uwe hodari
JF-Expert Member
- Dec 16, 2022
- 4,045
- 8,608
Mkuu ni kweli kabisa hii haliNatumaini wote mko poa ndg wana JF,, lakini poleni sana kwale wote wenye changamoto yoyote ya kiafya au maisha kwa ujumla poleni sana Mungu awasaidie mkae sawa [emoji120]
Ndg zangu nimeamua kuandika uzi huu kutokana na mambo yanayo fanyika kwenye jamii zetu haya mambo yanaumiza sana[emoji24] mitaani kumekuwa na vifo vingi sana vya watu baadhi vinaeleweka vizuri na wana jamii huku vingine vikiwa ni vya kuhisiwa tu kuwa huenda amefanywa hivi au
Lakini la kusikitisha zaidi kuna kuwa na watu wanao shuhudia kabisa mwanzo wa tukio mpaka mwisho lakini wanakausha kama vile hawajaona chochote ila mtu ndio tyr kafa hivo inabaki tu minong'ono ya chini chini wakifika polisi hao watu hujitenga kabisa tena wengine huondoka kabisa eneo la tukio,,, haya yote hutokea kwa sababu ya sheria na mifumo kwa askari walio wengi, shahidi akijitokeza kutoa ushahidi wake wana shughulika zaidi na huyo shahidi kuliko kushughulikia tukio zima yani yanageuka kuwa majuto kwa mtoa ushahidi hawafikirii kuwa huyo mtu ameguswa na matukio yanayo fanywa na baadhi ya watu wao hufikiria mtoa taarifa kuwa ana kiherehere kwahiyo wanakula sahani moja na shahidi tumeshuhudia watu wengi walio jaribu kusaidiana na askari kushughulikia waharifu lakini mwisho wa siku shahidi ndio anakuwa mwaharifu yaani,, yani askari badala ya kumpongeza mtoa ushahidi lakini wao wana mchallenge kupita kawaida hadi mwisho wa siku shahidi anashindwa anakuwa mtuhumiwa mwenyewe
Kwa kifupi hiyo ndio taswira tu ya mambo yanayo endelea kwenye jamii hadi kwenye suala la vifo kutoa ushahidi inakuwa ni kiherehere
Kuna siku moja nilipita barabara flani hivi nilikuta mtu amegongwa na gari gari lililo mgonga huyo bwana lilikuwa limepitiliza haraka kwahiyo halikueleweka kuwa ni gari gani japo kuna wengine walilitambua hilo gari lakini walikausha, huyo bwana alikuwa liye gongwa alikuwa amebaki pale barabarani hakuna mtu aliye msogelea wala kumgusa na vyombo vingine vya usafiri viliendelea kumkwepa akiwa pale pale,, mimi nilivoona watu wanashangaa tu hawataki kuenda kumsaidia nilijaribu kuwa hamasisha "jamani tuendeni tumsaidie mwenzetu..." watu walisema wanaogopa wakimgusa yule bwana eti wataacha alama za vidole itaonekana wao ndio wameua [emoji24][emoji24] kwahiyo tuliendelea kumshangaa pale huku wengine wakihangaika kuwaita polisi mwisho mimi uvumilivu ulinishinda niliamua kuenda hivo hivo bahati nzuri kuna jamaa mwingine alikuwa ameguswa na hilo tukio yeye alikuwa ana bajaji kwahiyo tulimbeba yule hadi hospitalini alikuwa bado hajapoteza maisha ila alikuwa amepoteza fahamu,, lakini kitu kingine cha ajabu tulivo mfikisha hospitalini tulijielezea na kueleza hali ilivo kuwa madaktari wakasema huu msalaba tunaubeba sisi tulio mpeleka pale kwa kuna gharama tulitakiwa tulipe kwa sababu haikujulikana kama ana bima au la! hivo sisi tulitakiwa kuullipia gharama zinazo husika kwenye ufunguaji wa faili bahati mbaya sana hiyo siku mimi na mwenzangu hatukuwa na hela za kutosha kulipia pale kwahiyo mgonjwa aliwekwa kando kwa muda 🥲 tukisubiri ndg zake waje na hii kesi siku sikia lolote mpaka sasa wala haikusemwa popote wala hakuna askari yeyote akijihusisha na hili tukio
Hii ndio hali halisi zinazo endelea kwenye jamii, watu wanaogopa kushiriki kwenye kutoa ushahidi hatakama mtu amepatika amekatwa katwa mapanga ikionekana tu uwezekano wa kupona huyo mtu ni mdogo watu wanakula kona,,
Mimi nimeandika tu huu uzi wala sifahamu kama unaweza kubadilisha chochote 🥲 lakini huku kwenye jamii zetu kumejaa maovu sana kama kuna mtu upo kwenye cheo fulani huko serikalini au upo kwenye harakati hizo nawaombeni mlitazame hili pia [emoji52] raia wanateseka sana watu wanapoteza ndugu zao bila sababu zozote za msingi HII AMANI INAYOSEMEKANA KUWA NCHI INA AMANI TUNATAMANI IWE NI AMANI YA KWELI KWA RAIA WOTE
Asanteni sana kwa kuvumilia kusoma huu uzi [emoji120][emoji120] naamini nimeeleweka maana yangu ni ipi
Mkuu ni kweli kabisa hii hali
Mi ilikua hivi
Mida ya usiku kama sa mbili kuna bodaboda alikua mbele yangu mi nna kibajaji sasa mbele kuna Lori lilikua bovu halina reflecta wala halijawasha taa sas yule boda hakuliona akaligonga kwa nyuma akaanguk hp hp na kupoteza faham watu walikuj wengi kushuhudia ila hawakutaka kumbeba bahT nzuri mm nikajitolea kumplek hospital ila baada ya jamaa kupandushwa kweny bajaj kila mtu akpita na njia zake hawatki ushahid bahat akatokea jamaa tu muokt kopo tukaend nae hospt na mgonjwa
Tumefk hospital wakagom kumtib had tuend polis kuchukua pf3. Tumefika polisi wanaanz kutuuliza jamaa anaitwa nani anakaa wap na maswali personal kibao na sis hatumjui ...tukajieleza tumerudi tena hospital nao wanatak hela za kufungua file na matibabu ..kiukwel polisi na mahospitali inabidi suala la ajali liangaliww uppya watu wanaacha kusaidia watu kwa kukwepa kubeba mizigo juu ya mizigo labda kama jamaa angekata moto naona kabisa mimi na muokta kopo tungewekwa ndani kwa ajili ya ushahidi
Tunaomba sheria au sera za majanga au ajali ziangaliwe upya ..pia ikiwezekqna pf3 ziwepo hospital na sio polisi
Asante
Kwa hiyo wewe 'whistle blower' unatumika kama condom, ikiishakutumika hutupwa?Ukitoa taarifa polisi ya labda muhalifu wa mtaani, na wao wanamfata mhalifu wanamwuliza unaishi vipi na wenzako mtaani! Maana ndio wametupa taarifa zako.
