Sababu gani zitakufanya usipige Kura zoezi la Uchaguzi litakapofika?

Sababu gani zitakufanya usipige Kura zoezi la Uchaguzi litakapofika?

Kupiga kura tanzania ni kupoteza muda tu

Ova
 
Swali zuri sana hili. Kama wote tunaokiri kuliona tatizo tungeungana na kukubaliana kwa kauli moja kuwa 2025 tukaiondoe CCM, mimi ningekuwa wa kwanza kupanga foleni kutekeleza, Lakini sioni kwenye upinzani chama au mtu wa kumwamini kama mwenye nia ya kutenda kwa maslahi ya nchi, wengi kulingana na program zao, kauli zao na hata matendo yao hayatofautiani sana na watawala wa sasa. Itachukua muda kwa watu kuelimika zaidi kuwa hatujapata uhuru bado na kadiri tutakavyokuwa wengi walio hamasika itakuwa rahisi kulisukumia kuzimu hili gogo CCM.
GwaB: Umetekwa na propaganda za chawa wa CCM. Ni sera zipi unataka uzisikie toka kwa vyama vya upinzani? Vyama vinaundwa na nani kama siyo Mimi, wewe, yule na wao? Usisubiri mwingine akufanyie na wewe shiriki ktk kufanya. Kila mmoja wetu anayo haki na wajibu wa kufanya jambo kwa taifa letu.

Kwa kawaida nchi ina malengo ya muda mrefu na mfupi. vyama vya siasa utunga sera na kutafuta ridhaa ya kutimiza malengo yaliyokwisha wekwa. Serikali ya CCM ina sera mbovu sana na ndiyo maana kila Rais anapoingia madarakani uachana na mipango pamoja na miradi mikubwa ya kitaifa iliyoachwa na mtangulizi wake. Kwao wao mwenye sera ni mtu siyo chama. Chunguza, chambua na tafakari, kwasasa hivi hakuna chama cha ovyo Tanzania kama CCM, viongozi wake wapo kwa ajili ya kugawana kilichopo.
 
Kwakua majibu ya atakaye kuwa kiongozi yapo hata kabla ya kupiga kura. Mfumo mbovu wa uchaguzi. Kuna watu wameamua kujipa uhalali wakutuongoza yet hawajui hata Nini raia wanachokihitaji zaidi ya kulinda maslahi Yao kama kundi.

Kinachonishangaza ni watanzania wote kukubali haya na wengine kutumika kulinda hima za watu hawa ambao wamekuwa wafaidika tangu uhuru
 
GwaB: Umetekwa na propaganda za chawa wa CCM. Ni sera zipi unataka uzisikie toka kwa vyama vya upinzani? Vyama vinaundwa na nani kama siyo Mimi, wewe, yule na wao? Usisubiri mwingine akufanyie na wewe shiriki ktk kufanya. Kila mmoja wetu anayo haki na wajibu wa kufanya jambo kwa taifa letu.

Kwa kawaida nchi ina malengo ya muda mrefu na mfupi. vyama vya siasa utunga sera na kutafuta ridhaa ya kutimiza malengo yaliyokwisha wekwa. Serikali ya CCM ina sera mbovu sana na ndiyo maana kila Rais anapoingia madarakani uachana na mipango pamoja na miradi mikubwa ya kitaifa iliyoachwa na mtangulizi wake. Kwao wao mwenye sera ni mtu siyo chama. Chunguza, chambua na tafakari, kwasasa hivi hakuna chama cha ovyo Tanzania kama CCM, viongozi wake wapo kwa ajili ya kugawana kilichopo.
Mbussi; Nikupe taarifa tu kuwa kamwe siwezi kutekwa na laghai za vyama au wanasiasa. Kama kuna chawa wa CCM wanajaribu kurubuni watu kwa propaganda nikuhakikishie tu kuwa sidanganyiki na katika maeneo ninayoishi wanafahamu kuwa sina hizo za vyama.
Mawazo yangu ni huru kabisa na sihitaji usaidizi katika kufanya maamuzi.

Nchi hii inakwenda mrama kwa kuwa CCM ambayo ni ya hovyo inaendelea kutesa kwa kuwa hatuna vyama mbadala wa CCM, tuna vyama na wanasiasa wanaoibuka wakati wa uchaguzi ili waiingie kwenye nafasi za maamuzi yatakayo wanufaisha wao binafsi na sio Kama taifa.

