Sababu gani zitakufanya usipige Kura zoezi la Uchaguzi litakapofika?

Sababu gani zitakufanya usipige Kura zoezi la Uchaguzi litakapofika?

Ccm watawachukua wanafunzi wawapangishe mistari mirefu kuhalalisha upigaji wao
 
Bila Tume huru ya Uchaguzi hakuna sababu ya kwenda kupiga kura kwani kura sio inayoamua ni maigizo na kupoteza hela tuu.
 
Kama tarehe hiyo ya kupiga kura nitakuwa hai na nguvu yenye afya sitaenda kupiga kura ila nitaheshimu maamuzi ya tume kwa watakaye mtangaza na kumheshimu kiongozi/viongozi watakao tangazwa.

Sababu ni tofauti iliyowekwa na watawala katika kipindi cha utekelezaji wa majukumu kipindi cha utawala kwa watumishi na wateule kuwa na dharau kwa kujitumikia wao wenyewe zaidi kuliko wananchi.

Hili neno STAFF linaleta shida katika idara nyingi na ndio maana mwananchi hupuuza kuziendea idara inayohusika na jambo linalomtatiza
 
Kila sekta iliyoshikwa na ccm imefeli kuanzia uchumi, biashara, barabara mbovu wakandarasi matapeli wa kichina wanajenga zinaharibika , maji hakuna pamoja na kusifiwa kote kwa awesu mkwe wa mama

umeme ndio kizungumkuti mpaka watu wanatamani magufuli JP asingekufa umeme usingechezewa na wahuni.

Nauli zimepanda ili hali mishara haitopanda na haiakisi maisha ya watu, mwendokasi tuu imewashinda.

Upo wakati tukisoma success stories za Rwanda huwa tunatamani kagame angekuwa raisi wetu tungekuwa na maisha mazuri kama 2nd world semi periphery nations. Ame attract a lot of viable investment to his country simply kwa ku set standards procedure na sio kujipeleka kwenye conferences kila siku. Angalia uwekezaji wa NBa rwanda, Volkswagen, Renault, Univeristies za maana, Business incubators, hotel ndio usiseme na sasa asylum seekers wanaokwenda UK wataishi rwanda vizuri tuu.
 
Binafsi sio uchaguzi huu ujao tu, sitokaa nipige kura tena maisha yangu yote kama mambo yatabaki kuwa hivihivi na sheria zao mbovu za uchaguzi.

Kitu pekee nitafanya ni kujiandikisha nipate kitambulisho basi maana kinasaidia sometimes.
Wewe ni mimi mtupu yani niache shughuli zangu au kupumzika nikafanye ujinga never hii nchi tumuachie mungu tu maji shida umeme shida sasa nipige kura ili isaidie nini kweli
 
Kwa upande wangu sitokuja kushiriki hilo zoezi kwa sababu kuu zifuatazo:-

1) Tume ya uchaguzi haina uhuru kwa sababu inateuliwa na Mwenyekiti wa chama tawala.

2) Wakurugenzi wa Halmashauri/Miji/ Manispaa, nk wote ni Makada wa CCM na wanayeuliwa na Mwenyekiti wa CCM! Halafu wamepewa jukumu la kuwa wasimamizi ngazi ya Wilaya.

3) Matokeo ya Rais yakishatangazwa, hata yawe feki au yawe na dosari! Bado hayawezi kupingwa mahali popote pale mfano Mahakamani, nk.

4) Vyombo vya dola mfano polisi na usalama wa Taifa wamekuwa wakitumiwa waziwazi kwenye kukinufaisha chama tawala kwa kuwatisha wapiga kura na wagombea wake, kuwalinda Wakurugenzi wanaowatangaza wagombea ambao hawakushinda kihalali, nk.

5) Mara nyingi mshindi wa uchaguzi amekuwa akijulikana hata kabla ya matokeo. Kwa mfano mgombea wa Urais kupitia CCM akishapitishwa na chama chake; tayari huyo anatambulika kuwa Rais mtarajiwa hata kabla ya zoezi la uchaguzi kufanyika.

Kutokana na hizi sababu zangu hapo juu; aisee kupiga kura ni majaliwa. Ni mpaka hapo nitakapo jiridhisha kura yangu itaheshimiwa.
Umejieleza vizuri sana; hata mimi katika mazingira hayo siwezi kupiga kura.