Hapo ni baada ya kuchukua hela ya kiwi.
Mwanaume kamili huwezi kulewa hata kama bia umenunuliwa ikiwa home hakuna msosiHuwezi jua pombe alikunywa kwa hela yake au alipewa offa na marafiki zake. Wanaume wanapitia mengi
Hili kwakweli lipo aisee .
Hata mimi kuna tukio ilibidi tu nicheze part ya kumfikisha mtu kwenye sehemu salama na nikimbie nikabaki mtazamaji wa mbali tu aisee . Polisi siwaamini kabisa .
Muhimu kama unaweza kuokoa maisha jitahidi okoa maisha
Kama unaona kuna mtu anaenda kuonewa kwa wewe kutotoa ushahidi unaoweza kumpa haki zake jitahidi tu basi tu
Ila polisi hawaaminiki na haswa kama hujiamini na sio mwongeaji mzuri ni shughuli
Unaona WANAWAKE WALIVYO. Yaani hayo matoto yameshasetiwa kitambo kuwa mkiona ugomvi semeni baba anamuua mama.Hii hali ni mbaya sana. Juzi uswahili kwetu huku tulisikia makelele ya watoto "Baba ana mchinja Mama" muda wa jioni tu kama saa kumi na moja kasoro.Watoto wamepiga kelele wee hadi wanaita majina ya jirani zao lakini waliotoka nje waliishia milangoni mwao tu hakuna aliyesoge
Mimi nikatoka nikasogea eneo ambalo kuna jamaa ni mafundi seremala. Nikiwaomba twende tukaamlie ugomvi watoto wamepiga kelele muda mrefu
Lengo langu na mimi ilikuwa kukwepa "kiherehere" kama mtoa mada alivyosema ili angalau tuwe wengi wengi
Ile kuingia ndani tukakuta "Hamadiii" mama wa watu yuko uchi kama alivyozaliwa kamakalia jamaa kifuani anaminya shingo jamaa katoa macho kuhema hawezi. Watoto wanalia "Baba anamchinja Mama" kumbe Mama ndo anamchinja Baba na kweli tusingeingia ndani muda ule huenda madhara makubwa yangetokea maana jamaa alikuwa kalewa hana uwezo wa kujitete na kisa cha ugomvi jamaa amerudi kalewa wakati familia kaiacha bila chakula ndani Mama hasira zikampanda akaona ampe adabu kidogo
Baada ya kuamlia ule ugomvi na kufikisha taarifa kwa mjumbe wa mtaa, jamaa alienda kuwashukuru wale fundi seremali kwa kuokoa uhai wake kwasababu ndio wanaofahamika zaidi pale kitaa. Wakamwambia wao waliogopa kuingilia ugomvi wasioujua wakasema mshukuru fulani aliyekuja kutushawishi (wakinitaja mimi) vinginevyo kwa hali tuliyoikuta ungekuwa historia sasa hivi
Ukiuliza kwanini watu hawakwenda kuamlia, ni kukwepa kutoa ushahidi tu hakuna kingine.
Kuna haja sana ya polisi na vyombo vya sheria kubadili mindset zao juu ya mashuhuda ili watu wasaidiane huku kitaa
Fanya ujinga Wote ktk Maisha yako, lakini sio kuwaeleza Polisi Taarifa ya Muarifu, Polisi WATANZANIA Ni Waajabu, Wakimpata mwalifu wanamwambia ukweli Wote kua we ndo umechomeshwa mpaka akamatwe.
Pia kutoa ushirikiano kwa Polisi Ni kujitafutia shida.
Inaumiza sana mtu kushindwa kumsaidia binadamu mwenzako kisa kuhofia kuangushiwa msala.
Yani hilo ndio tatizo kubwa mkuu kumsaidia mtu ni kununua kesi
Kilichonikuta 2003 sina hamu na polisi