Mimi naamini kuwa safari ya kutafuta uhuru wa nchi hii bado ni ndefu sana maana CCM ndio imechukua nafasi ya wakoloni kwa miaka zaidi ya 60.
 
Mbussi; Nikupe taarifa tu kuwa kamwe siwezi kutekwa na laghai za vyama au wanasiasa. Kama kuna chawa wa CCM wanajaribu kurubuni watu kwa propaganda nikuhakikishie tu kuwa sidanganyiki na katika maeneo ninayoishi wanafahamu kuwa sina hizo za vyama.
Mawazo yangu ni huru kabisa na sihitaji usaidizi katika kufanya maamuzi.

Nchi hii inakwenda mrama kwa kuwa CCM ambayo ni ya hovyo inaendelea kutesa kwa kuwa hatuna vyama mbadala wa CCM, tuna vyama na wanasiasa wanaoibuka wakati wa uchaguzi ili waiingie kwenye nafasi za maamuzi yatakayo wanufaisha wao binafsi na sio Kama taifa.

Mimi naamini kuwa safari ya kutafuta uhuru wa nchi hii bado ni ndefu sana maana CCM ndio imechukua nafasi ya wakoloni kwa miaka zaidi ya 60.
CCM imekula matunda ya uhuru na kwa sasa wameamua kuula uhuru wenyewe...prof.

Suruhu si kususa kupiga kura hisipokuwa ni kushiriki,.
.... kura yako ndiyo silaha uliyonayo ktk kuhamua.
 
Binafsi nawashauri MSIPIGE KABISA KURA Ili CCM ishinde (maana mimi nitapiga) na iendelee kubaki madarakani ili nchi iendelee kuwa na amani na maendeleo.
Wewe ni miongoni mwa chawa waliokaririshwa neno "amani" bila kujitambua. Amani itaenda wapi kama chama pinzani kikichukuwa dola? CCM imejiandaa kwenda msituni baada ya kupoteza? Usikariri yanayosemwa na wanasiasa majukwaani
 
Swali zuri sana hili. Kama wote tunaokiri kuliona tatizo tungeungana na kukubaliana kwa kauli moja kuwa 2025 tukaiondoe CCM, mimi ningekuwa wa kwanza kupanga foleni kutekeleza, Lakini sioni kwenye upinzani chama au mtu wa kumwamini kama mwenye nia ya kutenda kwa maslahi ya nchi, wengi kulingana na program zao, kauli zao na hata matendo yao hayatofautiani sana na watawala wa sasa. Itachukua muda kwa watu kuelimika zaidi kuwa hatujapata uhuru bado na kadiri tutakavyokuwa wengi walio hamasika itakuwa rahisi kulisukumia kuzimu hili gogo CCM.
Tulianza kuona matumaini chini ya CHADEMA.
CHADEMA iliyopambana na kusulubiwa wakati wa Magufuli na hatimaye kubaki salama baada ya mateso yote yale, tulitegemea kuwa wangeendelea na nguvu zilezile, baada ya Magufuli kuondoka; pasingekuwepo na shaka yoyote ile kuwa CCM wangefikia mwisho wake.

Sasa mambo yamekuwa ni tofauti kabisa. Baada ya hadaa za "Maridhiano" CHADEMA ikabadilika kabisa na kuondoa matumaini yote kwa wananchi waliokuwa wameanza kuwa na mategemeo ya kuuona mwisho wa CCM!

Hatujui kilichotokea, lakini ni dhahiri kuwa CHADEMA walimwagiwa sumu, hasa kupitia kwa mwenyekiti Mbowe.

Sasa sijui, tuwategemee akina nani katika mapambano haya. Akina Mwambukusi, Slaa, bila kujipanga kuwaongoza wananchi kimkakati, watabaki wakipiga kelele tu pembeni na kupuuzwa.
 
Sikumbuki mara ya mwisho nilipiga kura lini!
Na hiyo ndiyo ilikuwa mara ya mwisho, sitakuja kupiga kura tena.
 