Sasa ngoja nami nikueleze ni wakati gani ni muhimu kabisa kuhimizana kwenda kupiga kura; tena kwa wingi kabisa, na kama ingewezekana hata iwe kwa asili mia ya waTanzania wote wenye sifa ya kupiga kura; ikiwa ni pamoja na kujiandikisha kufanya hivyo.

Nitakwenda kupiga kura na kuhimiza wenzangu wote wakapige kura; hata kama CCM watakuwa wameng'ang'ania yote uliyo yaorodhesha hapo juu, iwapo kutakuwepo na vuguvugu la wananchi (kundi), lililopania kupambana na CCM katika uhalifu wao katika zoezi la upigaji kura.
Kundi hili linaweza kuwa linaongozwa na chama cha siasa, au hata asasi maalum itakayokuwa imejitoa kusimamia uongozi na utekelezaji wa mikakati ya kupambana na CCM.

Kujitokeza kwa wingi kwa waTanzania kupiga kura katika mazingira kama hayo kutawafanya hata CCM wenyewe waogope kufanya uhalifu.
Pia kujitokeza kwa wingi na kupiga kura za kuwakataa CCM hata wizi wa kuziba pengo la kura zilizowakataa litakuwa haliwezekani.

Kujitokeza kwa wingi na kupiga kura kuwakataa CCM, hata hao wateule wanaotumika kuharibu kura za wananchi wataogopa kufanya kazi hiyo.
Kujitokeza kwa wingi na kupiga kura kuwakataa CCM, ni ushahidi utakaokuwa wazi hata kwa mataifa mengine na washiriki wa kutoa misaada wataiona hali hiyo bila kujificha.

Kwa hiyo ni muhimu, kujitokeza kwa wingi wetu kupiga kura nyingi sana kuwakataa CCM, na kujipanga vizuri kukabiliana nao endapo watataka kuendeleza uhalifu katika mazigira hayo.

Jambo la muhimu sana hapa, ni huko kujipanga kwa wananchi, kuwa tayari kulinda kura zao zisiharibiwe.

Ukweli ni huu: pakiwepo na kundi la watu kama laki tano tu, watakaokuwa tayari kujitoa na kusimamia HAKI za waTanzania wenzao katika zoezi hilo la uchaguzi nchi nzima, CCM watakuwa hawana uwezo wa kufanya uhalifu juu ya uchaguzi huo.

Nisisitize tena. Nitahimiza watu wajitokeze kwa wingi sana kwenda kupiga kura iwapo kutakuwepo na chama, au kundi lililo tayari kusimamia haki za wananchi wa nchi hii.
Kutokwenda kupiga kura kukiwa na matumaini hayo, ni kuisaliti nchi yetu; na kuwafanya CCM wazidi kutamba.
 
Kila sekta iliyoshikwa na ccm imefeli kuanzia uchumi, biashara, barabara mbovu wakandarasi matapeli wa kichina wanajenga zinaharibika , maji hakuna pamoja na kusifiwa kote kwa awesu mkwe wa mama

umeme ndio kizungumkuti mpaka watu wanatamani magufuli JP asingekufa umeme usingechezewa na wahuni.

Nauli zimepanda ili hali mishara haitopanda na haiakisi maisha ya watu, mwendokasi tuu imewashinda.

Upo wakati tukisoma success stories za Rwanda huwa tunatamani kagame angekuwa raisi wetu tungekuwa na maisha mazuri kama 2nd world semi periphery nations. Ame attract a lot of viable investment to his country simply kwa ku set standards procedure na sio kujipeleka kwenye conferences kila siku. Angalia uwekezaji wa NBa rwanda, Volkswagen, Renault, Univeristies za maana, Business incubators, hotel ndio usiseme na sasa asylum seekers wanaokwenda UK wataishi rwanda vizuri tuu.
Mkuu, ya Rwanda na Kagame yaache huko huko. Tunajua tumekwama chini ya CCM, lakini hizo stori za Rwanda na Kagame achana nazo. Hazitufai kabisa.
Sijasema hayapo mazuri ya kuiga, kama hizo unazosema Standard Operaring Procedures; lakini Rwanda hawezi kuwa mfano wa kutaka kuuiga na kuuleta hapa.

