibu na sisi tungeuanzisha. Nadhani ni mzuri kwa namna yake. Na hasa kwenye kipengele cha kuhakikisha viongozi wa dini wanakuwa na elimu husika ya dini. Na siyo bla bla tu.
Naunga mkono kwasababu kuna watu hata qur an hawajui lakin wamejivika usheikh wanafanya na kuongea mambo kinyume na dini halaf watu wasioelewa wanawafanya hoja ya kupinga au kutukana dini lazim watu wasomee wanachohubiri.
 
Tanzania tumekuwa na mtindo wa kuwaona Baadhi ya Viongozi wa madhehebu ya dini kama miungu watu wasioguswa kisa tuu wanatiwa maaskofu sijui mapadri nk ambao wamekuwa Wanaochanganya masuala ya dini na siasa na kuhatarisha Umoja wa Kitaifa.

Huwa wanaenda mbali zaidi Kwa kutoa nyaraka na Miongozi Kwa waumi wao waegemee mlengi Fulani wa kisiasa.

Ila Cha kusikitisha Serikali Huwa inawaacha na haichukui hatua Kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi.

Ikumbukwe Hawa watu wa dini ni hatari sana Kwa kuweza kusababishia mtafaruku wa Kisiasa na Kuharibu Amani ya Nchi kama wataachwa Waendelee kutumia uhuru wao vibaya Kwa kufanya siasa Kwa mgongo wa dini.

Kama Nchi jirani inaweza kuwashughulikia hapa Tanzania tunapata kigugumizi Cha nini? Serikali ianze kuchukua hatua,Tanzania ni ya thamani zaidi kuliko dini zao.👇👇

View: https://www.instagram.com/p/DBHYU8qtgza/?igsh=MW5qcjEyMTJmMWxkNQ==
 
Kagame anajua anachokifanya ila hata hivyo muda wake umekaribia atapita na utawala wake utapita. Kila zama na kitabu chake. Anamalizia kuandika kurasa za mwisho katika kitabu chake.
Uzuri wa tawala za kurithishana ,,maono yanaweza yakaendelea tofauti na nchi ambazo zimejiweka kwenye mfumo wa kidemorasia hasa Africa, kila anaeingia anakua na mipango yake,,,,ila za kurithishana unaendeleza pale mtangulizi alipoishia, ndo anachofanya Kagame na Museveni
 
Naungamkono ...mimi natamani serikali zipige marufuku madhehebu ya dini zote tubaki na ukristo na uislamu usio wa madhebebu hivyo kuwe na nyumba chache za ibada zilizo hulia ambazo zitajengwa na serikali moja kila wilaya basi pia ipige marufuku shule za elimu dunia kuwa za kidini yaani kama mkristo akifungua shule hiyo shule iweshule tu siyo kwa mlengo wa dini ya mmiliki au dini ya dhehebu felani na kwa waislamu hivyo hivyo kwa sasa hadi fremason watafungua shule zao ya primary na secondary na kuzidi kuligawa taifa vibaya kupitia roho za watoto toka wadogo ....kumbukeni maandiko yanayo sema ufalme uliofarakana hauta simama .. serikali ipige marufuku vipindi na masomo ya dini kwenye shule zote za serikali na binafsi watoto wasomeshwe dini kwenye shule zisizo toa elimu.lasmi ya dunia
Na freemason wanapitia humohumo kwenye dini,,na wanaanza kuwawahi watoto kwa matumizi ya baadae
 
Safi sana. Huwa simkubali kabisa Kagame isipokuwa kwenye hili.
Ila taarifa ingeelezea hayo yaliyokiukwa na Kanisa la RC ingependeza
Ni siri kubwa sana, si unajua serikali ya rumi na warumi tuliopo hapa jukwaani namna tunatetea "cult" yetu, sakata la ushoga tulimpinga mpaka kiongozi wetu tukasema yeye hajasema.
Ndoa jinsia moja tumempinga kiongozi wetu.
 
Ni kuyapiga pin yote sio wagalatia wala wazee wa makubazii...dini zenye asili ya Africa ndo ziruhusiwe tuu.
Haya madini yenye utamaduni wa kiarabu na kizungu ndo changamoto ya mtu mweusi.
Mkuu una hasira sana.
So far sijaona dini ya Kiafrika iliyoleta machafuko, kuitana majina ya kishenzi , eti unamuita mweusi mwenzio "kafiri" mara gentiles, asiyeamini !
 
Serikali ya Rwanda chini ya Paul Kagame imezifunga Parokia 47 za Kanisa Katoliki kwa madai ya kukiuka kanuni na sheria za nchi hiyo. Kwa mujibu wa ripoti ambayo imetolewa na Maaskofu wa Kanisa Katoliki, inasema kuwa suala la uhuru wa kuabudu limekuwa changamoto kubwa nchini Rwanda.

Ripoti hiyo inasema kuwa kati ya Parokia 231 zilizopo nchini humo, 47 tu ndizo ambazo zimefungwa kutoka katika Dayosisi tisa.

Hadi kufikia mwanzano mwa mwezi wa Septemba mwaka huu, Serikali ya Rais Paul Kagame ilikuwa imeyafunga Madhehebu na Misikiti takribani 10,000 kwa kile ilichokiita kukiuka sheria za nchi hiyo.


Misikiti mingi haina vyoo, ni michafu na makosa mbalimbali huku wakufunzi wake wakiwa hawana elimu dunia kitu ambacho utawala wa Kagame unasema ndio unasababisha kupotosha watu na kuleta machafuko. Ikumbukwe ilianza na walokole wote walikuwa wachungajinna manabii ambao hawana digrii ya dini walifungiwa na makanisa yao yakafungiwa.

65% ni Wakatoliki
9% Walokole
1% Waislamu

Uislamu ndio cult inayokuwa kwa kasi hapo Rwanda.

Wakati kagame anafunga makanisa ya walokole, baadhi ya Cult zilifurahia sana, zikafanya sherehe , sasa nazo cult zimefikiwa huku Makanisa yanayomwamini Yesu yakiwa yamejirekebisha na kuhubiri amani na mshikamano tofauti na cult!
Mwamakula inamuhusu hii!
 
Back
Top Bottom