Wewe ni miongoni mwa chawa waliokaririshwa neno "amani" bila kujitambua. Amani itaenda wapi kama chama pinzani kikichukuwa dola? CCM imejiandaa kwenda msituni baada ya kupoteza? Usikariri yanayosemwa na wanasiasa majukwaani
Dogo usinitilie maneno mdomoni. Wapi nimesema wapinzani wakichukua madaraka "amani" itatoweka? Nioneshe!
Mimi nawaambia hao wanajifanya "eti" hawatapiga kura. Watamkomoa nani? Mimi nitapiga na nitaipigia CCM. Itashinda na itaendelea kuwa madarakani ili ituletee maendeleo na kidumisha amani.
Umeielewa sasa pointi yangu?
 
. Itachukua muda kwa watu kuelimika zaidi kuwa hatujapata uhuru bado na kadiri tutakavyokuwa wengi walio hamasika itakuwa rahisi kulisukumia kuzimu hili gogo CCM.
Wapo waTanzania wa kutosha sana waliohamaki kutokana na matendo yanayofanywa na CCM.

Fahamu kwamba, katika nchi yoyote ile huwezi kupata wananchi wote wakawa na mwelekeo mmoja.
Hata huko kwenye nchi zinazojigamba kuwa na Demokrasia; hakuna wakati wowote wananchi wa huko wote wakashikiria msimamo mmoja. Chaguzi zao mara nyingi utakuta wanaokwenda kupiga kura kuchagua viongozi hata asili mia hamsini haifiki.

Ninachokueleza hapa, ni kuwa, kukipatikana uongozi, iwe wa kisiasa au kitaasisi ukawaunganisha kwa pamoja hawa waTanzania walio tayari kushiriki katika kuleta mageuzi, nchi itayapata mageuzi hayo.

Kwa hiyo, kinachotakiwa ni uongozi wa kundi lililo tayari kuleta mageuzi.

Kumbuka, hata huko ndani ya CCM, usichukulie kwamba ni wanaCCM wote wanaopendezwa na hali mbovu tuliyoifikia sasa hivi chini ya chama hicho. Kuna kundi dogo kabisa la wahalifu, ndilo linalokichafua chama kizima.
Hili kundi ndilo linalotakiwa kudhibitiwa na wananchi wa nchi hii.
 
Hebu leo tushirikishane

Kwanini wengi wanaona kwenda kupiga kura ni kupoteza Muda?
Kuzacsizo zinazoamua nani awe raisi au mbunge. Rais na tume ndo wanaamua kwa hiyo niende kupiga kura ili iweje?
 
Kwa kweli kwa mfumo uliopo ni ngumu kwa watu wengi kuwa muitikio mzuri wa kupiga kura.
Uchaguzi unashindikana kuwa wa haki kwa sababu hakuna neutrality kuanzia kwenye campaigns, uandikishaji wa wapiga kura, usimamizi, kuhesabu na pia utangazaji wa matokeo. Kwa mfumo huu ulivyo there is no way mgombea asiyekubalika na mfumo uliopo anaweza kushinda hata kama amepata kura nyingi. Hauwezi kuwa kocha, ukawa mchezaji, ukawa pia msimamizi wa mashindano na mlinzi wa usalama kisha timu yako isishinde!
 
Binafsi nawashauri MSIPIGE KABISA KURA Ili CCM ishinde (maana mimi nitapiga) na iendelee kubaki madarakani ili nchi iendelee kuwa na amani na maendeleo.
Ccm inashinda ikishindana na nani? Watu hawana muda wa kushiriki ukhanithi, na Isitoshe sio lazima viongozi wapatikane kwa njia ya kura. Hiyo njia ya kura ya njia ya kistaarabu, ambayo mmeshindwa kuiheshimu. Itatafutwa njia nyingine bila kujali madhara yake.
 
Nilipata kadi ya kupiga kura tangu 2010 na mpaka leo hii sijawahi kupiga kura na sina mpango wa kuja kupiga kura, mimi kwenye zoezi zote za kupata kitambulisho/vyeti ni lazima nishiriki ila baada ya hapo ndo kwaheri hvy
 
Ccm inashinda ikishindana na nani? Watu hawana muda wa kushiriki ukhanithi, na Isitoshe sio lazima viongozi wapatikane kwa njia ya kura. Hiyo njia ya kura ya njia ya kistaarabu, ambayo mmeshindwa kuiheshimu. Itatafutwa njia nyingine bila kujali madhara yake.
Sasa kelele za nini? Kaeni kimya sie tukapige CCM iendelee kutawala. Period!
 
Back
Top Bottom