Hatimae utataka nasi tukafanye biashara ya kulea wakimbizi wanaokataliwa ulaya? Hapana.

We can do better than that.
 
Kwa katiba hii na Tume hiyo huo muda sina kwa kweli.
Na wala huna muda wa kufikiri na/au kuunga mkono juhudi za kuwaondoa CCM madarakan!

Hilo litakuwa ni tatizo kubwa zaidi.i
 
Sina mpango tena wa kuidhinisha ufisadi wa kitaasisi kupitia sanduku la kura.
Nitashiriki kupiga kura baada ya nchi hii kupata uhuru kamili kutoka kwa wakoloni weusi.
Umewahi kujiuliza huo "Uhuru" utapatikana kwa njia zipi?

Kwa nini uhalifu wanao ufanya CCM wakati wa chaguzi isiwe chachu ya kutafuta huo uhuru? Mbona hii ni sababu nzuri kabisa ya kupambania huo uhuru. Kwa nini tusiitumie hii hii.
 
Kwa sababu wanotangaza matokeo wanatangaza matokeo ya uongo
 
Hebu leo tushirikishane

Kwanini wengi wanaona kwenda kupiga kura ni kupoteza Muda?
Sababu ya kwanza kabla ya kupiga kura mshindi teari anajulikana lakini pili Tanzania kuna semwa ni nchi inayofuata mfumo wa vyama vingi lakini sheria za uchaguzi zilizopo za mfumo wa chama kimoja yani kupiga kura nchi hii sawa sawa unauliza mwanamke anajinsia gani wataki ushasema mwanamke halafu unauliza jinsia gani ndio sawa sawa kwenda kupiga kura kumchagua mgombea unaemtaka halikua anetangazwa mshindi unamjua
 
Umewahi kujiuliza huo "Uhuru" utapatikana kwa njia zipi?

Kwa nini uhalifu wanao ufanya CCM wakati wa chaguzi isiwe chachu ya kutafuta huo uhuru? Mbona hii ni sababu nzuri kabisa ya kupambania huo uhuru. Kwa nini tusiitumie hii hii.
Swali zuri sana hili. Kama wote tunaokiri kuliona tatizo tungeungana na kukubaliana kwa kauli moja kuwa 2025 tukaiondoe CCM, mimi ningekuwa wa kwanza kupanga foleni kutekeleza, Lakini sioni kwenye upinzani chama au mtu wa kumwamini kama mwenye nia ya kutenda kwa maslahi ya nchi, wengi kulingana na program zao, kauli zao na hata matendo yao hayatofautiani sana na watawala wa sasa. Itachukua muda kwa watu kuelimika zaidi kuwa hatujapata uhuru bado na kadiri tutakavyokuwa wengi walio hamasika itakuwa rahisi kulisukumia kuzimu hili gogo CCM.
 
Binafsi sio uchaguzi huu ujao tu, sitokaa nipige kura tena maisha yangu yote kama mambo yatabaki kuwa hivihivi na sheria zao mbovu za uchaguzi.

Kitu pekee nitafanya ni kujiandikisha nipate kitambulisho basi maana kinasaidia sometimes.
Nifah: Unafanya kosa kubwa sana kususia hata kama kuna udanganyifu, wizi na dhuruma ktk uchaguzi. Husisusie haki bali itafute na kuipigania. Wewe kapige alafu linda kura yako lah kama uwezi ache wao waibe, ingawa hawana aibu ktk wizi wao lakini tukipiga wengi mwishowe zitawashinda kuiba. Haki itafute, ipiganie na kuilinda, lakini ukiacha au kususa, utawafanya hao wanaodhurumu wajione washindi na kuendelea kufanya watakavyo..
 
Wewe Fang mbona unatuuliza swali ambalo una majibu teyari au unataka tu kujaza server. Ni machawa tu ndio watapiga kura ili wandelee kula na kwa mtu anaejielewa uwezi kwenda kupiga kura ni kupoteza wakati. Nchi zetu za ulimwengu wa tatu nyingi hazina uchaguzi bali uchafuzi wa uchaguzi.
 
Back
Top Bottom